Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Mkuu jmushi1,

Upinzani umekuwa ushetani tena !

Ni ushetani kama ni wa kuwagawanya wananchi na huku hakuna kinachobadilika zaidi ya wanasiasa kununuliwa na kupoteza muda na pesa za walipa kodi.
Sasa kama huo si ushetani ni nini?
Kwani hata shetani mwenyewe si alianzisha chama cha upinzani huko mbinguni kwa mujibu wa Bible?
 
Taarifa ni kuwa kimbunga IKE katibua taratibu zote za kufungua tawi la CCM missouri!!
 
Imebidi nililete swalia hili kwenu wanandugu.
Kuna baadhi ya majina ya wana CCM yanatajwa tatwa sana.
Majina kama Dr. Salim Ahmed Salim, Prof. Mark Mwandosya na mengine.

Ingawa chama cha watu hawa (wanaotajwa tajwa) kinatia kichefu chefu lakini inaonekana kama jamii ina matumaini fulani na hawa watu.

Pengine wapo watu ndani ya CCM hawapendi yanayofanywa na chama chao lakini ndio hivyo hawana jinsi kwani wakikipinga watavuliwa uanachama na hivyo kupoteza ubunge na Uwaziri wao.

Pamoja na kwamba CCM imejijengea mizizi tena iliyokomaa lakini lazma ipo siku watatokea mashujaa wa kukisambaratisha chama hiki kinachotetea na kulinda mafisadi.

Swali la msingi ni Je, watu wa kukiteketeza Chama Cha Mafisadi watajitokeza kutoka humo humo ndani ya CCM? Pengine wakijitoa na kuanzisha chama chao au kuunganisha nguvu zao na wapinzani watafanikisha kukipoteza madarakani chama hiki ambacho kimelewa madaraka na kinaamua kufanya chochote kinachotaka kwa maslahi ya wachache?
 
Majina kama Dr. Salim Ahmed Salim, Prof. Mark Mwandosya na mengine.


Mkuu hawa mbona hatujawasikia kabisa kwenye ishu za Nape na Richimonduli? Wako upande gani?

Mbona hawajasema kitu publicly kuhusu lists of shame? Sasa watatusaidia vipi hawa Tanzania ya leo inayomezwa na mafisadi wakati wanyonge tunadhulumiwa? Wako wapi sasa wakati nchi inaliwa na wachache mafisadi?
 
---I'm not so sure na jinsi vile Ilani ya uchaguzi inavyosema kuhusiana na funding za vyama vya siasa.

---Lakini naamini swala la funding ya vyama hapa nchini bado lina matatizo.

---Mirija ya kunyonyea hela za EPA ambazo zinaaminika kufanikisha uchaguzi wa 2005 kwa upande wa CCM hivi sasa imesiribwa. Mianya mingine mingi pia imenyauka.

---Naamini CCM kuona mianya yao ya funding kwa 2010 inanyauka wameanzisha kampeni kabambe ya kufungua matawi nje ya nchi.

---Kampeni za uchaguzi hutumia pesa nyingi, hamna donor hata mmoja awe tajiri kiasi gani anayeweza kumudu.

---Wapinzani bado wamelala katika hili, wakitegemea ruzuku kutoka kwenye fungu la mgao wa uchaguzi mkuu.

---CCM itaweza kukusanya mfuko uliotuna zaidi kutoka kwa wanachama wake nje ya nchi.

---Pesa nyingi kwa ajili ya uchaguzi ni kigezo kikubwa cha kushinda uchaguzi wowote. Tumeyaona kwa Obama na Clinton. Hivyo CCM watakuwa na the upper hand saa kenda ikikaribia.

---Wapinzani watashindwa (sad-ugly prospect - but truth). Matokeo yatapingwa, kule kisiwani ndiyo kabisaa - fujo zinatabirika kutokea. CUF watashinda ila Katiba itajichanganya jinsi ya kuhandle ushindi huo.

---Serikali ya Mseto itaundwa. Wapinzani na Chama tawala kushare madaraka.

---Tanzania itaongezeka kwenye list ya powersharing deals in Africa.

---Na hiyo ndiyo itakuwa hatima ya Upinzani. (TANU inaweza kurudi!!!!!!!)
 
Swali la msingi ni Je, watu wa kukiteketeza Chama Cha Mafisadi watajitokeza kutoka humo humo ndani ya CCM? Pengine wakijitoa na kuanzisha chama chao au kuunganisha nguvu zao na wapinzani watafanikisha kukipoteza madarakani chama hiki ambacho kimelewa madaraka na kinaamua kufanya chochote kinachotaka kwa maslahi ya wachache?

Vipi wakuu hii ndoto ya Mwalimu, inaonekana iko mbali sana yaani ya CCM kujimaliza kutokea ndani yake, sasa tunafanya nini wananchi tuliochoshwa?
 
Nafahamu kuwa Dr. Slaa, Zitto na Wanasiasa wengine wamo humu jamvini. Je, tunaweza kupata maoni yenu na ya wadau wengine ni namna gani vyama vyote vya upinzanini vinaweza kushiriki majadiliano ya kuviunganisha na kuunda chama kimoja?

Ni vizuri kuwa na chama kimoja na chenye nguvu kukabiliana na CCM. Lakini hili litawezekana tu kama ubinafsi utawekwa pembeni na maslahi ya Taifa yatawekwa mbele.

Tulijadili kwa undani bila na kupendekeza ni vipi tulifanikishe hili.
 
Nafahamu kuwa Dr. Slaa, Zitto na Wanasiasa wengine wamo humu jamvini. Je, tunaweza kupata maoni yenu na ya wadau wengine ni namna gani vyama vyote vya upinzanini vinaweza kushiriki majadiliano ya kuviunganisha na kuunda chama kimoja?

Ni vizuri kuwa na chama kimoja na chenye nguvu kukabiliana na CCM. Lakini hili litawezekana tu kama ubinafsi utawekwa pembeni na maslahi ya Taifa yatawekwa mbele.

Tulijadili kwa undani bila na kupendekeza ni vipi tulifanikishe hili.


Baada ya kumerge hiyo vyama kila chama kitataka mgombea urais atoke kwenye chama chake original. They are fond of urais rather than maslahi ya wananchi kwa ujumla. Labda utupe experience za utokako.
 
Baada ya kumerge hiyo vyama kila chama kitataka mgombea urais atoke kwenye chama chake original. They are fond of urais rather than maslahi ya wananchi kwa ujumla. Labda utupe experience za utokako.


Mama, nimerudi sasa na nitakuwepo kwa muda. Nahitaji tusaidiane tupate maoni ya hawa viongozi wote wa kisiasa ni nini wanafikiri kuhusu hii hoja ya kuungana. Tukishapata mawazo yao basi tutajadili ni vipi tuwe na mjadala ambao pia utahusisha kuwaelemisha wanachama wao wajue faida za muungano.

Asiyetaka kuungana kwa sababu za maslahi binafsi ni lazima apigwe stop. Na naomba moto uwashwe hapa JF wa kuwaelimisha mpaka aelewe au aachie ngazi. Time for change is now. 2010 si mbali if we are all serious.

Hoja hapa ni kutaka kuwa na ushindani wa nguvu ambao tunatarajia utaleta mabadiliko ya kweli kwa kila sekta.
 
Wakuu salaam,
Hongera kwa sikukuu X Max na mwaka mpya.
Nina tatizo na huu mgawanyiko wa vyama vya upinzani.
Siku za karibuni wasiasa wa vyama vya upinzani {CHADEMA,CUF,TLP na NCCR MAGEUZI} walianza kutupa matumaini kwa kuunganisha nguvu zao dhidi ya CCM lakini umoja wao unazidi kuingia majaribuni kadri siku zinavyosonga mbele.

Uchaguzi wa Tarime pengine unaweza ukawa ndiyo chanzo cha kusambaratika kwa ushirikiano wa vyama vya upinzani.Nilitegemea baada ya uchaguzi viongozi wakuu wa vyama vya upinzani wangekaa na kuangalia wapi walipokosea na kusahihisha makosa lakini kwa mshangao wa wengi hilo halikufanyika !.Baada ya uchaguzi wa Tarime kila chama kinafanya mambo yake kivyake.
Nasikitika sana jinsi hali hii mbaya inavyoachiwa iendelee kuota mizizi.Tumesikia CUF imetumika kumwekea pingamizi mgombea wa CHADEMA huko Mbeya.Uchaguzi wa udiwani Arusha CHADEMA wamemnyakua dakika za mwisho mgombea udiwani kupitia TLP.
Wapenda mabadiko tumebaki tunasikitika kwakuelewa kama hali itaendelea kuwa hivi mwaka 2010 CCM kitaendelea kupeta.
Natoa mwito kwa viongozi wote wa vyama vya upinzani kukaa meza moja kutatua matatizo yao ndani.
Viongozi wa vyama vya upinzania lazima waelewe kwamba CCM imetapakaa kila kona ya Tanzania,ina matawi,ina rasilimali watu,ina vitega uchumi vingi hata kama vingine wametuibia,ina mbinu halali na chafu,ina dola, mwisho ina tume ya uchaguzi.
Bila umoja wa wapinzani hakuna namna mtakavyoweza kuingiza walau wabunge 100 mwaka 2010.Sitapennda kusikia viongozi wa upinzani wakija na excuse kibao mwaka 2010.
 
‘Ndoa' ya wapinzani inayumba -CUF
Chama cha Wananchi (CUF), kimesema ushirikiano wa vyama vinne vya upinzani, unayumba kutokana na viongozi wakuu wa vyama hivyo vya TLP, Chadema, NCCR-Mageuzi na chama hicho, kukacha mikutano ya pamoja.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara, Juma Duni Haji aliyasema hayo alipozungumzia kampeni za chama hicho zilizotarajia kuanza jana kuwania nafasi ya ubunge katika Jimbo la Mbeya Vijijini pamoja na masuala mengine yahusuyo muungano wa vyama vya upinzani.

Duni alisema Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba mara kwa mara amekuwa akiwaita viongozi wa vyama vingine kwa simu na barua ili wakutane, lakini wamekuwa wakishindwa kuhudhuria mikutano bila sababu za msingi na kusababisha vyama hivyo kukosa mwelekeo.

Alisema bila ya vyama vya upinzani kuungana, kamwe hawawezi kukiangusha Chama Cha Mapinduzi. "Siafu na sisimizi ili waweze kumwangusha tembo ni lazima waungane, wakati sisimizi akiingia kwenye mkonga wa tembo siafu anauma tumboni hadi tembo ataanguka," alisema Duni.

Aidha, Duni alipinga hoja ya Chadema iliyotaka wagombea wa vyama vilivyojitokeza katika uchaguzi huo wakutanishwe na kumpata anayekubalika kwa madai kuwa tamko la muungano wa vyama hivyo halisemi hivyo na kwamba wao walikiandikia barua chama hicho ili kiwaachie jimbo hilo.

Alisema CUF iliwaachia Chadema katika majimbo mbalimbali likiwamo Tarime mkoani Mara, lakini wanashangazwa na Chadema kutaka wakutane ili kumpata mgombea anayekubalika wakati wao hawakuwawekea masharti huko nyuma.

Katika hatua nyingine, Duni alisema wanaingia katika kinyang'anyiro cha kuwania ubunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini wakiwa hawana imani na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutokana na kuibiwa kura katika chaguzi zilizopita.

Alidai katika uchaguzi wa mwaka 2005, mgombea wao, Amina Ahmed alishinda lakini kutokana na wizi waliofanyiwa, marehemu Richard Nyaulawa alionekana kuibuka na ushindi na kumshinda mgombea wao. "Zanzibar tumeshinda mara tatu, lakini mara zote tumenyang'anywa na kila mtu anajua hilo, tutaendelea kupigania haki hadi mwisho," alidai Duni.

Alidai licha ya kuibiwa kura katika chaguzi mbalimbali wataendelea kushiriki katika chaguzi zinazofanyika nchini kwa kuwa lengo la chama hicho ni kuwakomboa wananchi kutoka katika fikra za kikoloni alizodai zimepandikizwa na CCM.

Hata hivyo wakati CUF ikidai kuwa iliiandikia barua Chadema, Mkurugenzi wa Vijana Taifa wa Chadema, John Mnyika alisema CUF iliandika barua ya kuomba kuachiwa nafasi katika kinyang'anyiro hicho na hawakuomba mazungumzo. Akizungumzia suala la Tarime, alisema CUF yenyewe haikusimamisha mgombea na kwamba NCCR-Mageuzi haikuwaunga mkono.

Katika hatua nyingine, hatima ya wagombea wa CCM, Chadema na DP waliowekewa pingamizi kutokana na kukiuka taratibu mbalimbali kisheria katika ujazaji wa fomu za kuwania kuteuliwa kuwania ubunge, inatarajiwa kujulikana leo.

Hadi kufikia jana majira ya saa 10 alasiri, wagombea wa vyama vilivyokuwa vimewekewa pingamizi walikuwa tayari wamerudishiwa majibu ya pingamizi walizowekewa na wagombea wenzao. Hata hivyo, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Juliana Malange kupitia kwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Damson Ntangu, aliwaeleza wanahabari saa 11:20 kuwa bado anapitia majibu yaliyotolewa na wagombea.

"Msimamizi amesema niwaambie kuwa bado anapitia maelezo ya wagombea, alitegemea atatoa maamuzi leo, lakini hatafanya hivyo na badala yake atawapa taarifa kesho saa tatu asubuhi," alisema Nthangu na kuongeza kuwa waandishi wanaweza kupata majibu kwa njia mbili, moja kwa kuwasiliana na wagombea wenyewe au kusubiri hadi kesho asubuhi.

‘HabariLeo' ilipata nakala ya majibu ya mgombea wa Chadema, Sambwee Shitambala aliyekuwa anajibu pingamizi alizowekewa na vyama vya CUF na CCM; la kwanza likihoji uhalali wake wa kugonga kuapa na kugonga muhuri wa wakili badala ya hakimu kama Sheria ya Uchaguzi inavyoelekeza.

Katika majibu yake, alisema Tume ya Uchaguzi ilitangaza kuchukua fomu ni Desemba 27 na kurudisha ni Desemba 27, huku ikitambua fika kuwa Desemba 25 na 26 ni siku za sikukuu na Desemba 27 ni Jumamosi ambayo mahakama hazifanyi kazi. Aidha, Shitambala amemweleza Msimamizi wa Uchaguzi kuwa Sheria ya Uchaguzi haisomwi na wala haipaswi kusomwa peke yake na pia kiini cha kuapishwa na hakimu kieleweke.

Alisema kimsingi hakimu anapata uwezo wa kuapisha kisheria kutokana na Sheria ya Viapo (Judicial Proceedings) and Statutory Declarations Act 1996) katika kifungu cha 11 ikisomwa pamoja na Sheria ya Notaries Public and Commissioner for Oaths kifungu cha 10 kinachotaja nani wanaruhusiwa kuapisha. Kadhalika ametupilia mbali madai kuwa alijiapisha mwenyewe ofisini kwake pamoja na kutojaza kipengele cha kama amewahi kushitakiwa au la kwa kile alichodai wawekaji pingamizi hawajasoma vizuri taratibu za ujazaji wa fomu hizo.
Source: Habari leo
 
Je, vyama vya Upinzani kweli wameshindwa kukaa meza moja na kuja na mkakati wa kuunganisha nguvu?

Inasikitisha sana . . . . Mbeya is an example. Inatia aibu.
 
Allien ushauri wako ni mzuri lakini labda hiki kizazi cha uongozi wa akina Mrema,Lipumba,Mbowe na Cheyo kitapoondoka na hao watakaokuja labda wanaweza kufuata huo ushauri
 
Nisingependa CCM ivunjike au ijimegue kwenye kipande kingine. Ningependa iwe united in whatever they believe in and try to achieve.

Ningependa wale wote wa Mbadala (kama ndugu yangi John Mwanyika anavyopenda kusema), wapate muafaka wa kukaa pamoja na kuwa na sauti moja.

[1] Bila shaka kuna mengi CCM imesimamia ambayo kila Mtanzania anayapenda na anataka yakae na yaendelezwe.

[2] Kuna mengi ambayo CCM imesimamia na ni kero kubwa kwa kila Mtanzania - yanatakiwa yapigwe vita na mwelekeo kugeuzwa kabisa
[3] Kuna mengi ambayo vyama mbadala vingi ama vyote vinakubaliana ni tofauti na CCM na kila Mtanzania anayapenda

[4] Kuna mengi ya vyama Mbadala kila Mtanzania havitaki na wamechoshwa navyo.

Katika kuweka Umoja wa madhumuni na nia, nadhani vyama Mbadala vyote vinaweza kujijenga kwa kutumia [2] and [3] na kuacha [4] kwa makusudi kabisa.

This will be good for national unity, development and competitive politics with nation's interests at heart. Utitiri wa vyama vingi ni vurugu tupu and ni ujenzi wa migawanyo isio na faida kwa Taifa.
 
Nisingependa CCM ivunjike au ijimegue kwenye kipande kingine. Ningependa iwe united in whatever they believe in and try to achieve.

Ningependa wale wote wa Mbadala (kama ndugu yangi John Mwanyika anavyopenda kusema), wapate muafaka wa kukaa pamoja na kuwa na sauti moja.

[1] Bila shaka kuna mengi CCM imesimamia ambayo kila Mtanzania anayapenda na anataka yakae na yaendelezwe.

[2] Kuna mengi ambayo CCM imesimamia na ni kero kubwa kwa kila Mtanzania - yanatakiwa yapigwe vita na mwelekeo kugeuzwa kabisa
[3] Kuna mengi ambayo vyama mbadala vingi ama vyote vinakubaliana ni tofauti na CCM na kila Mtanzania anayapenda

[4] Kuna mengi ya vyama Mbadala kila Mtanzania havitaki na wamechoshwa navyo.

Katika kuweka Umoja wa madhumuni na nia, nadhani vyama Mbadala vyote vinaweza kujijenga kwa kutumia [2] and [3] na kuacha [4] kwa makusudi kabisa.

This will be good for national unity, development and competitive politics with nation's interests at heart. Utitiri wa vyama vingi ni vurugu tupu and ni ujenzi wa migawanyo isio na faida kwa Taifa.
__________________
Taasisi

- Mkuu Taasisi, Heshima mbele sana,

- Respect kwa the spirit ya msimamo wako ambayo ni unity na maendeleo kwa kuzingatia umoja wa vyama ambao ni wa kweli na wenye manufaa kwa taifa letu na sio wa kutafuta power tu.

Mengi uliyosema ninakubaliana nayo, isipokuwa bado ninatatizwa sana na la umoja wa upinzani Tanzania, nimeona hoja nyingi sana humu JF kuhusu hilo, lakini sielewi kama kweli ni umoja wa upinzani ndio tatizo letu katika vyama mbadala. Ninaamini to this day, Upinzani haujapata a strong leader anayeweza kukubalika na vyama vyote kusimamia interest zao wote as chama kimoja, ninaamini kwamba Mrema peke yake ndiye aliyewahi kuwa na huo uwezo wa kuviunganisha vyama vyote mbadala, lakini toka alipoishiwa nguvu hizo za kisiasa ikawa ndio mwisho wa hii ndoto.

- CUF nao pia ni tatizo kubwa sana kwa hii ndoto, kwa sababu sio siri kuwa malengo yao kwa visiwani hayako sawa na kwa upande wa bara, ingawa hawataki kusema wazi in the public, sasa kama wao wenyewe wamegawanyika wataweza vipi kujiunga na umoja wa taifa as a political alternative?

Vyama vya upinzani wajaribu kujitanua kwa taifa zima, badala ya kusubiri mijini na mbio za Ikulu, nafikiri Operation Sangara ni one of the best thing kutoka upinzani sasa lengo liwe kujijenga kwanza vijijini na kuongeza wabunge, Ikulu itakuja tu yenyewe in the process!

Thanxs!
 
Mdogo wangu Mnyika, i do appreciate you are coming up politically, but you can't hide from the truth,no way.

If Tanzanians wants the true changes and developments politically they have to support CCM manifesto of 2005-2010.the mision and vision of CCM is very clearly thats why the people of Tanzania trust the ruling party.

Yes offcourse opposition party are coming up politically but it will take time for them to be strong .

Just one example, in Rural mbeya, ambapo mgombea wa CHADEMA, Anaenguliwa just because amekosea kufuata masharti ya Ujazaji form za kuombea kugombea, to my perception this is a sign of unseriousness, unresponsiblity. kama umeshindwa kuwa responsible kwenye kujaza form kweli unatakuwa serious kuwaletea wananchi wa mbeya vijijini maendeleo? ni kama vile unafanya mtihani kama wa chuo kikuu au form six then unacha kujaza examination number au registration number? utapataje matokeo yako?

Pia unawaeleza wananchi wasipige kura wakusubili 2010, wakati hilo ni kosa kikatiba? we need time for political parties to be strong enough to lead this national otherwise if we rush to make changes,majuto ni mjukuu.



Andrew, M ,+255 787 403865
 
Mkuu - nipo nawe na pia nakubaliana nawe kabisa.

Nadhani tunaongelea hilo hilo juu ya Umoja wa Upinzani, unless nimekusoma tofauti. Kampeni sangara ni vizuri kuona wanagusa mawazo toka humu ndani. Safi.

Unalosema juu ya Uongozi shupavu pale juu ni kweli. Anahitajika JKN calibre ila mwenye kusimamia alternatives to failing CCM policies and how the go about implementing their manifesto etc, na awe genuine mtu wa watu, asie na makuu na alie safi kama neno safi.
 
Wana JF mimi ningependa sana tulumbane ktk swala hili ili kuwasaidia vyama vya Upinzani ktk uchaguzi Ujao mwaka 2010..nachotaka kufahamu ni kitu kidogo sana lakini chenye maana kubwa ktk uwakilishi wao.

- Ili wewe mwananchi mpiga kura uweze kuwapa kura yako utapenda kuona mambo gani yalifanyika within vyama hivyo..Iwe Muundo, Viongozi, Mikakati, na mengineyo mengi ambayo nitapenda sana kama tutaweza kuyaorodhesha hapa kuvisaidia vyama hivi kuweza kuweka angalau ushindani utakaokuwa na matumaini.

Imani yangu ni kwamba hata kama CCM wameweza kujenga mfumo mbaya wa uchaguzi chini ya chama kimoja kwa kuvitumia vyama vingi bado kuna nafasi ya wananchi kuwachagua viongozi wao nje ya chama hiki..

Kura yako ndio mwamuzi wa mfumo wowote ule utakaowekwa hata kama kura zitaibiwa kama ilivyotokea huko Zimbabwe lakini bado ushihidi utawasuta. Na mara zote tumeona mifano mizuri ya matokeo kama haya ushindi hurudi kwa wananchi na nguvu..

Ikiwa vyama vya Upinzani vimeshindwa kutekeleza yale wananchi mnayotarajia kuyaona ili kuwapa tumaini, nadhani itakuwa vizuri tuwe na uhakika wanatuelewa tunatarajia vitu gani vifanyike, kwani siii Malaika au Miungu wa kufikiria yote yaliyo vichwani mwetu..

Vile vile sii vibaya kama tutaorodhesha pia mambo muhimu ambayo tunapenda kuona mabadiliko ktk chama tawala yaani CCM ikiwa bado wanataka kupata support ya wananchi kwa sababu hadi leo hii inaonyesha wazi vyama vyote nchini - They don't get it!...Wanafikiria wananchi watahadaika vipi kuliko nini mahitaji yao kiasi kwamba Siasa nchi Tanzania zimekuwa ni Utapeli... Mwongo na mwenye kutoa ahadi kubwa kubwa ndiye huchukua mwali nyumbani..Sasa ni wakati wa wananchi kusema TUMECHOKA na ahadi, tumechoka na sura, tumechoka na mapambo ya vyeti..TUMECHOKA...
Enough is Enough!
 
Kwa upande wa wapinzani Rai ya kila mmoja nafikiri ni kuona waungana na kuachiana majimbi. Uamuzi huu unapaswa kufanywa baada ya kufanya Tafiki yakinifu huru nchi nzima kujua maeneo ambako vyama husika katika muungano vinakubalika. Kwa mfano kwa haraka haraka pamoja na kukosa wawakilishi bungeni, CUF inakubalika Tanga, Pwani, Bukoba, Tabora, ZNZ na Mtwara wakati CHADEMA inawafuasi wengi Musoma, Tarime, Kigoma, Kilimanjaro na Kanda ya ziwa. Kwa upande wa TLP iko vizuri vunjo na Arusha mjini wakati NCCR ina mzizi Babati. Ni rahisi sana kutumia kukubalika huku kama mtaji muhimu kupata wabunge wengi.

Ila kwa bahati mbaya, suala la wapingazi kuungana linazidi kufanywa gumu na serikali kwa kutumia madhaifu na uchoyo wa viongozi wa upinzani.

Tazama, serikali inajua urafi wa watu wa upinzani. Tayari imetenga bajeti ya ruzuku kwa vyama vyote vilivyosajiriwa kushiriki katika uchaguzi katika ngazi zote.

Ebu kwa mfano, chama kihakikishiwe ruzuku ya TShs. 5M kwa kila mgombea wa Ubunge na TShs. 100M kwa mgombea wa urais. Unafikiri ni chama gaini cha upinzani kitaacha kusimamisha mgombea??

Uamuzi huu umefikiwa baada ya Study makini ya CCM kubaini kwa wastani wanaungwa mkono kwa asilimia 40 nchi nzima. Na hivyo namna pekee ya kushinda ni kuwagawa wapinzani kwa kuwachochea kusimamisha wagombea kila jimbo ili CCM ishinde hata kwa minority vote.

Wamefahamu kuwa wananchi wameanza kubaini mipaka na tofauti iliyopo kati ya mtendaji kama mtendaji wa serikali na balozi wa CCM mtaani. Awali watendaji walikuwa wanatumika kujua misimamo ya wananchi kivyama na kuwarubuni kwa kununua shahada zao. Sasa hii mbinu inaanza kupitwa na wakati.
 
Back
Top Bottom