Okay..
Ndio maana nilisema kuna sababu ya kuzaliwa kwake kwa jinsi alivyo zaliwa.. Ni kaeleza huko juu kwamba Yesu alikuja kwa kazi moja tu kuokoa watu na dhambi..
Kifo chake kusulibiwa.. Aliyempoint Yesu alikuwa Yuda mmoja wa wanafunzi wake.. Sababu ya kufa kwake ni iliitwa kutupatanisha na Mungu..
Kufufuka kwake ni ili tuwe na asili kama yake(Haki) tusitumie nguvu tena kuushinda mwili na tamaa zake
Yohana 1:1.,2.,3.,4.,5.,10.,11.,12.,13.
1. Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
3. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
4. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
5. Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.
10. Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.
11. Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.
12. Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
13. waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.