Sio kwamba alikuwa hana muuono; baada ya 9/12/1962 Baba wa taifa alikuwa na muuono wa kuendelea lakini sio kwa Tanganyika tu bali kwa kwa Afrika Mashariki na Afrika kwa Ujumla (Umajumui wa kiafrika) ambapo yeye alikuwa tayari hata kutumia rasilimali za nchi yake kupigania muungano wa Afrika Mashariki na hatimaye Afrika kitu ambacho wenzake hawakunacho na daima hakukiona kwao yeye alizidi kutumia rasilimali zetu kupigania wengine wakati taifa likiwa halina cha kututosheleza kitu ambacho kilituangusha sana hasa pale ambapo hata lile soko dogo la bidhaa zetu (EAC)lilipoanguka hatukuwa na namna ya kufanya biashara yoyote kwa ufanisi na vita iliyofuata (Kageran War) ambayo ilitumaliza kabisa kiuchumi ambapo inasemekana aliposema miezi kumi na nane ya kufunga mkanda alificha uhalisia ambapo kiuhalisia ilikuwa ni miaka 18 ya kufunga mkanda!
Kiukweli Mwalimu alijenga misingi thabiti ya uongozi katika nchi hii na kuisimamia vilivyo kuliko kiongozi yeyote katika historia ya nchi hii hadi leo. alituunganisha watanzania wote akiwa na nia ya kutengeneza taifa la Tanzania na sio vitaifa vidogo vidogo ndani ya Tanzania kitu alichofanikiwa kwa kiwango kikubwa na sehemu ya matunda yake tunayaona leo. Alisimamia thabiti, upatikaji wa elimu hadi kwa watu wazima na hata wale maskini kabisa ambao hawakuwa na tumaini kwa watoto wao kupat elimu walisoma na kusomeshwa katika shule na taasisi kubwa za kielimu ndani na nje ya nchi bure kabisa kwa nia ya kuja kujenga taifa kiasi kwamba Tanzania ikaongoza Afrika kwa watu wanojua kusoma na kuandika na mengineyo mengi...
Kwa mimi namwona Nyerere kama kiongozi jasiri mwenye kukemea pasipo kujali wewe nani, msema kweli, mhalisia, mwanadiplomasia mahiri na kiongozi aliye kiri wazi kuwa anaondoka madarakani baada ya kuona kuwa sera zake zimeshindwa na hakuwa tayari kuzipa nafasi sera kandamizi za kimagharibi akiwa yeye madarakani akaona bora apishe mtazamo mpya.Ni kiongozi gani Afrika anayeweza leo kufanya hivi?
Kimapungufu Mwalimu alibana sana uhuru wa kujieleza hadi ikafika mahali kukosoa serikali ilikuwa kama kufuru, aliweka kizuizini waliotofutiana na mitazamo yake, na hakuweza tambua haki za binadamu katika katiba ya nchi, aliifanya serikali na viongozi wake waogopwe na watu na hakuruhusu juhudi binafsi na ubunifu katika kutafuta maendeleo.
Zaidi ya yote ndo maana kaitwa Mwalimu anatufundisha na sisi tunaiga kwake; hivyo tuyaige yale yake mazuri na kuachane na yale mabaya aliyotenda enzi za utawala wake!. vita ya kagera ilituua kiuchumi na ilikuwa na umuhimu mkubwa , vita ya kukomboa nchi zingine zilikuwa na umuhimu sana tu. lakini nyerere alitakiwa awe na akili kwamba sio watu wote/nchi zote zinamawazo kama yake ya kuunganisha africa (hakuwa na Maono ).
NAWASILISHA HOJA!