Wanaleta hasira kama siyo nyerere hata saa hii ucku uhuru wa kuchat ungetoka wapi. Watu wengine ni kama mafurushi tu wamejikuta hapo walipo hawajui chochote.
Nakubaliana nawewe 100%, kunamambo yapo wazi kabisa hatuhitaji kukashifu vitu vinavyojieleza waziwazi.
Sisi tupingane na kuzodoana kwa vyama vyetu vya sasa na viongozi wetu wasasa ndiyo siazi yetu, mwalimu pamoja na mapungufu yake upeo, uwezo na misimamo yake haina wakumlinganisha na hawa wasasa, si waupinzani wala wa serikalini
Moja ya walimu wangu Prof. Masuha (marehem kwa sasa, mungu amlaze mahalapema peponi) - alimsimlia nyerere alivyowawezesha watoto wa maskini kupata elimu, yeye Prof. Masuha akiwa mmojawapo kwa hisia ya ajabu sana. Nakumbuka wakati wa msiba wa mwl JK pale mlimani maprof na maDr walilia sana tena hadharani, mmoja wapo namkumbuka ni Dr Mhiru, kilichowaliza si kingine ni uadilifu na utendaji wa mwalimu.
Nasikitika kusema kwamba tumekuwa na kizazi kisicho na shukrani wa aibu kwa kuzusha na kushuhudia uwongo kwa watangulizi wetu hususani mwl JK Nyerere.
