Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

sasa kipi kilichokufanya utake kuzuwa kuwa nimetafsiri maana ya system? na ilhali unajuwa kuwa mimi sina hiyo tafsiri? jee, unaijuwa system ni nini?

Swali lako kuwa unaijua badala ya unazijua system ndilo linakufunga hapa. Hakuna system moja duniani. Kuna system nyingi sana na kila watu na jamii na profesion wana tafsiri yao ya neno system.

Dakitari anatafsiri yake ya neno system kama vile mchimba mitaro alivyo na tafsiri yake ya neno mitaro.

Na hiki ndicho nilikukosoa kwenye msisitizo wako wa kuijua system (umoja):


Mwafrika wa kike said:
Ha ha ha ha haha,

Naona kuna tafsiri nyingi na matumizi mengi sana ya neno ukweli hasa kutoka kwa mchangiaji ambaye anasisitiza kuwa kuna tafsiri moja tu ya neno system!
 
Swali lako kuwa unaijua badala ya unazijua system ndilo linakufunga hapa. Hakuna system moja duniani. Kuna system nyingi sana na kila watu na jamii na profesion wana tafsiri yao ya neno system.

Dakitari anatafsiri yake ya neno system kama vile mchimba mitaro alivyo na tafsiri yake ya neno mitaro.

Na hiki ndicho nilikukosoa kwenye msisitizo wako wa kuijua system (umoja):
eeehhhh, mwanamke wee hutupwi? (sijui kama ki-mwambao utakipata).

kwa kifupi hii ni forum ya "jukwaa la siasa Tanzania" sasa hizo system zingine sijuwi za nini, ningekuwa kule kwenye "zilipendwa" ningekuwa kwenye music system, au siyo?
au huijuwi system ni nini?
 
eeehhhh, mwanamke wee hutupwi? (sijui kama ki-mwambao utakipata).

kwa kifupi hii ni forum ya "jukwaa la siasa Tanzania" sasa hizo system zingine sijuwi za nini, ningekuwa kule kwenye "zilipendwa" ningekuwa kwenye music system, au siyo?
au huijuwi system ni nini?

eehhhhheee mwanamke/mwanamme wee kumbe unatupwa?

Hata kwenye siasa kuna system zaidi ya moja kama ulikuwa hujui
 
eehhhhheee mwanamke/mwanamme wee kumbe unatupwa?

Hata kwenye siasa kuna system zaidi ya moja kama ulikuwa hujui
Haya mwanamke wa kiafrika nielimishe, halafu ukimaliza urudi kwenye mada. Au huijuwi system ni nini?
 
Haya mwanamke wa kiafrika nielimishe, halafu ukimaliza urudi kwenye mada. Au huijuwi system ni nini?

Hujaona kuwa wewe ndio umetoka kwenye mada hata umesahau ulianzisha hii thread kwa nia gani na sasa umebaki kujigonga na maana ya system ambayo very likely hauna a clear single definition?

Nitakupa muda wa kutosha ili urudi kwenye mada uliyoanzisha hapa!
 
Hakuna upinzani Tanzania, ni uwongo tuu, "viongozi wote wa upinzani ni system" kwa maelezo zaidi soma mwanzo wa thread. Mwanamke wa kiafrika kanipagawisha. au huijuwi system ni nini?
 
Zomba,
Sote tunajua system ni nini. Lakini kumbuka system is not infinite. Hata kama unaamini vyama vya upinzani vilianzishwa na system, sidhani system ina uwezo wa kuendelea kuvi"control" ad infinitum.
 
Wana JF
Huu ni mjadala mzuri, ni vizuri kama tukaelimishana vizuri kuhusu hili jambo. Pamoja na kuwa Zomba ameweka picha ya jumla, lakini ana ukweli ndani yake.
Tanzania mpka leo ukiwa kwenye chama cha upinzani unaonekana kama deviant au outcast, na hii aliianzisha Nyerere kwa kumfanya hivyo Zubere Mtemvu. Na Kama mkikumbuka CCM ilikubali kwa shingo upande Tanzania kuwepo opposition, ni kama Nyerere aliwashinikiza. Na ukiangalia wengi walioanzisha vyama vya upinzani mwanzo( Mapalalas, Marandos, Jafu etc etc utaona walikuwa ni maofisa wa usalama wa taifa. Na utaona kuwa wengine walifanya kazi nzuri sana kudestabilize "opposition". Hii inawafanya baadhi ya watu kuona kama hawa jamaa wanaojiita wapinza tuwatilie shaka.
Kila siku nikijiuliza kwa nini pamoja na fyongo zote inazofanya CCM, wananchi hawashituki au kwanini "opposition" haiwashtui watanzania ili waone hali halisi na kutaka alternative?
Tuliona Mrema akijaribu hivyo, lakini baada ya kuangalia kwa undani ikaja kuonekana kuwa haikuwa opposition, ilikuwa ni watu ndani ya serikali waliokuwa wamechoshwa na ujinga, waliamua tu kutumia mdomo wa Mrema.
Unaona hata hili sakata lote la BOT unaona kama ni initiatives za watu ndani ya Serikali waliochoshwa na wizi, ndio wakaamua kutumia mdomo wa wapinzani kusema, lakini bado siamini kama Slaa as a person aliweza kutafuta issue zote hizo. Wabunge wengi wa CCM wanaonekana kuwa hawakujua hili na wengine walijaribu hata kulitetea kwa jina la Mwalimu.
Lakini wajuvi ndani ya serikali( sio oppostion)wenye uchungu na Tanzania waliamua kuvurumua hayo mambo, na kuwatumia wapinzani kufanya mambo. Sasa the question comes, kama wapinzani ni watu wa kutumiwa, can we really trust them to rule or lead us? Kwanini chama cha mapunduzi kisisafishwe ili kiendelee?
Ukiangalia vyama vingi ni kama vyama vya kutoa mabomu tu, na havituoneshi a real alternative tunayoitaka, ya kuleta mabadiliko Tanzania. Hii ndio inatusumbua wabongo, watanzania wako tayari lakini bado hakuna wakuwapeleka wanakotaka!
 
Mimi naona kwamba upinzani Tanzania is hampered by a number of things lakini hii argument ya kuwa ilianzishwa na system naona kama si sababu ya kwanza. Naomba muda nirudi na baadhi ya sababu hizi zinazokwaza upinzani Tanzania.
 
Mwafrika wa kike, ukipenda usipende huo ndio ukweli, au huijuwi system ni nini?

Kuna watu wana mawazo ya kizandiki kuliko SISIEMU yenyewe.Watu hawa ni hatari kuliko systemu tupambanayo kwa sababu ni watu wa kujikomba kwa kila hali, hata kama faida yao ni kuchakaza soli za viatu na kukausha sauti za makoo yao kwa kushangilia upuuzi wenye kuwadharirisha utu wao wenyewe.

Kingine kibaya zaidi ni ving'ang'anizi wa hoja zisizo weza simama kwa miguu yake mpaka ziwe juu ya hoja nyingine za kufikirika.
Kuthibitisha jambo kutokana na source moja tena ya mtu ambaye ndoto yake ilikufa kabla haijaotwa ni Uzandiki na Uhabithi mkubwa na pengine ni kujikana utu wako mwenyewe.
Kuna watu wanajipendekeza kwenye System kana kwamba mwisho wa Uhuni wao wa kisiasa uko sambamba na kiama.Katika maana kwamba maovu ya SISIEMU ni kama Natural Principle( Gravitation Force, Magnetism and Density) ambazo ni ujuha kutaka kwenda kinyume nazo.

Wakati ni kweli kwamba kuna maofisa kibao Usalama wa SISIEMU ndani ya vyama vya upinzani;pia kwamba SISIEMU wanatumia fedha walizo iba BOT kununua na wapinzani na kudhoofisha juhudi zao, si kweli kwamba vyama hivi vimeundwa na SISIEMU au serikali ya SISIEMU. Sisi wengine tulikuwapo toka enzi za akina James Mapalala wakieneza propaganda za mageuzi kinyume na sheria za serikali ya SISIEMU tunajua kianachoendelea.
Ukiona mtu ambaye kalelewa ndani ya Thermos( Uniform Tempeture and Pressure) anasimama na kudhihaki mapambano ya halisi ya kujikomboa Kiuchumi na kifikra ili tu joto la Thermos inamuhifadhi lisibadirike, ujue ni dalili moja kubwa kwamba ameng'amua kwamba joto la maji ndani ya Thermos linapungua na maji yameanza geuka barafu. Hakuna Shwari, sasa anatapatapa.

Sishangai, utamaduni wa kusema uongo na kujidanganya ni hulka ya SISIEMU na wanachama wake wengi. Ndani ya miezi 12 iliyo pita SISIEMU na Vikaragosi wake wamejidanganya zaidi ya mara 1000 katika masuala kibao ambayo sasa hivi wanajaribu kujitoa kimaso maso kwa kupaka rangi Upumbavu wa makanusho yao kwa mafanikio haba au bila mafanikio kabisa.

Madai haya kwamba Upinzani Tanzania ni uongo mtupu yanaweza tolewa na mtu ambaye yuko kwenye kada ya juu ya SISIEMU, ni mtoto wa kiongozi wa SISIEMU, ni mke wa kiongozi wa SISIEMU au Kimada ambaye anafaidika moja kwa moja na Uharamia wa $133 Bill.
Lakini maneno haya kama yanasemwa na mwanachama mtiifu wa SISIEMU ambaye anaiona SISIEMU kwenye Fremu ya 1977, mwanachama huyu inabidi azinduliwe kutoka kwenye usingizi ulo mzito mithili ya ule wa pono na kuambiwa:

" Hi Mr Pono mkia wako umeshika moto unateketea, tena unateketezwa kwa moto wa hila za pono wenzako."
 
Zomba ana point, ila kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo juu ame generalise.
 
Mheshimiwa Ndugu Zomba, Nimesoma wakala wako si chini ya mara moja. Pia nimesoma mawazo ya wengine katika mada hii, Kadhalika nimepata kiasi cha muda wa kutafakari yote katika pande mbili za mjadala yaani upande wako na ule unaopingana nawe. Yangu ni machache tu kwako.

Siwezi kuyakubali wala kuyakataa yako kwa kuwa sina ushahidi. Na katika uliyoyazungumza sioni popote unapoyatolea ushahidi. Hali kadhalika siuoni ushahidi unaotoka kwao pia. Ili mradi, mtaniwia,
mnabishana kama wototo wadogo.

Mimi nafikiri, ungetoa maelezo yako, kisha ukayatolea ushahidi na kuyapa uzito maelezo hayo na mwisho ungetueleza nini cha kufanya ili tuweze kuupata huo upinzani/ushindani wa kisiasa. Labda cha ziada, kama itawezekana utueleze jinsi ya kuuendesha upinzani huo na labda utupe majina ya akina nani wanastahili kuwa viongozi wa upinzani huo.

Sisi wengine, pengine hatujui system ni nini na watu gani wamo au hawamo katika system yenyewe.
 
Vyama vyoooote vya upinzani Tanzania "vilianzishwa na system", na hii niliambiwa na rafiki yangu aliyekuwa mwenyekiti wa NCCR kabla ya mrema, mzee Kassim Maguto (M/Mungu amsamehe dhambi zake na amuweke pema peponi, Amin.).

Vyama ambavyo havikuwa kwenye system vilishindwishwa kuanza, havikusajiliwa mpaka leo hii.

kwa kifupi, upinzani kwa sasa hakuna kabisa Tanzania, kuna kina sisi huku nje tunaeshangilia siasa kama mpira tuu, tukijuwa nini kinachoendelea na kuna wengi sana wenye kupandisha hasira na ghadhabu, wasiojuwa nini kinaendelea.

Narudia, upinzani kwa sasa hakuna Tanzania. Si CUF, si Chadema, Si NCCR wala si kingine chochote chenye usajili ambacho hakina viongozi ambao wapo kwenye system.

kwa kifupi, si mbowe, si lipumba, si sharif, si mrema, wote hao ni system (according to Marehem Kassim Maguto) ambae na yeye mwenyewe alikiri kuwa ni system wa miaka mingi na alinipa siri kuwa aliitwa Ikulu kuelekezwa waanzishe vyama vya upinzani na wakawa wanafundishwa kila kukicha ni nini cha kufanya na funds zote zikatoka huko, kwa vyama vyote vilivyosajiliwa.

kuna baadhi ya wanachama (wengi tuu) ambao masikini hawalijuwi hili, wapo kwa nia moja ya upinzani na wapo tayari kufa lakini masikini roho zao, laiti wangelijuwa hili nadhani wasingekuwa na hamu hata ya siasa.

Enyi kina Lipumba, Sharifu, Mbowe na Mrema wacheni dhulma hii, haya mnayajuwa lakini mtasababisha watu wauwane bure wakati nyinyi mnajuwa nini mnakifanya. Hebu rudini kwa mola wenu kabla ya watu wasiyoyajuwa haya hawajaanza kughadhibika na kumwaga damu.

Na hayo yote yalipangwa na kuanzishwa na nyerere, ndio maana ufisadi haufi Tanzania na aliyeuanzisha huo ufisadi ni nyerere.

Naapa kuwa hayo yote niliyoyasema ni kweli tupu.



Jee, hamjuwi system ni nini?

Mie sielewi point yako ipo wapi?Unamaanisha wananchi wasiviunge mkono vyama vya upinzani kwa sababu vyote vipo kwenye system?Je njia mbadala ni ipi?Kwa nini usianzishe chama chako kisicho kwenye system ili utuonyeshe mfano?
 
Ndg ZOMBA maana yako ni general mno.LABDA mimi ndo ninataka nikuelewe tofauti ila kama sivyo, basi tukubaliane wote kuwa ni kweli CCM unayoiita wewe system ndo ilianzisha vyama vya upinzani kwa matinki moja kuwa wao hao CCM ndo walikubali mfumo wa vyama vingi nchini.

Ukisema Tanzania hakuna Upinzani unakosea sana. Nakumbuka mwaka 2005 wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu ilivuma kuwa Mrema ni pandikizi la CCM.Sawa watu wakakubali,Lakini wakati Mrema akiwa Singida pale jengo la Utamaduni akikampeni alisema kuwa,nanukuu"Watu wananituhumu mimi kuwa ni mwana CCM,sawa nakubali,sasa ndg wana-CCM wenzangu naombeni kura zenu.Wakati huu msimpe kura Mwana-CCM Kikwete bali nipeni mimi Mwana CCM Mrema" Mwisho wa kunukuu.Swali,Je kwa nini hawakumpa kura Mrema kama kweli ni CCM mwenzao???

Unaedai kuwa Tanzania hakuna Upinzani una maana gani hasa zaidi ya hiyo ya kuanzishwa na system??? Hebu tufikirie mwaka kama Maalim Seif au Mbowe wangeshinda wakati wa Uchaguzi tungesema hayo maneno leo??Au tufikirie kama mwaka 2010 tukimchagua mtu atakae simama na mgombea wa CCM na akashinda,tutasema hakuna upinzani au tumechagua CCM mwenzao????
Mimi nafikiri wasio na Upinzani wa kweli ni sisi wananchi.Na kama unabisha chaguzi zijazo tuonyeshe Upinzani wa kweli kwa kuchagua wagombea wa upinzani uone kama kuna upinzani halisi au la.

Kuhusu CCM kuwa na watu wa Usalama kwenye vyama vya Upinzani,hilo ni jambo la kawaida ktk Siasa sawasa na Vyama vya upinzani vilivyo na watu wao (Sijui tuwaite Usalama au la)ndani ya CCM.Huwezi amini ila ukweli ni kuwa Vyama Vya Upinzani vina watu wao na wako makini sana ndani ya CCM na ndani ya Serikali.Kusingekuwa na watu wao basi siri nyeti na za muhimu kuhusu maamuzi ya CCM ZISINGEKUWA ZINAVUJA.
©Majita Kunashida!!!!!
 
Inawezekana kweli kuwa baadhi ya waasisi wa vyama vya upinzani walikuwa mamluki wa CCM. Kuna baadhi ya watu hao wanaojulikana wanaoweza kutajwa kuwa kweli walikuwa mamluki.


Hata hivyo sikubaliani kabisa na dhana ya kuwa vyama vyote vya upinzani bado ni vya mamluki. Miaka takriban 15 tangu tunzishe mfumo wa vyama vingi, kumekuwa na mageuzi ya namna mbalimbali kwenye vyama vya upinzani na kwa leo hii vimebaki na mamluki wachache sana kama wapo. Wengi wa viongozi wa upinzani wamekuwa ni mwiba kooni mwa serikali kiasi ambacho hawawezi kufanya hivyo kama kweli ni mamluki. Mifano michache ya Zitto kuibua mzengewe wa Buzwagi, Slaa kuibua mzengwe wa BOT, na minginiyeo kadhaa ianyoendelea kweli kunaonyesha kuwa kuna upinzani. Tatizo letu ni kuwa mfumo tuliona nao unabana nafasi kwa upinzani kukua. Kwa hiyo mara nyingi upinzani wetu ni goi goi ingawa upo kweli kweli; hilo si kosa la upinzani bali ni kosa la kikatiba litokanalo na mfumo wetu.
 
Ndugu zomba ushauri wako ni upi? Tuanzishe vyama vipya vya upinzani au CCM idumuuuuuu!!!!!! Maana kwa hoja yako hata hivyo vitaingiliwa na the so called system!!!!
 
Dhana ya ni nani alishiriki kuanzisha vyama hivyo vya upinzani kwa sasa haina mantiki yeyote,wapo wakina Kabouru na Lamwai mbona wamerudi CCM? lakini wapo wakina Slaa na wengine wengi wapo Upinzani sasa hivi na wayafanyayo tunayaona.Pengine Zomba angetueleza kiwango cha upinzani kiko chini tofauti na ATAKAVYO YEYE ningemuelewa lakini sio kusema Hakuna Upinzani ni uongo mtupu.Zomba utufahamishe vema ,upinzani uutakao ni upi?Viongozi kuwahamasisha wananchi kuandamana na mapanga na rungu barabarani huku wakichoma matairi na kuvunja maduka? Hivi huoni kuwa mapambano ya hoja toka kwa wapinzani hao hao unaowabeza yalivyo itikisa serikali ya CCM? Tatizo ni kuwa serikali hii haina SONI,ingekuwa zile zilizostarabika mshikemshike wake ungeuona.
 
Mtu ambaye alikuwa mamluki kibaraka wa serikali ya mafisadi aliyejifanya mpinzani ni huyu jamaa anaitwa Mabere Marando
 
Back
Top Bottom