toplemon
JF-Expert Member
- Mar 26, 2017
- 4,581
- 4,626
TAMAA YA UTAJIRI ILIVYONIPONZA
Akiwa ni kijana bado Nico anaamua kuanza maisha mapya na mpenzi wake aliyempenda sana. Mpenzi wake anaitwa Anna. Nico ni kijana anayeishi kijijini mpambanaji anayetamani kuyafikia mafanikio makubwa. Analima,anafuga na lengo lake ni kufanikiwa na kufika mbali na anaishi kwenye maisha ya kimasikini sana. Alimaliza kidato cha nne na akaamua kuishi na kufunga ndoa na mpenzi wake walipomaliza kidato cha nne kijijini kwao kiufupi ni kuwa wawili hawa walioanana utotoni na wameshaishi muda mrefu sana na wamekua vijana wazima na watoto wawili.
Mwaka huo kulitokea ugonjwa wa mazao ulioharibu mazao kiasi kikubwa sana kiasi cha kumfanya Nico kupata hasara kubwa liyompelekea kwenye umasikini zaidi ya mwanzo." Dah hebu una mke wangu Anna mwaka huu tutaishije? Ona mazao yote yamekwisha na ugonjwa shambani na mifugo yenyewe ndo hii haieleweki mambo yanazidi kuwa mabaya sana hata sijui tutaishije mpenzi wangu" anaongea nico kwa uchungu sana
"Usijali mume wangu hayo yote tutayavuka tu tutalima tena mwakani ila usijali kwa kua hatuna chakula ndani nitaenda kuomba kwa shangazi yangu walau unga kidogo utusaidie mlo kwa siku kadhaa"
Maisha yao ya kijijini ni magumu sana.Wanaishi kwenye kijumba cha udongo juu kimeezekwa na mabati machakavu kitanda cha kizamani na godoro na ndani kuna vyombo,kitanda chao,godoro la watoto la kulalia,majembe, na taa ya chemli pamoja na vibatari kadhaa inayoashiria kwamba Wana maisha magumu sana.
Nico anaishi mbali kidogo na kwao kilomita 3 kutoka nyumbani hadi makazi ya Nico. yeye na mkewe Ana na amejenga hicho kijumba cha matope kwenye shamba alilopewa na wazazi na ndo hulitumia kwenye shughuli za kilimo.
"Kesho asubuhi nitaenda kwa shangazi kuomba unga au mahindi alivuna sana alipata gunia 40 na alilima na terekta natumai atanipa unga au mahindi"anaongea Anna huku akiwa kampampasa mume wake Nico kifuani wakiwa wamelala.
"Sawa tu ukajaribu tuone kama utafanikiwa ila shangazi yako kama kavuna najua atakupa tu"...."ndio mume wangu bila shaka".
Baada ya kunong'ona na mkewe wanaamua kulala usiku huku wakiwa na mawazo mazito sana kuhusu Hatma ya maisha yao ya kimasikini wanayoishi.Kulipokucha mke wa Nico alienda hadi kwa shangazi yake ambao kidogo maisha yao yalikua mazuri kiasi maana walikua wakulima wa kisasa na walikua wanatumia zana za kisasa kwenye kilimo na walivuna sana mwaka huo maana walitumia dawa za kisasa na wataalamu katika kupambana na magonjwa yanayoshambulia mimea.
Ana aipofika kwa shangazi yake alimsalimu pamoja na aliowakuta nyumbani.Walianza kuongea mengi sana na alielezea kuhusu jinsi walivyopata hasara ya mazao na hawajui watakula nini.Ndipo shangazi yake akampa pole sana Anna kwa yaliyowatokea.
"Asante sana shangazi kwa kunipa pole ila nina shida kubwa sana yaani hata sijui nitamlilia nan?"..."ipi hiyo niambie mimi nitakusaidia"...shangazi nakuomba tu msaada wako wa hata vibaba viwili vya unga tukale nyumbani au hata ukinipa mahindi sawa tu au hata ukinikopesha mahindi walau kidogo vibaba vichache tu niende nikale na wanangu na mume wangu nyumbani hali ni mbaya sana nimeacha watoto wanalia njaa tu wanaokota hadi maganda ya miwa njiani wanatafuna kwa hali ilivyo"anaongea mke wa Nico yaani Anna kuonyesha kuwa ana shida sana na anataka msaada
Shangazi naye anafikiria kwa dakika kadhaa kisha anamjibu "Yaani mimi nilikulimia wewe?
Umejuaje nilivuna sana kama siyo umbea umbea tu mimi sina unga wa kuwapa wala mahindi na mungu ananisimamia kwamba nawanyima kwa roho nyeupe tu mkalime huko chini mjue uchungu wa jembe biblia inasema asiyefanya kazi na asile kwa kweli nisiwe mnafiki kabisa mahindi ninayo lakini siwapi hata punje huyo baba mkwe wako (babake nico) alivyokua anauza mashamba hovyo hovyo alitaka huyo nico wake aje kulima wapi hata kama mnalima lakini baba yake nico aliuza mashamba mengi sana zamani kisa pombe sasa hivi mnateseka mnaomba omba kama matonya mimi sina mahindi ya kuchezea mwanangu"anaongea shangazi yake Anna kwa harakaharaka utadhani ni cherehani.
"Sawa nimekuelewa shangazi"anajibu mke wa nico kwa upole kabisa."Sasa hata nikiwakopesha mahindi mtanilipa na nini unajua nyie mna mambo ya ajabu sana hebu ukashike jembe huko"anaongea tena shangazi mtu akitumia maneno ya kashfa na masimango.
Mke wa Nico baada ya kuona maneno ya shangazi yake alianza kuondoka huku akianza kufuta machozi. Shangazi yake Ana alivyoona machozi ya Anna yakianza kumtiririka kutokana na maneno aliyomtolea anaamua kuingia ndani anachota unga kilo mbili anampa mke wa nico "haya huu utakusaidia mwanangu Anna nenda na huu"anasema shangazi yake Anna lakini tayari ashamsimanga Ana vya kutosha.
Baada ya kupewa unga Anna anashukuru ili aondoke lakini kabla hajaondoka,shangazi anamwiita "kwanza nimesahau Ana kuna mradi wa kusaidiwa na Uchumi saccos mnapewa mkopo na usimamizi wa kilimo chukua hili jarida lao ni taasisi nzuri humo pia zipo namba zao". Mke wa Nico yaani Ana anakabidhiwa Jarida na analipokea na kuondoka nalo.
Alipofika nyumbani alikuta watoto wanalia njaa sana na nico yupo hana hata mia mfukoni ikabidi akoroge uji kwanza wakanywa na familia yake na watoto wakafurahi kwa ule unga aliyopewa na Shangazi yake."Halafu mume wangu nimepewa hili jarida na shangazi yangu kasema hawa wanakopesha na usimamizi wa mradi unaokopeshwa nao kila kitu" alisema Ana akimkabidhi Nico lile jarida na nico akaanza kulisoma.
Baada ya kulisoma Nico akavutiwa na hiyo saccos ya kukopesha,anamweleza mkewe ana nia ya kukopa huko kwenye hiyo sacoss maana maelezo ya sacoss ni kwamba wanakukopesha pesa unafanya mradi wako na wanakusimamia na kukushauri kwa muda kisha unaendeleza mradi wako lakini unarejesha deni lao kwa riba.Baadaye Ana naye akasoma na kuridhishwa na hilo jambo la kwenda kukopa saccos.
Siku zilisogea na ndipo Nico alipoamua kwenda kwenye ofisi za Uchumi saccos ambazo zipo sehemu inaitwa Bomang'ombe Kilimanjaro.Alienda ofisini ambapo alieleza kuvutiwa na saccos hiyo na akaomba akopeshwe pesa.Baada ya mazungumzo marefu Nico aliomba akopeshwe milioni 5 ili akaendeleze kilimo na dhamana aliamua kuliweka shamba lake la hekari sita ambalo ndo anaishi na kulima huko na ni shamba la kupewa na familia yake.
Ndipo wakakubaliana kwamba Saccos waje wakague na wathibitishe kwamba muhusika yaani Nico ana vigezo vya kukopeshwa.Ndipo Nicco akakubaliana nao na Nico akaondoka kurejea nyumbani kusubiria siku saccoss wanakuja kutazama kujiridhisha.
Nico alipofika nyumbani alimwelezea mkewe kila kitu na kwamba ameaumua kukopa milioni 5." Mhh ila mume wangu si tulikubaliana ukope milioni 2 tu?sasa mbona umesema unakopa milioni 5 sasa?huoni kama itakua ni ngumu kurejesha ukizingatia wana riba kubwa?"...."usijali kwani shida iko wapi weee nataka nifanye kilimo kikubwa hapa cha umwagiliaji mfereji unapita hapa hapa nyumbani tukikopa milioni 5 tukilima nyanya hekari hizi zote 6 nina uhakika tutapata hata milioni 30 na tutalipa deni lao kabisa na tutabakiwa na pesa nyingi na sisi tunajenga mke wangu tukipata milioni 30 zinatutosha kabisa nimeshapiga mahesabu".
Baada ya maneno ya Nico mkewe alijikuta akifurahi sana na kumwambia mumewe "yaani nico ndo maana nakupenda yaani umenifanya niwaze zaidi kachukue mume wangu tuje tulime kwa bidii tupate hela".."sana mke wangu nina ndoto ya kuja kuwa tajiri mkubwa sana".
Kesho yake saccos walikuja na kukagua eneo ambalo nico anaweka dhamana ili apewe mkopo lilikua ni hilo eneo la hekari 6 aliamua kuliweka dhamana lote.Baada ya taratibu zote za uhakiki na kuhakikisha eneo ni kweli ni la Nico,mwishoni wakaandikishana kila kitu na sahihi wakaweka.Ndipo akaambiwa kuwa ataenda ofisini kupewa mkopo huo."Tumeridhika sana na tumeshasaini kila kitu kimeenda sawa Bwana Nicolas na mke Anna kwa sasa mnaweza kuja kuchukua pesa yenu baada ya siku 3 ofisini hongera sana kwa kua mnufaika wetu"
Nico hakuamini maneno yale na aliuliza mara mbili mbili na kuambiwa ni kweli kakidhi vigezo vya mkopo.Alifurahi sana na kurukaruka huku akiwabeba wanae juu na kusema kwamba safari ya mapambano ya kuuaga umasikini yanaenda kuanza.
Ilikua ni furaha kwa Nico na Anna na watoto wao kwani waliona kwamba kwa kua wangali vijana wanaenda kuanza mapambano ya kilimo cha kufa na kupona ili wauondoe umasikini.Siku zilienda huku wakitamani siku ya kwenda kuchukua hizo pesa hatimaye hiyo siku ilifika.
Ilikua ni asubuhi nzuri sana ambapo Nico alijiandaa kwenda mjini kuchukua pesa za mkopo kwani ndo siku ya kukabidhiwa rasmi.Akiwa anajiandaa mke wa Nico aling'ang'ania waende na mumewe yaani amsindikize."Sijui tuende wote jamani nikusindikize tu natamani kweli nikashuhudie"...."hapana mke wangu nitalishugulikia mwenyewe we baki tu na watoto naleta pesa mamaaaa" nico alimjibu mkewe kwa mbwembwe kweli na akimtaka abaki japo Anna aling'ang'ania aende na mumewe lakini Nico alikataa
Safari ya kuelekea mjini nico aliianza na akawasili pale mapema tu na kusubiri utaratibu akiwa na form zake.Mwisho akapata nafasi ya kuhudumiwa ili akabidhiwe pesa zake lakini akaulizwa "Ndio mkopo wako wa milioni 5 upo tayari tupe namba ya account yako ya Bank tukuwekee itakua poa zaidi"alisema mmoja wa wafanyakazi wa ile saccos.
Katika kitu ambacho Nico alielezwa siku ile maafisa wa saccos walipokuja kujiridhisha na eneo lake aliloliweka dhamama ni kuwa aliambiwa ajitahidi awe na account ya bank ili iwe awekewe pesa zake huko kuliko kubeba pesa taslim na mabegi kwani siyo salama. Lakini kutokana na Nico kuwa na furaha iliyozidi siku ile hakukumbuka hata kidogo."Haina haja ya akaunti ya benki mimi najiamini nipewe tu kwa cash nimekuja na mfuko wa kiroba kikubwa tu nitaweka humo.
Kutokana na kuamua hivyo ilibidi tu Saccos wamueleze awe makini maana milioni 5 bado ni kiwango kikubwa sana kubeba kwenye mfuko wa kiroba.Baada ya kusaini tena walielekea benki ambapo ni dakika chache tu kutoka hapo ambapo alikabidhiwa fedha zake milioni 5 cash na akaziweka kwenye kiroba lakini Saccos wakataka wampeleke hadi nyumbani kwa usafiri.Lakini Nico aliona kama utakua ni mlongolongo mrefu au atachelewa sijui aliwaza nini akakataa kupelekwa hadi nyumbani na aliona labda atachelewa yeye ashapata pesa zake anataka azipeleke mwenyewe nyumbani.Basi wakamwacha na pesa zake wakaondoka zao.
Nico akiwa na burungutu la fedha taslimu shilingi milioni 5 kwenye mfuko akiwa anatoka hapo benki wa nje alitokea Dada mmoja mrefu aliyeshuka kwenye gari mpya aina ya Harrier nyeusi mpyaa huyu mwanadada alikua mrembo hatari mrefu na mwenye umbo namba 8,lakini Nico hakubabaishwa na huyo mwanamke maana alikua anawaza tu kuwahi nyumbani na hizo pesa.
Lakini ghafla yule mwanamke aliteleza na kiatu kirefu alichovaa kikamdondosha chini "puuu",Nico alishtuka ghafla na kuwahi kumnyooshea yule dada mkono anyanyuke."Pole sana dada kuwa makini"alisema Nico na kumnyanyua yule mdada.Yule dada alinyanyuka na kumshukuru nico lakini akasema kaumia na hawezi kutembea vizuri."nimeumia kiasi siwezi kutembea vizuri oooh mungu wangu kaka samahani naweza kukuomba kitu?" ......"nambie dada"alisema nico akiwa mkono mmoja kabeba roba lenye milioni 5.
"Unaweza kunishika bega mpaka hapo ndani ya bank pls nitoe tu pesa maana nimeanguka nimeumia naogopa nitateleza kwenye tiles/tailizi za hapo benki plzz"huyu mdada alidai kaanguka kaumia hivyo anaomba nico amshike japo begani hadi hapo ndani benki maana alidai ataanguka.
Nico aliwaza akakubali kumsaidia huyo mwanamke na akamshika bega na kuingia naye benki huku yule mwanamke akitembea kwa kuchechemea.
Walipoingia ndani yule mwanamke alijikongoja mwenyewe hadi kwa wahudumu na akajaza fomu ya kutoa pesa kisha akamuomba nico amshike tena hadi nje kwenye ATM mashine maana zilikua kwa nje. Nico alifanya hivyo hadi akamshika yule mwanamke bega ili asianguke akitembea hadi kwenye Atm mashine na akaingiza card yake na kutoa kiasi cha shilingi milioni moja. Yule mwanamke baada ya kutoa milioni moja aliondoka na nico akiwa kamshikilia bega kuelekea kwenye gari yake na yule mwanamke ghafla alinyanyua simu na kuanza kupiga na kuongea "asante sana nimetoa milioni moja mshahara wangu wa siku moja kweli hii fursa ni nzuri sana na haiihitaji hata elimu mimi nina elimu ya la saba tu lakini napokea milioni moja kwa siku kweli hii fursa ni nzuri asante sana boss"
Kisha akakata simu.
Maneno ya yule mwanamke kupokea milioni moja kila siku yalimgusa Nico na akajikuta amemuuliza yule mwanamke "unapokeaga milioni moja kwa siku?"..."ndio Kaka milioni moja kama mshahara ila usiongee kwa sauti ndugu yangu watu wakitusikia naweza kuporwa"aliongea yule dada.
Kisha akaendelea kusema "mimi nimeishia la saba tu lakini hii fursa nilijiunga leo hii nina magari na unatajirika majibu ni muda huo huo"..."kivipi jaman?" Nico aliuliza."Naitwa Rosemary wewe je?" Naitwa "Nicolaus au kwa kifupi "nico"...Yule dada alianza kumweleza nico hiyo fursa inavyonufaisha watu na akaenda mbali zaidi akatoa vithibitisho,uhalali,na kila kitu ili nico aweze kuamini.Yule dada alimfanya Nico atamani hiyo fursa na mwisho wakaingia kwenye gari yake na akaanza kumuonyesha Nico majumba na magari anayomiliki kupitia hiyo fursa kwenye laptop ndani ya gari. "namiliki nyumba na magari kwa hii fursa na ukiweka pesa nyingi yaani dau kubwa ndo unapata zaidi" Nico alijikuta akitamani akauliza mfano mtu akiweka milioni 5 itakuwaje "milioni 5 ukiweka ndani ya masaa kadhaa tu utaingiza milioni 25 kwa mpigo maana hii fursa ni mtandao wa kimataifa.
Mawazo ya Nico yalibadilika hapo hapo akitamani hiyo fursa badala ya kwenda nyumbani.Yule dada alimuahidi nico kwamba atamsaidia kujiunga na mwishowe wakawasha gari ili nico akajiunge.Waliondoka bomang'ombe hadi moshi mjini na kutua nje ya jengo la bank moja hivi ambayo huyo dada alidai ndo hapo mtu hujiunga na hiyo fursa na pesa zinaanza kuwa nyingi.
Baada ya kufika pale walipokelewa na dada mmoja aliyejiita customer care wa benk ile na huyo Rosemary alimtambulisha Nico kwa yule customer care "oooh kaja kujiunga na fursa eeh sawa ila tuongee taratibu jamani maana hii fursa ni hela nyingi sana na wakitusikia tutaporwa fedha"aliongea yule mdada na Rosemary huyo aliyekuja na Nico akakubaliana na yule Dada.
Mwishoni kabisa Nico aliambiwa aweke milioni moja akakubali na zile pesa zikaingizwa ndani na akaambiwa asubiri kwa dakika chache tu akiwa na Rosemary pale nje,ndani ya dakika 10 tu akaletewa mabulungutu ya fedha milioni 2 akafurahi sana akasema mambo si ndo hayo?akapanda dau akawa milioni 3 analetewa milioni 4 tena ,akaona isiwe tabu akatoa pesa zote milioni 5 pamoja na hiyo milioni 3 jumla aliyoipata pale jumla ikawa milioni 8 na Huyo rosemary naye akasema naye fursa hiyo isimpite akaweka ile milioni moja aloitoa bank ikawa jumla milioni 9.Nico akaahidiwa asubiri tena dakika kadhaa na ataletewa hapo hapo jumla milioni 20 na rosemary naye akaahidiwa milioni 2 maana aliweka milioni moja.
Ili kusubiri kwa kua ilikua pesa nyingi hiyo waliambiwa waingie ndani wasubirie pesa zao ndipo Nico na rosemary wakaingia ndani kusubiria pesa ziletwe maana zilikua zinachezeshwa kwa chumba cha ndani ya hiyo benki.Ndipo ghafla Rosemary akamwambia nico kuwa kabanwa na haja ndogo anatoka ajisaidie huku akimwachia Nico Mkoba wake."nishikie huu mkoba wangu una hela milioni 2 hizi huku (akafunua akamuonyesha)naenda kujisaidia dakika moja tu na kurudi tuje kuchukua magawio yetu maana hii fursa ni nzuri na ya kitajiri sana"...."sawa fanya haraka"alisema nico na rosemary akatoka haraka haraka hadi alipoegesha gari lake na kuwasha gari kimya kimya na kuondoka.
Nico alisubiria akicheka akijiona ashakua tajiri na akawaza jinsi atakavyopata milioni 20 kwa haraka kichwani aliwaza mengi sana akawa anaona jinsi atakavyokabidhiwa na jinsi atakavyofika nyumbani na kuanza maisha upya mazuri.Na aliwaza mengi sana pia kuhusu Rosemary na kumuona kama mkombozi mwaminifu maana aliacha hadi vitambulisho pale."ana hela sana huyu dada hii fursa imemfanya tajiri sana milioni moja kila siku daaah pesa mingi sana ana hela sana daaah hadi huu mkoba anatembea na milioni mbili sio mchezo na mimi leo naandika historia napokea milioni 20 zangu mie" aliwaza hayo nico akicheka kimoyomoyo kwa furaha.
Alisubiri lisaa lizima rosemary hakurudi.Alijshangaa lile jengo yupo peke yake na kwenda huko kwenye vyumba na kukuta patupu "inamaana mimi na rosemary tumedanganywa?hapana hatuwezi kudanganywa kirahisi hivyo maana hata rose mwenyewe kaweka pesa zake tena ngoja nimwiite labda kabanwa na haja chooni" aliwaza na kuongea mwenyewe akilini hayo nico.
Alitoka nje na kumtafuta Rosemary hakumuona akatizama gari ya rosemary pia haikuwepo akaanza kutafuta nyumba nzima lile jengo likawa kimyaaa hakuna mtu alikwenda hadi njiani kuulizia wapita njia kama wamemuona rosemary wakabaki wakimshangaa sana "hatumjui unamzungia nani hatujamuona yoyote huku njiani tanzania ina warosemary wapo maelfu unamzungumzia yupi umechanganyikiwa?"
Watu walimshangaa na kumjibu nico hivyo.Nico alizidi kuchanganyikiwa akaona hebu achukue zile pesa kwa mkoba wa rosemary alioachiwa ile kufungua hivi mungu wanguuu!!!!!!!!!!hazikua pesa yalikua ni mabulungutu ya karatasi zilizofanana na fedha zilizofungwa kwa "raba band" utadhani ni fedha kweli.Na vile vitambulisho vilikua ni feki,na vya uongo,na pale hapakua benki bali hilo jengo liliwahi kuwa bank zamani lakini miaka 20 iliyopita
Rosemary alikua tapeli wa kimataifa mwenye kujua ulaghai na utapeli wa kila aina.
Nico akawa amekwishatapeliwa milioni 5 ya mkopo mchana kweupe,na hakubakiwa na hata senti tano mfukoni akawa ameshachezewa kekundu. Nico hakuamini alichokiona, alihisi yupo ndotoni, alihisi labda ni utani tu alijikuta akiangua kilio umma ukajaa na kumshangaa na watu wakamwambia "kaka umelizwa matapeli ni wengi mjini.Nico ndipo alipata kichaa zaidi akajikuta anavua hadi suruali na kuanza kutembea uchi njiani huku akipiga mayowe ya msaada maana alikua keshachanganyikiwa.
Jee B
Nico atamwambia nini mkewe?
ITAENDELEA
Akiwa ni kijana bado Nico anaamua kuanza maisha mapya na mpenzi wake aliyempenda sana. Mpenzi wake anaitwa Anna. Nico ni kijana anayeishi kijijini mpambanaji anayetamani kuyafikia mafanikio makubwa. Analima,anafuga na lengo lake ni kufanikiwa na kufika mbali na anaishi kwenye maisha ya kimasikini sana. Alimaliza kidato cha nne na akaamua kuishi na kufunga ndoa na mpenzi wake walipomaliza kidato cha nne kijijini kwao kiufupi ni kuwa wawili hawa walioanana utotoni na wameshaishi muda mrefu sana na wamekua vijana wazima na watoto wawili.
Mwaka huo kulitokea ugonjwa wa mazao ulioharibu mazao kiasi kikubwa sana kiasi cha kumfanya Nico kupata hasara kubwa liyompelekea kwenye umasikini zaidi ya mwanzo." Dah hebu una mke wangu Anna mwaka huu tutaishije? Ona mazao yote yamekwisha na ugonjwa shambani na mifugo yenyewe ndo hii haieleweki mambo yanazidi kuwa mabaya sana hata sijui tutaishije mpenzi wangu" anaongea nico kwa uchungu sana
"Usijali mume wangu hayo yote tutayavuka tu tutalima tena mwakani ila usijali kwa kua hatuna chakula ndani nitaenda kuomba kwa shangazi yangu walau unga kidogo utusaidie mlo kwa siku kadhaa"
Maisha yao ya kijijini ni magumu sana.Wanaishi kwenye kijumba cha udongo juu kimeezekwa na mabati machakavu kitanda cha kizamani na godoro na ndani kuna vyombo,kitanda chao,godoro la watoto la kulalia,majembe, na taa ya chemli pamoja na vibatari kadhaa inayoashiria kwamba Wana maisha magumu sana.
Nico anaishi mbali kidogo na kwao kilomita 3 kutoka nyumbani hadi makazi ya Nico. yeye na mkewe Ana na amejenga hicho kijumba cha matope kwenye shamba alilopewa na wazazi na ndo hulitumia kwenye shughuli za kilimo.
"Kesho asubuhi nitaenda kwa shangazi kuomba unga au mahindi alivuna sana alipata gunia 40 na alilima na terekta natumai atanipa unga au mahindi"anaongea Anna huku akiwa kampampasa mume wake Nico kifuani wakiwa wamelala.
"Sawa tu ukajaribu tuone kama utafanikiwa ila shangazi yako kama kavuna najua atakupa tu"...."ndio mume wangu bila shaka".
Baada ya kunong'ona na mkewe wanaamua kulala usiku huku wakiwa na mawazo mazito sana kuhusu Hatma ya maisha yao ya kimasikini wanayoishi.Kulipokucha mke wa Nico alienda hadi kwa shangazi yake ambao kidogo maisha yao yalikua mazuri kiasi maana walikua wakulima wa kisasa na walikua wanatumia zana za kisasa kwenye kilimo na walivuna sana mwaka huo maana walitumia dawa za kisasa na wataalamu katika kupambana na magonjwa yanayoshambulia mimea.
Ana aipofika kwa shangazi yake alimsalimu pamoja na aliowakuta nyumbani.Walianza kuongea mengi sana na alielezea kuhusu jinsi walivyopata hasara ya mazao na hawajui watakula nini.Ndipo shangazi yake akampa pole sana Anna kwa yaliyowatokea.
"Asante sana shangazi kwa kunipa pole ila nina shida kubwa sana yaani hata sijui nitamlilia nan?"..."ipi hiyo niambie mimi nitakusaidia"...shangazi nakuomba tu msaada wako wa hata vibaba viwili vya unga tukale nyumbani au hata ukinipa mahindi sawa tu au hata ukinikopesha mahindi walau kidogo vibaba vichache tu niende nikale na wanangu na mume wangu nyumbani hali ni mbaya sana nimeacha watoto wanalia njaa tu wanaokota hadi maganda ya miwa njiani wanatafuna kwa hali ilivyo"anaongea mke wa Nico yaani Anna kuonyesha kuwa ana shida sana na anataka msaada
Shangazi naye anafikiria kwa dakika kadhaa kisha anamjibu "Yaani mimi nilikulimia wewe?
Umejuaje nilivuna sana kama siyo umbea umbea tu mimi sina unga wa kuwapa wala mahindi na mungu ananisimamia kwamba nawanyima kwa roho nyeupe tu mkalime huko chini mjue uchungu wa jembe biblia inasema asiyefanya kazi na asile kwa kweli nisiwe mnafiki kabisa mahindi ninayo lakini siwapi hata punje huyo baba mkwe wako (babake nico) alivyokua anauza mashamba hovyo hovyo alitaka huyo nico wake aje kulima wapi hata kama mnalima lakini baba yake nico aliuza mashamba mengi sana zamani kisa pombe sasa hivi mnateseka mnaomba omba kama matonya mimi sina mahindi ya kuchezea mwanangu"anaongea shangazi yake Anna kwa harakaharaka utadhani ni cherehani.
"Sawa nimekuelewa shangazi"anajibu mke wa nico kwa upole kabisa."Sasa hata nikiwakopesha mahindi mtanilipa na nini unajua nyie mna mambo ya ajabu sana hebu ukashike jembe huko"anaongea tena shangazi mtu akitumia maneno ya kashfa na masimango.
Mke wa Nico baada ya kuona maneno ya shangazi yake alianza kuondoka huku akianza kufuta machozi. Shangazi yake Ana alivyoona machozi ya Anna yakianza kumtiririka kutokana na maneno aliyomtolea anaamua kuingia ndani anachota unga kilo mbili anampa mke wa nico "haya huu utakusaidia mwanangu Anna nenda na huu"anasema shangazi yake Anna lakini tayari ashamsimanga Ana vya kutosha.
Baada ya kupewa unga Anna anashukuru ili aondoke lakini kabla hajaondoka,shangazi anamwiita "kwanza nimesahau Ana kuna mradi wa kusaidiwa na Uchumi saccos mnapewa mkopo na usimamizi wa kilimo chukua hili jarida lao ni taasisi nzuri humo pia zipo namba zao". Mke wa Nico yaani Ana anakabidhiwa Jarida na analipokea na kuondoka nalo.
Alipofika nyumbani alikuta watoto wanalia njaa sana na nico yupo hana hata mia mfukoni ikabidi akoroge uji kwanza wakanywa na familia yake na watoto wakafurahi kwa ule unga aliyopewa na Shangazi yake."Halafu mume wangu nimepewa hili jarida na shangazi yangu kasema hawa wanakopesha na usimamizi wa mradi unaokopeshwa nao kila kitu" alisema Ana akimkabidhi Nico lile jarida na nico akaanza kulisoma.
Baada ya kulisoma Nico akavutiwa na hiyo saccos ya kukopesha,anamweleza mkewe ana nia ya kukopa huko kwenye hiyo sacoss maana maelezo ya sacoss ni kwamba wanakukopesha pesa unafanya mradi wako na wanakusimamia na kukushauri kwa muda kisha unaendeleza mradi wako lakini unarejesha deni lao kwa riba.Baadaye Ana naye akasoma na kuridhishwa na hilo jambo la kwenda kukopa saccos.
Siku zilisogea na ndipo Nico alipoamua kwenda kwenye ofisi za Uchumi saccos ambazo zipo sehemu inaitwa Bomang'ombe Kilimanjaro.Alienda ofisini ambapo alieleza kuvutiwa na saccos hiyo na akaomba akopeshwe pesa.Baada ya mazungumzo marefu Nico aliomba akopeshwe milioni 5 ili akaendeleze kilimo na dhamana aliamua kuliweka shamba lake la hekari sita ambalo ndo anaishi na kulima huko na ni shamba la kupewa na familia yake.
Ndipo wakakubaliana kwamba Saccos waje wakague na wathibitishe kwamba muhusika yaani Nico ana vigezo vya kukopeshwa.Ndipo Nicco akakubaliana nao na Nico akaondoka kurejea nyumbani kusubiria siku saccoss wanakuja kutazama kujiridhisha.
Nico alipofika nyumbani alimwelezea mkewe kila kitu na kwamba ameaumua kukopa milioni 5." Mhh ila mume wangu si tulikubaliana ukope milioni 2 tu?sasa mbona umesema unakopa milioni 5 sasa?huoni kama itakua ni ngumu kurejesha ukizingatia wana riba kubwa?"...."usijali kwani shida iko wapi weee nataka nifanye kilimo kikubwa hapa cha umwagiliaji mfereji unapita hapa hapa nyumbani tukikopa milioni 5 tukilima nyanya hekari hizi zote 6 nina uhakika tutapata hata milioni 30 na tutalipa deni lao kabisa na tutabakiwa na pesa nyingi na sisi tunajenga mke wangu tukipata milioni 30 zinatutosha kabisa nimeshapiga mahesabu".
Baada ya maneno ya Nico mkewe alijikuta akifurahi sana na kumwambia mumewe "yaani nico ndo maana nakupenda yaani umenifanya niwaze zaidi kachukue mume wangu tuje tulime kwa bidii tupate hela".."sana mke wangu nina ndoto ya kuja kuwa tajiri mkubwa sana".
Kesho yake saccos walikuja na kukagua eneo ambalo nico anaweka dhamana ili apewe mkopo lilikua ni hilo eneo la hekari 6 aliamua kuliweka dhamana lote.Baada ya taratibu zote za uhakiki na kuhakikisha eneo ni kweli ni la Nico,mwishoni wakaandikishana kila kitu na sahihi wakaweka.Ndipo akaambiwa kuwa ataenda ofisini kupewa mkopo huo."Tumeridhika sana na tumeshasaini kila kitu kimeenda sawa Bwana Nicolas na mke Anna kwa sasa mnaweza kuja kuchukua pesa yenu baada ya siku 3 ofisini hongera sana kwa kua mnufaika wetu"
Nico hakuamini maneno yale na aliuliza mara mbili mbili na kuambiwa ni kweli kakidhi vigezo vya mkopo.Alifurahi sana na kurukaruka huku akiwabeba wanae juu na kusema kwamba safari ya mapambano ya kuuaga umasikini yanaenda kuanza.
Ilikua ni furaha kwa Nico na Anna na watoto wao kwani waliona kwamba kwa kua wangali vijana wanaenda kuanza mapambano ya kilimo cha kufa na kupona ili wauondoe umasikini.Siku zilienda huku wakitamani siku ya kwenda kuchukua hizo pesa hatimaye hiyo siku ilifika.
Ilikua ni asubuhi nzuri sana ambapo Nico alijiandaa kwenda mjini kuchukua pesa za mkopo kwani ndo siku ya kukabidhiwa rasmi.Akiwa anajiandaa mke wa Nico aling'ang'ania waende na mumewe yaani amsindikize."Sijui tuende wote jamani nikusindikize tu natamani kweli nikashuhudie"...."hapana mke wangu nitalishugulikia mwenyewe we baki tu na watoto naleta pesa mamaaaa" nico alimjibu mkewe kwa mbwembwe kweli na akimtaka abaki japo Anna aling'ang'ania aende na mumewe lakini Nico alikataa
Safari ya kuelekea mjini nico aliianza na akawasili pale mapema tu na kusubiri utaratibu akiwa na form zake.Mwisho akapata nafasi ya kuhudumiwa ili akabidhiwe pesa zake lakini akaulizwa "Ndio mkopo wako wa milioni 5 upo tayari tupe namba ya account yako ya Bank tukuwekee itakua poa zaidi"alisema mmoja wa wafanyakazi wa ile saccos.
Katika kitu ambacho Nico alielezwa siku ile maafisa wa saccos walipokuja kujiridhisha na eneo lake aliloliweka dhamama ni kuwa aliambiwa ajitahidi awe na account ya bank ili iwe awekewe pesa zake huko kuliko kubeba pesa taslim na mabegi kwani siyo salama. Lakini kutokana na Nico kuwa na furaha iliyozidi siku ile hakukumbuka hata kidogo."Haina haja ya akaunti ya benki mimi najiamini nipewe tu kwa cash nimekuja na mfuko wa kiroba kikubwa tu nitaweka humo.
Kutokana na kuamua hivyo ilibidi tu Saccos wamueleze awe makini maana milioni 5 bado ni kiwango kikubwa sana kubeba kwenye mfuko wa kiroba.Baada ya kusaini tena walielekea benki ambapo ni dakika chache tu kutoka hapo ambapo alikabidhiwa fedha zake milioni 5 cash na akaziweka kwenye kiroba lakini Saccos wakataka wampeleke hadi nyumbani kwa usafiri.Lakini Nico aliona kama utakua ni mlongolongo mrefu au atachelewa sijui aliwaza nini akakataa kupelekwa hadi nyumbani na aliona labda atachelewa yeye ashapata pesa zake anataka azipeleke mwenyewe nyumbani.Basi wakamwacha na pesa zake wakaondoka zao.
Nico akiwa na burungutu la fedha taslimu shilingi milioni 5 kwenye mfuko akiwa anatoka hapo benki wa nje alitokea Dada mmoja mrefu aliyeshuka kwenye gari mpya aina ya Harrier nyeusi mpyaa huyu mwanadada alikua mrembo hatari mrefu na mwenye umbo namba 8,lakini Nico hakubabaishwa na huyo mwanamke maana alikua anawaza tu kuwahi nyumbani na hizo pesa.
Lakini ghafla yule mwanamke aliteleza na kiatu kirefu alichovaa kikamdondosha chini "puuu",Nico alishtuka ghafla na kuwahi kumnyooshea yule dada mkono anyanyuke."Pole sana dada kuwa makini"alisema Nico na kumnyanyua yule mdada.Yule dada alinyanyuka na kumshukuru nico lakini akasema kaumia na hawezi kutembea vizuri."nimeumia kiasi siwezi kutembea vizuri oooh mungu wangu kaka samahani naweza kukuomba kitu?" ......"nambie dada"alisema nico akiwa mkono mmoja kabeba roba lenye milioni 5.
"Unaweza kunishika bega mpaka hapo ndani ya bank pls nitoe tu pesa maana nimeanguka nimeumia naogopa nitateleza kwenye tiles/tailizi za hapo benki plzz"huyu mdada alidai kaanguka kaumia hivyo anaomba nico amshike japo begani hadi hapo ndani benki maana alidai ataanguka.
Nico aliwaza akakubali kumsaidia huyo mwanamke na akamshika bega na kuingia naye benki huku yule mwanamke akitembea kwa kuchechemea.
Walipoingia ndani yule mwanamke alijikongoja mwenyewe hadi kwa wahudumu na akajaza fomu ya kutoa pesa kisha akamuomba nico amshike tena hadi nje kwenye ATM mashine maana zilikua kwa nje. Nico alifanya hivyo hadi akamshika yule mwanamke bega ili asianguke akitembea hadi kwenye Atm mashine na akaingiza card yake na kutoa kiasi cha shilingi milioni moja. Yule mwanamke baada ya kutoa milioni moja aliondoka na nico akiwa kamshikilia bega kuelekea kwenye gari yake na yule mwanamke ghafla alinyanyua simu na kuanza kupiga na kuongea "asante sana nimetoa milioni moja mshahara wangu wa siku moja kweli hii fursa ni nzuri sana na haiihitaji hata elimu mimi nina elimu ya la saba tu lakini napokea milioni moja kwa siku kweli hii fursa ni nzuri asante sana boss"
Kisha akakata simu.
Maneno ya yule mwanamke kupokea milioni moja kila siku yalimgusa Nico na akajikuta amemuuliza yule mwanamke "unapokeaga milioni moja kwa siku?"..."ndio Kaka milioni moja kama mshahara ila usiongee kwa sauti ndugu yangu watu wakitusikia naweza kuporwa"aliongea yule dada.
Kisha akaendelea kusema "mimi nimeishia la saba tu lakini hii fursa nilijiunga leo hii nina magari na unatajirika majibu ni muda huo huo"..."kivipi jaman?" Nico aliuliza."Naitwa Rosemary wewe je?" Naitwa "Nicolaus au kwa kifupi "nico"...Yule dada alianza kumweleza nico hiyo fursa inavyonufaisha watu na akaenda mbali zaidi akatoa vithibitisho,uhalali,na kila kitu ili nico aweze kuamini.Yule dada alimfanya Nico atamani hiyo fursa na mwisho wakaingia kwenye gari yake na akaanza kumuonyesha Nico majumba na magari anayomiliki kupitia hiyo fursa kwenye laptop ndani ya gari. "namiliki nyumba na magari kwa hii fursa na ukiweka pesa nyingi yaani dau kubwa ndo unapata zaidi" Nico alijikuta akitamani akauliza mfano mtu akiweka milioni 5 itakuwaje "milioni 5 ukiweka ndani ya masaa kadhaa tu utaingiza milioni 25 kwa mpigo maana hii fursa ni mtandao wa kimataifa.
Mawazo ya Nico yalibadilika hapo hapo akitamani hiyo fursa badala ya kwenda nyumbani.Yule dada alimuahidi nico kwamba atamsaidia kujiunga na mwishowe wakawasha gari ili nico akajiunge.Waliondoka bomang'ombe hadi moshi mjini na kutua nje ya jengo la bank moja hivi ambayo huyo dada alidai ndo hapo mtu hujiunga na hiyo fursa na pesa zinaanza kuwa nyingi.
Baada ya kufika pale walipokelewa na dada mmoja aliyejiita customer care wa benk ile na huyo Rosemary alimtambulisha Nico kwa yule customer care "oooh kaja kujiunga na fursa eeh sawa ila tuongee taratibu jamani maana hii fursa ni hela nyingi sana na wakitusikia tutaporwa fedha"aliongea yule mdada na Rosemary huyo aliyekuja na Nico akakubaliana na yule Dada.
Mwishoni kabisa Nico aliambiwa aweke milioni moja akakubali na zile pesa zikaingizwa ndani na akaambiwa asubiri kwa dakika chache tu akiwa na Rosemary pale nje,ndani ya dakika 10 tu akaletewa mabulungutu ya fedha milioni 2 akafurahi sana akasema mambo si ndo hayo?akapanda dau akawa milioni 3 analetewa milioni 4 tena ,akaona isiwe tabu akatoa pesa zote milioni 5 pamoja na hiyo milioni 3 jumla aliyoipata pale jumla ikawa milioni 8 na Huyo rosemary naye akasema naye fursa hiyo isimpite akaweka ile milioni moja aloitoa bank ikawa jumla milioni 9.Nico akaahidiwa asubiri tena dakika kadhaa na ataletewa hapo hapo jumla milioni 20 na rosemary naye akaahidiwa milioni 2 maana aliweka milioni moja.
Ili kusubiri kwa kua ilikua pesa nyingi hiyo waliambiwa waingie ndani wasubirie pesa zao ndipo Nico na rosemary wakaingia ndani kusubiria pesa ziletwe maana zilikua zinachezeshwa kwa chumba cha ndani ya hiyo benki.Ndipo ghafla Rosemary akamwambia nico kuwa kabanwa na haja ndogo anatoka ajisaidie huku akimwachia Nico Mkoba wake."nishikie huu mkoba wangu una hela milioni 2 hizi huku (akafunua akamuonyesha)naenda kujisaidia dakika moja tu na kurudi tuje kuchukua magawio yetu maana hii fursa ni nzuri na ya kitajiri sana"...."sawa fanya haraka"alisema nico na rosemary akatoka haraka haraka hadi alipoegesha gari lake na kuwasha gari kimya kimya na kuondoka.
Nico alisubiria akicheka akijiona ashakua tajiri na akawaza jinsi atakavyopata milioni 20 kwa haraka kichwani aliwaza mengi sana akawa anaona jinsi atakavyokabidhiwa na jinsi atakavyofika nyumbani na kuanza maisha upya mazuri.Na aliwaza mengi sana pia kuhusu Rosemary na kumuona kama mkombozi mwaminifu maana aliacha hadi vitambulisho pale."ana hela sana huyu dada hii fursa imemfanya tajiri sana milioni moja kila siku daaah pesa mingi sana ana hela sana daaah hadi huu mkoba anatembea na milioni mbili sio mchezo na mimi leo naandika historia napokea milioni 20 zangu mie" aliwaza hayo nico akicheka kimoyomoyo kwa furaha.
Alisubiri lisaa lizima rosemary hakurudi.Alijshangaa lile jengo yupo peke yake na kwenda huko kwenye vyumba na kukuta patupu "inamaana mimi na rosemary tumedanganywa?hapana hatuwezi kudanganywa kirahisi hivyo maana hata rose mwenyewe kaweka pesa zake tena ngoja nimwiite labda kabanwa na haja chooni" aliwaza na kuongea mwenyewe akilini hayo nico.
Alitoka nje na kumtafuta Rosemary hakumuona akatizama gari ya rosemary pia haikuwepo akaanza kutafuta nyumba nzima lile jengo likawa kimyaaa hakuna mtu alikwenda hadi njiani kuulizia wapita njia kama wamemuona rosemary wakabaki wakimshangaa sana "hatumjui unamzungia nani hatujamuona yoyote huku njiani tanzania ina warosemary wapo maelfu unamzungumzia yupi umechanganyikiwa?"
Watu walimshangaa na kumjibu nico hivyo.Nico alizidi kuchanganyikiwa akaona hebu achukue zile pesa kwa mkoba wa rosemary alioachiwa ile kufungua hivi mungu wanguuu!!!!!!!!!!hazikua pesa yalikua ni mabulungutu ya karatasi zilizofanana na fedha zilizofungwa kwa "raba band" utadhani ni fedha kweli.Na vile vitambulisho vilikua ni feki,na vya uongo,na pale hapakua benki bali hilo jengo liliwahi kuwa bank zamani lakini miaka 20 iliyopita
Rosemary alikua tapeli wa kimataifa mwenye kujua ulaghai na utapeli wa kila aina.
Nico akawa amekwishatapeliwa milioni 5 ya mkopo mchana kweupe,na hakubakiwa na hata senti tano mfukoni akawa ameshachezewa kekundu. Nico hakuamini alichokiona, alihisi yupo ndotoni, alihisi labda ni utani tu alijikuta akiangua kilio umma ukajaa na kumshangaa na watu wakamwambia "kaka umelizwa matapeli ni wengi mjini.Nico ndipo alipata kichaa zaidi akajikuta anavua hadi suruali na kuanza kutembea uchi njiani huku akipiga mayowe ya msaada maana alikua keshachanganyikiwa.
Jee B
Nico atamwambia nini mkewe?
ITAENDELEA