Nyerere Alifanya Makosa Makubwa...

Nyerere Alifanya Makosa Makubwa...

Bibie,
Naona umerudi kiaina. Kikwete nchi imemshinda. Kikwete ni janga la taifa. Lakini ninyi wafahidhina zimwi la Nyerere linazidi
kuwanyima usingizi.

Janga ni wewe na mleta uzi mnaotaka mbereko za kuwabeba.
 
chama pitia hapa ona wanaweza kuinua mdomo na vidole eti mwalimu alikosea.
 
Last edited by a moderator:
Mmezoea kudhulumu. Sheria gani ulitaka wewe. Nyerere aliandika katiba bila wasomi wengi imeongoza nchi hadi leo. Nchi imejaza wasomi lakini mmeshindwa hata kuedit katiba ili muweke hiyo misingi ya hizo sharia zako unazotaka.
sio hivyo Mamdenyi . nyererere hakuweka mazingira ya wataWAla waNaokuja kufuata sheria tuliokubaliana
 
Last edited by a moderator:
I have utmost respect for Nyerere. He wasn't perfect. Most of his policies failed but at least he had good intentions for this nation. At least aliona makosa yake na akakiri kuwa he was wrong.
The good thing about him hakuiba even a single dime!!!!
Aliiondoka voluntarily akaenda zake.
Waliofuatia wote ni majizi kama fat cats na ndio waliiotufikisha hapa tulipo
 
hatuendeshi nchi kulingana na emotoins kuhusu walimu wako au walimu wa yeyote. tunaendesha kwa misingi ya sheria na sheria inategemea context.

Sheria zipi mkuu naona umeshikilia sana hiki kipengele hebu funguka anamaanisha nini??
 
sio hivyo Mamdenyi . nyererere hakuweka mazingira ya wataWAla waNaokuja kufuata sheria tuliokubaliana

Red Giant mazingira gani tena wakati sheria zipo? Tatizo ni jamii ya walioko madarakani kufanya siasa kila kitu na wasomi wanasheria kutofuata viapo vyao
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, umesema kweli.

Ninachoona mimi ni UNAFIKI kwa watu wetu. Mashabiki wa serikali tatu ndio haohapo wanajifanya kupigania legacy ya Mwalimu.

Wanaonunua kura wakati wa uchaguzi ndio haohao wanajifanya kupigania legacy ya Mwalimu. Vinara wa kuomba misaada nje ya nchi ndio haohao wanaojidai kupigania legacy ya Mwalimu. Mabepari ndio hao hao wanaojifanya kupigania legacy ya Mwalimu.

Huu ni UNAFIKI.

Huwezi kusema ugombei Urais mpaka uahidiwe pesa nono kama mshahara wa mbunge halafu ukajifanya unapigania legacy ya Mwalimu.

Huwezi kusema chama chako hakihitaji wanachama Zanzibar halafu ukajidai unapigania legacy ya Mwalimu[/QUOTE].

Lets be true,

Legacy gani ya Mwalimu tunaishi nayo leo?


Unaonesha ufahamu wako ni wakimulugomulugo.

Hoja yetu inasema hivi; Nyerere Alifanya Makosa Makubwa..

Je hayo uloyaandika kwenye rangi nyekundu hapo juu yanauhusiano ndiyo makosa makubwa alofanya nyerere? fafaua
 
Nadhani mzee aachwe apumuzike kwa amani kuanza kukumjadili sasa ni ujinga tena ni kukosa heshima kwa mzee huyu aliyepigania taifa hili kwa nguvu zake zote.
 
sio hivyo Mamdenyi . nyererere hakuweka mazingira ya wataWAla waNaokuja kufuata sheria tuliokubaliana

Ni katiba na sera tu ndo vinafuatwa. sema ni wapi wamekiuka nyerere hakuzikwa na katiba wala sera za chama hazikufukiwa kule kaburini na vinaboreshwa kila siku ili nchi itawalike.
 
Last edited by a moderator:
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kmabarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.

Natamani ningekuona nikakuparua na kucha usoelimika. Mi naenda shamba bahati yako tungechanana hadi kesho chama pokea hapa.
 
Last edited by a moderator:
Nadhani mzee aachwe apumuzike kwa amani kuanza kukumjadili sasa ni ujinga tena ni kukosa heshima kwa mzee huyu aliyepigania taifa hili kwa nguvu zake zote.

Hatumjadili tunaweka record sahihi hatuwezi kuacha mtu aibuke na kuanza kupotosha ukweli kwa lengo analojua yeye mwenyewe
 
sio hivyo Mamdenyi . nyererere hakuweka mazingira ya wataWAla waNaokuja kufuata sheria tuliokubaliana

1. Mkuu unaikumbuka posti hii, rejea maelezo yake kisha utueleze mazingira gani zaidi?

2. Unaifahamu miiko na matakwa ya azimio la ARUSHA? hili lilijumuisha kila kitu.



quote_icon.png
By adolay

Hebu fafanua tuijadili vizuri hapo kwenye red, mimi naanza halafu wewe pinga hoja zangu......tujadiliane.

-Madini
Alikuachieni tena kwa ahadi kwamba mtavuna mkiwa teyari

-Elimu
wakati wake JK Nyerere, japo walifaidika wachache lakini wote masikini kwa matajiri walisoma shule za aina moja na waliofaulu waliendelezwa mpaka mwisho, leo hii watu binadamu fedha, walalahoi shule za kata hakuna chochote....

-Dawa za kulevya,
Wakati wa nyerere mlipata kusikia ujinga wa madawa haya kama ilivyo sasa na jinsi watanzania wanavyoteketea?

-Afya,
Pamoja na uchache wa dhahati na vituo vya afya, ukienda kutibiwa unapata dawa za uhakika, bure wahudumu na madakitari walifundwa na walikuwa wazalendo wa kweli.

-Polisi, jeshi na usalama wa raia,
Wakati wa Nyerere vikosi hivi vilitawaliwa na nidhamu ya hali ya juu, uzalendo na ushilikiano kwa raia, walihifadhi siri za serikali kwa umakini mkubwa leo hii kila kitu ni upuuzi tu

-Mbuga za wanyama na maliasili

Mliwahi kusikia meli kusafilisha meno ya tembo?, Ndege kubebe twiga, Loliondo kupigwa mnada na akina Katabalo kuuwawa?

-Udini na mshikamano miongoni mwa raia wa tanzania
Mliwahikusikia watu kugawanyika kama ilivyo sasa kwa mitazamo ya udini, ukabila na ukanda? (Tulisifika duniani kote kwa jina moja - tuliitana Ndugu FaizaFoxy, Ndugu Red Giant nk)

Mnataka misingigani nyinyi??? unaweza kumpeleka punda hadi mtoni lakini jukum la kunywa au asinywe maji linabaki kuwa hiari yake sio mchungaji.
 
Ingekuwa rahisi sana kama ungetuambia hiyo misingi ambayo haikuwekwa imara ili tuijadili!
 
Mamdenyi, utakuwa unasinzia nini maana umemshambulia jamaa wakati mko naye upande mmoja?

Najua kwa nn wanakoti mapungufu nyerere alisema tuchukue mazuri mabaya yaachwe ndo maana nimempa za uso kidogo naye achangamke ha ha haaa.
 
Natamani ningekuona nikakuparua na kucha usoelimika. Mi naenda shamba bahati yako tungechanana hadi kesho chama pokea hapa.


Wishing you all the best Mamndenyi, and many thanks for your contributions, you made my day perfect.
 
Sheria zipi mkuu naona umeshikilia sana hiki kipengele hebu funguka anamaanisha nini??

marais wanaokuaja sasa wanajiamulia wao. kama sheria Inasema kunyonga wa hawanyongi sababu ni marafki zao. watu wanapesa huko uswiswi wanasema warudishe harafu wasamehewe!. je ndio misingi yetu tuliyojiwekea?.
 
Back
Top Bottom