Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Na uzoefu unaonyesha kwamba CCM haiwezi kutoka pale ilipo kutokana na kwamba Viongozi wengi wa vyama vya upinzani ni wepesi sana kurubunika na hela za Mafisadi kama tulivyoona hivi karibuni na bado naamini tutaendelea kuwaona.

CCM haiwezi kutoka kwa hiari, italazimishwa kutoka tu pale wanyonywaji tutakapoamka na ku-realize hali halisi ilivyo. Haishangazi baadhi ya wapinzani wananunuliwa na mafisadi maana ni strategy za CCM kuwadhoofisha. Wapinzani wenyewe njaa kali kama maskini yeyote mwingine wa nchi hii, na sisi wenyewe ndio wakwanza kuwatia majaribuni kwa kisingizio cha mafisadi. Kama hatuwaungi mkono kupambana na maovu, lazima wakate tamaa na kukubali kurubuniwa. Wanasema 'if you can't beat them, join them'. Tumewaona wengi ndio, na tutawaona wengi ndio, lakini mapambano yataendelea hadi siku iliyokubalika na mabadiliko yatatokea.
 
Tatizo lilliloko sasa ni kukosekana kwa uwajibikaji kwa hali ya juu. mtu akipewa dhaamana ya uongozi lazima awajike kwa lolote litakalotea ktk himaya yake. mashirika ya umma ni muhimu yafanyiwe perfomance auditing kila mwaka na kama kuna uzembe sheria ifuate mkondo sio kuhamishiwa shirika au kitengo kingine. hilo halipo kabisa sasa.

yapo mengi ambayo kutokana na mazoea ni ngumu kubadilika. upinzania ukiingia madarakani hata kama ni serikali ya umoja na ccm mambo yatabadilika sana.

ki ujumla mabadiliko muhimu sana kwa sasa
 
Mbona makampuni ya private yana ufanisi wa juu siku zote, na wafanyakazi wake ni watanzania? Inakuwaje tuko bize kushawishi wenzetu kwamba eti watanzania hawawezi kufanya mambo mazuri, makubwa wakati mifano hai ipo? Uongozi wa CCM unamgusa kila mtu. Mtu akichemsha kazi au akienda kinyume na taratibu na achukuliwe hatua sirias. Litakuwa fundisho kwa wengine kama system yote iko hivyo, na nchi itabadilika.

Makampuni ya private kuwa na ufanisi wa juu si ipo katika kila nchi mzee? Huwezi kutumia kigezo cha private companies kuonyesha kuwa wananchi wana uwezo wa kufanya kazi. Ukiangalia nchi zote duniani, private companies have proven this, maana wao wako katika profit maximisation. Pia private companies wana uwezo wa kutoa ajira kwa mtu hata wa nje ya nchi, kama itabidi kuweza kutimiza lengo lao. Lakini kwa upande wa public entities, hicho hakipo kabisa. Wewe unadhani kwa nini Tz ina-slow down EAC? Sio hofu ya wakenya kukomba kazi bongo?
Swali linabaki pale pale, kutawekwa vigezo gani kuhakikisha kuwa hizi public entities zitafanya kazi kwa ufanisi upinzani ukiingia? Sijasikia wapinzani wakiongelea hilo kabisa.
 
Makampuni ya private kuwa na ufanisi wa juu si ipo katika kila nchi mzee? Huwezi kutumia kigezo cha private companies kuonyesha kuwa wananchi wana uwezo wa kufanya kazi. Ukiangalia nchi zote duniani, private companies have proven this, maana wao wako katika profit maximisation. Pia private companies wana uwezo wa kutoa ajira kwa mtu hata wa nje ya nchi, kama itabidi kuweza kutimiza lengo lao. Lakini kwa upande wa public entities, hicho hakipo kabisa. Wewe unadhani kwa nini Tz ina-slow down EAC? Sio hofu ya wakenya kukomba kazi bongo?
Swali linabaki pale pale, kutawekwa vigezo gani kuhakikisha kuwa hizi public entities zitafanya kazi kwa ufanisi upinzani ukiingia? Sijasikia wapinzani wakiongelea hilo kabisa.

Kwa hiyo wewe unaamini ni kitu kipo tu automatic kutoka kwa Mungu? Hujui kama zipo nchi nyingi tu zenye wageni kwenye serikali zao? hasa nchi za kiarabu. Kama unadhani wa-tz watashindwa basi wazungu na wageni wengine waruhusiwe kutufanyia kazi kwenye mawizara, kwani tatizo liko wapi, shida yetu si ufanisi? Au unataka niku-convince vipi kwamba watanzania wana uwezo wa kuendesha nchi yao wakipata uongozi bora?
 
mheshimiwa....hapa tunabadilishana mawazo. Sidhani kama kuna one right answer. Swali liko open for discussion, na mimi sijapinga point zenu, nazi-discuss...pros and cons. Au sio?
Nyie mmetoa mfano wa makampuni ya private kuwa na ufanisi zaidi. Point taken. Inaelekewa wewe usomi vizuri. Mimi nimetoa sababu zinazowafanya wao wawe na ufanisi zaidi - profit maximasation. Hujaona hiyo point? The next question ni kitu gani kinatoa motivation katika kazi za serikali? THATS MY POINT. WaTz watakubali kuachia kazi zao BOT, Muhimbili, Magazetini, nk kwa kusudi la kuleta watu wenye ufanisi zaidi? It's a problem not just facing us, but all countries in the world. Wapinzani hawaongelea hili tatizo hata kidogo. Matatizo yameelekezwa kwa CCM tu. Do you see the bigger picture?
 
Wengi wanaweza kukubali kwamba, kilicho muhimu kwa Watanzania kwasasa ni uwakilishi ulio mkubwa wa vyama vya upinzani katika Bunge letu. Uwakilishi wa kizalendo utakaoweza kupingana na mfumo wa kuburuzwa wa muda mrefu ambao umelifanya Taifa hili lizidi kudumaa na kutambulika kama moja ya nchi maskini duniani, kunakosababishwa na miswada mbalimbali yenye maslahi kwa Taifa kupitishwa bila ya kuhojiwa ipasavyo na wabunge waliowengi wa chama tawala. Uwakilishi wa wapinzani Bungeni iwe dhamira ya kwanza badala ya wote kukimbilia Urais tu kama ionekanavyo hivi sasa.

Kwa sababu kujiunga pamoja na kutengeneza "rainbow coalition" ni kitu ambacho ni kama hakiwezekani kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo ile ya ubinafsi; basi kama changamoto, yafuatayo ni bora yafanyike ili uwakilishi wa Wabunge wa upinzani uwe mkubwa Bungeni kwa faida ya Watanzania wote ifikapo 2010 na mbeleni.

-- Cha kwanza ni kukubali kuwa CCM have got better strategies katika mambo ya uchaguzi kuliko nyinyi. Hii itawafanya mtafakari na kugundua weaknesses zenu na kujijenga zaidi katika hizo. Ile ya kipesa - ni bora kuiacha, maana hamtowashinda, they've got the rugged muscle. Nevertheless, there's still a room to reshape your position to a better one.

-- Tambueni strongholds zenu kwenye majimbo na kukubaliana wote kuwa huyu anakubalika zaidi huku au kule.

-- Stronghold zenye wabunge wa upinzani tayari ziendelee kuwa na mbunge huyohuyo wa upinzani au mwingine kutoka chama hicho. Vyama vingine vyote vim-support mbunge huyo mmoja. (Kumbukeni CCM na Urais wa kuachiana wa miaka kumikumi - si kwamba hamna ma-aspirants wengine ndani, bali ni makubaliano tu!).

-- Gawaneni majimbo ya uchaguzi. Mkiacha yale ambayo yanawawakilishi tayari yakibakia hivyo.

-- Kule ambako upinzani haukubaliki kwa sana, jimbo liachwe mikononi mwa mmoja kutokana na tathmini mtakayokuwa mmefanya kutambua majimbo yote magumu na kuwa mmegawana nafasi sawasawa za kuyawakilisha. Jimbo la uchaguzi liwe na mwakilishi mmoja kutoka upinzani na siyo multitude of opposition candidates dhidi ya chama tawala.

-- Lakini kama kuungana kutawezekana (maombi ya Watanzania walio wengi), basi kufanyike walau miezi sita kabla ya uchaguzi mkuu. Mkiungana mapema sana, CCM ni ma-guru katika kuwavuruga, they've got the experience. Watapata muda wa kutosha kuweza kuwatawanya muda mchache uchaguzi ukikaribia. Na mkifanya mmechelewa sana, hamtapata muda mwanana wa kuweza kuwafikia wapiga kura vijijini.

Nawatakia utekelezaji mwema wa strategies zenu.

SteveD.
 
Jambo la muhimu kabisa vyama vya upinzani na wanachama wake wote hasa wale wanaotafuta nafasi za uongozi waweke mbele mapenzi ya taifa hili na wasiwe wabinafsi, bila hivyo hakuna mkakati wowote ule utakaofanikiwa.
 
Kwa ufupi WAUNGANE!. La sivyo wataendelea kushindwa MILELE kwa kuendekeza njaa na ubinafsi!
 
Tatizo la vyama vya upinzani ni ubinafsi wa baadhi ya viongozi hasa viongozi wa CHADEMA kufikiri chama chao kinakubalika sehemu zote Tanzania.
Uchaguzi wa Tarime kwa kiasi kikubwa uliwatia kiburi wanachadema pengine kushindwa kwao katika jimbo la Busanda kunaweza kuwarudisha mezani viongozi wa wote wa upinzani katika mstari hasa kuelekea uchaguzi wa jimbo la Biharamuro.

Viongozi wa upinzani lazima watambue kwamba CCM ina nguvu kubwa ya fedha na ina mtaji mkubwa wa wananchi wengi wasiokuwa na uelewa wa elimu ya uraia.Bila kuungana wapinzani wasahau kuishinda CCM.
 
Kuwashinda CCM ni lazima wapindani wajipange kuwa wanashinda kwa kiwango kikubwa (mass victory) ili hata kama kula zitaibiwa basi zisiweze kubatilisha ushindi wao.
 
-- Cha kwanza ni kukubali kuwa CCM have got better strategies katika mambo ya uchaguzi kuliko nyinyi. Hii itawafanya mtafakari na kugundua weaknesses zenu na kujijenga zaidi katika hizo. Ile ya kipesa - ni bora kuiacha, maana hamtowashinda, they've got the rugged muscle. Nevertheless, there's still a room to reshape your position to a better one.

-- Tambueni strongholds zenu kwenye majimbo na kukubaliana wote kuwa huyu anakubalika zaidi huku au kule.

-- Stronghold zenye wabunge wa upinzani tayari ziendelee kuwa na mbunge huyohuyo wa upinzani au mwingine kutoka chama hicho. Vyama vingine vyote vim-support mbunge huyo mmoja. (Kumbukeni CCM na Urais wa kuachiana wa miaka kumikumi - si kwamba hamna ma-aspirants wengine ndani, bali ni makubaliano tu!).

-- Gawaneni majimbo ya uchaguzi. Mkiacha yale ambayo yanawawakilishi tayari yakibakia hivyo.

-- Kule ambako upinzani haukubaliki kwa sana, jimbo liachwe mikononi mwa mmoja kutokana na tathmini mtakayokuwa mmefanya kutambua majimbo yote magumu na kuwa mmegawana nafasi sawasawa za kuyawakilisha. Jimbo la uchaguzi liwe na mwakilishi mmoja kutoka upinzani na siyo multitude of opposition candidates dhidi ya chama tawala.

-- Lakini kama kuungana kutawezekana (maombi ya Watanzania walio wengi), basi kufanyike walau miezi sita kabla ya uchaguzi mkuu. Mkiungana mapema sana, CCM ni ma-guru katika kuwavuruga, they've got the experience. Watapata muda wa kutosha kuweza kuwatawanya muda mchache uchaguzi ukikaribia. Na mkifanya mmechelewa sana, hamtapata muda mwanana wa kuweza kuwafikia wapiga kura vijijini.

Nawatakia utekelezaji mwema wa strategies zenu.

SteveD.

Wewe ni CCM? Basi pili pili ya shamba isikuwashe.

Ni upinzani? Basi join the efforts, usikae hapo unatoa vi lecture vya "wapinzani fanyeni hiki na kile."

Huwezi kuwa mshangiliaji tu unasubiri wengine wakujengee nchi, wakishindwa uchaguzi tuna point fingers tu.
 
MWENYEKITI wa a Tanzania Labour Party (TLP) Bw. Augustino Mrema amesema kuwa endapo vyama vya upinzani vitaendeleza ubinafsi wa kutoshirikiana katika chaguzi mbalimbali havitaweza kukiangusha Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Mbali na hilo pia amekitaka Chama Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuacha rafu wanazotaka kuzifanya katika Jimbo la Biharamulo badala yake wamuunge mkono mgombea wa TLP Kwani ndiye anayepaswa kuchukua nafasi hiyo.


Hayo aliyasema jana katika kipindi cha Mambo Leo kinachorushwa na kituo cha Radio 100.5 Times fm, ambapo kiongozi huyo alisisitiza kuwa bila mshikamano wa wapinzani, CCM itaendelea kubaki madarakani.


Alisema kuwa tatizo kubwa ambalo limekuwa likiviangusha vyama vya upinzani katika chaguzi mbalimbali ni ubinafsi unaofanywa na baadhi ya vyama kwa kujiona wanaweza zaidi ya vingine.

“CCM ina raslimali watu na fedha hivyo kwa kuendekeza ubinafsi wetu hatutafika mahali popote, hakuna asiyekumbuka mimi nilivyokuwa juu kisiasa lakini CCM walinishughulikia na kufika hapa nilipo hivyo hata wanaojiona kuwa wana wabunge wengi nao watashughulikiwa tu hivyo dawa ni kuungana mkono kwa kusimamisha mgombea mmoja katika chaguzi zinazofanyika ili kuishinda CCM,” alishauri Bw. Mrema.

Alisema kuwa ubinafsi wa CHADEMA ndio unaosababisha kushindwa kuunga mkono TLP katika Jimbo la Biharamulo kiti ambacho kilikuwa kinashikiliwa na TLP.


“Unajua TLP ndio wafiwa, hivyo kama ni kurithi mali alitakiwa arithi lakini kwa ubinafsi wa CHADEMA wameonekana wazi kuanza kucheza rafu huko Biharamulo kwa kumurubuni Katibu wa TLP wilaya kutangaza kuwa hatusimamishi mgombea...waache hizo! Mbona mimi sijasimamisha mgombea kwenye chaguzi zingine kwa nia ya kuunga mkono vyama vingine?,” alihoji BW. Mrema.

Alisema kuwa kumalizika uchaguzi wa viongozi ndani ya TLP na yeye kupewa nafasi ya uenyekiti,kumekiimarisha chama hicho na kujipanga kupata majimbo 10 likiwemo la Vunjo alilipania kwenda kugombea.


Alisema kuwa ili kuweza kufanikisha mikakati hiyo ni lazima wanachama wote wa TLP kushirikiana na kuvunja makundi ambayo yalisababishwa na uvumi mbaya dhidi yake kwani tayari Mkutano Mkuu umemsafisha kwa kumpa kura 111 hivyo washirikiane na viongozi wote waliochaguliwa kujipanga upya.

Akizungumzia suala la yeye kuitwa kibaraka wa CCM alikanusha na kusema kuwa kama angekuwa kibaraka wa chama hicho basi kingeweza kumpa nafasi nzuri au kumwachia nafasi ya urais ili agombee.

“Pamoja na madai ya mimi kuwa kibaraka lakini hakuna kiongozi wa upinzani ambaye ameweza kuvunja rekodi zangu za kura kwani nilishawahi kupata kura milioni 1.8 ambapo Mbowe ( Bw.Freeman) alipata kura 600,000 huku Prof. Ibrahim Lipumba akipata kura milioni 1.2 hivyo hapa utaona kuwa mimi sio kibaraka bali nakubalika kwa uongozi wangu uliotukuka,” alitamba Bw. Mrema.

Kwa upande wa Naibu Katibu Mkuu wa TLP Bw. Rajab Tao aliwataka wanachama wa TLP ambao walifukuzwa na Halmashauri Kuu kuomba msamaha na kurejea kundini ili kukiendeleza chama.


Source: Majira
 
Mzee Mrema alitoa sharti moja:

Wapinzania washirikiane huku chini, kuanzia vitongoji, Udiwani, na hata Ubunge, lakini suala la uraisi kila chama kiende kivyake!

Hata hivyo anawaomba waiachie TLP kwenye uchaguzi mdogo Biharamulo kwani eti ni jimbo lao!
 
Mzee Mrema alitoa sharti moja:

Wapinzania washirikiane huku chini, kuanzia vitongoji, Udiwani, na hata Ubunge, lakini suala la uraisi kila chama kiende kivyake!

Hata hivyo anawaomba waiachie TLP kwenye uchaguzi mdogo Biharamulo kwani eti ni jimbo lao!



Basi ana taka tu TLP iachiwe ubunge Biharamulo. Iweje aseme haya halafu atoke moja kwa moja na kusema TLP waachiwe? Hapa inaelekea ana taka tu kuserve interest zake. Sijui kama isingekua kutaka TLP iachiwe Biharamulo ange sema yote haya, anyway Icould be wrong.
 
MWENYEKITI wa a Tanzania Labour Party (TLP) Bw. Augustino Mrema amesema kuwa endapo vyama vya upinzani vitaendeleza ubinafsi wa kutoshirikiana katika chaguzi mbalimbali havitaweza kukiangusha Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Mbali na hilo pia amekitaka Chama Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuacha rafu wanazotaka kuzifanya katika Jimbo la Biharamulo badala yake wamuunge mkono mgombea wa TLP Kwani ndiye anayepaswa kuchukua nafasi hiyo.

Alisema kuwa tatizo kubwa ambalo limekuwa likiviangusha vyama vya upinzani katika chaguzi mbalimbali ni ubinafsi unaofanywa na baadhi ya vyama kwa kujiona wanaweza zaidi ya vingine.

Alisema kuwa ubinafsi wa CHADEMA ndio unaosababisha kushindwa kuunga mkono TLP katika Jimbo la Biharamulo kiti ambacho kilikuwa kinashikiliwa na TLP.

“Unajua TLP ndio wafiwa, hivyo kama ni kurithi mali alitakiwa arithi lakini kwa ubinafsi wa CHADEMA wameonekana wazi kuanza kucheza rafu huko Biharamulo kwa kumurubuni Katibu wa TLP wilaya kutangaza kuwa hatusimamishi mgombea...waache hizo! Mbona mimi sijasimamisha mgombea kwenye chaguzi zingine kwa nia ya kuunga mkono vyama vingine?,” alihoji BW. Mrema.
.....i just threw-up in my mouth after reading the above😕😕,huku si kufilisika kisiasa tu bali kimawazo vileX2.
 
Kwa sasa Mrema atulie tu....ajitibu kisukari chake....
Maana siasa zake ni kwishneeii.........
Hawezi kuheshimika na kusikilizwa na watu kama kipindi kile alivyokuwa Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza Tanzania. Cheo ambacho hakuna mtu aliyeshika mpaka sasa.........

TULIA BABAAA..........
 
Kwa sasa Mrema atulie tu....ajitibu kisukari chake....
Maana siasa zake ni kwishneeii.........
Hawezi kuheshimika na kusikilizwa na watu kama kipindi kile alivyokuwa Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza Tanzania. Cheo ambacho hakuna mtu aliyeshika mpaka sasa.........

TULIA BABAAA..........

Mkuu Shiumiti Cheo cha naibu waziri mkuu kiliwahi kushikwa na Salim A Salimu
 
Back
Top Bottom