Magurudumu
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 1,748
- 493
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi.
Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kmabarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?
Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?
Tujadili.
Kwa hiyo haya ndiyo maoni yako uliyowasilisha kwenye marekebisho ya katiba? Tunataka Tanzania mpya yenye kusonga mbele wewe unaleta ngonjera za kijinga kwa vile mnamchukia Nyerere?