Kwani ni lazima ukaishi kwa wabaguzi?waachieni nchi yao.mbona kuna nchi nyingi tu africa za kukufanya ukawa na maisha boraNipo Johannesburg,South Africa hapa mitaa ya Jeep street tumejifungia ndani toka saa 10 jioni wenye nchi yao wanapiga wageni,kuwaua na kuwachoma moto kama kuku.Wanapita mtaa kwa mtaa wakikuona mgeni hakuna kuuliza ni kipondo bila huruma.
Wanachoma matahiri barabarani na kuyachoma moto magari ya wageni wote kwenye nchi yao cha ajabu sasa wanaowapiga ni watu weusi wenzao na sio wazungu,wachina au waarabu mpaka unajiuliza hawa hawataki wageni au hawawataki wageni weusi.
Kesho natakiwa kurudi kwangu Cape Town maana nilikata ticket ya go & return hapa najiuliza nitaenda vipi uwanja wa ndege na kurudi kwangu Cape Town maana kule hakuna fujo za kijinga na kipuuzi kama hivi
J'burg niijuayo mimi kuna mobile court twenty four hours in almost part of the city. Na jiji hili lilivyo linazidi majiji mengi tu ya Ulaya (kwa uzuri na infrastructure). Police ni wa kumwaga,blacks, indians, whites etc kwa nini mleta mada asijisalimishe kwa hawa?
Nafikiri unyama unafanyika kwa wazamiaji.
Mi nimejifungia ndani hapa Cape Town, Hawa wasauz hawa noma
Mdau wewe Komaa hukono mkuu nina nyumba bongo ipo kibada ila huku ndio biashara zangu zilipochanganya na mke wangu pia ni msouth africa na watoto pia na tabia za watu wa nchi hii sio rahisi kumshawishi kwenda kuhishi nje ya nchi yake tena nchi yenyewe ikiwa kama Tanzania...ndio maana nimeng'ang'ania ndani ya nchi hii ili wanangu wakue kue nirudi nao nyumbani siwezi kumuachia huyu mwanamke hawa sio waleaji wazuri
Pole sana, endelea kujifungia humohumo mpaka uhakikishe vurugu zimeisha hiyo ticket wala isikusumbue uhai wako kwa sasa ndicho cha muhimu. tatizo serikali ya Zuma nayo ni legelege hivi watu wanauwaje wenzao kama vile hakuna polisi.
Kwa kuwa Unafanya biashara huko fikiria mara mbili je wakivamia na kupora biashara yako si watakuwa wamekurudisha nyuma sana. Kama vipi vurugu zikiisha funga virago urudi nyumbani kuliko kuishi kwa mashaka huko South.
nilifikiri unapanga kurudi bongo kumbe unakwenda cape town halafu unakusifia cape town utadhani haipo ndani ya South Africa. Kwa mtazamo kama huu wako mtakula kipondo na kuchinjwa sana. Maana unachukulia nchi ya watu kama yako. kauli ya PM ipo kazini WAPIGWE TU
S.A wamesahau walikotoka. Hawa hawa waafrica wenzao weusi ndo waliowasaidia kuwatoa gizani kwa makaburu leo hii ndo wamekuwa maadui
Msanga ngongele tatizo hakuna maghorofa kama huku mkuu
We mvivu wa kufikiri badala ya kurudi nchi yako Tanzania yenye amani na upendo pamoja na mafisadi kibao unalaumu kuchelewa kurudi Cape town!! inafaa wakuvunje miguu kabisa.