Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Vile vile sii vibaya kama tutaorodhesha pia mambo muhimu ambayo tunapenda kuona mabadiliko ktk chama tawala yaani CCM ikiwa bado wanataka kupata support ya wananchi kwa sababu hadi leo hii inaonyesha wazi vyama vyote nchini - They don't get it!...Wanafikiria wananchi watahadaika vipi kuliko nini mahitaji yao kiasi kwamba Siasa nchi Tanzania zimekuwa ni Utapeli... Mwongo na mwenye kutoa ahadi kubwa kubwa ndiye huchukua mwali nyumbani..Sasa ni wakati wa wananchi kusema TUMECHOKA na ahadi, tumechoka na sura, tumechoka na mapambo ya vyeti..TUMECHOKA...
Enough is Enough!

Mkandara, SISIEMU imeoza! Tusitegemee mabadiliko ya aina yoyote ile ndani ya SISIEMU. Swala la UFISADI liko wazi na MAFISADI wanafahamika, kuna chochote kile kilichofanywa na Serikali ya SISIMU?? Swala la DOWANS, RICHMOND nk, linajulikana na walioisababishia nchi hasara kubwa kutokana na kampuni hizi wanajulikana lakini kuna yeyote yule aliyeshughulikiwa kikamilifu???

Ukija kwenye swala la IPTL nchi imekula hasara ya kutosha kabisa, nini kiliendelea au kinaendelea kwenye mchakato mzima wa kuwawajibisha waliosababisha hasara hii kubwa kwa Taifa?

Kwa kifupi tusitegemee mabadiliko yoyote yale ndani ya SISIEMU. Wakati wa mabadiliko umefika. "TANZANIA BILA YA CCM INAWEZEKANA"
 
Kitu muhimu kwanza ni kuwaelewesha Wananchi walio wengi ,kuwa upinzani kwa hapa ulipo hauwezi kuleta maendeleo yeyote kwa mwananchi na yakaonekana, wananchi wanaweza kuhoji kwa nini hamjengi zahananti ,mahospitali na kila kitu japo iwe kwa kulipa lakini kwa bei nafuu ,jawabu ni kuwa Sultani CCM anatia mguu wake na kuzuia kwa hila za kila aina.

Pili wananchi waeleweshwe kuwa wataweza kupima maendeleo ya Wananchi pindipo watafanikiwa kuwakilishwa na wabunge wengi kutoka kambi ya Upinzani kwa maana asilimia kubwa ipatikane katika upinzani kiasi ya kuweza kutumia nguvu ya kura katika kupitisha na kupinga na vilevile nguvu ya uwingi katika kuhoji na kushinikiza bungeni.

Sasa hayo ni baadhi ya mambo ambayo upinzani utatakiwa uwajulishe wananchi kila wakati na kila kwenye mikutano ili mwananchi ajue kinachoendelea na kinachowasibu wapinzani hata ikawa hawaonekani katika kuendeleza maisha ya mwananchi,maana tunawasikia pembeni wananchi wakihoji upinzani haujatufanyia chochote na kura tunawapa,kunahitaji mwananchi huyu kueleweshwa ili kuilinda kura yake isirudi au isipotee kwa kukata tamaa,ni lazima aeleweshwe na aelewe.

Ikiwa kama nipo upande wa uwananchi ningependa Vyama vya upinzani kuwa na msimamo uliomkali rightwing,fundametalist,ngangari,usiotetereka usioyumba wala kuyumbishwa ,yaani hakuna mchezo wala kulegeza kamba ,tunaposema CCM ni mafisadi basi tuwachanganye wote ,hakuna kumuona mmoja ni afadhali kuliko mwengine,hilo napenda uwe msimamo wa Upinzani,kama upinzani ukisema serikali iliyopo madarakani inawalinda mafisadi basi ijumuishe vyombo vyote vya serikali bila ya kukibakisha hata kimoja,kwamba vyote havitendi sawa na kama kipo kinachodai kutenda sawa lakini utendaji wake haufuatwi ,ningeomba upinzani udai kujiuzulu kwa huyo anaesema maneno hayo ,kama tuliiimbia serikali ipambane na madawa ya kulevya na Saidi Mwema akasema kuwa mambo hayo si rahisi na kuna maneno aliongezea nimeyasahau,basi upinzani udai kuwa Saidi mwema ameshindwa kazi hafai na aondoke katika cheo hicho, kama kasi ya mauaji ya albino imezidi na Waziri husika haonekani kupambana na hali hiyo ,upinzani umvalie njuga na kumuumbua kila kona ya Tanzania hii kuwa ameshindwa kazi haina haja ya Raisi wala Waziri Mkuu kumtetea ,halikadhalika katika ujambazi ,na hivyo hivyo katika elimi na hivyohivyo katika afya ,Vyama vya upinzani ni lazima vipambane na vituo hivi vya serikali katika kudai hali ya maisha bora kwa kila Myanzania ,ni lazima nyenzo hizi zikandiwe na vyama vya upinzani bila ya kuvipa nafasi ya kupumua ,kwa lugha nyingine vipambane katika mazingira ya wizara na shughuli zake zinazoonekana hazipo hazionekani mbele ya wananchi ,kuna maji,umeme ,zahanati,walimu wenye taaluma,ulinzi wa raia ,tunaona majambazi wanatoka toka wanakotoka mpaka wanafika katikati ya jiji na kufanya ujambazi na kisha wanatoka ndani ya mji wakiwa hai ,hii inamaana security ni mbovu na ni ndogo.natumai nimeeleweka.
 
Mkandara, SISIEMU imeoza! Tusitegemee mabadiliko ya aina yoyote ile ndani ya SISIEMU. Swala la UFISADI liko wazi na MAFISADI wanafahamika, kuna chochote kile kilichofanywa na Serikali ya SISIMU?? Swala la DOWANS, RICHMOND nk, linajulikana na walioisababishia nchi hasara kubwa kutokana na kampuni hizi wanajulikana lakini kuna yeyote yule aliyeshughulikiwa kikamilifu???

Ukija kwenye swala la IPTL nchi imekula hasara ya kutosha kabisa, nini kiliendelea au kinaendelea kwenye mchakato mzima wa kuwawajibisha waliosababisha hasara hii kubwa kwa Taifa?

Kwa kifupi tusitegemee mabadiliko yoyote yale ndani ya SISIEMU. Wakati wa mabadiliko umefika. "TANZANIA BILA YA CCM INAWEZEKANA"

Mkuu sote tunaelewa fika mapungufu yote haya na nadhani wewe na mimi ndio tunaelewa kwamba CCM imeoza..lakini je wao wanafahamu au wanaamini hivyo?.. na kama hawaamini nadhani huu ni uwanja mzuri wa kusema Uozo huo ili wapte kuona makosa yao ktk utawala..Na pnengi kuonyesha nguvu ya kura yako kwa maneno ya leo.. Mkuu wangu tunda CCM limeoza na halifai kabisa kuliwa, sio lazima ziliwe lakini mbegu zake zinaweza tumika kama mbegu ya mazao mapya.
Binafsi nadhani tunapotazama swala la Richmond na Dowans ni swala la kufahamu utata wake unatokana na kitu gani. Ni swala la kuwauliza CCM wameshindwa kipi kuwasimamisha wahusika ktk swala ambalo ndilo chimbuko la kuundwa kwa taasisi maalum ya TAKUKURU kushughulikia maswala lkama hayo..Ni ujinga mkubwa, upotoshaji na matumizi mabaya ya fedha ya serikali kama tutaunda sheria na chombo kushughulikia Ufisadi kisha chombo hicho kimeshindwa kumsimamisha mtu hata mmoja toka kimeundwa. Sheria hutungwa kutokana na mazingira yaliyopo hivyo sioni sababu kabisa ya kuunda sheria mpya zinazohusianana na Mafisadi lakini hadi leo hatuna case hata moja. Hao kina Jeetu Patel, Yona na Mramba walikuwa hatiani toka enzi za Mkapa na sheria zote walizovunja zilikuwepo toka wakati ule...

Wizi wa EPA na BoT ambao hata waziri wa fedha Mama Meghji alifikia kulidanganya bunge ni ushahidi tosha kabisa wa sisi wananchi kukiwajibisha chama kizima cha CCM..Na uwanja huu ni katika jitihada za kupanga madai yetu kwa kile tunachotaka kuona kikifanyika iwe na vyama vya Upinzani au chama tawala...Nadhani ni wakati muafaka wa kuuliza kwa nini Lowassa hajafikishwa mahakani kuhusiana na Richmond.. tusipouliza CCM hawana sababu ya kujibu..

Tusijidanganye mkuu wangu CCM is here to stay na itakuwepo hata kama Kikwete ataondoka, lakini madudu yao yanaweza kukoma tu ikiwa sisi tutaweza kuwaonyesha kwamba uwezo,sababu, na nia tunayo..
 
- Hivi Zitto ni Chadema au CCM-Mtandao?

FMES!

ni vigumu kuusemea moyo wa mwenzi wako, lakini tunavo muona ni CHADEMA na kiongozi wa chama hicho, lakini kikubwa zaidi juzi alifanya mkutano wa kumnadi mgombea wa chama chao huko Busanda, halikusalia jiwe juu ya jiwe, full picture anayo Ngeleja ambaye ilibidi akimbie kama mwizi kukwepa kibano cha walala hoi.
 
Vyama vya upinzani either viongozi wao waende shule or wa hire consultants in various fields and develop policy.. They all lack policy, CCM likes us to think they have it but in effect they too dont. But they're not the ones that want change.. SO I suggest policy be developed. Then I can run it across my head whether or not I want such a government. We dont want upredictability. Anyone with an average sized brain and upwards knows ufisadi is not even the main problem in Tanzania. It is only a manefestation of the problem. So we dont need a governemnt of 'pop' culture. We need a leadership of vision. EDUCATION.
 
Tatizo ni njaa dot com,wanapewa kidogo dogo wakati uchaguzi ukikaribia wanaingia mkenge. Na sheria ya kupata ruzuku ni idadi ya kura za Ubwana Magogoni ndio maana Lyatonga never miss. Hawana nia nao ya dhati ya kutukomboa.
 
Naona ishu kubwa inayotawala discussion humu ndani ni huu ufisadi. Kitu tunachokisahau ni watumishi wa umma (public servants) walivyooza Tz. Kwa mfano polisi, wizarani, nk.

Swali: Je hata kama CCM itaondolewa madarakani, upinzani utaweza kuboresha nchi na muozo uliopo ndani?

Labda tunasahau kuwa tatizo letu ni zaidi ya chama kinachoongoza. Maana upinzani hautaweza kuanza na timu mpya katika kila sekta. Na hivyo, watu hawa tutapambanaje nao?
Na kuipeleka serikali mahakamani ndo ujue utakufa ukisubiri haki yako.
 
Naona ishu kubwa inayotawala discussion humu ndani ni huu ufisadi. Kitu tunachokisahau ni watumishi wa umma (public servants) walivyooza Tz. Kwa mfano polisi, wizarani, nk.

Swali: Je hata kama CCM itaondolewa madarakani, upinzani utaweza kuboresha nchi na muozo uliopo ndani?

Labda tunasahau kuwa tatizo letu ni zaidi ya chama kinachoongoza. Maana upinzani hautaweza kuanza na timu mpya katika kila sekta. Na hivyo, watu hawa tutapambanaje nao?
Na kuipeleka serikali mahakamani ndo ujue utakufa ukisubiri haki yako.

Uzoefu unaonyesha kuwa watanzania ni wachapa kazi wazuri sana wakipata uongozi bora. Mfano mzuri mdogo ni makampuni/institution za serikali zinazo/zilizo binafsishwa. Ukiangalia utakuta sana sana wafanyakazi wapya wanaoletwa mle hawazidi kumi, na wengi wao ni kwenye management level. Pia wanaokuwa retrenched ni wachache sana (wezi na wazembe). Vivyo hivyo kwenye serikali kama chama chenye viongozi bora kikichukua nchi, ni wachache sana watakaoachishwa kazi (hiyo lazima maana kuna mizigo isiyobebeka), ila cha msingi ni kuhakikisha kila sekta inapata uongozi wenye discipline kutokea juu. Kukishakuwa na dira na ground rules, hii nchi hutaiamini ndio ile ilikuwa ikiteswa na CCM kivile.

Matatizo ya watanzania yanasababishwa na CCM. Nasita kumlaumu mwingine yeyote kwa uzembe na kutowajibika wakati pale juu pameoza. Watu wanaongozwa kwa mifano bwana. Usifikiri hawa dada dala tunaowalaumu kila siku kusimama ovyo barabarani na kuvunja sheria watakavyo bila kujali kwamba ni bahati mbaya. Mtu gari linamharibikia barabarani hajali kulisukuma pembeni anatengenezea hapo hapo tena bila hata ya kuwa na triangular reflector wala nini. Mama wajawazito kutukanwa na manesi hospitalini hadi watoto kufa kabla ya kuzaliwa, Au pale ardhi uko ofisini kwa mtu badala ya kukusikiliza anapiga soga kwenye simu unangoja saa nzima kisha anakuambia nenda urudi kesho. Wafanyakazi kufika ofisini saa 1 lakini wanaacha koti kwenye kiti siku nzima na mambo kama hayo. Yote ni mazao ya CCM. Watu wanajijali wao tu, hawana hata chembe ya kuwajali wenzao. Ndicho kikubwa CCM ilichojengea watu wake.

Ni kwa sababu pale juu hakuna mtu anayejali wenzake. Aliye pale juu yuko bize kwenye dili na Rostam. Na hawa watu wa chini wanalijua hilo, kwamba jamaa yuko bize anaiba. Mtu wa chini yake akimpelekea ishu ya wizi, yeye ndio eti ashupae nayo, ataanzia wapi? Na huku anajua akiipeleka popote anajishtaki mwenyewe, maana alipokuwa anasuka dili na Rostam aliwahusisha baadhi ya watendaji wake ambao sasa akitaka kumshughulikia huyu mwizi lazima pia awahusishe. Anaona haina tija hivyo anakaa kimya. Kesho huyu jamaa akiletewa kesi ingine kama hiyo wala hahangaiki tena kuipeleka mbele. Finally wezi wote wanashtukia kwamba kumbe hata ukiiba hakuna wa kukufanya lolote maana wote wezi. Basi kila mmoja kazi kuiba tu. Kuiba si lazima uwe ofisini. Hata kusimamisha gari liliokufa katikati ya barabara na kuwasimamisha wenye haraka zao bila sababu ni wizi. Nchi haiwezi kuendelea kama watu hawathamini muda wa wenzao. Watathamini je kama wanajua hata wasipofanya hivyo hakuna wa kuwachukulia hatua?

CCM imeondoa dhana ya uwajibikaji. Watu hawajali tena wenzao wala mambo ya umma. Ukiondoa CCM na kurestore hiyo hali mambo yatabadilika by far by fast.
 
Na unategemea itachukua muda gani kwa upinzani kubadilisha utendaji ndani ya serikali?
Sina uhakika serikali ina-employ watu wangapi, lakini nadhani inaweza ikawa karibia asilimia hamsini ya wafanyakazi wote nchini.

Njia moja ya kuboresha utendani ni kupunguza wafanyakazi. Na itapelekea kuwagusa hiyo asilimia 50 ya total work force. Upenzi (popularism) kwa upinzani kweli utaendelea hapo?

Tatizo la utendaji bora nadhani lilianza kwanzia enzi za ujamaa, ambapo sera ya serikali ilikuwa kutoa employment kwa watu wote. Na hivyo kutoa job security hata kama unaboronga kazini. Sasa kurekebisha hapo sio kitu cha siku moja.

Kurudisha integrity katika system nzima itachukua zaidi ya miaka mitano na hata kumi. Walimu kurudi mashuleni, Ma-profesa kufundisha kikweli, polisi kuwatii wananchi na sio kuwaonea, nk...

Pia ukumbuke, power is corruptive. Mpinzani na yeye anaweza kugoma kuondoka - eg: Kenya. Sasa hapo si tutakuwa tunazunguka mbuyu?
 
Naona ishu kubwa inayotawala discussion humu ndani ni huu ufisadi. Kitu tunachokisahau ni watumishi wa umma (public servants) walivyooza Tz. Kwa mfano polisi, wizarani, nk.

Swali: Je hata kama CCM itaondolewa madarakani, upinzani utaweza kuboresha nchi na muozo uliopo ndani?

Labda tunasahau kuwa tatizo letu ni zaidi ya chama kinachoongoza. Maana upinzani hautaweza kuanza na timu mpya katika kila sekta. Na hivyo, watu hawa tutapambanaje nao?
Na kuipeleka serikali mahakamani ndo ujue utakufa ukisubiri haki yako.

Ngugu yangu wala usiwe na wasi katika hili la kubadilika kwa WaTanzaia. Mtoto akizaliwa akiishi na mbwa tu, atatembea, kula na kulia kama mbwa kutokana mfumo wa masiha yake. Kwa maana hiyo watanzania wameharibiwa na mfumo tu, ukiubadilisha nao watabadilika.

Hata siku moja usitegemee eti raia fulani akiamua kuwa mbaya sana (MUWAJI, MWIZI n.k) ukadhani itakuwa na athari kwa taifa, lakini pale kiongozi mkuu wa nchi anaposhindwa kusimamia nafasi yake, ndipo rushwa, kulindana, wizi utawala wa kibabe na mambo kama hayo hushamiri.

Vyama vitaweza zaidi tu, ilimradi atakayepata fursa (hapa ni kwa mujibu wa sheria na sio kubebwa na wenye masilahi, yaani awe mtu SAFI) asimame katika nafasi yake kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo. Jikumbushe JK alivyochukua nchi miezi ya kwanza, lakini alipojiszungushia na huku nyuma akijua siri ya kufikia ukuu.... siku hizi kapoa kuliko maji ya mtungi.
 
Na unategemea itachukua muda gani kwa upinzani kubadilisha utendaji ndani ya serikali?
Sina uhakika serikali ina-employ watu wangapi, lakini nadhani inaweza ikawa karibia asilimia hamsini ya wafanyakazi wote nchini.

Njia moja ya kuboresha utendani ni kupunguza wafanyakazi. Na itapelekea kuwagusa hiyo asilimia 50 ya total work force. Upenzi (popularism) kwa upinzani kweli utaendelea hapo?

Tatizo la utendaji bora nadhani lilianza kwanzia enzi za ujamaa, ambapo sera ya serikali ilikuwa kutoa employment kwa watu wote. Na hivyo kutoa job security hata kama unaboronga kazini. Sasa kurekebisha hapo sio kitu cha siku moja.

Kurudisha integrity katika system nzima itachukua zaidi ya miaka mitano na hata kumi. Walimu kurudi mashuleni, Ma-profesa kufundisha kikweli, polisi kuwatii wananchi na sio kuwaonea, nk...

Pia ukumbuke, power is corruptive. Mpinzani na yeye anaweza kugoma kuondoka - eg: Kenya. Sasa hapo si tutakuwa tunazunguka mbuyu?

Unajichanganya sana...... weka wazi point yako
 
Uzoefu unaonyesha kuwa watanzania ni wachapa kazi wazuri sana wakipata uongozi bora.
Mmmhhhhh!!! una uhakika na hilo? Mwalimu unashindwa kufundisha utasingizia uongozi? Lecturer unatoa marks za chupi kweli utasingizia uongozi? Wewe unachukua pesa kwa mafisadi ili wasilipe kodi TRA, kweli matatizo ni uongozi?

Uongozi nakubali ni tatizo lakini pia sisi wote kama Watanzania tuna matatizo makubwa sana.

Unakuta watu mpaka kwenye nyumba zao ambako wao ni viongozi bado ni maguvu tu, kwenda kujichana nje huku familia inaumia na ujinga mwingine.

Sawa CCM ni tatizo lakini wanafanikiwa kuafanya hivyo kwasababu sisi pia wananchi tuna matatizo mengi sana kwenye utendaji na kuwajibika.
 
Tatizo kubwa watanzania ni sisi wenyewe.Kuna kamanda fulani polisi hapa nchini alijaribu kurudisha nidhamu na kuwakamata askari wake wala rushwa.mungu wangu alifanyiwa vituko,vya askari kunyanyasa wananchi nk.kwa uapnde wa matrafiki walinyanyasa wenye magari na madereva mpaka ikawa adha.Kiongozi akisimamamia uwajibikaji wafanyakazi wakawa na malalamiko kibao.Kiongozi akiwa mzuri tutamkosoa.Tanzania na watanzania balaa.
 
Mmesahau yaliyowakuta Kenya 2001? Kung'oa ujinga sio kazi rahisi.
Huyu jamaa amesema vizuri sana:
Mmmhhhhh!!! una uhakika na hilo? Mwalimu unashindwa kufundisha utasingizia uongozi? Lecturer unatoa marks za chupi kweli utasingizia uongozi? Wewe unachukua pesa kwa mafisadi ili wasilipe kodi TRA, kweli matatizo ni uongozi?

Uongozi nakubali ni tatizo lakini pia sisi wote kama Watanzania tuna matatizo makubwa sana.

Unakuta watu mpaka kwenye nyumba zao ambako wao ni viongozi bado ni maguvu tu, kwenda kujichana nje huku familia inaumia na ujinga mwingine.

Sawa CCM ni tatizo lakini wanafanikiwa kuafanya hivyo kwasababu sisi pia wananchi tuna matatizo mengi sana kwenye utendaji na kuwajibika.

Uzoefu unaonyesha kuwa watanzania ni wachapa kazi wazuri sana wakipata uongozi bora.

TTCL imebadilika? Mfano mwingine je?
 
Unajichanganya sana...... weka wazi point yako

My point is....IT'S NOT AS SIMPLE AS ABC. Kubadilisha utendaji nchini sio rahisi hata kidogo. Blame kubwa imewekwa juu ya CCM, lakini pia lazima ujiulize, CCM inamgusaje profesa wa chuo kikuu katika kuwafundisha wanafunzi?...and so forth....

Umeelewa? I suggest u shld re-read my post slowly.
 
My point is....IT'S NOT AS SIMPLE AS ABC. Kubadilisha utendaji nchini sio rahisi hata kidogo. Blame kubwa imewekwa juu ya CCM, lakini pia lazima ujiulize, CCM inamgusaje profesa wa chuo kikuu katika kuwafundisha wanafunzi?...and so forth....

Umeelewa? I suggest u shld re-read my post slowly.

Kikubwa kinacho control maisha ya mwanadamu ni attitude. Ukishaamini huwezi kufanya jamo fulani lazima utashindwa. No body says it's simple but it doesn't mean it's impossible. CCM ndio inachukua blame yote maana ndio kiongozi wetu. Hao maprofesa na walimu ambao hawafundishi au wanatoa maksi za chupi wanachukuliwa hatua gani? That's the key point! Ni maprofesa wa vyuo gani? serikali tu au hata vya private? Kwa nini? Ni nani anaiongoza serikali?? Manesi, madaktari, walimu, n.k wenye matatizo ni wa serikali tu sijawasikia wa sekta binafsi. Ni kwa sababu huko kuna uongozi wa kuwajibika.

Mbona makampuni ya private yana ufanisi wa juu siku zote, na wafanyakazi wake ni watanzania? Inakuwaje tuko bize kushawishi wenzetu kwamba eti watanzania hawawezi kufanya mambo mazuri, makubwa wakati mifano hai ipo? Uongozi wa CCM unamgusa kila mtu. Mtu akichemsha kazi au akienda kinyume na taratibu na achukuliwe hatua sirias. Litakuwa fundisho kwa wengine kama system yote iko hivyo, na nchi itabadilika.
 
Uzoefu unaonyesha kuwa watanzania ni wachapa kazi wazuri sana wakipata uongozi bora. Mfano mzuri mdogo ni makampuni/institution za serikali zinazo/zilizo binafsishwa. Ukiangalia utakuta sana sana wafanyakazi wapya wanaoletwa mle hawazidi kumi, na wengi wao ni kwenye management level. Pia wanaokuwa retrenched ni wachache sana (wezi na wazembe). Vivyo hivyo kwenye serikali kama chama chenye viongozi bora kikichukua nchi, ni wachache sana watakaoachishwa kazi (hiyo lazima maana kuna mizigo isiyobebeka), ila cha msingi ni kuhakikisha kila sekta inapata uongozi wenye discipline kutokea juu. Kukishakuwa na dira na ground rules, hii nchi hutaiamini ndio ile ilikuwa ikiteswa na CCM kivile.

Matatizo ya watanzania yanasababishwa na CCM. Nasita kumlaumu mwingine yeyote kwa uzembe na kutowajibika wakati pale juu pameoza. Watu wanaongozwa kwa mifano bwana. Usifikiri hawa dada dala tunaowalaumu kila siku kusimama ovyo barabarani na kuvunja sheria watakavyo bila kujali kwamba ni bahati mbaya. Mtu gari linamharibikia barabarani hajali kulisukuma pembeni anatengenezea hapo hapo tena bila hata ya kuwa na triangular reflector wala nini. Mama wajawazito kutukanwa na manesi hospitalini hadi watoto kufa kabla ya kuzaliwa, Au pale ardhi uko ofisini kwa mtu badala ya kukusikiliza anapiga soga kwenye simu unangoja saa nzima kisha anakuambia nenda urudi kesho. Wafanyakazi kufika ofisini saa 1 lakini wanaacha koti kwenye kiti siku nzima na mambo kama hayo. Yote ni mazao ya CCM. Watu wanajijali wao tu, hawana hata chembe ya kuwajali wenzao. Ndicho kikubwa CCM ilichojengea watu wake.

Ni kwa sababu pale juu hakuna mtu anayejali wenzake. Aliye pale juu yuko bize kwenye dili na Rostam. Na hawa watu wa chini wanalijua hilo, kwamba jamaa yuko bize anaiba. Mtu wa chini yake akimpelekea ishu ya wizi, yeye ndio eti ashupae nayo, ataanzia wapi? Na huku anajua akiipeleka popote anajishtaki mwenyewe, maana alipokuwa anasuka dili na Rostam aliwahusisha baadhi ya watendaji wake ambao sasa akitaka kumshughulikia huyu mwizi lazima pia awahusishe. Anaona haina tija hivyo anakaa kimya. Kesho huyu jamaa akiletewa kesi ingine kama hiyo wala hahangaiki tena kuipeleka mbele. Finally wezi wote wanashtukia kwamba kumbe hata ukiiba hakuna wa kukufanya lolote maana wote wezi. Basi kila mmoja kazi kuiba tu. Kuiba si lazima uwe ofisini. Hata kusimamisha gari liliokufa katikati ya barabara na kuwasimamisha wenye haraka zao bila sababu ni wizi. Nchi haiwezi kuendelea kama watu hawathamini muda wa wenzao. Watathamini je kama wanajua hata wasipofanya hivyo hakuna wa kuwachukulia hatua?

CCM imeondoa dhana ya uwajibikaji. Watu hawajali tena wenzao wala mambo ya umma. Ukiondoa CCM na kurestore hiyo hali mambo yatabadilika by far by fast.


Na uzoefu unaonyesha kwamba CCM haiwezi kutoka pale ilipo kutokana na kwamba Viongozi wengi wa vyama vya upinzani ni wepesi sana kurubunika na hela za Mafisadi kama tulivyoona hivi karibuni na bado naamini tutaendelea kuwaona.
 
Back
Top Bottom