Hili nalipa 90% kwa mtazamo wangu lakin so dont get me wrong,
Je vitu vyangu ntavipataje baada ya hatua hii?
Advice please
Kama nlivyosema mwanzo nlikuwa nachukulia masihara, sasa hata sima la kufanya eti
sipendi tabia ya jinsia yoyote ku-underestimate mtu kwa sababu ya shule, kuna watu wana elimu kubwa na hakuna la maana wanalolifanya hapa duniani.
Kuwa na mtoto sio sababu ya kutokumpenda kama ana tabia nzuri maswala ya kujiamini endelea kum shape ivoivo unaweza kumuacha ukapata kimeo zaidi, ukipata anaekumegea penzi nnje, si bora huyo aliye tulia we mpende tu isimtende utaja juta siku moja, hata asipo kufa ukimwacha akakunung,unikia hutapata baraka. Mpende tu huyo huyo
hizi sheria za mtaani kazi kweli aiseeNdio ukome kucheza na hisia za watu. Hata yeye anajijua kuwa soko limeshadoda ndio maana amekuganda mkuu huyo ni mkeo huna jinsi.
Sheri ya ndoa inasema ukiishi na mwanamke kwa mda wa miezi6 huyo tayar ni mkeo hata bila ya cheti cha ndoa hata kama utamwacha utalazmika kugawana vitu vyote hata kama ulikuwa na nyumba au shamba mtauza na mtagawana.......
Ndg acha kucheza na hisia za watu ni mwiko kabisa
mueleze ukweli kuwa hauna future naye, hawez ishi bila wewe siku ukifa ataishije?
Habari zenu wana jf, nsiwachoshe na salaam nyingi natumai ni wazima
Ok mimi nina girlfriend ambaye kaishia form 3, mapenzi naye nilianza kama mzaa vile, lakini badae nikajikuta nimezama mazima,
yeye hana kazi na nmejaribu kumtafutia sehemu nyingi lakini hataki kwenda kwani hajiamini na anaogopa sana ki-english, nami sina sehemu nyingine ya kuntafutia zaidi ya sehu hizo mana ndo wengi nawafahamu.
Kiukweli naona napoteza na kumpotezea mda mana siwezi kumuoa kwa sababu hizi
1: kwanza hajiamini hata kidogo,
2: Alishazaa mtoto mmoja na jamaa flani huko nyuma na mimi siwezi oa mtu aliyesha zaa, ( huu ni uamuzi wangu samahani kwa wale watakaohisi nmewakosea ama siko sahihi)
3: Elimu ni changamoto nyingine mana napenda mtu wa kusaidiana maisha
Swala lenyewe sasa:
Mara nyingi tunapogombana huwa anakimbilia kijiua na alishantamkia kuwa kama ntaamwacha basi maisha yake yataisha siku hiyo, hivi hili limekaa aje kisheria? Will I be held guity?
Kwa sasa nina kaa naye na ni mwaka saa natamani haya siku moja niende kazini na nipitilizie huko huko.
Jamani niko katika hali ngumu maana sijui nini cha kufanya, wana jf nawategemea sana kwa ushauri wenu juu ya hili, thanks
Allency, Eti nini? Umekaa nae mwaka mzima? Huyu tayari ni mkeo halali kisheria. Hauwezi tu ukaamka na kumwacha kizembe zembe tu.
Cha kufanya basi,
1. Ukiweza ondoka umwache pale na umwachie kila kitu.
ANGALIZO
2.Mweleze ukweli kwamba hauna mipango ya kuishi nae kama mke na mme. Hii ni hatari sana ukizingatia wewe ndiye tegemeo lake na ndio maana hataki kufanya kazi.
- Mbinu hii inaweza isikusaidie sana maana anapajua unapofanyia kazi, ndugu na marafiki zako hivyo itakuwa ni rashisi sana kukupata na yeye kuhamia kwako yaani kwenye makazi yako mapya
3. Fanya umafia, tafuta demu mwingine wa kisha uwe close nae kiasi kwamba yeye mwenyewe alifahamu hilo. Hii inaweza kukugharimu na usijaribu kuifanya.
kwanza kosa kubwa unalo wewe mwenyewe, kwani ulishajiwekea masharti hutaki kuoa mwanamke aliye na mtoto sasa ilkuwaje ukaanza kuishi na huyu mama wa watu. Na lengo lako hasa lilikuwa ni nini maana ukishaanza kuishi na mtu jamii inatambua huyo ni mkeo, sasa wewe ulilkuwa unawaza nini?
Kwanza hutakuwa fair kabisa ukimuacha, madhaifu ni jambo la kawaida hata wewe unayo sema hakuna mtu wa kutueleza hapa. Nakushauri kaa nae mueleze unachokitegemea kutoka kwake na vitu usivyovipenda kwake, na mwambie ajirekebishe maana, mpeleke shule maana ni mkeo mtarajiwa tayari, uwe serious na yeye naamini atabadilika.
Unaweza ukamuacha huyo ukapata bomu kuliko huyo ukaja kujuta katika maisha yako daima, wanadamu hatujakamilika, ni kuvumiliana, kusameheana na kuchukuliana na zaidi sana kupendana
Mjinga huyo....sikushauri umuoe hata kwa nini.....atakutishia kujinyonga au kukuua for any and each misunderstanding.Kujinyonga ndo one of her very first option, advice please
florence hili jina lina mkanganyiko sanammh nasikia harufu ya third party kwenye hayo mahusiano yenu
mwambie ukweli kama anataka kuwa na wewe afuate unayomshauri kwasababu ni muhimu kwenu nyote.