Nyerere alisingiziwa mengi sana

Nyerere alisingiziwa mengi sana

1) Unajua maana ya 'kusingiziwa' wewe?

2) Nyerere anasingiziwa na nani kuwa kapigania uhuru wa Tanganyika?

3) Neno 'kupigania' halina maana moja kama unavyotaka kuaminisha watu humu.

Hivyo, kupigania uhuru haimaanishi kuwa watu waliingia msituni na kuanza kupigana kwa mapanga na bunduki.

Haya lete namba mbili.

Usiwe na kiherehere, namba mbili tutaenda tu tartiiibu, naona hujajibu umeuliza, kwa kuwa nimetoka kulijibu swali hilo sasa hivi ngoja nikubandikie na wewe, llinakidhi kuwa jibu la maswali yako pia:

Kwanini iwe kapigania? kwanini isiwe kajitahidi sana kadai Uhuru kisiasa na kwa amani na kidiplomasia na kuweza kwa jitihada hizo katupatia Uhuru bila kupigania.

Unajuwa dhanna ya "kupigania Uhuru" anayosingiziwa Nyerere ndiyo inatumika sasa Tanzania hii na watu fulani ambao mpaka huo "upiganaji" ndiyo imekuwa kauli yao ya kawaida na pengine ni sera yao. Wanadai wanataka kuikomboa Tanzania, sasa sijuwi wanataka kuikomboa kutoka kwa nani? na wanachokipigania ni nini? na mpaka wamefikia kusema "nchi haitotawalika". Sasa hiyo ni siasa kweli? au kutishana (terrorism)?

Mpaka wanafikia kuitana wapiganaji, jee huoni kuwa hii "brain washing" ina madhara na si kutengeneza?

Fikiri vizuri na usiwe biased kwa kutaka kufundisha lugha kuwa eti upiganaji si lazima umwage damu au ukunjiane ngumi. Na ethics zipi tunazozifundisha kwa kuacha kutumia sifa kamili ya Nyerere kudai uhuru kisiasa na kwa amani na kuita kuwa "kapigania Uhuru".

Huko ni kumsingizia kubaya sana na kwa kuwa imezoweleka sasa wanatokea wanasiasa na sera za "upiganaji" na bado hatuioni athari yake.

Tafadhali tumpe Nyerere sifa anayostahili na tusimsingizie kwa matakwa yetu tu. Yeye mwenyewe sikumsikia hata mara akisema kuwa "tulipigania Uhuru", bali nimemsikia mara nyingi akisema "tulidai Uhuru".

Nimeeleza juu huko kuwa wapo wa kabla ya Nyerere waliopigania Uhuru na kumwaga damu zao na wengine kuhukumiwa kifo na Wajerumani na kuuliwa kwa kupigania Uhuru, hao tuwaandike kwa wino wa dhahabu na ni kweli walipigania Uhuru ingawa hawakufanikiwa lakini walipigania.

Nyerere kadai Uhuru kisiasa na kafanikiwa bila kukunja mgumi wala kumwaga damu, kwanini na yeye tusimwandike hivyo kwa wino wa dhahabu na tumtie hila ya kumsingizia kwa ambalo hajalifanya? Fikiri.
 
Nyani Ngabu kwa kuwa umetaka namba mbili, hii hapa:

2) Nyerere anasingiziwa kuwa kaasisi TANU.

Si kweli, Nyerere hakuasisi TANU wala hajatowa jina la TANU.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli kuwa Nyerere alikuwa mtu wa kwanza kupata digrii ya Master of Arts digrii kutoka huko Scotland. Wasomi wote wa wakati huo waliokuwa wamesoma Makerere tu hawakuwa na digrii kwa vile Makerere ilikuwa inatoa diploma tu. Diploma za Makerere zilianza kutumaka kama kigezo cha kupatia digrii huko University of London mwaka 1963, yaani baadaye sana.

KIBASILA alikuwa chifu wa wazaramo, ila kuna "Dr" Kibasila aliyekuwa na diploma ya Uganga aliyopata Makerere mwaka 1958 baada ya Nyerere kuwa alishapata hiyo Masters yake. "Dr" Kibasila hakuwa na digrii hata ya bachelor

SEWA HAJI PAROO alikuwa mfanya biashara wa kiarabu na wala hakuwa Daktari. Wodi la Sewa Haji hapo Muhimbiri ni kumbukumbu tu kuwa alianzisha hospatali hiyo ya kusaidia maskini wakati huo wa utawala wa mjerumani lakini hakuwa tabibu na wala hakuwa na digrii.

MUHIMBILI: Sina uhakika na jina hilo ila kwa vyovyote hata kama alikuwa Daktari, basi hakuwa na digrii. Madaktari maarafu wa kwanza kama vile DR MWAISELA, DR Mutahangarwa, Dr Vedastaus Kyaruzi, Dr Luciana Tsere hawakuwa na digrii bali walikuwa na diploma za uganga (Assistant Medical Officer- AMO) walizopata Makerere. Mtanganyika wa kwanza kupata diploma hiyo ya Uganga (AMO) kutoka Makerere alikuwa DR Mutahangarwa aliyopata mwaka 1942.

Ahsante sana nimekubali na nimeridhika na majibu yako lakini haujamalizia namba 4 ilipoanzia hayo hayo ya namba tano.

Tuchambulie na hilo tafadhali.
 
Usiwe na kiherehere, namba mbili tutaenda tu tartiiibu, naona hujajibu umeuliza, kwa kuwa nimetoka kulijibu swali hilo sasa hivi ngoja nikubandikie na wewe, llinakidhi kuwa jibu la maswali yako pia:

Haya, ngoja tuone kama jibu lako linakidhi maswali yangu.

Kwanini iwe kapigania? kwanini isiwe kajitahidi sana kadai Uhuru kisiasa na kwa amani na kidiplomasia na kuweza kwa jitihada hizo katupatia Uhuru bila kupigania.

Naona umeamua kucheza mchezo wa semantiki tu.

Unajuwa dhanna ya "kupigania Uhuru" anayosingiziwa Nyerere ndiyo inatumika sasa Tanzania hii na watu fulani ambao mpaka huo "upiganaji" ndiyo imekuwa kauli yao ya kawaida na pengine ni sera yao. Wanadai wanataka kuikomboa Tanzania, sasa sijuwi wanataka kuikomboa kutoka kwa nani? na wanachokipigania ni nini? na mpaka wamefikia kusema "nchi haitotawalika". Sasa hiyo ni siasa kweli? au kutishana (terrorism)?

"Wanachokipigania"? Umetoka kukataa kuwa Nyerere hakupigania uhuru halafu wakati huo huo unauliza hao watu fulani "wanachokipigania" ni nini? Kwani kuna watu wako vitani wanapigana?

Mpaka wanafikia kuitana wapiganaji, jee huoni kuwa hii "brain washing" ina madhara na si kutengeneza?

Hakuna brainwashing yoyote hapo.

Fikiri vizuri na usiwe biased kwa kutaka kufundisha lugha kuwa eti upiganaji si lazima umwage damu au ukunjiane ngumi. Na ethics zipi tunazozifundisha kwa kuacha kutumia sifa kamili ya Nyerere kudai uhuru kisiasa na kwa amani na kuita kuwa "kapigania Uhuru".

Maneno huwa na maana zaidi ya moja. Na kupigania kitu si lazima upigane mangumi, mateke, na mapanga. Mtu unaweza ukapigania jambo kwa hali.

Huko ni kumsingizia kubaya sana na kwa kuwa imezoweleka sasa wanatokea wanasiasa na sera za "upiganaji" na bado hatuioni athari yake.

Hapana. Unachofanya wewe ni kulazimisha mambo kwa kujaribu kucheza cheza na maana za maneno.

Tafadhali tumpe Nyerere sifa anayostahili na tusimsingizie kwa matakwa yetu tu. Yeye mwenyewe sikumsikia hata mara akisema kuwa "tulipigania Uhuru", bali nimemsikia mara nyingi akisema "tulidai Uhuru".

Vipi nawe ukianza kumpa heshima yake anayostahili kuliko kuja mada za kutaka kumchafua mzee wa watu?

Nimeeleza juu huko kuwa wapo wa kabla ya Nyerere waliopigania Uhuru na kumwaga damu zao na wengine kuhukumiwa kifo na Wajerumani na kuuliwa kwa kupigania Uhuru, hao tuwaandike kwa wino wa dhahabu na ni kweli walipigania Uhuru ingawa hawakufanikiwa lakini walipigania.

Uhuru ulipiganiwa kwa namna na njia tofauti.

Nyerere kadai Uhuru kisiasa na kafanikiwa bila kukunja mgumi wala kumwaga damu, kwanini na yeye tusimwandike hivyo kwa wino wa dhahabu na tumtie hila ya kumsingizia kwa ambalo hajalifanya? Fikiri.

Sioni tofauti ya kudai na kupigania katika muktadha wa kupata uhuru.
 
Unaona jinsi Watanzania tunavyokosa mantiki.

Hapa tunachotaka si maswali, kama unayajuwa elezea, ilikuwa hivi na hivi na hivi.

Soma vizuri, hayo ni "kusingiziwa", yanaweza kuwa yote anasingiziwa na si ukweli.

Kama unaujuwa ukweli kuhusu point yooyote katika hayo saba utuelezee.

Wewe naona unajitafutia maradhi sugu.. kwa kujichosha kujenga chuki na kuchochea jamii hadi kujawa na chuki kuu ..inayobeba msururu wa magonjwa. tena usinibishie kuwa hutaugua ukiendelea na huu uhayawani wako.. . tubu jirudi .. uzima sio lelemama. Hakika utaugua na kujuta.
 
Mkuu naona umepanga hoja zako vizuri, sasa tusaidie please weka nodo kwa kueleza in details unayo yafahamu maanake mpangilio huu si bure, utakuwa umeufanyia utafiti siku nyingi tu - tusaidie FAIZA kututoa matongo tongo machoni - watu wana kiu ya kujua mengi kuhusu Ndugu yetu huyu ambayo yalikuwa yamefungiwa kwenye closet.
 
Neno kusingiziwa hapa halikutumika kwa maana halisi. mtu hasingiziwi kufanya mazuri bali yasiyostahili mfono wizi, uuaji, ubakaji n.k. Wenye uelewa wa kiswahili watanisaidia hapa kama nakosea.
Nikirudi kwenye hoja yako ni kama unataka ku - "reverse" historia kwa kupachika mawazo binafsi yasiyo ya kitafiti.Yaliyotokea duniani wakati wa mwalimu yameandikwa na kurekodiwa si na Watanganyika au Watanzania pekee bali na watu wengi dunia nzima. Dunia inamtambua pia kama mwanafalsafa. Kielimu pia ameingia katika historia kwa falsafa yake ya "elimu ya kujitegemea".
Ikiwa Wote hawa walimsingizia basi ilikuwa dunia isiyo na macho na ni ajabu! Basi haya uliyosema ni sawa na kutaka kuuangusha mbuyu kwa kujaribu kuupiga teke!
 
Huyu black widow ni mchimvi sana, anampenda Osama bin laden na Mohammed emmwazi ,kuweni nae makini sana
 
7) Nyerere anasingiziwa kuwa hajaiba,

Si kweli, BOT kabla ya Nyerere kung'atuka iliwaka moto na hakuna senti moja iliyobakia, ni nani alichukuwa? ni nani alichunguza?
Bora hata Nyerere ambaye miaka 30+ baada ya kutoka madarakani ndio anatuhumiwa kuiba bila hata ushahidi kuliko wanaoiba na kujulikana pamoja na ushahidi ulio wazi wakiwa madarakani bado.
Ni kweli isiyopingika kuwa Mwalimu alijenga taasisi imara (ccm) kitu ambacho kimesaidia hata watu dhaifu waweze kuingia madarakani ilimradi tu wamejipenyeza kwenye hiyo taasisi!

 
Ni nini ambacho hukubaliani nacho kuwa kasingiziwa au hajasingiziwa? sikuelewi.

Tuanza na namba moja, nieleze ni nini usichokubaliana nacho:

1) Nyerere anasingiziwa kuwa kapigania Uhuru wa Tanganyika.

Si kweli, Nyerere hakupigania "Uhuru wa Tanganyika". Vita gani alivyopigana kudai Uhuru kama "Kapigania Uhuru"?
mara ngapi tunasikia KAPIGANA SANA MPAKA KUIPATA MALI, huwa kuna vita yoyote imefanyika.
 
Tundu lissu wakati wa kikao cha bunge la katiba alieleza sana kuhusu nyerere, kuna mpaka mashehe walilia eti anakashifiwa baba wa taifa. Mfano mdogo tu ni waraka wa muungano, lakini watu ukieleza upande mwengine wa shilingi kumhusu nyerere wamakuwa wakali kweli daaah, wakuu alikuwa binaadamu wa kawaida hakuwa mungu nae ana makosa kibao

Nchi hii siku wakiamua kumsahau nyerere basi ndio itaanza safari ya kweli ya maendeleo.
Sasa bado watu wengi na wana siasa wana fikra zile zidumu milele .
Mpaka masalia yote yaindoke akili ndio tutanza kupiga hatua. Bila hivo tutaona jirani zetu wakituacha mbali sanaaaa
 
Chuki chuki chuki till death.
Mwalimu Nyerere atabaki kuwa legend wetu, atabaki kuwa kipenzi chetu, historia imeandikwa hata utembee uchi kila mlango wa Nyumba kueneza chuki uwezi tena maana historia imendikwa kwa electronic ink.

Ni upumbavu uliokithiri kuangaika na Marehemu, Nyerere alifanya aliyoweza, wewe jiulize umeifanyia nini nchi hii zaidi ya kukaa siku nzima JF bila kazi na kueneza chuki?, anyway, an idle mind is the house of devil, ufanyi kazi, unatia umasikini nchi hii, kwa miaka kadhaa sasa umekuwa ukishinda kwenye Jamii Forum without producing
 
Nchi hii siku wakiamua kumsahau nyerere basi ndio itaanza safari ya kweli ya maendeleo.
Sasa bado watu wengi na wana siasa wana fikra zile zidumu milele .
Mpaka masalia yote yaindoke akili ndio tutanza kupiga hatua. Bila hivo tutaona jirani zetu wakituacha mbali sanaaaa

support ushoga uone kama huwaachi mbali majirani zako...
 
Hii mtu ilikuwa dictator na ilikuwa wizi za naiba jumba ya indian community halafu naandika msajili,yeye ndiyo nafundisha tanzanians namna ya iba sasa nchi zima wizi,naiba hata finiko ya choo barabarani halafu napikia watoto yao transformer oil.
 
Nchi hii siku wakiamua kumsahau nyerere basi ndio itaanza safari ya kweli ya maendeleo.
Sasa bado watu wengi na wana siasa wana fikra zile zidumu milele .
Mpaka masalia yote yaindoke akili ndio tutanza kupiga hatua. Bila hivo tutaona jirani zetu wakituacha mbali sanaaaa

Mkuu niko tofauti na wewe. Nchi zote duniani huwa hazisahau viongozi au binadamu yeyote aliefanya mazuri, kupitia role models hao ndio mwanzo wa Mendeleo, mfano China Wana Mao, India wana Mahatma Gandhi, Marekani wana akina Abraham Lincoln, SA wana Mandela nk. Hili tusonge mbele ni lazima tuenzi mazuri ya Nyerere. Unaposema tumsahau Nyerere maana yake unasema Tuwe wadini, Tuwe Wakabila, Tuwe na Utanganyika/Uzanzibar nk. Moja ya madhara ya kusahau usia wa Nyerere ni pamoja na Ufisadi tunaouona leo kupitia akina Chenge
 
= hubadilika

Hilo la "kupigania maisha yake" mimi kwa Kiswahili sijawahi kulisikia.

Kwanini iwe kapigania? kwanini isiwe kadai Uhuru kisiasa na kwa amani na kidiplomasia na kuweza kutupatia Uhuru bila kupigania.

Unajuwa dhanna ya "kupigania Uhuru" anayosingiziwa Nyerere ndiyo inatumika sasa Tanzania hii na watu fulani ambao mpaka huo "upiganaji" ndiyo imekuwa kauli yao ya kawaida na pengine ni sera yao. Wanadai wanataka kuikomboa Tanzania, sasa sijuwi wanataka kuikomboa kutoka kwa nani? na wanachokipigania ni nini? na mpaka wamefikia kusema "nchi haitotawalika". Sasa hiyo ni siasa kweli? au kutishana (terrorism)?

Mpaka waanafikia kuitana wapiganaji, jee huoni kuwa hii "brain washing" ina madhara na si kutengeneza?

Fikiri vizuri na usiwe biased kwa kutaka kufundisha lugha kuwa eti upiganaji si lazima umwage damu au ukunjiane ngumi. Na ethics zipi tunazozifundisha kwa kuacha kutumia sifa kamili ya Nyerere kudai uhuru kisiasa na kwa amani na kuita kuwa "kapigania Uhuru".

Huko ni kumsingizia kubaya sana na kwa kuwa imezoweleka sasa wanatokea wanasiasa na sera za "upiganaji" na bado hatuioni athari yake.

Tafadhali tumpe Nyerere sifa anayostahili na tusimsingizie kwa matakwa yetu tu. Yeye mwenyewe sikumsikia hata mara akisema kuwa "tulipigania Uhuru", bali nimemsikia mara nyingi akisema "tulidai Uhuru".

Nimeeleza juu huko kuwa wapo wa kabla ya Nyerere waliopigania Uhuru na kumwaga damu zao na wengine kuhukumiwa kifo na Wajerumani na kuuliwa kwa kupigania Uhuru, hao tuwaandike kwa wino wa dhahabu na ni kweli walipigania Uhuru ingawa hawakufanikiwa lakini walipigania.

Nyerere kadai Uhuru kisiasa na kafanikiwa bila kukunja mgumi wala kumwaga damu, kwanini na yeye tusimwandike hivyo kwa wino wa dhahabu na tumtie hila ya kumsingizia kwa ambalo hajalifanya? Fikiri.

mimi sijawahi kusoma shuleni wala popote kuhusu historia ya NYERERE katika uhuru...ikaishia tu NYERERE kapigania uhuru, bila kufafanua hiyo kwa amani na pasipo kumwaga damu.....sasa hicho kisingizio kinanitatanisha labda ufafanue zaidi...
 
Jee unalifahamu jumba la IPS ? Lipo kona ya Samora na Azikiwe linaangali sanamu ya askari pale round about.
Lile jumba lilijengwa na Akha Khan foundation na wakalifungua pamoja Nyerere na Agha khan . Sasa sijui ni uchoyo wivu ama wizi lakini Nyerere alili taifisha wiki ile ile.
Gazeti la Nation likiandika wizi huu uitwao kutaifisha liliandika heading kubwa DAYLIGHT ROBBERY BY NYERERE.
 
Jee unalifahamu jumba la IPS ? Lipo kona ya Samora na Azikiwe linaangali sanamu ya askari pale round about.
Lile jumba lilijengwa na Akha Khan foundation na wakalifungua pamoja Nyerere na Agha khan . Sasa sijui ni uchoyo wivu ama wizi lakini Nyerere alili taifisha wiki ile ile.
Gazeti la Nation likiandika wizi huu uitwao kutaifisha liliandika heading kubwa DAYLIGHT ROBBERY BY NYERERE.

kwahiyo unalalamika aliibia wahindi au?
 
Back
Top Bottom