Ilikuwa kosa kubwa Mwl. Nyerere kuzingatia siasa za kikanda Tanganyika bila kuzifungamanisha na uchumi na bado nchi ikiwa changa

Ilikuwa kosa kubwa Mwl. Nyerere kuzingatia siasa za kikanda Tanganyika bila kuzifungamanisha na uchumi na bado nchi ikiwa changa

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
60,721
Reaction score
100,252
Katika mambo ambayo yameigharimu sana Tanganyika na kuidumaza huenda hata sio siasa ya ujamaa zaidi bali siasa za kikanda(geopolitics) za Nyerere ambazo hazikuzingatia maslahi ya uchumi wa Tanganyika wakati huo na ya muda mrefu.

Ukitafakari kwa kina katika fikra huru ni jinsi gani tulivyonufaika kama nchi kuzisaidia kwa jasho na damu nchi za SADCC kama South Africa, Namibia, Zimbabwe, Msumbiji na Angola kupata uhuru ni vigumu sana kupata jibu lolote lenye mashiko kuthibitisha kunufaika kwetu.

Muungano wa Jumuiya ya Africa Mashariki nao hakuwa na umuhimu wowote kabisa kiuchumi miaka ya 1960's kwa nchi zetu changa ambazo hazikuwa na bidhaa za kuuziana sisi kwa sisi. Nyerere alitakiwa kuzingatia zaidi Bilateral relationships kuliko Jumuiya za OAU, SADC na EAC.

Vita vya Uganda navyo huenda vingeweza kuepukika na kuepusha hasara kubwa ya kiuchumi kama Nyerere angempuuza Iddi Amin na kuwaacha Uganda wafanye siasa zao wenyewe wanavyojua wao.

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar nao ni kizungumkuti kikubwa mpaka leo ambapo dola ya TANU na CCM haijawahi kuwa na hoja za maana za kuonyesha Tanganyika inanufaikaje nao.

Kiujumla ukitazama wote Tanganyika tuliowasaidia katika harakati zao au kuungana nao walitupa au wana manufaa gani kwa Tanzania mpaka sasa hivi hakuna jibu kwa hakika.
 
Subiri uchumi wa nchi za SADC na EaC ukue ndio utaelewa ubora wa Mwalimu.ni upuuzi kusaka soko Marekani wakati una population ya kufa mtu imekuzunguka kila kona.
 
Subiri uchumi wa nchi za SADC na EaC ukue ndio utaelewa ubora wa Mwalimu.ni upuuzi kusaka soko Marekani wakati una population ya kufa mtu imekuzunguka kila kona.
Kwani bila SADC au EAC tusingeweza au hatuwezi kuuza na kununua kutoka Kenya, DRC, Zambia, Malawi na hizo nchi nyingine??
 
Katika mambo ambayo yameigharimu sana Tanganyika na kuidumaza huenda hata sio siasa ya ujamaa zaidi bali siasa za kikanda(geopolitics) za Nyerere ambazo hazikuzingatia maslahi ya uchumi wa Tanganyika wakati huo na ya muda mrefu.
Sera za siasa ya ujamaa hazikuwa na tija . Kwa mfano kuingiza siasa meneo ya kazi , huduma na uzalishaji.
M/kiti wa Chama wa Kiwanda X alikuwa na nguvu kuliko Meneja wake. Vivyo hivyo ktaika kila sekta
Ukitafakari kwa kina katika fikra ni jinsi gani tulivyonufaika kama nchi kuzisaidia kwa jasho na damu nchi za SADCC kama South Africa, Namibia, Zimbabwe, Msumbiji na Angola kupata uhuru ni vigumu sana kupata jibu lolote lenye mashiko kuthibitisha kunufaika kwetu.
Kuna tafsiri potofu kuhusu kusaidia nchi za SADC. Wakati wa ukombozi kulikuwa na vita baridi duniani. Nchi za SADC zilijifungamanisha na za kisoshalisti kama Urusi, China, Cuba n.k. Misaada ilitoka nchi hizo. Tanzania ilikuwa mwenyeji wa Wapigania Uhuru lakini si kwamba ilitoa kwenye uchumi

Mreno akiwa Msumbiji alisumbua sulinzi wa mikoa ya kusini. Kuondoka kwake kulikuwa nafuu ya gharama za ulinzi. Katika vita ya 1978 Msumbiji ilisaidia askari kule Kagera.
Kwa ufupi usiangalie kwa uchumi tu bali gharama na manufaa yasiyo onekana moja kwa moja katika uchumi

Muungano wa Jumuiya ya Africa Mashariki nao hakuwa na umuhimu wowote kabisa kiuchumi miaka ya 1960's kwa nchi zetu changa ambazo hazikuwa na bidhaa za kuuziana sisi kwa sisi. Nyerere alitakiwa kuzingatia zaidi Bilateral relationships kuliko Jumuiya za OAU, SADC na EAC.
Tulikuwa bora sana kama EAC kabla ya kuvunjika. EAC ilikuwa block kubwa kiuchumi ikinufaisha nchi zaote 3
Kuvunjika kwa Jumuiya 1977 Nchi zote zilipata hasara. Kwa waliokuwa katika EAC ya 1977 ni masikitiko kwanini ilivunjika. Tungekuwa mbali. Sioni sababu za kumlaumu Nyerere. Aliyeivunja ni Charles Njonjo na Kenyatta
Vita vya Uganda navyo huenda vingeweza kuepukika na kuepusha hasara kubwa ya kiuchumi kama Nyerere angempuuza Iddi Amin na kuwaacha Uganda wafanye siasa zao wenyewe wanavyojua.
Idd Amin alianza chokocho alipopindua akiitumia Tanzania kama kisingizio. Mwaka 1973 Amin alishambulia Tanzania kule Mwanza. Mzozo ulisuluhishwa na Mfalme Haile Selassie wa Ethiopia.
Mwaka 1978 Amin akavamia Kagera. Sijui kama ungekuwa Mwalimu Nyerere ungeacha kipande hicho kiondoke!
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar nao ni kizungumkti kikubwa mpaka leo ambapo dola ya TANU na CCM haijawahi kuwa na hoja za maana za kuonyesha Tanganyika inanufaikaje nao.
Hapa Nyerere aliboronga! Hakuna faida yoyote ya kuungana na Zanzibar ! In fact huu si muungano kwa maana ya muungano, ni mbeleko iliyobeba kaeneo bila kuwa na faida kwa Tanganyika.

JokaKuu
 
Hadi wimbo wa Taifa akachukua kutoka south Africa inaitwa Nkosi Sikelel' iAfrika


Cha kushangaza Zambia, south Africa wenyewe na Zimbabwe baada ya Uhuru walibadirisha maneno ya huo wimbo ila Tanzania chini ya Nyerere ulibaki vile vile Hadi Leo.


Zambia na Zimbabwe walifuta maneno yote ya huo wimbo na kuweka maneno kuhusu nchi zao ila walibakisha melody tu. Sisi Hadi Leo ubeti wa Kwanza TUNAIMBA MUNGU IBARIKI AFRICA kuliko hata kutaja nchi yetu kwanza.
 
Hadi wimbo wa Taifa akachukua kutoka south Africa inaitwa Nkosi Sikelel' iAfrika


Cha kushangaza Zambia, south Africa wenyewe na Zimbabwe baada ya Uhuru walibadirisha maneno ya huo wimbo ila Tanzania chini ya Nyerere ulibaki vile vile Hadi Leo.


Zambia na Zimbabwe walifuta maneno yote ya huo wimbo na kuweka maneno kuhusu nchi zao ila walibakisha melody tu. Sisi Hadi Leo ubeti wa Kwanza TUNAIMBA MUNGU IBARIKI AFRICA kuliko hata kutaja nchi yetu kwanza.
Tunajiona ndio wanamajumui wenyewe haswa.
 
Kwani bila SADC au EAC tusingeweza au hatuwezi kuuza na kununua kutoka Kenya, DRC, Zambia, Malawi na hizo nchi nyingine??
Labda ungejiuliza kwanza, kwanini Nchi za DRC, Rwanda na Burundi ikiwemo S.Sudan na Somalia zimepigana sana kuwa sehemu ya EAC?
 
Kuna tafsiri potofu kuhusu kusaidia nchi za SADC. Wakati wa ukombozi kulikuwa na vita baridi duniani. Nchi za SADC zilijifungamanisha na za kisoshalisti kama Urusi, China, Cuba n.k. Misaada ilitoka nchi hizo. Tanzania ilikuwa mwenyeji wa Wapigania Uhuru lakini si kwamba ilitoa kwenye uchumi

Mreno akiwa Msumbiji alisumbua sulinzi wa mikoa ya kusini. Kuondoka kwake kulikuwa nafuu ya gharama za ulinzi. Katika vita ya 1978 Msumbiji ilisaidia askari kule Kagera.
Kwa ufupi usiangalie kwa uchumi tu bali gharama na manufaa yasiyo onekana moja kwa moja katika uchumi


Tulikuwa bora sana kama EAC kabla ya kuvunjika. EAC ilikuwa block kubwa kiuchumi ikinufaisha nchi zaote 3
Kuvunjika kwa Jumuiya 1977 Nchi zote zilipata hasara. Kwa waliokuwa katika EAC ya 1977 ni masikitiko kwanini ilivunjika. Tungekuwa mbali. Sioni sababu za kumlaumu Nyerere. Aliyeivunja ni Charles Njonjo na Kenyatta

Idd Amin alianza chokocho alipopindua akiitumia Tanzania kama kisingizio. Mwaka 1973 Amin alishambulia Tanzania kule Mwanza. Mzozo ulisuluhishwa na Mfalme Haile Selassie wa Ethiopia.
Mwaka 1978 Amin akavamia Kagera. Sijui kama ungekuwa Mwalimu Nyerere ungeacha kipande hicho kiondoke!

Hapa Nyerere aliboronga! Hakuna faida yoyote ya kuungana na Zanzibar ! In fact huu si muungano kwa maana ya muungano, ni mbeleko iliyobeba kaeneo bila kuwa na faida kwa Tanganyika.

JokaKuu
Hasara ya kiuchumi nchi inaweza kuipata sio tu kwa kuwekeza pesa katika mambo yasiyo na tija kiuchumi kwake bali hata kutumia rasilimali watu na muda. Hata kama kweli hatukuwekeza pesa zetu kuzisaidia hizo nchi kupata uhuru lakini tulipoteza rasilimali watu na muda kuhangaika na mambo ambayo hayakuwa na faida kwetu badala ya kujikita kujiletea maendeleo yetu.

Kama Mreno alisumbua ulinzi mikoa ya Kusini ni kwa sababu alikuwa anajua Tanganyika ndio ilikuwa lango kuu la kuwasambua wao.

Nyerere angeweza kuepusha vita vya Uganda kama asingekuwa anasapoti wapinzani wa Iddi Amin na hata hao Msumbiji tusingewahitaji kuja kutusaidia hiyo vita kwa sababu isingetokea kwa kuanzia.

Unaweza kusema ni faida kiasi gani tuliipata katika EAC ya zamani wakati ambapo wote tulikuwa tunazalisha bidhaa za Kilimo zaidi kama kahawa, tumbaku, chai n.k kuuza Ulaya? Biashara gani hasa ya maana ilikuwa inafanyika katika EAC ya zamani kati ya nchi washirika?

Nakataa kabisa hoja ya kusema kama nchi hatupaswi kutanguliza maslahi ya uchumi wetu kwanza. Kitu cha kwanza katika mahusiano yetu inapaswa kuwa manufaa ya uchumi kisha mambo mengine ndio yafuate.
 
Sera za siasa ya ujamaa hazikuwa na tija . Kwa mfano kuingiza siasa meneo ya kazi , huduma na uzalishaji.
M/kiti wa Chama wa Kiwanda X alikuwa na nguvu kuliko Meneja wake. Vivyo hivyo ktaika kila sekta

Kuna tafsiri potofu kuhusu kusaidia nchi za SADC. Wakati wa ukombozi kulikuwa na vita baridi duniani. Nchi za SADC zilijifungamanisha na za kisoshalisti kama Urusi, China, Cuba n.k. Misaada ilitoka nchi hizo. Tanzania ilikuwa mwenyeji wa Wapigania Uhuru lakini si kwamba ilitoa kwenye uchumi

Mreno akiwa Msumbiji alisumbua sulinzi wa mikoa ya kusini. Kuondoka kwake kulikuwa nafuu ya gharama za ulinzi. Katika vita ya 1978 Msumbiji ilisaidia askari kule Kagera.
Kwa ufupi usiangalie kwa uchumi tu bali gharama na manufaa yasiyo onekana moja kwa moja katika uchumi


Tulikuwa bora sana kama EAC kabla ya kuvunjika. EAC ilikuwa block kubwa kiuchumi ikinufaisha nchi zaote 3
Kuvunjika kwa Jumuiya 1977 Nchi zote zilipata hasara. Kwa waliokuwa katika EAC ya 1977 ni masikitiko kwanini ilivunjika. Tungekuwa mbali. Sioni sababu za kumlaumu Nyerere. Aliyeivunja ni Charles Njonjo na Kenyatta

Idd Amin alianza chokocho alipopindua akiitumia Tanzania kama kisingizio. Mwaka 1973 Amin alishambulia Tanzania kule Mwanza. Mzozo ulisuluhishwa na Mfalme Haile Selassie wa Ethiopia.
Mwaka 1978 Amin akavamia Kagera. Sijui kama ungekuwa Mwalimu Nyerere ungeacha kipande hicho kiondoke!

Hapa Nyerere aliboronga! Hakuna faida yoyote ya kuungana na Zanzibar ! In fact huu si muungano kwa maana ya muungano, ni mbeleko iliyobeba kaeneo bila kuwa na faida kwa Tanganyika.

JokaKuu
GT vipi kuhusu Tanzania kuunga mkono Vita ya Biafra (1967 - 1970) kule Nigeria,kulikuwa na tishio gani Kwa Tanzania, Ukiweka mazingira kama ya Mpaka wa Msumbiji kipindi Cha Wareno.

Na,kabla ya matukio ya Idd Amin kufanya mashambulizi ya Kagera na Mwanza.Nini kilipelekea Mogadishu Accord ya mwaka 1971
 
Katika mambo ambayo yameigharimu sana Tanganyika na kuidumaza huenda hata sio siasa ya ujamaa zaidi bali siasa za kikanda(geopolitics) za Nyerere ambazo hazikuzingatia maslahi ya uchumi wa Tanganyika wakati huo na ya muda mrefu.

Ukitafakari kwa kina katika fikra ni jinsi gani tulivyonufaika kama nchi kuzisaidia kwa jasho na damu nchi za SADCC kama South Africa, Namibia, Zimbabwe, Msumbiji na Angola kupata uhuru ni vigumu sana kupata jibu lolote lenye mashiko kuthibitisha kunufaika kwetu.

Muungano wa Jumuiya ya Africa Mashariki nao hakuwa na umuhimu wowote kabisa kiuchumi miaka ya 1960's kwa nchi zetu changa ambazo hazikuwa na bidhaa za kuuziana sisi kwa sisi. Nyerere alitakiwa kuzingatia zaidi Bilateral relationships kuliko Jumuiya za OAU, SADC na EAC.

Vita vya Uganda navyo huenda vingeweza kuepukika na kuepusha hasara kubwa ya kiuchumi kama Nyerere angempuuza Iddi Amin na kuwaacha Uganda wafanye siasa zao wenyewe wanavyojua.

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar nao ni kizungumkti kikubwa mpaka leo ambapo dola ya TANU na CCM haijawahi kuwa na hoja za maana za kuonyesha Tanganyika inanufaikaje nao.

Kiujumla ukitazama wote Tanganyika tuliowasaidia katika harakati zao au kuungana nao walitupa au wana manufaa gani kwa Tanzania mpaka sasa hivi hakuna jibu kwa hakika.
Tusimlaumu Nyerere kuhusu Tanganyika kutotumia fursa. Nyerere alikuwa na mawazo ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia. Hakua mchumi na bahati mbaya hakuwa na mawazo ya kuongoza nchi kichumi. Alijitahidi kuunganisha watu kudai uhuru, hilo lilikuwa jambo jema, hata hivyo ilitakiwa mara tu baada ya uhuru aondolewe. Lile jaribio la kijeshi la kumwondoa kinguvu lilikuja muda mwafaka bahati mbaya likafeli, ndo maana tuko hovyo. Wazungu wakati wanaondoka waliacha wawekezaji kibao, kwa kutokujua akawatimua badala ya kuwawekea mazingira mazuri ya biashara. Leo tunatumia fedha na nguvu nyingi kuwatafuta. Madini alikuwa nayo badala ya kuyachimba na kuchukulia mabondi na mashare huko kwenye mabenki ya Dunia na mataasisi ya kifedha akawa anayaangalia tu eti watakuja kuchimba wajukuu wake. Wajukuu wenyewe wamewapa wazungu wayachimbe, wazungu wakichimba wanachukulia mashare na bondi huko kwenye duniani kwenye mataasisi ya kifedha, sisi wenye madini tunaenda kukopa hela zetu kwenye hayo mataasisi na kuwarudishia cha juu (riba) ambacho wachimba madini yetu wanatupa kama mrahaba wakiuza madini. Halafu tunatoka kama mazuzu tumefurahi kwamba nchi yetu ina madini wazungu wanatuonea wivu.
 
Hasara ya kiuchumi nchi inaweza kuipata sio tu kwa kuwekeza pesa katika mambo yasiyo na tija kiuchumi kwake bali hata rasilimali watu na muda. Hata kama kweli hatukuwekeza pesa zetu kuwasaidia hizo nchi kupata uhuru lakini tulipoteza rasilimali watu na muda kuhungaika na mambo ambayo hayakuwa na faida kwetu badala ya kujikita kujiletea maendeleo yetu.

Kama Mreno alisumbua ulinzi mikoa ya Kusini ni kwa sababu alikuwa anajua Tanganyika ndio ilikuwa lango kuu la kuwasambua wao.

Nyerere angeweza kuepusha vita vya Uganda kama asingekuwa anasapoti wapinzani wa Iddi Amin na hata hao Msumbiji tusingewahitaji kuja kutusaidia hiyo vita kwa sababu isingetokea kwa kuanzia.

Unaweza kusema ni faida kiasi gani tuliipata katika EAC ya zamani wakati ambapo wote tulikuwa tunazalisha bidhaa za Kilimo zaidi kama kahawa, tumbaku, chai n.k kuuza Ulaya? Biashara gani hasa ya maana ilikuwa inafanyika katika EAC ya zamani kati ya nchi washirika?

Nakataa kabisa hoja ya kusema kama nchi hatupaswi kutanguliza maslahi ya uchumi wetu kwanza. Kitu cha kwanza katika mahusiano yetu inapaswa kuwa manufaa ya uchumi kisha mambo mengine ndio yafuate.
Wataalamu wa historia waje watupe msaada,kabla ya Uganda chini ya Amin,kufanya mashambulizi Mwanza na Kagera ni matukio gani ya nyuma yalileta Hali hiyo ? Mimi sitaki kuamini kwamba Amin alikuwa mjinga wa kuanzisha vita bila sababu ya msingi.
 
Labda ungejiuliza kwanza, kwanini Nchi za DRC, Rwanda na Burundi ikiwemo S.Sudan na Somalia zimepigana sana kuwa sehemu ya EAC?
Kwa sababu ni nchi ndogo, au landlocked, zenye migogoro mikubwa ya kisiasa na pia nyingi bado hazina uongozi thabiti, inawezekana zinanufaika zaidi na na Jumuiya kuliko nchi kama Tanzania kama ingejielekeza kwenye bilateral relationships ambapo kila nchi tungeshirikiana nayo kwa terms binafsi na sio kwa umoja.
 
Kwa sababu ni nchi ndogo, au landlocked, zenye migogoro mikubwa ya kisiasa na pia nyingi bado hazina uongozi thabiti, inawezekana zinanufaika zaidi na na Jumuiya kuliko nchi kama Tanzania kama ingejielekeza kwenye bilateral relationships ambapo kila nchi tungeshirikiana nayo kwa terms binafsi na sio kwa umoja.
Unakubali kwamba Jumuiya ina faida! Tanzania haina eneo au population zaidi ya DRC yet unasema Rwanda na Burundi zilijiunga kwa udogo!

Tatizo la Tanzania ni kushindwa kutumia fursa za Jumuiya, si suala la kwenda ''solo''

Nitajie nchi moja tua barani Afrika iliyokwenda 'Solo' ikafanikiwa ili tuifanya kama model ya Tanzania
 
GT vipi kuhusu Tanzania kuunga mkono Vita ya Biafra (1967 - 1970) kule Nigeria,kulikuwa na tishio gani Kwa Tanzania, Ukiweka mazingira kama ya Mpaka wa Msumbiji kipindi Cha Wareno.

Na,kabla ya matukio ya Idd Amin kufanya mashambulizi ya Kagera na Mwanza.Nini kilipelekea Mogadishu Accord ya mwaka 1971
Vatican iliitambua Biafra kama nchi huru ikisukumwa zaidi na sababu za kibinadamu na mateso yaliyoambatana na vita hiyo kwa raia wa Biafra na Mwalimu akiwa muumini wa Vatican alifuata huo mkondo.

Kama Nyerere asingewapa hifadhi maadui wa Amin huenda Ile vita isingetokea.

Anyway... tuna ya kujifunza kwenye haya yote.
 
Katika mambo ambayo yameigharimu sana Tanganyika na kuidumaza huenda hata sio siasa ya ujamaa zaidi bali siasa za kikanda(geopolitics) za Nyerere ambazo hazikuzingatia maslahi ya uchumi wa Tanganyika wakati huo na ya muda mrefu.

Ukitafakari kwa kina katika fikra huru ni jinsi gani tulivyonufaika kama nchi kuzisaidia kwa jasho na damu nchi za SADCC kama South Africa, Namibia, Zimbabwe, Msumbiji na Angola kupata uhuru ni vigumu sana kupata jibu lolote lenye mashiko kuthibitisha kunufaika kwetu.

Muungano wa Jumuiya ya Africa Mashariki nao hakuwa na umuhimu wowote kabisa kiuchumi miaka ya 1960's kwa nchi zetu changa ambazo hazikuwa na bidhaa za kuuziana sisi kwa sisi. Nyerere alitakiwa kuzingatia zaidi Bilateral relationships kuliko Jumuiya za OAU, SADC na EAC.

Vita vya Uganda navyo huenda vingeweza kuepukika na kuepusha hasara kubwa ya kiuchumi kama Nyerere angempuuza Iddi Amin na kuwaacha Uganda wafanye siasa zao wenyewe wanavyojua wao.

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar nao ni kizungumkuti kikubwa mpaka leo ambapo dola ya TANU na CCM haijawahi kuwa na hoja za maana za kuonyesha Tanganyika inanufaikaje nao.

Kiujumla ukitazama wote Tanganyika tuliowasaidia katika harakati zao au kuungana nao walitupa au wana manufaa gani kwa Tanzania mpaka sasa hivi hakuna jibu kwa hakika.
Ni muda sasa Tanganyika urudi sasa tuachane na hizi ndoto za One Afrika ni siasa zimepitwa na wakati na hazina msaada wowote.
 
GT vipi kuhusu Tanzania kuunga mkono Vita ya Biafra (1967 - 1970) kule Nigeria,kulikuwa na tishio gani Kwa Tanzania, Ukiweka mazingira kama ya Mpaka wa Msumbiji kipindi Cha Wareno.
Msimamo wa Biafra ulitokana na siasa za nje (Foreign Diplomacy) ambayo ni sehemu ya uhai wa Taifa lolote
Ni sawa na Tanzania kuunga mkono Wapalestina au upunguzaji wa silaha za maangamizi (Disarmament)

Nguvu ya Tanzania zama hizo ilikuwa katika Diplomasia na ilitujengea heshima sana. Mfano, Reli ya TAZARA ni zawadi kutoka China kwa msimamo wa Tanzania chini ya Dr Salim A Salim kuhusu China ndani ya UN.
Kila tulipopata matatizo China walisimama na sisi kwasababu ya Diplomasia. Ilituharimu nini? Jibu ni hakuna

Kutolea kauli suala la Biafra ilitugharimu vipi kiuchumi?? Jibu ni hakuna.

Katika mambo ambayo Tanzania imepoteza ni diplomasia ya Kimataifa! sasa ukichanga na ufukara uliokithiri, heshima yetu Duniani imepungua sana. Viongoziwetu hawapati heshima iliyokuwepo!
Na,kabla ya matukio ya Idd Amin kufanya mashambulizi ya Kagera na Mwanza.Nini kilipelekea Mogadishu Accord ya mwaka 1971
Amin aliamini Obote yupo Tanzania na ilikuwa kweli. Aliamini Nyerere anataka kumrudisha Uganda

Tangu mapinduzi ya Uganda, Amin alitumia Tanzania ku diffuse interna strife
Kila Waganda walipoonyesha kukataa hali ya Uchumi kuwa mbaya Amin alitumia Tanzania kama kisingizio

Tanzania ilijihami kwa kurudisha mashambulizi, hayo ndiyo yalipelekea kuwa na Mogadishu accord chini ya Siad Barre. Makubaliano yalilenga kupunguza tension kati ya mataifa mawili
 
Iddi amin Hajawahi kuivamia Tanzania ni Uswahiba wa Nyerere na Milton Obote ndio uliopelekea ile vita ya Kipumbavu.

Nasikitika sana kuona vijana wa Leo wanashindwa kuelewa jambo dogo kama hili.
 
Katika mambo ambayo yameigharimu sana Tanganyika na kuidumaza huenda hata sio siasa ya ujamaa zaidi bali siasa za kikanda(geopolitics) za Nyerere ambazo hazikuzingatia maslahi ya uchumi wa Tanganyika wakati huo na ya muda mrefu.

Ukitafakari kwa kina katika fikra huru ni jinsi gani tulivyonufaika kama nchi kuzisaidia kwa jasho na damu nchi za SADCC kama South Africa, Namibia, Zimbabwe, Msumbiji na Angola kupata uhuru ni vigumu sana kupata jibu lolote lenye mashiko kuthibitisha kunufaika kwetu.

Muungano wa Jumuiya ya Africa Mashariki nao hakuwa na umuhimu wowote kabisa kiuchumi miaka ya 1960's kwa nchi zetu changa ambazo hazikuwa na bidhaa za kuuziana sisi kwa sisi. Nyerere alitakiwa kuzingatia zaidi Bilateral relationships kuliko Jumuiya za OAU, SADC na EAC.

Vita vya Uganda navyo huenda vingeweza kuepukika na kuepusha hasara kubwa ya kiuchumi kama Nyerere angempuuza Iddi Amin na kuwaacha Uganda wafanye siasa zao wenyewe wanavyojua wao.

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar nao ni kizungumkuti kikubwa mpaka leo ambapo dola ya TANU na CCM haijawahi kuwa na hoja za maana za kuonyesha Tanganyika inanufaikaje nao.

Kiujumla ukitazama wote Tanganyika tuliowasaidia katika harakati zao au kuungana nao walitupa au wana manufaa gani kwa Tanzania mpaka sasa hivi hakuna jibu kwa hakika.
Kama Chadomo mnavyowadanganya Wafuasi wenu kwamba mtawapa asali na Maziwa
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
Unakubali kwamba Jumuiya ina faida! Tanzania haina eneo au population zaidi ya DRC yet unasema Rwanda na Burundi zilijiunga kwa udogo!

Tatizo la Tanzania ni kushindwa kutumia fursa za Jumuiya, si suala la kwenda ''solo''

Nitajie nchi moja tua barani Afrika iliyokwenda 'Solo' ikafanikiwa ili tuifanya kama model ya Tanzania
Nimetaja mambo kadha yanayoweza kupelekea nchi kuhitaji Jumuiya kama hii ya EAC ambayo either ni nchi ndogo au landlocked au zenye migogoro mikubwa ya kisiasa au pia nyingi bado hazina uongozi thabiti.
Jumuiya ya EAC kama ilivyo inaweza kuwa na faida kubwa kwa nchi za Burundi, Rwanda, Uganda, DRC lakini isiwe na maana sana kwa Tanzania. Hata hivyo hizi Jumuiya za Kikanda miaka ya 1960s mpaka angalau 2000s hazikuwa na mashiko yoyote kiuchumi kwa nchi zote za Africa.

Kuna wakati Morroco haikuwa OAU kwa muda mrefu na maisha yaliendelea tu kama kawaida.

Kiujumla Jumuiya za Kikanda hazijawa na msaada mkubwa kwa nchi za Africa. Hazijapunguza gharama za kufanya biashara, hazijarahisisha movement za watu wake sana, hazijaondoa utegemezi wa Africa kwa US, Ulaya, Russia, China, Japan au Korea na pia hazijaweza kutatua matatizo ya kisiasa na kuimarisha utawala bora.
 
Back
Top Bottom