Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Dua,
kuhusu UPEO nimekuletea makala ina-quote watu waliofanya kazi na sokoine. nadhani umejionea kwamba alikuwa mtu wa mtulinga, asiyefanya tafakuri ya kina kabla hajatoa uamuzi.

Kuhusu kuruhusu bidhaa toka nje, ni kweli Sokoine ndiye aliyefikia uamuzi huo. kabla ya hapo alikataa pendekezo la kufungua milango ya uchumi, na kuendelea kuwaletea mateso wananchi. hivi umesahau kwamba sokoine huyo huyo alikuwa akiwasweka watu jela kwa kuwa wamepatikana na colgate, kimbo toka kenya?

kwa kifupi mwalimu na sokoine waliwanyanyasa na kuwadhalilisha wale waliokuwa wakipendekeza mbinu tofauti na zao kuhusu kuokoa uchumi miaka ya 1980. wako waliolazimishwa kuacha kazi, wapo waliopikiwa majungu ili waonekane wabaya mbele ya jamii.

kitu cha kushangaza baada ya mambo kuharibika kabisa mwalimu na sokoine wakaanza kutekeleza yaleyale waliyoyakataa mwanzo. halafu bila haya, wala soni, wanajaribu kuchukua credits zote.

Kuhusu ubavu wa kumweleza mwalimu matatizo yaliyokuwepo....ni kweli mwalimu alimsikiliza sana sokoine, tatizo ni kwamba, sokoine alikuwa hana idea ya chanzo cha matatizo ya wakati ule, na wala mikakati[nguvu kazi,wahujumu uchumi]

Sokoine alikuwa waziri mkuu bora mpaka bale alipojitwisha jukumu la kutoa muongozo wa uendeshaji uchumi tanzania. sokoine alikataa kata kata ushauri mzuri ambao ungeokoa uchumi wetu miaka ya 1980. hiyo ndiyo sababu inayonifanya nimpe maksi mbaya.

Mwalimu aliona mawazo ya sokoine hayafai na ndiyo maana akaachana na kampeni ya uhujumu uchumi. kampeni ile ilikuwa ikikiuka misingi ya haki za binadamu na utawala wa sheria.

Unahitaji ushahidi upi kwamba nchi ilimshinda Mwalimu zaidi ya hali mbaya ya uchumi aliyotuachia alipotoka madarakani?

Mwalimu alitufanyia mengi mazuri, lakini ktk uchumi kwa kweli......mhhh
 
Wanabodi,
Mtakumbuka toka huko nyuma niliwahi kusema kuwa Nyerere alikuwa na agenda yake.. Agenda ambayo ktk utekelezaji wake - tuliumia wengi bila dini, kabila wala jinsia.
Kwa nguvu hiyo hiyo nitazidi kuwakumbusha ya kwamba Maazimio mengi magumu na ambayo bado leo hii ni kitendawili yalipitishwa wakati Tanzania hatuna waziri mkuu (1963 - 1972).
Kwa hiyo kumpachika Sokoine hizi lawama hali Kawawa alirudi kabla kumtangulia Sokoine na mambo yote haya yalikuwepo na yalizidi kuendelea hadi Msuya alipokuja kamata ktk awamu yake ya kwanza.
Sote tumehenya kwa maazimio haya na pengine kuna mazuri yake ambayo yametujaza ULIMBUKENI ambao wengi wanafikiri ndio UJANJA na UMJINI (tukiwaita Wakenya washamba).
Jamani hata wakati wa Hitler, mkuu wa majeshi yake aliyesifika ni yule aliyetekeleza maazimio ya Nchi yake. Utekelezaji ulikuwa mbaya kwa sababu hatukutaka kabisa kuwa wajamaa.
hali hii imetushinda hata leo huku nje kila jumuiya za Kitanzania ni Mkenge! tunashindwa kuwa wamoja zaidi ya vijiwe na vikundi vya Udaku na kukejeriana. UMOJA kwetu ni ustaarabu wa kigeni...Kila mtu (kijiwe) na mzigo wake ndio mwendo wetu.. We are friendly to each other not friends! that's the fact.
Mbona sisikii mtu akiwazungumzia mawaziri wa mambo ya ndani?...Wakuu wa upelelezi n.k hali hawa ndio tuliokuwa tukipambana nao kila siku.
 
Wooh?

Mbona hujibu swali ulilolirukia bila ya kuombwa? Hayo ya Malecela yanahusiana nini na swali langu?

Halafu ukijibiwa inavyotakiwa unakimbilia kwa mwenye forum kulia, mbona unaaanza tena ndugu yangu? Sasa bwana admin hebu nisaidie hapa maana mara ya mwisho nilimjibu huyu kijana ukasema nimetumia jazba, je nimjibu vipi this time, maana kama unavyojua I am always ready kwa majibu ya kejeli na fedhuli maana ndio raha yangu kupambana na watu fedhuli? Kuanzia wanasiasa mpaka wapuuzi kwenye forum!

Kwa hiyo kama hakuna majibu, nitamjibu huyu ipasavyo na hayo maneno yake ya chooni!
 
Na wewe si uliaga???? Lakini naona bado uko hapa ukitafuta beef. Mi nilijua tu....yalikuwa ni manjonjo yako tu. You're a fraud.
 
Jokakuu,
Bahati mbaya humjui Sokoine na from what you puport, hujawahi kusoma au kusikiliza maoni au hata hotuba za Sokoine.
Kwanza kabisa mwaka 1977 Sokoine alivyopewa cheo cha uwaziri mkuu, watu wengi hawakuamini maskio yao. Lakini baada ya miezi sita tu kila mtu ambaye ni makini alianza kusema kuwa huyu ndiyo waziri mkuu hasa. Kwa mara ya kwanza mwaka 1979, nyerere alisema hadharani kuwa sasa nimempata mtu ambaye ananielewa na amabae anaweza kufanya kazi na mie nikalala usingizi. Sijui kama utakumbuka hilo. Siasa za ujamaa na kukamata watu ovyo zilikuwa hata kabla ya Sokoine. Watu kupigwa ovyo, na kuwekwa ndani ulikuwa ni utekelezaji mbaya ambao ulikuwa kabla ya Sokoine.

Mwalimu alifeli vile vile kutokana na watekelezaji wabaya. Kwa mfano. Kuna mwaka ambao Nyerere alihutubia taifa na kusema kuwa tunahitaji maduka ya Ushirika zaidi ili yawahudumie watu. Kesho yake Kawawa akakurupuka na kuwaeleza watekelezaji wake maduka yote ya watu binafsi yafungwe. Nyerere alisimama na kusema kuwa yeye hakusema hivyo. Hiyo ndivyo hata mengi yale ya Azimio la Arusha nyerere alikuwa na watendaji wabovu ambao hawakumelewa.

Alipoingia Sokoine mambo yalikuwa vingine. Achana na hiyo nguvu kazi ambayo umeng'anag'ania; Sokine alitaka all issues ziwe more transparent, how people procure wealth, do their daily activities and all businesses. Yeye aliamini kuwa kama watu watafanya mambo kiuwazi basi hakutakuwa na matatizo ya rushwa nk.
Kwa mfano: Yeye ndiyo alianzisha kuwa daladala zifanye kazi kiuwazi zisiwe zinaiba iba vile husababisha accident na vilevile ni changamoto kwa UDA kufanya kazi vizuri.
Uuzaji wa Vyakula na bidhaa nyingine: Alienda kwa wauza mahindi na kuwaambia kuwa wauze vyakula vyao na bidhaa nyingine kiuwazi, wasiogope, na kuwaambia wapange bei ambazo wanataka ilimradi tu wananchi watanunua.

Jumuia ya Africa Mashariki ilikufa mwaka 1977, na kabla ya hapouhusiano wa Tanzania na Kenya ulikuwa ni mbaya sana. Mipaka ya nchi ilifungwa, unajua nani alimsihi Nyerere mipaka ifunguliwe? Sokoine.

Utekelezaji wa mambo siku saba unajua nani alileta?

Mwaka '80 alipojiuzulu alienda kusoma, aliporudi alihutubia kamati kuu kwa muda wa at least 1 hour, unajua content za hiyo hotuba? Kwa taarifa yako ndiye alyesema kuwa ujamaa au ubepari hakuna meaning kama wananchi wanalala na njaa; suala hapa ni wajibu wa kila mtu kufanya kazi. Aliongelea wajibu wa Serikali pamoja na wajibu wa wananchi, na viongozi wao. Alipohitimisha hiyo hotuba alimwomba Nyerere kwa kusema kuwa: Naomba tena nipate nafasi kuwa Waziri Mkuu; in a week time akawa Waziri Mkuu kwa mara nyingine.

Je unakumbuka baada ya hapo alianza nini?
Aliwaita viongozi wote Bagamoyo na kuwahutubia, akawaambia hii Serikali inanuka, na karibu nusu nzima lazima ibadilishwe au iondolewe.
Acha ile ya uhujumu uchumi, if you listen to media, especially Western Media ilikuwa inaandika mambo kivingine. Sokine hakuamrisha watu wanyanganywe mali zao. Alitaka watu wawe transparent how did they get wealth. Everywhere in the world vitu hivi ni transparent.

Yako mengi. Kwa mara ya mwisho aligundua kuwa viongozi wengi hawafanyi kazi zao vizuri. Alitembelea mikoa mbalimbali na kugundua kuwa suala la uzalishaji wa mazao nk unakwama kutokana na uzembe wa viongozi. Kila akiona huo uzembe aliwaambia hao viongozi kuwa kikao kijacho cha bunge Dodoma kitakuwa ni kuwatengue viongozi wazembe. Kikao hicho kweli kilikuwa kizito.
Alikuwa ndiyo arudi Dar na kutekeleza mambo yake, akafariki njiani.
Remember that by him being very near to the president he made many enemies, you guess who are those?!
 
DrWHO

But you havent stated on why we had to ditch Socialism for free market economy! for your information we were not a lot of third world countries tried socialism (or something they called socialism) in the 1960s and 1970s after independence. Three cases come to mind - India, Mexico, and (we)Tanzania, They didn't work out too well. For example India's economy was derided abroad as the "Permit Raj" and slugged along at the "Hindu rate of growth," until a series of liberal reforms started propelling India upwards in the 1980s and 1990s.While Mexico's "Institutional Revolutionary Party" started rolling back central institutions until, amid corruption allegations, they got shown the door in a genuinely free election by Vincente Fox, who offered more radical liberalization.And for us Tanzanians we attempted a pretty genuine system of planning and protectionism until the 1980s, when the ruling party said rather bluntly "This isn't working" and started on a program of liberalization and this was said by none but JK NYERERE

Umerukia gari hujui linakokwenda issue ilitolewa na maswali aliulizwa jokaKuu, ni vizuri uangalie previous postings sina haja ya kuanza kukuelezea why socialism was ditched its off topic , kama unataka fungua thread ya hilo utapata majibu.
 
DrWHO

Haya tena naona unaendelea kuTWIST mambo humu

wapi nilijitambulisha kama Mzanzibari? au Mtu wa visiwani

vipi?

Sikusema umetoka Zanzibar bali nafikiri ni Zanzibar pekee ndio mlikuwa manaomba ruhusa kwa DC na RC's kwenda sehemu nyingine sio Bara ….. KUTOKANA NA MFANO WAKO NA EXPERIENCE YA ABEID KARUME. Inawezekana kabisa ulikaa kule wakati ule I don't know. And anyway what is wrong if you are from there?
 
jokaKuu

Dua,
Naona maswali yao umeyatoa kwa hamaki, na hivyo basi hakuna haja ya mimi kuyajibu moja baada ya jingine. pamoja na hayo, jinsi tunavyoendelea kuzungumza taratibu maswali yako yatapata majibu.

Dua,
kuhusu UPEO nimekuletea makala ina-quote watu waliofanya kazi na sokoine. nadhani umejionea kwamba alikuwa mtu wa mtulinga, asiyefanya tafakuri ya kina kabla hajatoa uamuzi………………………….

Ulikataa kujibu maswali halafu unaanza kododosa nikueleweje?

Kuhusu upeo una uhakika gani kwamba mimi sikufanya kazi na Sokoine?
artical uliyoweka nimekujibu inamweleza Edward Richmonduli sio Edward Sokoine jaribu kusoma halafu jibu maswali rasmi kama ulivyopewa kama unataka au tafuta mtu aje akujibie bila kupoteza muda. Andika mambo ambayo unauhakika nayo sio vinginevyo.
Umeulizwa tangu mwanzo tueleze nani alikuwa PM zaidi kuliko wote na nafikiri Mzee Es alikutajia majina ya wote mbona hujajibu suala hili? Sina sababu ya kurudia rudia mzee Observer na Mzee Mkandara hapo juu wamefafanua vizuri maswali yako.
 
Mzee IO,

Strong uchambuzi, tuko kwenye nchi inyoendeshwa na political system ambayo si perfect na haijawahi kuwa, but in the process tumeshawahi kuwa ni viongozi waelewa angalau kidogo, na katika historia yetu toka tupate uhuru kuacha Mwalimu, Sokoine stands the best,

Mzee Joka,

anayo point moja muhimu, kwamba idea za Mwalimu kuhusu uchumi hazikuwa safi, hilo halina ubishi, ila tu tatizo ni kwamba ni kwa nini since then viongozi wote waliofuatia wameshindwa kurekebisha hilo? Badala yake mpaka leo bado tunamlaumu Mwalimu tu? Tunawezaje kuwa wazuri wa kuona ya zamani na tunashidnwa kurekebisha ya sasa? Mkapa alijaribu na alijitahidi kwenye hili la uchumi, lakini kabla hajaenda mbali yakaanza majungu kutoka kwa wale walioanza kukosa kula kutokana na njia mpya za uchumi zilizoanza kuwekwa na wataalamu, kina huyu mama wa World Bank aliyeolewa na Gavana wa BOT, yaani wakamzushia mpaka kwamba ati ni hawara wa Mkapa, ikabidi Mama Anna aje juu na mama akaondoka, na jama awengine wote waliokuwa wameazimwa toka nje ikabidi waanze kutimka, the next thing Kigoda na kundi lake wakachukua mkanda, matokeo yake tumerudi pale pale, tena na zaidi maana sasa hata umeme hatuna lakini enzi za Mwalimu hatukuwahi kuwa na shida ya umeme.

Mambo ya nguvu kazi hayakuwa ya Sokoine, yalikuwa ni ya chama cha Mapinduzi, CCM collectivelly, kama ni wananchi kuhamishwa kwa nguvu hiyo ilikuwa ni katika miaka ya sabini, kulikuwa na matatizo yake, lakini pia kulikuwa na faida zake, Mwalimu alishindwa kwa sababu hakuwa tayari kuuuwa wananchi wabishi kama Mao, alivyoua millions ili siasa yake ifanikiwe kule China. Na hili nimelisema mara nyingi kuwa moja ya mafanikio ya Mwalimu ni Vijiji vya ujamaaa, kwa sababu leo wabongo wote tuna addresss, ukimtafuta mwananchi bongo utampta tu maana utaambiwa yuko kijiji fulani, kuna tatizo moja kubwa na watu kama kina Joka kuuu na mtizamo wao wakumlaumu Mwalimu, huwa hawasemi alternative, na hawasemi vizuri ni kwa nini waliopo sasa wanashindwa kurekebisha makosa ya Mwalimu, yaani angalau kidogo, lakini bado ninatoa heshima kwa Mzee Joka Kuu, kwa kuendesha mjadala huu bila jazba wala kutoka nje ya mstari, Bravo Mzee Joka Kuuu,


Sasa with all that said, ni kwamba binadamu unakuwa fraud pale unapofikia mahali ukapigwa marufuku kushiriki katika mijadala ya forum au society, na hayo niliwahi kuyaona kijijini kwetu huko Msanga, mzee mkorofi siku zote alikuwa akifukuzwa kwenye vikao vya kijiji, sasa binadamu ukiona umefikia hatua ya kuwa banned kwenye vikao vya society kamahii forum, basi wewe hakuna matumaini tena, the next step ni jela tu au kuwasaidia wananchi wote kwenye hiyo society au forum, kwa kufa mwenyewe.

Tarehe yangu ya mwisho hapa nimesema ni tarehe 31/12/2006, sasa kwa mtu kama wewe ambaye kuwepo kwangu hapa ni tatizo kwenu, iliyobaki ni kula chupa, maana mimi ni kumkoma nyani mpaka siku ya mwisho.

Botswana na South Africa, hazijawahi kuwa na viongozi wasaniii au mabomu toka zipate uhuru, maana ama sivyo nazo tungezisikia kuwa hazina umeme kama sisi, na sisi wabongo tusingekuwa tunakimbilia huko kutafuta ajira kila siku, ni kwamba simply put hizo nchi zina viongozi bomba na sio manabiii wa Mungu kama kwetu,

Halafu hii point ya Malecela, aliporudi UK alikuwa akiongea sana na viongozi wa UK kwa simu na usalama walikuwa wamkislikiliza, kwa hiyo Mwalimu akaona kuwa atauza nji, what a joke? Sasa hawa waliouza nchi yetu kwa kuibinfsisha na huko kwa Richmond, walikuwa wakiongea na nani kwenye simu au hawakuongea na watu nje kabisaaaa, hebu waulize hao jamaaaa wa usalama waliokupa hizi data, damn! ama kweli bongo kuna data! Kwa hiyo ina maana hawa viongozi wasaniii tulionao Mwalimu aliwaamini kwa sababu hawakuongea na simu za nje na kusikilizwa na usalama?

Unajua kuna mzee mmoja wa hii forum, wakati ule wa uchaguzi bongo kule BCS, jamaaa alisema Mungai angekuwa waziri mkuu na tayari ameshapewa walinzi bado kutangazwa tu maana yeye ameshapata data toka usalama, nakumbuka huyu mzee alimjibu kuwa hizi data zingine sometimes ni za nchi za jirani lakini usalama wetu wanazichanganya na za bongo!
 
DrWHO



Sikusema umetoka Zanzibar bali nafikiri ni Zanzibar pekee ndio mlikuwa manaomba ruhusa kwa DC na RC’s kwenda sehemu nyingine sio Bara ….. KUTOKANA NA MFANO WAKO NA EXPERIENCE YA ABEID KARUME. Inawezekana kabisa ulikaa kule wakati ule I don’t know. And anyway what is wrong if you are from there?



really? unless mko mapacha humu lakini wewe huyo huyo ulisema hivi:

DrWHO

Nafikiri ni Zanzibar pekee ndio mlikuwa mnaomba ruhusa kwa DC na RC's kwenda sehemu nyingine sio Bara. Jaribu kuuliza wana bodi mimi sikuliona hilo. Kwa hiyo hizo ndio zilikuwa dark ages zenu kule visiwani.



au ulighafilika kidogo mzee?
 
ES

hebu chill kwanza mzee
duh!!!

yaani tumefikia huku? juu ya nini haswa? mbona kuna mengi tuu yanayozungumzwa? je uliwahi kusikia kuwa secretary wa Mwalimu yule mama mzungu kuna watu walikuwa wanasema alikuwa CIA?

Sasa tukizisikiliza na kuhamaki kwa kila kitu tutafika?
 
haya wewe wa MSANGA ipi kwa sababu itabidi tujuane kidogo mwinyi,sie kwetu kule mbele kidogo kunaitwa KIBUTA si mbali sana na MASAKI

aa kweli dunia ndogo
 
DrWHO

Huo mfano wa karume una maana gani? karume alikuwa anatawala Bara?
 
DrWHO

Basi bwana kama hilo lilikuwa nje ya mstari, leo ni mkesha wa christmas enjoy the season.
 
Back
Top Bottom