Mheshimiwa Ndugu Zomba, Nimesoma wakala wako si chini ya mara moja. Pia nimesoma mawazo ya wengine katika mada hii, Kadhalika nimepata kiasi cha muda wa kutafakari yote katika pande mbili za mjadala yaani upande wako na ule unaopingana nawe. Yangu ni machache tu kwako.
Siwezi kuyakubali wala kuyakataa yako kwa kuwa sina ushahidi. Na katika uliyoyazungumza sioni popote unapoyatolea ushahidi. Hali kadhalika siuoni ushahidi unaotoka kwao pia. Ili mradi, mtaniwia,
mnabishana kama wototo wadogo.
Mimi nafikiri, ungetoa maelezo yako, kisha ukayatolea ushahidi na kuyapa uzito maelezo hayo na mwisho ungetueleza nini cha kufanya ili tuweze kuupata huo upinzani/ushindani wa kisiasa. Labda cha ziada, kama itawezekana utueleze jinsi ya kuuendesha upinzani huo na labda utupe majina ya akina nani wanastahili kuwa viongozi wa upinzani huo.
Sisi wengine, pengine hatujui system ni nini na watu gani wamo au hawamo katika system yenyewe.
Ahsante kwa wazo lako zuri, ushahidi wa mwanzo:
1) sina sababu ya kutia maneno yangu mdomoni mwa maiti (Mzee Kassim Maguto)(yaani sina sababu ya kumzulia uwongo) aliyekuwa rafiki yangu aliyeweza kunieleza hayo na mengine mengi tuu, ambayo yakifika wakati wake nitayaanika, sio mahala pake hapa.
2) sina sababu ya kuvichukia vyama vya upinzani ambavyo ndani yake kuna wanachama ambao kwa dhati kabisa wanataka mabadiliko ya kweli na wana-upinzani wa kweli, lakini wanarudishwa nyuma na hao viongozi niliowataja.
3) Ninayatowa haya kwa kuhofia yasitufike kama ya Kenya, kwani ni wengi walipomchaguwa Kibaki walijuwa kuwa ni mpinzani wa kweli, lakini masikini roho zao, damu inamwagika huko Kenya, simply kwa sababu Kibaki alikuwa kwenye system ya Kanu na aliweza kuwahadaa "wapinzani" na kupokeya nchi kwa urahisi uchaguzi wa mwanzo, nikimaanisha kuwa bila damu kumwagika. Sasa hivi baada ya wengi kujuwa, nini kilijiri, Kanu wapo nyuma yake wanamsaidia na watu wasio na hatia wanakufa bila sababu ya maana, hawataki system ibadilike, ndio sababu ya kuuwana sasa hivi. Hapo mwanzo ingawa ilionyesha kuwa ni mpinzani mkuu wa kanu, lakini kwa kifupi haikuwa hivyo na ndio maana haikumwagika damu na kanu wakaachiya madaraka kwa urahisi wakijuwa kuwa system inaendelea (of course si wana Kanu wote walijuwa hilo, ni wale viongozi tuu).
4) Jamani hamuoni, jinsi sefu sharifu anvyowadanganya wanachama wake? anawafanya kama vifaranga vya kuku, mtanyonya kesho, mtanyonya kesho, mpaka wanazeeka. Huo tuu, ni ushahidi tosha kuwa huyu muheshimiwa ni system.
5) Hamkuona ya viongozi wengi walioachia ngazi vyama vya upinzani, wengi wanarudi sisiem na wanaula kama kawaida.
6) Hamkuyaona ya Mrema, kila chama anachohamia anakidhoofisha mpaka kinakuwa hakina nguvu ya kupinga chochote, kama mrema si system ni nini?
7)Hamuyaoni ya lipumba, mara tuu baada ya uchaguzi, wakati alitowa ahadi kibao za kubainisha "siri za wizi wa kura", kachoropoka pyuu na kwa sasa yupo majuuuu, habari za upinzani anazitazama kwenye JF tuu, anangoja uchaguzi ujao ufike, aje kufanya kazi yake anayoijuwa vizuri. Kwa nini asikae nchini akakiimarisha chama chake? au CUF hawawezi kumlipa? au nchi hii hawezi kutowa mchango wa taaluma yake hata akiwa nje ya chama tawala? utakuta no, si hivyo bali ni system ndio anayoifanyia kazi na ndio inayomruhusu nini afanye na nini asifanye.
Kwa sasa naona hayo machache yanatosha na nina uhakika kuna watakaonisaidia kwa mengine nisoyajuwa, kwani haiwezekani binadamu nikajuwa kila kitu. Kama vile wengi wetu humu hatujuwi system ni nini, Jee unaijuwa system ni nini?