Ninauguliwa na baba watoto wangu

Ninauguliwa na baba watoto wangu

Status
Not open for further replies.
Ni kweli ana roho nzuri. Ila kama ni mkristo, sio tu ugonjwa, hata mwenza anapofariki hawaziki had mke/mume awepo. Hata kama mlitengana kitambo
Teh..watagoma kuzika mpaka lini kama mwenza kakataa kwenda? Hao watakuwa si wakristu bali wakristu jina!
 
I am a christian, Na ninajitahidi sana kubadilika. Kwa suala hilo itategemea na vitu vingi. Unitelekeze ule ujana peke yako, uzeeni uugue hlf utegemee nikuuguze. Mungu anisaidie yasinitokee!
Roho hii
 
Mimi bana utanisamehe siwezi kukupa pole kwakuuguliwa na jambazi huyu. Umeandika uzi wako ili uweze kuonewa huruma na Watanzania kwakuwa ni watu wa ajabu sana eti wanajifanya wanahuruma na mtu aliyetelekeza watoto wako tena wanne kwa miaka yote hiyo, huruma hii inatoka wapi, anafaida gani huyu mtu aliyeacha watoto ili wawe chokoraa pasi na wewe kujifunga kibwebwe. Hata wewe na kina mama wote nawashangaa sana huwa mnahurma za ajabu sana, wewe ulipaswa kuja hapa kuomba msaada tukusaidie kusomesha watoto ningekuelewa na kukusaidia kwa moyo mmoja, lakini baada ya miaka kadhaa ya kuteseka kusomesha watoto bila mume, leo huyu jamaa anaibuka eti anaumwa, mwache tu afe wamekufa watu muhimu kuliko yeye ambaye amepotezea watoto wako. Mimi nawashauri watu msitoe mchango, si kwamba kila mtu akiomba mchango lazima tumpatie eti kwakuwa tunamfahamu bila kuangalia kuwa hizo sababu ni juftiable. Kuna watoto yatima wengi wanapatashida, hawana ada, hawana vyakula, mavazi wanahitaji msaada pelekeni huko lakini si kwahili baba lililotelekeza watoto wake mwenyewe. Sorry kama nimewakwaza naomba tu tujifunze kukubali kutofautina hoja na tuliheshimu hilo. Sikupi pole kwahili.

Nimekuja kwenu rasmi kuleta taarifa hii ya kuuguliwa na bwana ambaye nimezaa naye watoto wangu wote wanne.

Kweli tulifikia mahali kimaisha tukatengana tokea 2001. Kila mmoja akiwa na maisha yake huku nikiwa na changamoto kubwa na kali za kulea watoto ambao ilibidi nibaki nao, hayo kwa sasa tuyaweke pembeni.

Hadi ninavyoandika huu uzi hakuna mtoto hata mmoja ambaye ameshapata kibarua wote wapo kwenye kuhangaika kutafuta kazi.

Ilipofikia mwaka jana mwishoni nikapata taarifa ya kuwa yule bwana niliezaa naye anaumwa, nikajuwa ni homa za kawaida tu.

Leo kaka yake ndo ananipigia simu na kusema kuwa mdogo wake amezidiwa sana na alikuwa amezimia ila kazinduka tena juzi.

Kwangu hiki kitu ni kikubwa nimeshindwa kukibeba.

Kwenu wana jamii kwa upendo wenu ninaomba mnichangie nauli ili niweze kwenda huko Mbeya kumwona huyo mgonjwa. Kama mnavyojua mahali penye ugonjwa mkubwa pia panahitajika hela ya matumizi mengineyo.

Kwa wana jamii wa Mbeya mnaweza kwenda kumuuona nyumbani ni Sae.

Naomba tu msinitukane maana nitalia;[/QUOTE]
 
Ushimen naona ulikua haujatoka kwenye lindo ndo umeliviwa sasa hivi.
Nilikumiss kwa mda na hiyo avatar yako...maana naona kama ya kweli na utani wako inaendana.
Em njoo chemba kwanza tuunge urafiki.
 
Ushimen naona ulikua haujatoka kwenye lindo ndo umeliviwa sasa hivi.
Nilikumiss kwa mda na hiyo avatar yako...maana naona kama ya kweli na utani wako inaendana.
Em njoo chemba kwanza tuunge urafiki.
 
Be positive itakusaidia sana kama hauwezi basi ukiona jambo linakukereketa unakaa kimya.

Tulioguswa acha tuchange tukiibiwa ni za kwetu na siku ukiwa na shida andika tukiguswa tutatoa pasipo hata kuchunguza Id yako. Uwe na wakati mwema.
Usipokunywa yale matapu tapu yako unakua na akili sana wewe
 
Jamani wana jamii, wengi ni watoto wangu, wengine ni wahenga wenzangu;
Hivi hao wanaonitukana huko juu hawamwogopi Mungu?

Laiti mngejuwa kuwa ni maisha gani nimeisha tokea huyo baba yenu
tutengane wala msingeenda huko;

Nashukuru kwa michango; pia kuna kijana wangu amesema atanipa tiketi so
niwasiliane naye kesho jumamosi.

Mungu akipenda nitaondoka dar jumapili kwenda huko mbeya
kumwona huyo mgonjwa; na nitakuwa nawajulisha hatua kwa hatua kuhusu hiyo safari.

Kweli nawashukuru sana, watu wa MUNGU mlioguswa hata mkaingiza mikono yenu mfukoni
na kumega mkate wa familia yenu kunipa. Naamini kuna siku Mungu atawakumbusha michango
yenu mliyonitolea;
Hao wanaokeji ni watoto wapuuzie tu Mamie... Tuko pamoja
 
Asanteni kwa wote mlioguswa na ujumbe wangu huu;
Mungu awabariki tu jamani;

Kuna aliyeuliza kama nilishaingia mahusiano mengine, jibu ni hapana;
nilikuwa na changamoto kubwa ya kusomesha sikuweza tena kuanza mahusiano.

Yupo pia alieuliza why nimekosa nauli, hapa siwezi kusema sana ila kweli
hela ingekuwepo wala nisingekuja huku;

Naomba niweke tu namba yangu kwa ajili
ya hao wapendwa waliouliza huko juu 0755 557094.

Asanteni sana!
ADELINE SIAME nimejaribu kukutumia chochote mtambo ukasema NOT ALLOWED
 
Mkuu Kayaman

Unakosea.

Kwanza ni haki yao kutoa mawazo yao kama wewe ulivyotoa hapa.Aidha kupinga au kukubali.Usi-criminilize mtu kwa kua tofauti na wewe.

Huyu dada Mamdenyi angewafata wote anaojuana nao wangemsaidia.Ndio tunavyofanya wote humu duniani!Sio kuweka pakuli kwenye public namna hii ambapo tupo wengine huku wenye haki ya kuongea chochote!

Wote tunapata vipato hivi hivi anavyopata Mamdenyi na wewe na wengine.Tuna shida the same.Tatizo ni upayukaji.

Watu aina ya Mamdenyi wapo kwenye jamii,tunakaa nao..wanapenda shida zao wapayukie jamii ibebe kumsaidia.Wapo sana tu,mimi binafsi I can not lie,I hate them to the guts!
Sasa kama amewaomba hao uliowataja na hakupata ulitaka akajiuze ili apate hiyo hela? haya maisha tu ipo siku utaelewa kwanini watu huwa wanaomba msaada!
 
Salaam sana wana MMU wote;

Nimekuja kwenu rasmi kuleta taarifa hii ya kuuguliwa na bwana ambaye nimezaa naye watoto wangu wote wanne.

Kweli tulifikia mahali kimaisha tukatengana tokea 2001. Kila mmoja akiwa na maisha yake huku nikiwa na changamoto kubwa na kali za kulea watoto ambao ilibidi nibaki nao, hayo kwa sasa tuyaweke pembeni.

Hadi ninavyoandika huu uzi hakuna mtoto hata mmoja ambaye ameshapata kibarua wote wapo kwenye kuhangaika kutafuta kazi.

Ilipofikia mwaka jana mwishoni nikapata taarifa ya kuwa yule bwana niliezaa naye anaumwa, nikajuwa ni homa za kawaida tu.

Leo kaka yake ndo ananipigia simu na kusema kuwa mdogo wake amezidiwa sana na alikuwa amezimia ila kazinduka tena juzi.

Kwangu hiki kitu ni kikubwa nimeshindwa kukibeba.

Kwenu wana jamii kwa upendo wenu ninaomba mnichangie nauli ili niweze kwenda huko Mbeya kumwona huyo mgonjwa. Kama mnavyojua mahali penye ugonjwa mkubwa pia panahitajika hela ya matumizi mengineyo.

Kwa wana jamii wa Mbeya mnaweza kwenda kumuuona nyumbani ni Sae.

Naomba tu msinitukane maana nitalia;

Sasa tukifika SAE tunaanzaje kumuuliza maana hujatoa location halisi nyumba ilipo. Mie nimekuja kikazi mbeya nimefikia hapa Golden City Hotel SAE
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom