Gambamala
JF-Expert Member
- May 13, 2014
- 1,045
- 766
Kweli alitaifisha shule za kanisa lakini hata za waislam nazo alizitaifisha.
Mm nahisi vijijini anachukiwa zaidi kuliko mjini hasa lililo mchukiza ni uhujumu uchumi.
Ukizingatia waislam wengi ni wajasiria mali kuliko kuajiriwa.
Na usiwaone kina mzee ilunga na ponda tu kila utwala wake unawatu wanauchukia leo tunao kina gwajima na mapadri wengi tu wanaohubiri chuki dhidi ya utawala halali wa ccm na kikwete.
Kuhusu ustawi wa kanisa hili halina shaka kuwa serikali ina msukumo mkubwa ktk ustawi huo leo serikali inatoa mabilion ya shg kwenda ktk kanisa na sijawahi kusikia Cag akikagua matumizi ya pesa hizo.
Kama mm mtu wa mtaani nitajuaje kama zinatumika kwa malengo yalio kusudiwa?
Nikisema pesa hizo zinajenga makanisa zina nunua magari ya mapdri zinasomesha wakiristo tu nk nitakuwa nimekosea?
Serikali kutoa mabilioni kwenda kwenye kanisa hilo halikwepeki. Hivi wewe ukijenga Hospitali zako halafu serikali ikasema inataka pia watu wake watibiwe kwenye hospitali hizo kwa bei nafuu, wewe utatoa bure?, je kama utasema Serikali nayo ichangie gharama utahitaji tena Serikali ijue unatumiaje/CAG?, kutumia si juu yako?. Mfano pale Muheza, kuna hospitali moja kubwa inaitwa Teule, hii ilijengwa na kanisa, lakini kama 85% ya wakazi wa Muheza ni Waislam, wanahudumiwa na hospitali hii, sasa kwanini serikali isitoe ruzuku watu wapate huduma.
Kuhusu Kikwete kuchukiwa na Mapadre sina uhakika sana maana asilimia kubwa ya Uzinduzi wa Project za Kanisa zimezinduliwa na Kikwete, sijui hiyo kama ndio definition ya kuchukiwa. Viongozi wa dini hawamchikii Kikwete bali bali wanamkosoa kwa Idea yake ya kugawa watu kwa dini zao kwa kuahidi Mahakama ya kadhi wakati akijua kuwa nchii hairuhusu dini kuingia kwenye katiba. Ukristo hauna chuki na mtu, ukikuta Mkristo ana chuki ujue ni shetani tu kamuingia maana Yesu anasema amri kuu kupita zote ni UPENDO