Kwamba Upinzania na Mageuzi ya kweli kuletwa na CCM!!!!
La hasha!
Hizi ni ndoto za walevi wa Siasa potofu za Ki CCM.
Upinzani wa kweli utatoka kwa Watanzania wenye nia na dhamira ya kujenga nchi yao.
Ni uongo mkubwa tena ni upotoshaji wa ukweli kuleta na kutetea dhana kwamba upinzani wa kweli utatoka CCM.
CCM ni chama Mfu kilichovunja nguzo zote muhimu za kukisetiri chama chochote cha kisiasa Duniani na kubakiwa na nguzo fikirivu isiyo weka mizizi yeyote ndani na nje ya chama, nguzo ya Fedha.
Ukitoa Ngawira hakuna CCM wanabakia hayawani wenye roho za kinyang'au waliotayari kutumia makucha yao marefu na midomo yao yenye meno marefu na ya kuchongoka.
CCM kama kundi la kisiasa limemeza matapishi yake ya mwaka 1967,ni Mbadala wa Ukoloni na Kansa katika mwili wa Tanzania.
CCM ni Mbweha halisi katika ngozi za binadamu.
Viongozi wa CCM, wanachama wa CCM, mashabiki wa CCM na wapambe wa wana CCM wote wako hapo na wanafanya hayo wafanyayo kwa sababu ya fedha au kwa mategemeo ya kupata fedha au chochote kile chenye maslahi binafsi kiuchumi au cha kuwawezesha kupooza hamu zao za kimwili.
Suala la kujenga nchi, au kujenga chama chao wenyewe kwao wana CCM limepitwa na kupewa kisogo kama ilivyo pitwa na kupewa mgongo siasa ya ujamaa na kujitegemea na mjomba wake Azimio la Arusha.
Upinzani wa kweli kamwe hauwezi kutoka katika chama Mfu na kilichojaa uoza, yaani chama cha CCM. Upinzani wa kweli utatoka kwa Watanzania walio Sturbon na walioshinda vishawishi vingi, Watanzania wawekao maslahi ya taifa mbele, Watanzania wenye Nia Dhamira na Mwelekeo Chanya wa kuiendeleza nchi yao, Watanzania wenye utu na wasio na kutu.
Macho yetu, masikio yetu na matumaini yetu sisi wanasiasa wa mwituni hayako ndani ya mduara wa Kinyang'au wa CCM,Matumaini yetu yako nje ya mduara huo haramu.
Matumaini yetu yako juu ya kizazi kipya chenye mawazo mapya cha uzao usio na damu iliyo hirimishwa ya Ki CCM. Kizazi hicho kilikuwepo kabla ya Uhuru, kilikuwepo siku ya Uhuru na kipo leo hii miongoni mwa Mamillioni ya Watanzania.