mzaramo
JF-Expert Member
- Sep 4, 2006
- 6,371
- 5,194
Nipo Johannesburg,South Africa hapa mitaa ya Jeep street tumejifungia ndani toka saa 10 jioni wenye nchi yao wanapiga wageni,kuwaua na kuwachoma moto kama kuku.Wanapita mtaa kwa mtaa wakikuona mgeni hakuna kuuliza ni kipondo bila huruma.
Wanachoma matahiri barabarani na kuyachoma moto magari ya wageni wote kwenye nchi yao cha ajabu sasa wanaowapiga ni watu weusi wenzao na sio wazungu,wachina au waarabu mpaka unajiuliza hawa hawataki wageni au hawawataki wageni weusi.
Kesho natakiwa kurudi kwangu Cape Town maana nilikata ticket ya go & return hapa najiuliza nitaenda vipi uwanja wa ndege na kurudi kwangu Cape Town maana kule hakuna fujo za kijinga na kipuuzi kama hivi
UPDATES
nashukuru mungu nimefika salama kwangu Cape Town na nina furaha kuiona tena familia yangu...Vuruga zimepungua kwa kiasi kikubwa mno serikali ya South Africa imeona aibu kwa hili na imejitaidi kudhibiti...Asanteni sana kwa dua zenu.Tuendelee kuomba mapigano yakome kabisa na yasirudi tena...Amen
Wanachoma matahiri barabarani na kuyachoma moto magari ya wageni wote kwenye nchi yao cha ajabu sasa wanaowapiga ni watu weusi wenzao na sio wazungu,wachina au waarabu mpaka unajiuliza hawa hawataki wageni au hawawataki wageni weusi.
Kesho natakiwa kurudi kwangu Cape Town maana nilikata ticket ya go & return hapa najiuliza nitaenda vipi uwanja wa ndege na kurudi kwangu Cape Town maana kule hakuna fujo za kijinga na kipuuzi kama hivi
UPDATES
nashukuru mungu nimefika salama kwangu Cape Town na nina furaha kuiona tena familia yangu...Vuruga zimepungua kwa kiasi kikubwa mno serikali ya South Africa imeona aibu kwa hili na imejitaidi kudhibiti...Asanteni sana kwa dua zenu.Tuendelee kuomba mapigano yakome kabisa na yasirudi tena...Amen