Nyerere Alifanya Makosa Makubwa...

Nyerere Alifanya Makosa Makubwa...


Nyerere hakua na "luxury" ya kuwa na watu wasomi wa kumsaidia, aliingia madarakani na "a handful" ya wasomi wa kumsaidia kutawala Watanzania Mil.9

Kumbuka hata madaktari wa liletwa kutokea Cuba, Ujerumani nk

Kulikua hakuna chuo kikuu hata kimoja, alirithi watanzania wasiokua na elimu kwa saana, bila elimu hata uwe na akili km "Einstein" ni ngumu lakini pamoja na hayo yote mpaka leo hakuna kiongozi atakaye weza aliofanya "leo akisimamia ujenzi wa barabara anasema yeye katoa hela halafu anatulazimisha wote tuamini barabara ni maendeleo na sio wajibu wa serikali" .... hata ujenzi wa mashule, na zahanati ni maendeleo lakini vinachangiwa na wananchi.... kwanini barabara hua hazina harambee? Iweje ujenzi wake uitwe maendeleo km si udhaifu wa viongozi wa sasa kutafuta sifa kwa migongo ya wananchi wao?

Nyerere hakuwahi kuelekezwa na mtu au kuwa mtumwa wa wakubwa kama alikua hivyo asingeweza kushirikiana na Cuba, au kuunga mkono PLO au Kupambana na wakoloni nchi jirani yaani Zambia, Msumbiji, Angola, Namibia na Africa ya kusini
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kambarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.

hana lolote huyu. ana machungu ya kufutwa kwa East Africa Muslim League. ambayo lengo lake ilikuwa ni kuifanya nchi ya Tanganyika kutawaliwa kwa sharia za kiislamu. pole sana Ndg yangu maana hizo ndoto zako hautaziona kamwe.
 
A. achievements kubwa za Mwalimu Nyerere
1. Uhuru Wa Tanganyika
2. Ukombozi Wa Mataifa ya Africa

B. Achievements tunazotakiwa kuziboresha ili zidumu
1. Aina ya Muungano Wa Tanganyika na Zanzibar
2. Katiba ya wananchi

C. Failure ambazo hatupaswi kuzirudia
1. Utaifishaji Wa Mali za watu
2. Siasa za chama kimoja
3. Sheria za kuweka watu kizuizini
4. Madaraka makubwa mno mikononi mwa MTU mmoja
5, Kuzuia private sector kushiriki kikamilifu kiuchumi
 
Ni ujinga kujadili mtu ambaye ameshakufa.
Mwacheni Mwalimu apumzike, aliyoyafanya ndio yalikuwa ndani ya uwezo wake tena mengi mazuri.
Mh. Magufuli ambaye ndo anaongoza sas ndo anapaswa kujadiliwa sio watu waliopumzika.
Nachelea kusema kwamba , hatutakuja kumpata Rais bora kama Mwl. Nyerere.
 
unajuwa kwanini KIKWETE !!!!! Ataki kumuita NYERERE BABA wataifa?????
 
Kosa lingine ni kuwafanya watanzania kuwa mazezeta yasiyojua kuhoji hatma za maisha yao ktk kudai haki za msingi.
 
Nyerere hakuwahi kuelekezwa na mtu au kuwa mtumwa wa wakubwa kama alikua hivyo asingeweza kushirikiana na Cuba, au kuunga mkono PLO au Kupambana na wakoloni nchi jirani yaani Zambia, Msumbiji, Angola, Namibia na Africa ya kusini
Labda ulimaanisha Zimbabwe (southern Rhodesia)
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kambarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.

Una uhakika alishindwa? umetumia vigezo vipi kufikia hitimisho kuwa alishindwa? Je, una habari kuwa kipindi cha Nyerere Tanzania ilikuwa ya pili Africa nyuma ya msumbiji kuwa na mashirika ya umma yenye kuzalisha vitu mbalimbali? Hivi leo baada ya Nyerere haya mashirika na viwanda yaliishia wapi? Yalipotea wakati gani? (Angalia nyakati na mabadiliko ya sera za kiuchumi za dunia zilivyoathiri utawala uliokuja baada ya Nyerere)
 
Hilo ni kosa kubwa sana kati ya makosa yaliyowahi kufanywa na kiongozi wa nchi. Usilitaje wala usilikumbushe.
Ni kosa kubwa kwa mantiki ipi? Azimio la Arusha lilikuwa zuri sana. Tatizo muda wa implementation yake ndio ulikuwa sio sahihi maana ilikuwa wakati nchi za kibepari zilikuwa zinapigana kufa kupona kuua Ujamaa. Leo hii China inaikopesha Marekani kwa sababu walikuwa na nguvu ya kusimamia malengo ya kijamaa.
 
Nakubaliana nawewe 100%, kunamambo yapo wazi kabisa hatuhitaji kukashifu vitu vinavyojieleza waziwazi.

Sisi tupingane na kuzodoana kwa vyama vyetu vya sasa na viongozi wetu wasasa ndiyo siazi yetu, mwalimu pamoja na mapungufu yake upeo, uwezo na misimamo yake haina wakumlinganisha na hawa wasasa, si waupinzani wala wa serikalini

Moja ya walimu wangu Prof. Masuha (marehem kwa sasa, mungu amlaze mahalapema peponi) - alimsimlia nyerere alivyowawezesha watoto wa maskini kupata elimu, yeye Prof. Masuha akiwa mmojawapo kwa hisia ya ajabu sana. Nakumbuka wakati wa msiba wa mwl JK pale mlimani maprof na maDr walilia sana tena hadharani, mmoja wapo namkumbuka ni Dr Mhiru, kilichowaliza si kingine ni uadilifu na utendaji wa mwalimu.

Nasikitika kusema kwamba tumekuwa na kizazi kisicho na shukrani wa aibu kwa kuzusha na kushuhudia uwongo kwa watangulizi wetu hususani mwl JK Nyerere.

Mkuu mada imebebwa na itikadi zaidi, nothing more. Wakati mwingine ni kupuuza mada kama hizi.
 
Viongozi wengi wa Afrika kwa kipindi kile cha mihemko ya uhuru walikua wanafiki tu akiwemo na huyu. Nakumbuka alishawahi kusema katiba immempa madaraka makubwa sana na inaweza kitumika vibaya na kiongozi mjeuri anayeweza kuja baadae. Hii ilikua kama sikosei ni miaka ya 80. Je alifanya nini kurekebisha hilo. Hata yeye alipenda kuwa Mungu mtu ndio maana hakuigusa. Katiba yetu ina misingi ya kikoloni na kila mtu analijua hilo. It’s all about selfishness and power. Human are selfish by nature. Huwezi kung’ang’a na ujamaa kwenye ulimwengu wa ubepari kamwee. Afrika hatotokea kamwe kiongozi kama aliyekuwa raisi wa Uper Volta(Burkina Faso) Thomas Sankara. Huyu alishaona usaliti kutoka kwa viongozi wanafiki wa Afrika ndio maana akaamua kufanya yake.
 
A. achievements kubwa za Mwalimu Nyerere
1. Uhuru Wa Tanganyika
2. Ukombozi Wa Mataifa ya Africa

B. Achievements tunazotakiwa kuziboresha ili zidumu
1. Aina ya Muungano Wa Tanganyika na Zanzibar
2. Katiba ya wananchi

C. Failure ambazo hatupaswi kuzirudia
1. Utaifishaji Wa Mali za watu
2. Siasa za chama kimoja
3. Sheria za kuweka watu kizuizini
4. Madaraka makubwa mno mikononi mwa MTU mmoja
5, Kuzuia private sector kushiriki kikamilifu kiuchumi
Uliona mbali
 
Wewe ndie unajua Kiingereza au Kiswahili? "Hujuwi", "nna" ndicho Kiswahili??? Kabebeshwe sembe na wewe kama hujaanza bado, maana ndicho mnachokishabikia kwa huyo mnaemshabikia!

Na sijui ni kwa nini nimepoteza muda wangu kujibu ----- wako!
Leten hoja msingi mambo ya kukosoana lugha hayajengi ila kama kakosea mrekebishe
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kambarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.
Bi mkora umeadimika!
 
Back
Top Bottom