Nyerere alisingiziwa mengi sana

Nyerere alisingiziwa mengi sana

1) unajua maana ya 'kusingiziwa' wewe?

2) nyerere anasingiziwa na nani kuwa kapigania uhuru wa tanganyika?

3) neno 'kupigania' halina maana moja kama unavyotaka kuaminisha watu humu.

Hivyo, kupigania uhuru haimaanishi kuwa watu waliingia msituni na kuanza kupigana kwa mapanga na bunduki.

Haya lete namba mbili.
kupigania ni kushika jambia na milipuko
 
Ungekuwa wewe ndiyo mtia maradhi saa hizi mimi ni taabani lakini bahati mbaya sana kwako, huna uwezo huo.
Ni kweli mimi sina uwezo huo. Nasijasema nina uwezo huo.
Ninahakika CHUKI zina uwezo huo ndio maana kwa upendo wangu ..NAKUONYA ...ukome kueneza CHUKI kwenye jamii vinginevyo hakika chuki itakujengea maradhi ..ambayo yatakutesa .. na utajuta. Nasema tena usinibishie.
 
11. Wanasema kuwa alikuwa mkabila ndio maana idadi kubwa jeshini na polisi ilikuwa ni wakurya, si kweli ndio maana neno "arro" linaonekana ni la kipolisi.

misikiti ya akina Faiza wanajua Nyerere ni mkurya na ana nyumba Kitunda! Kumbe Mzanaki
 
We utakua umebeba mimba kichwani badala ya tumboni.
 
Nyerere hakupenda wasomi wazalendo na pia aliwanyima fursa watz kujua mambo ya dunia

Miaka 30 toka atoke madarakani walimu hawatoshi mashuleni. Ulitaka ajenge majengo bila walimu?
Kujua mambo ya dunia ni kusoma na kujifunza, ukisema TV fikiria na hili takribani 13% ndiyo wanapata umeme nchi nzima nusu yake ndiyo wanatazama tv
 
Bora hata Nyerere ambaye miaka 30+ baada ya kutoka madarakani ndio anatuhumiwa kuiba bila hata ushahidi kuliko wanaoiba na kujulikana pamoja na ushahidi ulio wazi wakiwa madarakani bado.
Ni kweli isiyopingika kuwa Mwalimu alijenga taasisi imara (ccm) kitu ambacho kimesaidia hata watu dhaifu waweze kuingia madarakani ilimradi tu wamejipenyeza kwenye hiyo taasisi!


Kwa sababu bwana Mtei katika maandiko yake ameelezea jinsi hata picha na dhahabu aliyopewa ilivyounguwa mpaka kugeuka jivu.

The point is, uchunguzi upi uliofanyika? jee na zile strong room pia ziliyeyuka na kuunguza kila kitu.

Kama wewe unajuwa kuwa kuna pesa zilisalimika inabidi uelezee hilo, mimi baada ya kumsoma Mtei kuwa kila kitu kiligeuka jivu, ni dhahiri humo ndani hakuna kilichobaki.

Nimeelezea juu huko labda hukunisoma, ikiwa leo akaunti moja tu ya benki hiyohiyo zimetolewa fedha mtu aliyelipwa fedha zake kwa kutoa huduma uchunguzi unaendelea hadi hii leo, kumbuka huyo huyo anendelea kutowa huduma na analipwa. Leo iweje benki nzima iunguwe na hatujuwi uchunguzi uliofanyika? au wewe unajuwa?
 
FaizaFoxy bado tunazisoma uzi zako ambazo huwa unashadadia hiki harafu kinafanya kinyume chake, hivi huna aibu hata kidogo. Tibaijuka hawezi kufukuzwa, kafukuzwa, Muhongo hawezi kufukuzwa kafukuzwa, ESCROW ni hela za mtu binafsi, kumbe za UMMA hadi watu wanafiukuzwa, Katiba kura ya Maoni iko pale pale 30 April, imepita, CCM eti ni chama kubwa Mgombea uraisi atajulikana miezi 6 kabla ya Uchaguzi, sasa imebaki 4 hakuna kitu. Sasa umekuja na uzi wako kwa kijinga kama zile zilizopitaaaa, subiri utapata majibu unayostahili.

ndoa za mitala ni shida sana kwa huyu bibie, umesahau uzi wake wenye heading, "wana chadema hamna hoja, niko hapa kujibu hoja zenu"
 
Nisome vizuri hiyo point, punguza hasira.

Nimeandika kama si Nyerere basi ni Mtei na hili la Mtei tulitazame vizuri, Nyerere hakuna mali ayoacha kama tujuavyo, Mtei Jee? kama mtumishi wa umma wa enzi hizo mali kazitowa wapi?

unataka kweli Mzee Edwin Mtei akujibu naye kakuona kinyago cha mpapule.
 
Wewe mzenji tuanajua kwanini unamchukia Nyerere.
Kwa vile umeaminishwa na Mo'Said na mwenzake Ghassany kuwa Nyerere alimsaidia Karume kuchinja waarabu koko wa kule zenji.

Ila ujue kuwa Serikali ya Zanzibar ilitangulia kufanya utaifishaji mwaka 1964-65, wakati huku bara utaifishaji ulifanywa kuanzia 1967.
Pande zote mbili, utaifishaji ulifanywa na serikali na sio na Nyerere au Karume kama watu binafsi.

hapa mada ni nyerere , ukitaka dhambi za wengine fungua uzi mwengine tutachangia
 
majumba mengi na taasisi zilibinafsishwa na serekali je ni jumba gani alijimilikisha nyerere hata taasisi za kikatoliki ameziweka serekalini kwa faida ya mleta mada na enzake

ni kuwatia umasikini watu basi sio kwa ajili ya umma
 
Ooh, vyema kabisa, kwa hiyo Nyerere hakusingiziwa Udaktari, ni kweli kabisa ni Daktari na umedhihirisa hilo bila ya shaka yoyote. Ukweli kabisa nimeridhika na data ulizoshusha na Nyerere alipewa u Daktari wa heshima na ndiyo maana ni Dr. Nyerere.

Ajabu ni pale watu wanapokejeli u Daktari wa Kikwete. Hauoni kuwa ni "double standard" wakati wote wametunukiwa u Daktari wa heshima?

Upo hapo ulipo?

unataka kulinganisha I.Q ya Kikwete na Nyerere? Ni kama kichuguu na Kilimanjaro
 
Back
Top Bottom