Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Yesu mara kadhaa amejiita kama mwana wa adamu,je wewe nani umuite mwana wa mungu

Mathayo 9:6
[6]Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (amwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako.
But that ye may know that the Son of man hath power on earth to forgive sins, (then saith he to the sick of the palsy,) Arise, take up thy bed, and go unto thine house.

Che mittoga
 
Jamaa kashaumbuliwa! Ishu ni kwamba viumbe vingi visivyoonekana(malaika, majini e.t.c) ni vina uwezo au kiwango fulani za kujua siri za ulimwengu wa roho ambapo kule kila mtu yupo uchi. Ndo maana binadamu hata tufanye nini tayari mihuli ilishagongwa kwenye ulimwengu wa roho.
Ndo maana magonjwa, ukiua, ukizini ukijifanya hutaki mambo yako yajulikane watu wakienda kwenye watu waliopewa access ya ulimwengu wa roho kule hakujifichi kitu. Kule Unasoma maisha ya mtu hata kabla ya kuzaliwa, e.t.c

Nb; Ni rahisi kutabiriwa kuwa huyu mtu atakuja kuwa na mafanikio makubwa lakini atapitia changamoto kubwa. Laiti tungekuwa tunajua siri za ulimwengu wa roho tusingekua tunacheza na maisha ambapo shetani nae anaingia hapo kuvuruga maisha ya watu..kuna watu Leo hii walitakiwa kuwa watu wa nyazifa za juu, matajiri, e.t.c wamefariki kwa kucheza na maisha mfano kwa magonjwa ndoto hazijatimia. Ulimwengu wa roho unaweza ukatuelekeza ni namna gani tuishi na kuja kufanikiwa.Sema ndo hivo tumefungwa macho hatuoni yambeleni.

Aiseeh; ukijua siri za ulimwengu wa roho utamiliki na kutawala..yaani umeshatoboa...
Ndo maana hata leo hii mtu mwenye access ya ulimwengu wa roho ana uwezo wa kujua hata kubaini manabii feki, utajiri wa mtu kama ni halali au sio, kila kitu unachokitaka.

Nimeamua kufuata hili muda sana nimeelewa kuna mengi sanq tumefichwa nq tunaumizwa sana nq upande wa giza.
 
Kwanza ni Chano sio Chane vurugu nyingi uzi wa mwenzio kumbe wataka kujifunza si ungetuliza komwe lako kuliko chai chai hata sindikiza na maandazi.

Navyojua Chano hupewa kwa mubaliano mfano unataka jambo flani unaongea na jinn akifanikisha unarudisha chano kingine.

Kuna kikubwa na kidogo vinnapangwa kwenye sinia majani ya migomba halwa tende zabibu kavu hiriki mdalasini ndizi pukusa rose sherbet maji ya zamda arki rose essence maji ya zamzam mkate wa mchele hauna hamira pasipasi(manukato al oud) misk oud gulab jamn muwa asali fanta orange mirinda nyeusi(ila zipo zenyewe kwenye chupa walipewa zamani wagonjwa ukikosa basi soda) maziwa mtindi kahawa mpaka henna dhahabu kama jinn la kike kifupi ni hivyo navyokumbuka
Kisha inategemea jinn mwingine anakula anakula mwenyewe vingine anawapa mle mwingine kiwekwe kwa kifunikwa na kitambaa cheupe au chekundu inategemea siku 3/7 kisha kikatupwe baharini kwa Dar najua Salenda bridge kule chini na kurasini.
Chano au Chane ni suala la matamshi tu.

Wewe angalau tutaenda sawa.

Niambie sababu ,sinia kuwekwa kichwani kwa mtu mwenye matatizo.
 
Hata Waka
Ndio nikasema wewe hukuwa muislamu na hujui chochote,ungejua uislamu hata huko usingeenda

Yesu ndio sio mwana wa mungu hata biblia yako inakir hivyo,kuna mistari mingi sana watu wengi wanaitwa wana wa mungu,kwahiyo siyo ajabu yesu kuitwa mwana wa mungu

Nipe andiko moja yesu anasema kwa kauli yale kuwa yeye ni mungu

Pili yesu amekiri mara kadhaa kuwa yeye ametumwa na baba yake,kumbuka kusema baba yake haimaanishi kuwa ni mwana wa mungu,sawa sawa na wewe usema baba yetu wa mbinguni jina lako litukuzwe ufalme wako..... je mungu atakuwa baba yako?
Hata Wakatoriki huwa wananiambia kama unavyoniambia wewe.
Wasionijua nikiwaambia wanasema "Wewe huku wahi kuwa Mkatoriki la sivyo usinge uhama".
Mimi nilikuwa namwuliza Maswali Katekista Hadi ananifukuza kigangoni.

Mimi sio mtu wa Ndio Ndio.
Kwenye Uislamu sikuwahi kujifunza kitu zaidi ya kuzikremu baadhi ya Aya za Qurani na kuziimba kwa Kiarabu.

Baada ya kutulia na kuisoma Qurani na hadithi zake nikagundua kuwa hizi ni Dini tofauti kabisa.
Na Ukristo unajitegemea kama ulivyo Uislamu.
Swali la Uislamu linajibiwa na Qurani na Hadithi zake.
Mwislamu kuanza kumbishia Mkristo kwa mafundisho yake ni kukosa weledi.
Vivyo hivyo kwa Mkristo
 
Hata Waka
Hata Wakatoriki huwa wananiambia kama unavyoniambia wewe.
Wasionijua nikiwaambia wanasema "Wewe huku wahi kuwa Mkatoriki la sivyo usinge uhama".
Mimi nilikuwa namwuliza Maswali Katekista Hadi ananifukuza kigangoni.

Mimi sio mtu wa Ndio Ndio.
Kwenye Uislamu sikuwahi kujifunza kitu zaidi ya kuzikremu baadhi ya Aya za Qurani na kuziimba kwa Kiarabu.

Baada ya kutulia na kuisoma Qurani na hadithi zake nikagundua kuwa hizi ni Dini tofauti kabisa.
Na Ukristo unajitegemea kama ulivyo Uislamu.
Swali la Uislamu linajibiwa na Qurani na Hadithi zake.
Mwislamu kuanza kumbishia Mkristo kwa mafundisho yake ni kukosa weledi.
Vivyo hivyo kwa Mkristo
Acha porojo,jibu ni moja tu hujui uislamu na hata hizo aya hujui mafundisho yake hata kidogo

Kuhusu wakristo kukosa majibu ni sahihi kabisa,ukristo unajichanganya sana na hakuna majibu ya kuridhisha na mtu akakinai na kuelewa

Ndio maana hao mabwana wakubwa huwa hawapendi maswali kabisa
 
Wana ukumbi,

Narudia tena. Toka jana sijibu mtu PM. Mwenye lake, liwe swali au ushauri au ana tatizo aandike hapahapa jukwaa hili, Tutamjibu hapahapa. Nikimjibu mimi mtaona post nimeiandika simba chini, kama ni kajibu Arsis hamtaonakitu kwa sababu ID imekua ni jina lake.

Ahsanteni.
Simba.
 
Sawa, umejibu vyema kabisa.

Niambie unafahamu nini kuhusu jini maiti ?
Navyojua Kuna majini wabaya mapepo wachafu wapo wanakaa makaburini kwenye majalala miti mikubwa na kadhalika ambao huwa ni misubian anaweza kuwa wa kutumwa au Akakuvaa tu, unakuta lingine unatambaa kama nyoka lingine vurugu kuunguruma kama Simba mwingine bubu mwingine anakakamaa anakauka kama maiti anazima.
 
Navyojua Kuna majini wabaya mapepo wachafu wapo wanakaa makaburini kwenye majalala miti mikubwa na kadhalika ambao huwa ni misubian anaweza kuwa wa kutumwa au Akakuvaa tu, unakuta lingine unatambaa kama nyoka lingine vurugu kuunguruma kama Simba mwingine bubu mwingine anakakamaa anakauka kama maiti anazima.
Unafahamu taratibu za kumtoa mtu aliyepandisha jini maiti?
 
Mwanzoni nilianza kuuamini huu Uzi na visa vyake mpaka pale kiumbe Arsis alipoanza kujibu straight maswali ya wadau humu ndiyo nilipopata shaka na ujibuji wake wa maswali na maswali yenyewe-ni aidha hana huo uwezo na elimu niliokuwa naufikiria mwanzo au huu uzi umejaa vitu vya kweli kiasi na vyakusadikika vya kutosha.

Nitaendelea kuufuatilia ila kwa madhumuni ya kujiburudisha na kujifunza kwa masimulizi ya visa vyake.
Uzi huu haukukusudia kumuaminisha mtu chochote. Hii ni elimu iliojificha. Mwenzetu kama una elimu zaidi usiifiche. Wengine sisi ni maamuma. Tunachota kwa yeyote yule halafu akili mu kichwa..
Simba.
 
Kwanini baadhi ya familia hawafanikiwi kwa lolote wanalo fanya mfano ni familia yetu?
Kuna familia koo za kichawi zina maagano mavifungo ya mizimu inabidi muyafungue muone kiongozi wa dini kwa muongozo.
 
Acha porojo,jibu ni moja tu hujui uislamu na hata hizo aya hujui mafundisho yake hata kidogo

Kuhusu wakristo kukosa majibu ni sahihi kabisa,ukristo unajichanganya sana na hakuna majibu ya kuridhisha na mtu akakinai na kuelewa

Ndio maana hao mabwana wakubwa huwa hawapendi maswali kabisa
Hizi Dini wengi wamezirithi tu toka kwa wazazi.
Mkristo msomi hawezi kushindwa kujibu swali la Kikristo.
Kuitwa Shehe au Mchungani sio lazima mhusika ajue kila kitu katika Dini yake.
Elimu ya Dini ni taaluma kama zilivyo taaluma nyingine.

Tatizo wewe kwa mfano:
Unamwuliza swali Mkristo, halafu unataka akujibu kama Uislamu unavyo taka.
Ukristo hujibiwa kwa Ukristo na sio kwa Uislamu
 
Kama angejibu halafu ukaniambia hivi ningenyamaza ila kwa kuwa umeingilia basi inabidi pia kunyamaza nafkiri kwa uelewa wangu hapo ndio nimefika mwisho...kwahiyo nilitaka kuongezewa uelewa tu..!
Sa kwa kuwa wewe uliwaona kwenye movie siwezi kukupinga
Ila Mimi nimewasoma kwenye kitabu kinachheshimika sana..Kitabu cha Enoch...sioni mahusiano hapo kati ya hicho kitabu na Movies...!

Metatron ni henoko
 
Waganga waongo na wachawi wanaojidai waganga, wanaita tu hivyo kutisha watu wajippatie pesa. Huyo ni jini yu hai, anakua ni mtumwa wa kijini aliezeeka sana, anatumiwa kishirikina. Huyo kumtoa ni kama kusukuma mlevi kwa anaejua na mkweli.

Nikupe dawa ya kumkimbiza jini kwenye mwili wa yeyote yule na jini yoyote yule kwa muda?
Simba.
Andika hiyo dawa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom