Nimemsikiliza Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) na mipango ya kuinua uwekezaji hakika nimefarijika sana

Baba Oruch

Member
Nov 4, 2023
51
92
Leo nilikuwa nafuatilia mahojiano katika channel ya Zamaradi TV kati ya mtangazaji na Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji Tanzania ndg Gilead Teri. Katika mahojiano hayo, Mkurugenzi alijikita zaidi katika kuangazia mageuzi makubwa yanayofanywa na kituo hicho na zaidi namna wanavyotembea kwenye ndoto na maono ya Rais Samia katika kuona uwekezaji unakuwa nguzo kubwa ya kukuza uchumi wa nchi yetu. Mambo ambayo yamenifariji na naamini wale wenye ndoto ya kuwekeza watajifunza ni kama ifuatavyo;

1. Kuwawezesha wawekezaji kuanza kutumia mtaji wao wa uwekezaji bila kulipia Kodi ya VAT na badala yake mwekezaji anaweza kulipia ndani ya miezi 36. Ametolea mfano wa kichwa/vichwa vya roli kwamba mwekezaji anaweza akaanza shughuli za usafirishaji na akizalisha ndani ya muda uliopangwa atawasilisha/kulipia kodi ya VAT. Hii imeleta/italeta unafuu kwa wawekezaji na haya ndio mazingira wezeshi yanayopigiwa kelele kila siku na wadau na Kwa hatua hii, hakika uwekezaji utaongezeka sana ndani ya nchi yetu.

2. Kufanya vikao vya mara Kwa mara na wadau waliopo kwenye mnyororo wa uwekezaji kama vile TBS, TRA n.k. Lengo ni kuchochea ufanyikaji wa tathmini na kupunguza mlolongo wa vikwazo katika uwekezaji na hakika ni hatua nzuri katika kuchochea uwekezaji nchini.

3. Kuwatambua na kiwaunganisha wawekezaji wa ndani wenye nia ya kushirikiana na wawekezaji toka nje pindi wakijitokeza katika eneo la uwekezaji lonalofanana.

4. Katika kuyaongea haya alikuwa akiirejea Sheria ya uwekezaji Tanzania iliyotungwa na bunge ya mwaka 2022. Hii Sheria nitaiweka kama attachment ili kila anayetaka kuifahamu iwe rahisi kwake.

Yapo mengi sana mazuri yaliyoongelewa na kwa kifupi haya ni baadhi tu kwa leo. Asante sana Rais Samia na serikali kwa ujumla kwa jitihada za kuendeleza uwekezaji wenye tija Tanzania, asante TIC.
 

Attachments

  • 1674563013-Act No. 10 SHERIA YA UWEKEZAJI TANZANIA, 2022.pdf
    304.5 KB · Views: 11
Wawekezaji wa ndani wameshindwa kuwapa nishati ya uhakika umeme, ndio wataweza kuwavutia Wawekezaji wa nje waje kuwekeza?

NCHI YA AJABU KUWAHI TOKEA.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
Amezungumzia kuhusu umeme na jinsi uwekezaji wa mradi wa umeme wa bwawa la mwl Nyerere utakavyochochea uwekezaji kuanzia mwezi Februari
 
Leteni bandari huru kwa ajili ya nchi jirani ,nia ya kuleta bandari huru ni pamoja na kuchochoe ajiri ,na pia kukiza biashara ya malazi ,mfano atakatoka zambia kuja kununua ni lazima atatafuta mahali pa kulala
 
Changamoto kubwa katika uwekezaji ni FEDHA za kununua mitambo ya uzalishaji na WAFANYAKAZI wenye WELEDI. Bahati mbaya vyote hivyo havipo kwa Tanzania. Kinyume cha hapo nothing tangible will be realized. Serikali iwe pragmatic kushusha riba kwa wawekezaji na kufadhili mafunzo ya kitaalam kwa watanzania nje ya nchi kwa lengo la kuanzisha pool ya laborforce wenye sifa ya kufanya kazi na wawekezaji.
 
kwenye haya mambo ya kuongea ongea watanzania tuko vizuri sana, sasa subiria utekelezaji na matokeo chanya ya hizo hadithi...
 
Leo nilikuwa nafuatilia mahojiano katika channel ya Zamaradi TV kati ya mtangazaji na Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji Tanzania ndg Gilead Teri. Katika mahojiano hayo, Mkurugenzi alijikita zaidi katika kuangazia mageuzi makubwa yanayofanywa na kituo hicho na zaidi namna wanavyotembea kwenye ndoto na maono ya Rais Samia katika kuona uwekezaji unakuwa nguzo kubwa ya kukuza uchumi wa nchi yetu. Mambo ambayo yamenifariji na naamini wale wenye ndoto ya kuwekeza watajifunza ni kama ifuatavyo;

1. Kuwawezesha wawekezaji kuanza kutumia mtaji wao wa uwekezaji bila kulipia Kodi ya VAT na badala yake mwekezaji anaweza kulipia ndani ya miezi 36. Ametolea mfano wa kichwa/vichwa vya roli kwamba mwekezaji anaweza akaanza shughuli za usafirishaji na akizalisha ndani ya muda uliopangwa atawasilisha/kulipia kodi ya VAT. Hii imeleta/italeta unafuu kwa wawekezaji na haya ndio mazingira wezeshi yanayopigiwa kelele kila siku na wadau na Kwa hatua hii, hakika uwekezaji utaongezeka sana ndani ya nchi yetu.

2. Kufanya vikao vya mara Kwa mara na wadau waliopo kwenye mnyororo wa uwekezaji kama vile TBS, TRA n.k. Lengo ni kuchochea ufanyikaji wa tathmini na kupunguza mlolongo wa vikwazo katika uwekezaji na hakika ni hatua nzuri katika kuchochea uwekezaji nchini.

3. Kuwatambua na kiwaunganisha wawekezaji wa ndani wenye nia ya kushirikiana na wawekezaji toka nje pindi wakijitokeza katika eneo la uwekezaji lonalofanana.

4. Katika kuyaongea haya alikuwa akiirejea Sheria ya uwekezaji Tanzania iliyotungwa na bunge ya mwaka 2022. Hii Sheria nitaiweka kama attachment ili kila anayetaka kuifahamu iwe rahisi kwake.

Yapo mengi sana mazuri yaliyoongelewa na kwa kifupi haya ni baadhi tu kwa leo. Asante sana Rais Samia na serikali kwa ujumla kwa jitihada za kuendeleza uwekezaji wenye tija Tanzania, asante TIC.
Ulikuwa na umri gani kipindi Mkapa anatoa misamaha ya Kodi lukuki kwa Wawekezaji lakini tukaishia kupigwa.
Mnakaribisha Wawekezaji kwenye nchi ya rushwa na ukosefu wa Nishati ya uhakika!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Katika watanzania Rais Samia alipatia kuwapa nafasi eneo sahihi ni Gilead Teri. Ana maono,bidii na unyenyekevu wa kusaidia uwekezaji ndani na nje ya Tanzania na anafanya kazi nzuri. Mungu amsaidie kuutumia ujana na nafasi yake kwa uaminifu na kwa maslahi ya wengi.
 
Back
Top Bottom