Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Wana JF nimekuwa najaribu kutafakari kuhusu hali ya kisiasa na kiuongozi katika nchi yetu na maswali yanakuwa mengi zaidi ya majibu. Kuna kipindi marehemu Nyerere alisema kama niki-paraphrase kuwa mageuzi au upinzani wa kweli utakuja kutokea CCM, tukiangalia hali ya mambo yanavyokwenda na CCm kuwa na moto mpya wa kuanza kufungua matawi mapya na kutafuta wanachama wapya nchi za nje je hiki kinaashiria lolote lile au wanajaribu kupiga mahesabu ya mbali ambayo hatuelewi. Kampeni ya CCM inayoendelea ni kufungua matawi kadhaa katika miji mingi kwa kadiri itakavyowezekana nje ya nchi na kupata wanachama wapya walioko nje, kwa mfano CCM watakuwa wanafungua tawi jipya Missouri wikiendi hii na pia watakuwa katika miji mingine pia kwa mwezi huu na inayofuatia. Je tutegemee upinzani wa kweli kutokea ndani ya CCM? Je Kuna dalili za kutosha kuwa upinzani tulionao ukishirikiana na wote wanaopenda maendeleo ya kutetea nchi yao katika utaratibu mzuri wa kiuongozi na kuwajibika utatufikisha katika hali bora ya kimaisha?

What a load of crap!!​
 
Hao wanaokubali kufungua matawi ya chama cha kifisadi katika miji wanayoishi nchi za nje wote ni WADANGANYIKA, vinginevyo haingii akilini watu kupoteza muda wao eti wanafungua matawi ya chama cha mafisadi nje ya nchi!!!
 
Hao wanaokubali kufungua matawi ya chama cha kifisadi katika miji wanayoishi nchi za nje wote ni WADANGANYIKA, vinginevyo haingii akilini watu kupoteza muda wao eti wanafungua matawi ya chama cha mafisadi nje ya nchi!!!

BAK,

Heshima mbele mkuu, sijapata kuelewa kwa kufungua matawi ya nje watapata kitu gani au ni strategy gani inayoendelea, ila harufu ya udanganyifu inanukia hapa.
 
BAK,

Heshima mbele mkuu, sijapata kuelewa kwa kufungua matawi ya nje watapata kitu gani au ni strategy gani inayoendelea, ila harufu ya udanganyifu inanukia hapa.

Hakuna udanganyifu hapo! Mtu anapenda anachoamini anapenda huwezi mshurutisha apende unachopenda.

Ukitambua hilo utaiishi maisha matamu sana duniani ILA utapata wakati mugumu hapa duniani ukitaka kulazimisha upendacho wewe wote wapende ama uaminicho wewe ndio SAHIHI.

Na Ukitambua binadamu wote ni VICHAA ila digrii ya ukichaa inatofautiana basi wewe utakua na wakati mzuri sana DUNIANI ila usipotambua hilo na ukaamini binadamu wapo waliokamilika basi pia utakua nawakati MGUMU sana hapa duniani.

Ngoja nikupe mfano.
Unaweza enda nunua sharti wewe ukaliita zuri sana lakini rafiki yako akakushangaa kwa kununua sharti baya sana kuliko yote duniani ,ama unaweza ONa msichana/mvulana bomba kabisa lakini mwenzako akaona kituko,ama unaweza kuona jamaa ana akili sana darasani lakini akienda chooni yeye anapata furaha sana kujisaidia pembeni mwa shimo.

Ama unaweza kutana na mtu ambaye hujawahi kutana naye hapo kabla ukampenda/mchukia tu bila kosa lolote.

Hivyo Kama kakichaa kako kana digri ndogo lazima ujue kuna binadamu wapo ambao hawapendi contents za ndani bali wanapenda tu jina la chama lilivyo kaa kaa vivyo hivyo wengine hawapendi tu jina la chama lilivyolivyo Na wengine hawapendi tu viongozi wa chama husika .

Ni kama jamaa yangu mmoja tulikua tunasikiliza radio kila tukifungua radio ONE yeye anabadirisha nikamuuliza kulikoni yeye akasema hapendi radio one si kwa sababu haina vipindi vizuri ila hoja yake ni SASA RADIO ONE NI NINI yani inabeba ujumbe gani yakwamba haina ujumbe wowote.Lakini akasema ukisikia neno radio FREE AFRICA basi anaridhika kabisa kwa jina hilo na ndio maana anaipenda hiyo radio si kwa sababu inavipindi anavyopenda ILA jina limebeba ujumbe anaopenda kuusikia.
 
Hilolinaashiri kuwa kabla ya uchaguzi wa 20010 itapitishwa sheria kuwa walioko nje ya nchi nao wanhaki ya kupiga kura na hapo ndio zitaingizwa hesabu zilizokuwa hazijakamilika kwani inaeleweka kuwa wananchi wengi waliopo hapa Tz kwa sasa wameanza kuamka na walionje ya nchi waokule ni choma njama kula Beer serekali ikiwaitawanzishia starehe kama hizo huko nje mara kwa mara wanjuwa kuwa kura watawapigia tusubiri lakini hali ndiyo hiyo wacha tusivuke daraja kabla hatujalifika
 
Hilolinaashiri kuwa kabla ya uchaguzi wa 20010 itapitishwa sheria kuwa walioko nje ya nchi nao wanhaki ya kupiga kura na hapo ndio zitaingizwa hesabu zilizokuwa hazijakamilika kwani inaeleweka kuwa wananchi wengi waliopo hapa Tz kwa sasa wameanza kuamka na walionje ya nchi waokule ni choma njama kula Beer serekali ikiwaitawanzishia starehe kama hizo huko nje mara kwa mara wanjuwa kuwa kura watawapigia tusubiri lakini hali ndiyo hiyo wacha tusivuke daraja kabla hatujalifika

Spear,

Nafikiri hautakuwa sahihi ku-assume kuwa watu walioko nje kazi yao ni kunywa beer na kuchoma nyama na kuwa serikali ikiwaanzishia hivyo basi watapiga kura. Sidhani kama mtu kuwa nje basi utu wake udhalilishwe kiasi hicho, check your facts again my friend, na ukiwa na mantiki kuwa kura zote huwa zinanunuliwa kwa kitu kidogo kama hicho nafikiri utakuwa unaenda mbali sana.
 
Hakuna udanganyifu hapo! Mtu anapenda anachoamini anapenda huwezi mshurutisha apende unachopenda.

Ukitambua hilo utaiishi maisha matamu sana duniani ILA utapata wakati mugumu hapa duniani ukitaka kulazimisha upendacho wewe wote wapende ama uaminicho wewe ndio SAHIHI.

Na Ukitambua binadamu wote ni VICHAA ila digrii ya ukichaa inatofautiana basi wewe utakua na wakati mzuri sana DUNIANI ila usipotambua hilo na ukaamini binadamu wapo waliokamilika basi pia utakua nawakati MGUMU sana hapa duniani.

Ngoja nikupe mfano.
Unaweza enda nunua sharti wewe ukaliita zuri sana lakini rafiki yako akakushangaa kwa kununua sharti baya sana kuliko yote duniani ,ama unaweza ONa msichana/mvulana bomba kabisa lakini mwenzako akaona kituko,ama unaweza kuona jamaa ana akili sana darasani lakini akienda chooni yeye anapata furaha sana kujisaidia pembeni mwa shimo.

Ama unaweza kutana na mtu ambaye hujawahi kutana naye hapo kabla ukampenda/mchukia tu bila kosa lolote.

Hivyo Kama kakichaa kako kana digri ndogo lazima ujue kuna binadamu wapo ambao hawapendi contents za ndani bali wanapenda tu jina la chama lilivyo kaa kaa vivyo hivyo wengine hawapendi tu jina la chama lilivyolivyo Na wengine hawapendi tu viongozi wa chama husika .

Ni kama jamaa yangu mmoja tulikua tunasikiliza radio kila tukifungua radio ONE yeye anabadirisha nikamuuliza kulikoni yeye akasema hapendi radio one si kwa sababu haina vipindi vizuri ila hoja yake ni SASA RADIO ONE NI NINI yani inabeba ujumbe gani yakwamba haina ujumbe wowote.Lakini akasema ukisikia neno radio FREE AFRICA basi anaridhika kabisa kwa jina hilo na ndio maana anaipenda hiyo radio si kwa sababu inavipindi anavyopenda ILA jina limebeba ujumbe anaopenda kuusikia.

Mkamap,

Naweza kukubaliana na wewe kuwa objectivity ya kuliangalia swala zima la maendeleo na mageuzi yenye maana kwa wananchi ni kuviangalia vyama vyote bila pre-conception yeyote, ila I cant help to wonder strategy ya kuleta mabadiliko ya kweli ni kufungua matawi nje au nikuweka wazi plan inayotupa detail ya kipi wanapanga kufanya kubadilisha mtizamo uliopo kwa sasa.
 
Hongera kwa wale wote waliowezasha kufunguliwa kwa matawi ya CCM huko USA...
 
Kuna hakika gani kuwa upinzani huo utakaotoka CCM si wa kutengenezwa?
 
na kama upinzani wa kweli utatoka ndani ya Chama Cha Mafisadi na huo utakuwa ndio mwisho wake. alama za haya kutokea zinaanza kuonekana, angalia kauli za msuya, sumaye, warioba na butiku utajua
 
Mkamap,

Naweza kukubaliana na wewe kuwa objectivity ya kuliangalia swala zima la maendeleo na mageuzi yenye maana kwa wananchi ni kuviangalia vyama vyote bila pre-conception yeyote, ila I cant help to wonder strategy ya kuleta mabadiliko ya kweli ni kufungua matawi nje au nikuweka wazi plan inayotupa detail ya kipi wanapanga kufanya kubadilisha mtizamo uliopo kwa sasa.


kufungua tawi la chama na watanzania kujipatia kadi za vyama watakavyo ni haki yao ya msingi.

Mfano wapo watu wanaokaa nje ya nchi zaidi ya miaka 5 ama zaidi na ambition yake ni kua akitoka hapo anaenda kugombea uongonzi ktk chama husika hivyo kumpa kadi yake akiwa huko aliko ni haki yake ya msingi.

Hapa inamaana kupata kadi si lazima mtu atumie pesa nyingi kutafuta kadi hiyo kurudi nyumbani .Hii inaelekea kua sawa na pass ya kusafiria je? wewe ungelifurahi kama ingekulazimu kila mara kubadili pass yako lazima urudi nyumbani??

Suala la mabadiriko ya kweli ktk nchi yetu mimi naamini tofauti na wewe,mimi naamini VYAMA VYETU vyote havina dalili yoyote ya kuleta mabadiriko ila wapo hapo kimasilahi yao binafsi na mnyororo wa fungamano wa vyama vyao.
 
Suala la upinzani wa kweli utatoka CCM ni maneno ya Mwl Nyerere. Binafsi sisadiki hicho kitu. Nyerere ni mwanafalsafa. Alikuwa anapigia debe chama chake.

Watu hatuwezi kuwa watumwa wa mawazo kiasi hiki. Na Nyerere alitufunga kitambaa cheusi usoni kiasi cha kuweza kujivunia "emptiness". Tumetoka mbali.
 
Invicible said:
Suala la upinzani wa kweli utatoka CCM ni maneno ya Mwl Nyerere. Binafsi sisadiki hicho kitu. Nyerere ni mwanafalsafa. Alikuwa anapigia debe chama chake.

Watu hatuwezi kuwa watumwa wa mawazo kiasi hiki. Na Nyerere alitufunga kitambaa cheusi usoni kiasi cha kuweza kujivunia "emptiness". Tumetoka mbali.

..ina maana wa-Tanzania hawachagui upinzani wa sasa hivi, kwasababu wanasubiri utabiri wa Baba wa Taifa utimie?

..kweli Nyerere kiboko!!!
 
Suala la upinzani wa kweli utatoka CCM ni maneno ya Mwl Nyerere. Binafsi sisadiki hicho kitu. Nyerere ni mwanafalsafa. Alikuwa anapigia debe chama chake.

Watu hatuwezi kuwa watumwa wa mawazo kiasi hiki. Na Nyerere alitufunga kitambaa cheusi usoni kiasi cha kuweza kujivunia "emptiness". Tumetoka mbali.

Mkuu Invincible,
Nakubaliana na wewe kuwa Mwalimu alitumia falasafa ya hali ya juu katika usemi wake ila sidhani kama alikosea.


Kwa mtazamo wangu wa usemi wake Mwalimu ni kuwa, nguvu walizojilimbikizia CCM, ndizo zitakazokigawa au kutokigawa lakini kikabadilika na kuleta upinzani (demokrasia) ya kweli nchini kama ilivyokuwaUNIP- Zambia ya KK iliyomeguka na kuimarisha MMD ambayo nayo ikajisafisha baada ya Chiluba.

Hili limeshaanza kuonekana katika matukio ya hivi karibuni. Watu kama Mwakyembe, Nape na hata wakongwe kama Msuya, Butiku na Warioba wameanza kuona umuhimu wa uwazi ndani ya CCM. Wameshaona kuwa demokrasia haikwepeki hasa wakiangalia matukio ya Zim na Kenya.


Wale wa damu changa kama Mwakyembe na Nape, wao wanataka mambo yaende kama walivyofundishwa kwenye vitabu na kushuhudia walikotembelea (US, India n.k) au kuona kwenye luninga. Hawa wako wengi ingawa sio wote waliokwishang'aa na ndio watakaoichalenji old system ya CCM head on mpaka inyooke au ikishindikana igawanyike. Either way, maneno ya Mwalimu yatakuwa yametimia. Huo ndio utakuwa mwanzo wa upinzani wa kweli katika siasa za TZ.


Hata hivyo hii haina maana kuwa vyama vingine vya siasa visalimu amri, la hasha, vile vitakavyokuwa imara wakati kiama kikiifikia CCM, ndivyo vitakavyokuwa beneficiaries wa hayo mageuzi ndani na kuwa moja kati ya wapinzani wa kweli. Tuombe tu Mungu kuwa haya yatokee kwenye hiki kizazi cha akina Mwakyembe, Mnauye etc., na yasisubiri mpaka mjukuu wa JK atakapomaliza awamu yake ya pili.
 
Kama tunafikiri there is no good seeds pale sisiem ..tunakosea.

Kumekufa kwa kiasi kikubwa. but remember kufika mbinguni unafikishwa na shetani amabaye mnalumbana naye ..mpaka umshinde...na pigo la mwisho la kumshinda..ndio unaagukia mbingu.

Kuna watu wachache..watakuwa wanalumbana na mafisadi kamili pale ccm. patakuwa na group ndogo..watasota kweli..jasho litwatoka....maana ni lazima kuwe na antagonistic forces....n amoja definetly itakuw Good...and the other totaly evel.

Hawa wachache watakuwa wamekomaa kweli kama watabakia salama ...na watabaki salama hata kama ni wachache...kwa uzoefu watakao kuwa nao...wanaweza kuwa mbegu nzuri ..ya new step!
 
Kama tunafikiri there is no good seeds pale sisiem ..tunakosea.

Kumekufa kwa kiasi kikubwa. but remember kufika mbinguni unafikishwa na shetani amabaye mnalumbana naye ..mpaka umshinde...na pigo la mwisho la kumshinda..ndio unaagukia mbingu.

Kuna watu wachache..watakuwa wanalumbana na mafisadi kamili pale ccm. patakuwa na group ndogo..watasota kweli..jasho litwatoka....maana ni lazima kuwe na antagonistic forces....n amoja definetly itakuw Good...and the other totaly evel.

Hawa wachache watakuwa wamekomaa kweli kama watabakia salama ...na watabaki salama hata kama ni wachache...kwa uzoefu watakao kuwa nao...wanaweza kuwa mbegu nzuri ..ya new step!

Azimio Jipya,

Nimekusoma barabara na point yako kuwa better the devil you know than the angel you have never seen, sasa ni kuwa tutegemee kuwa something good will come out of CCM? pamoja na kuwa sio kwamba watanzania wamelala au wanangojea maneno ya falsafa ya Nyerere itimie, katika matukio ya karibuni ya ufisadi na uongozi usio na mwelekeo, CCM ina weza kujiokoa na kuleta mabadiliko hasa ndani yake na baadae katika nchi nzima?
 
Mkuu Invincible,
Nakubaliana na wewe kuwa Mwalimu alitumia falasafa ya hali ya juu katika usemi wake ila sidhani kama alikosea.


Kwa mtazamo wangu wa usemi wake Mwalimu ni kuwa, nguvu walizojilimbikizia CCM, ndizo zitakazokigawa au kutokigawa lakini kikabadilika na kuleta upinzani (demokrasia) ya kweli nchini kama ilivyokuwaUNIP- Zambia ya KK iliyomeguka na kuimarisha MMD ambayo nayo ikajisafisha baada ya Chiluba.

Hili limeshaanza kuonekana katika matukio ya hivi karibuni. Watu kama Mwakyembe, Nape na hata wakongwe kama Msuya, Butiku na Warioba wameanza kuona umuhimu wa uwazi ndani ya CCM. Wameshaona kuwa demokrasia haikwepeki hasa wakiangalia matukio ya Zim na Kenya.


Wale wa damu changa kama Mwakyembe na Nape, wao wanataka mambo yaende kama walivyofundishwa kwenye vitabu na kushuhudia walikotembelea (US, India n.k) au kuona kwenye luninga. Hawa wako wengi ingawa sio wote waliokwishang'aa na ndio watakaoichalenji old system ya CCM head on mpaka inyooke au ikishindikana igawanyike. Either way, maneno ya Mwalimu yatakuwa yametimia. Huo ndio utakuwa mwanzo wa upinzani wa kweli katika siasa za TZ.


Hata hivyo hii haina maana kuwa vyama vingine vya siasa visalimu amri, la hasha, vile vitakavyokuwa imara wakati kiama kikiifikia CCM, ndivyo vitakavyokuwa beneficiaries wa hayo mageuzi ndani na kuwa moja kati ya wapinzani wa kweli. Tuombe tu Mungu kuwa haya yatokee kwenye hiki kizazi cha akina Mwakyembe, Mnauye etc., na yasisubiri mpaka mjukuu wa JK atakapomaliza awamu yake ya pili.

Kubwajinga,

Nafikiri utakuwa hujakosea kuwa pamoja na kwamba mabadiliko yanaweza kuletwa na nguvu waliyonayo CCM, wapinzani pia wana nafasi yao katika kubadilisha sura ya Tanzania na kama hawatafanya hivyo sidhani kama wananchi watawasamehe kwa kushindwa kutimiza their end of the bargain.
 
..ina maana wa-Tanzania hawachagui upinzani wa sasa hivi, kwasababu wanasubiri utabiri wa Baba wa Taifa utimie?

..kweli Nyerere kiboko!!!

JokaKuu,

Sidhani watanzania hawachagui upinzani, mabadiliko yanakwenda kwa wakati na pia ufahamu wa maswala muhimu katika jumuia hasa wale ambao wanaona kwamba ili kufanikisha mambo fulani inabidi wachukue hatua fulani za haki ya msingi. Tukisema watanzania wanasubiri utabiri wa Nyerere utimie nafikiri tutakuwa very far from the truth, kila mwananchi ana sehemu yake katika maendeleo ya nchi yetu. tutakapo weka nguvu pamoja regardless of affiliation ya chama then nafikiri tutakuwa tunaiweka nchi yetu mbele.
 
Suala la upinzani wa kweli utatoka CCM ni maneno ya Mwl Nyerere. Binafsi sisadiki hicho kitu. Nyerere ni mwanafalsafa. Alikuwa anapigia debe chama chake.

Watu hatuwezi kuwa watumwa wa mawazo kiasi hiki. Na Nyerere alitufunga kitambaa cheusi usoni kiasi cha kuweza kujivunia "emptiness". Tumetoka mbali.

Invincible,

Pamoja na kuwa kila mtu ana uhuru wa kufikiria na kutoa mtizamo wake nafikiri kwangu inakuwa ngumu kidogo kukubaliana na idea yako kuwa Nyerere alitufunga kitambaa cheusi, Nyerere tukimuongelea in totality ana vitu vingi vya kuapreciate zaidi ya vibaya, kuanzia kwenye kupigania uhuru na kutuunganisha watanzania ambapo tunaweka undugu mbele na wala sio ukabila kama nchi zingine. Vile kumuongelea in one aspect hasa ya mabadiliko kutoka CCM is debatable na ndio maana tunadebate hii. Waweza rejea post ya Kubwajinga nafikiri mtizamo wake wa kuhusu mabadiliko na CCM unajinyambulisha kwa point.
 
kufungua tawi la chama na watanzania kujipatia kadi za vyama watakavyo ni haki yao ya msingi.

Mfano wapo watu wanaokaa nje ya nchi zaidi ya miaka 5 ama zaidi na ambition yake ni kua akitoka hapo anaenda kugombea uongonzi ktk chama husika hivyo kumpa kadi yake akiwa huko aliko ni haki yake ya msingi.

Hapa inamaana kupata kadi si lazima mtu atumie pesa nyingi kutafuta kadi hiyo kurudi nyumbani .Hii inaelekea kua sawa na pass ya kusafiria je? wewe ungelifurahi kama ingekulazimu kila mara kubadili pass yako lazima urudi nyumbani??

Suala la mabadiriko ya kweli ktk nchi yetu mimi naamini tofauti na wewe,mimi naamini VYAMA VYETU vyote havina dalili yoyote ya kuleta mabadiriko ila wapo hapo kimasilahi yao binafsi na mnyororo wa fungamano wa vyama vyao.

Mkamap,

Nakubaliana kabisa kuhusu haki ya msingi ya kila mtanzania ni pamoja na kukubali kuwa na affiliation ya chama au kukataa. kama CCM wameona kuwa haki ya msingi ya watanzania walioko nje ni pamoja na kuwapa matawi ya CCM nafikiri sitakuwa nimekosea kuwa wanakandamiza kwa namna moja au ingine haki ya msingi ya kupiga kura. Tukifocus kuwa matawi ni ya kuwasaidia wananchi walioko nje katika mambo mengine pamoja na kugombea uongozi wakirudi vile vile itakuwa bora kama wataruhusiwa kupiga kura huko waliko. Idea ya wananchi wa nje kupiga kura iliishawakilishwa kwa balozi aliyepita na hakuona umuhimu wa kufuatilia wala kutoa feedback ya swala zima linaendelea vipi. Itakuwa jambo la busara wala sio kwa CCM tu ila kwa chama chochote ambacho kitasimamia maslahi ya watanzania walioko nje kupiga kura. Na changamoto vile vile inaweza kuwa kwa watanzania walioko nje kusukuma hii idea kwa ajili ya maslahi yao.
 
Back
Top Bottom