- Thread starter
- #3,581
Tutafanya hivo.Kwanini hizi post yako usizi link pale kwenye post ya kwanza mtu au watu wakitaka kusoma post inayofuata wanaipata kwenye post ya kwanza
Simba.
Tutafanya hivo.Kwanini hizi post yako usizi link pale kwenye post ya kwanza mtu au watu wakitaka kusoma post inayofuata wanaipata kwenye post ya kwanza
leo chai ya kipemba ya pilipili manga, umeikosa chai ya Tanga ya Anjari, tukanywa chai ya Unguja, ya viungo vyote hio.Chai na joto lote hili
Limejibiwa sana hilo, labda hujaona, kwanza tulilijibu kisha tukakuuliza unafahamu maana ya "khodam"?Post #3201
Vionjo vya Arsis - Majini ya Kojani- Pemba 3.Kuingia tu,
Mzee; Nilitaka kuingia ndani kukufata na wewe unatoka.
Mimi; Mmekuja muda?
Mzee; Hapana, tulipita kwenda kugeuza gari mbele kidogo hapo, tunarudi na wewe unatoka.
Mimi; gari yangu ipo ple kituoni kwa mgteja yule...
Mzee; Basi sisi hatuna haja ya kuingia kule, tutasimama mshikaji shuke akichukue gari aje nayo nyumbani.
Mimi; Poa.
Kufika mshikaji akashuka akaelekea na sisi tukaeleka nyumbani.
Mzee;Npigie simu yule kijana anaweza kumyima gari.
Mimi; Mwache tumuone ujanja wake leo.
Mzee; Yule wanamjuwa mafari yao yote ankuja kuyachukua na kuyarudisha yeye, tatizo kama hajamkuta yule kijana.
Mimi; Wakimyima atapiga simu tutaongea nao. Mwache kidogo akomae.
Mzee; haya nipe habari za huko, maana hizi kazzi za babu yako zinataka moyo kweli kweli. Mimi siziwezi, tena msiniingize tena.
Nikamweleze mwanzo mpaka mwisho.
Mzee; Ndio usharithi hivyo, umekuwa bingwa sasa, unakwenda mpoka Kojani.
Mimi; Waoi hii kazi wamenisukumia tu.
Mzee; Ndio inavyokua hivyo. Simba, niliwaambia nyumbani anakuja mgeni tutakua nae usiku.
Mimi; Umefanya la maana kweli.
Mzee; Kama ni mkwe wetu mpoya nyumbani wamzoee kabisa.
Mimi: Aaah wapi.
Mzee: babu yako huyo ndio aliendsema, nimeongea nae ananambia nasikia leo mkweo wa Kiunguja anakuja kukuktenbelea.
Mimi; Babu utamuweza, kishanambia unakwenda Pemba tafuta wawili.
Mzww; Wawili tena?
Mimi; Mmoja wangu mmoja wake, ninae mumuoa lazima awe na dadake anaoa yeye.
Mzee: babu yako anaweza kweli, majini yashamchanganya kichwa cheke, mwenyewe hua anasema hakuna utani katika ndoa. Yule unafikiri anafanya utani? Yupo serious kweli uoe.
Mimi; Mbina wewe hukuoanmwingine.
Mzee; Mimi naishi maisha ya Kisimba, wewe uliyakimbia. Inabidi uoe.
Mimi: Hilo umesema kweli, sio utani inabidi nioe.
Tukafika nyumbani, ile tunaingiza gari tu hatujakaa dakika tano Mshikaji huyo kaingia na gari.
Mzee: Wamekupa gari?
Mshikaji; Kwani vipi Dingi?
Mzee; Mimi nilifikiri kwa kua kwawachia Simba hawampi mtu mwengine.
Mshikaji; Kwani mimi mtu mwengine, mshikaji yule anaujua ukoo wetu, kwani gari zo kila siku anazileta nani kwao, nani anakuja kuzichukua? Kule gereji wakija wanaomuona nani mtu wa kwanza?
Mzee; Nakuaminia mwanangu hujazubaa kabisa.
Mshikaji; Na nikiiacha mimi gari sehemu akienda Simba huyo hapewi, ataonekana mwizi wa magari tu. We mtu anzaiwasha gari bila funguo bila nini, sasa kama si wmizi wa magari huyu mwanao ni nini?
Mimi; Ujuzi tu, ukionge vizuri nakufundisha.
Mshikaji; hta sitaki kujua, nikujua hio, shetani anaweza kuniingia nikafungua magari ya watu niondoke nayo, nikayabanjue kila kitu nipate tiketi ya kuendea Ulaya.
Mzee: Ulaya tena? Dokta basi tena?
Mshikaji; Yule nikkipata safari ya Ulaya kwanza ananisubiria, huko nakwenda kuoa mdanish, si unajua wale hata wakilala juani hawabadiliki rangi, wanabaki vile vile kama mijusi ya ukutani na nyumaba yenye rangi nyeupe.
Mimi' Kwani wanakua tofauti?
Mshikaji; Wewe watazame mwanangu, mie chumba changu mpaka nikabadili tangi, kilikua na rangi nyeupe, basi mijusi ya chumbani kwangu unaiona mpaka mishipa yao ya damu, akimeza mdudu unamuona mpaka anavyoingia tumbini, sasa jamani eeh Muda umefika, soga baadae.
Huyo akachomoka, na sie tukaingia ndani ile yunaingia kujitayarisha kunaadhiniwa, mie nikaona Magharibi ya msikiti wetu siiwahi, maana yule imamu akimaliza kuadhini tu anakimu. Nikasali chumbani kwangu nikajitupa kitandani wigfe akaja na mwanae mdogo, huyo hamtaki mgtu anamtaka bibi yake tu, leo naona ajabu kakubali chumbai nikamchukua nikaanza kucheza kitandani, anapend nikimfanyia kinyuli.
Nikamuuliza mamake, yule mwengine yuko wapi?
Wofe; kawasikieni na kawaona kawachungukia kutoka jikoni leo anawapikia huko na mama, kapewa chapatizake akande, basi ana unga mwili mzima.
Mimi : na nyie mnamwacha acheze unga jamani?
Wife: Si anakupikia babake ule.
Mimi; Atakula babu yake huko. Maa nasikia sauti ya mshikaji nje huko, kelee. Hoyaaaaaa, mimi nakitoa.
Nikatika chumbani kwenda uani anapiga kahawa, hoyaa mimi sikai nakwenda kusali huko huko palepale jirani ya Barafaa kuna msikiti. Nikamwabia ngoja kidogo muda bdao, ikiadhiniwa unawahi kusali kabisa.
Mshikaji: Dingi anasisitiza hakuna kitu kinaleta mafanikio kama kua mtu kua miadi, on time. Dingi anakwambia bora ufoke mapema usubiri kuliko kuchelewa.
Mshikaji; Wewe ushaona kuna gari ya mteja inachekewa pale, akiona inachelewa siku hio gereji inawaka moto mpka mimi hua namuombea dua huyu Dingi mi presha isimpande. kwa hio mimi hio nimerirhi, wala hanambii, matokeo si nayaona mwanangu?
Mimi; haya nipe michapo na mimi.
Mshikaji; Si kama unanambia nimfundishe samaki kuogelea. Kwanini mimi sikujui wewe? Kuamuoga wa muda kama wewe duniani, hata Dingi kasingiziwa.
Mshikaji; Unasikia mwanangu, mnyonge mnyongeni, Dingi hapa karturuthisha vitu viwili hivyo, sijaviona mahali zaidi ya nyumba hii. Moja miadi, basi mkeo, ndio mwehu kabisa, maza nae ndio utafikiri ana ugonjwa wa wasiwasi. Jingine mwanangu, ukweli. Dingi anasema huo ufunguo wa milango yote, ukweli, hata umeharisha, sema kweli nimeharisha isiseme nimejamba...
... Mwanangu eeh, sinngoji adhana, moyo wa Dokta ushanidunda. Mazaaa eeeh. mie nakwenda kumchukua mgeni baada ya kusali isha tu nakuletea wife toibe hapa hapa.
Mama; Mungu akujaalie mwanangu kaupe yote unayoyatamani, In shaa Allah yawe na heri na wewe.
Mshikaji; Hio dua haizuiliwa na mtu yoyote, dua ya mazazi kwa mwanae hata aje nani haizuii. Mie si unaona dua za za maza, nyumba mikeswi yoiyte nimeshinda, mbegeres. sasa wananiangukia, Sasa mtoto wa halai wa mzee nilioabaki mimipeke yangu, leo mzee kadedi ndio mnajitokeza wanne ati wote sisi watoto wa mzee. Jaji yule kawaambia na gharama zote za kesi walipe mbegeres. kwaherini.
Akaenda zake.
...
Naunga mkono hoja 100%Kwanini hizi post yako usizi link pale kwenye post ya kwanza mtu au watu wakitaka kusoma post inayofuata wanaipata kwenye post ya kwanza
Kwanini hizi post yako usizi link pale kwenye post ya kwanza mtu au watu wakitaka kusoma post inayofuata wanaipata kwenye post ya kwanza
Simba,leo chai ya kipemba ya pilipili manga, umeikosa chai ya Tanga ya Anjari, tukanywa chai ya Unguja, ya viungo vyote hio.
Tukimaliza chai ya pilipili manga tunakwenda kunywa chai ya Vanilla nzima nzima ya Comoros.
Karibu chai. Rufiji chai yenu ipoje, maana ule mto kama chai ya maziwa. Yale maziwa ya mbuzi wa Kiiran bado mnatumia au mbuzi wote mlifanya mboga?
Simba.
Sana tu, ndio jadi, mila na desturi za Kisimba. Lakini nashukuru sasa sivuti tena.Simba,
Ulishawahi kuvuta bangi...?!
Naweza nikapata link...?! tofauti na ule wa zijue koo ya Simba...Sana tu, ndio jadi, mila na desturi za Kisimba. Lakini nashukuru sasa sivuti tena.
Zipo nyuzi za Simba za maganja na ushetani mwingine ambao hujaufikiria wala kuuwaza
Simba.
Arsis hili swala la kuwasiliana na viumbe wa kiroho lipoje?Telepathy 🤝..... Hii siwezi ielezea kiutaalam zaidi ila Arsis/Simba anamaelezo yake mazuri
(Hyo telepathy ni moja ya njia ya kufanya communication na viumbe wa kiroho)
Nakuomba umuulize Simba akueleweshe hapa, japo huko nyuma alishagusia kidogo...
(Mm sio mjuzi sana,,,, mwenyewe bado maamuma ndugu yangu
Mie nakushauri huna hata sababu ya kuzisoma, ni ushetani uliopindukia.Naweza nikapata link...?! tofauti na ule wa zijue koo ya Simba...
Niliyoyasoma kwenye hizo nyuzi zake zingine, ni kama upo coco beach unauliza baharini wapi.Simba,
Ulishawahi kuvuta bangi...?!
Nimeona, naona hivyo itakuwa vizuri sasa, jitahidi umalize, maana uzi unaenda mbio na raha ya story mtu akiianza simalize. Siyo aanze kutafuta uko wapi muendelezo.Tumeshaanza kufanya kwenye post namba 1 kidogo kidogo, kila episode itakua na links zake.
Natumai ipo sawa?
Alaah kumbeeHii nenda nayo tu mdogomdogo mkuu, Hii aishi leo
Mimi interest yangu zaidi ni kuhusu majini tu na si kingine kama hao washenzi wachawi.Huwa napenda kupata ilm ya hawa viumbe direct kutoka kwa mtu mwenye experience nao hususani kufanya nayo kazi,story za kwenye
kila kilicho chini ya jua ni cha Mali yake MUNGU, majini wanaishi majini, nchi kavu wanakuja tu na wanadamu wanatumia majini, halafu tunatofautiana kwa muda tu kama ilivyo hakuna jua kali sasa hivi Tanzania basi jua liko nchi nyingine soon linaingia inakuwa summer time kila kitu kina wakati wake tatizo ni wakati kuingiliana na matatizo kukutana, asubuhi mpaka jioni tunatakiwa wanadamu tuwe tumemaliza kazi kwaajili ya kupumzika, sasa nikiwa naruka majoka na kuna mbaya wangu ananiloga unafikiri itakuwaje?😂😂nitalogeka kirahisi, ukiachana na yote hata hal wachawi ni mali yaMUNGU😍😂😂😂Kama ushasema "sijui" si uulize uelimishwe?
UnKataa wachawi wakati mwenyewe unajiita roho ya kishetani?
Hizo nyuzi Zipo Wapi Simba la masimba!!Sana tu, ndio jadi, mila na desturi za Kisimba. Lakini nashukuru sasa sivuti tena.
Zipo nyuzi za Simba za maganja na ushetani mwingine ambao hujaufikiria wala kuuwaza
Simba.
Vionjo vya Arsis - Majini ya Kojani- Pemba 4.Alipoondoka mshikaji nikaingia ofisini kwangu nikamwita Jini 1. Baada ya kusalimiana.
Jini 1: Sasa Simba leo umenifurahisha kwa Mzee Ali ujue toka umeondoka Mzee Ali kamwita Jini wake mkiubwa akaja mara moja, akapiga smasolti zake akatulizana. Akaanz kiuonge na Mkewe Mzee Ali, akmuuliza unajua nini kinaendelea?
Mkewe: Sijui lakini kenzaia jana naona kiti chako hakipo vizuri kabisa. Anasema kuna wasaidizi wake wote kila akiwaita hawaji na wale hua wanapitia kwangu, mimi ndio kiti chao cha kuongea nao. Maana hata mimi sijawahisi kabisa leo wiki, koila nikimwambia anasema watakuja tu. Mwisho akanambia hata wewe hauji, kulikoni?
Mzee Ali; Nimekuja sasa hivi, kaniit kiti.
Mkewe; Nahisi alikua anataka kukuuliza hilohilo.
Mzee Ali; Sasa anajua kila kitu, asiwe na wasi wasi, wacha awaite tu wateja wake, akiniita tutafanya kazi, lakini wewe uwe karibu, mimi sitaongea sana kwa wageni. Kwaheri
Mkewe; Sawa kwaheri.
Jini 1; hayo ndio nilivowaacha ulipotoka wewe.
Mimi; Sasa nimekufurahish nini? Unajua sina muda na haya mambo, mimi nimekuita nikuulize, kuna nini kimetokea huko mpaka inabidi mimi niende kwenye kitovu huko cha majini yao?
Jini1; Simba imenifurahisha umekua Boss leo, tena Biss mkali kabisa hutaki mchezo...
Huko Simba, hakuna kazi yako hata moja, wewe unakwenda kwa ajili babu yako anataka ukajionee dunia, kazi imekwisha kule, ni kwenda kuwawachia wenazao tu. Kinachofanyika sasa hivi ni mchezo wa kuigiza ili wkuheshimu na wakuogope, wao na majini wao. lakini haukua na sababu wewe wala Dokta ya kwenda huko. Mimi nakuhauri nenda pia, uione dunia na mambo ya kijinga ya binadam. Kama hujayaona ukihadithiwa tu hayakuingii akilini. Nend Simba usijali, na mimi, mama, bakora utatukuta huko , tugtakuja kukusalimia wote, uzidishe heshima. Arsis hataki kutisha watu kwa picha za majeshi aliokwisha waonesha, mpaka mimi nimeogopa.
Mimi; majeshi ya nani?
Jini1; Ya majini na watu, lakini ilikua ni ile mwenyewe anita VR, lakini majini wanajua wa Kipenba wanajua ile VR lakini haiwezi kuwepo kama hawapo kweli. Wameogopa sana wakamalizana mikataba na Kamanda hapo hapo, unamkumbuka kamanda aliyekuja Unguja? Huyo huyo ndie amemalizana nao ndni hya kuda mchahe sana. Rafiki yako pia atakuwapo, mtakuta hukohuko. Anatamani na yeye aone mwaka koga wa kojani.
Mimi' Rafiki yangu yupi?
Jini 1; Mwanafunzi wa Arsis yule Mwarabu mlikua nae Unguja kumtoa kifungoni yule mtoto wa kike.
Mimi; Aaah, sawa.
Jini; Nikupe umbea?
Mimi: kama una faida nipe, kama umbea tu usinipe.
Jini 1; Unajua Mwarabu yupo karibi sana na yule Binti alieokolewa Unguja, yeye na mamake na wenyeji wao huko walipo wanajua wamekuta ghafla madukani, wakajuana, sasa wamekua marafiki wa nyumbani kabisa.
Mimi; kwanini?
Jini 1; Swali lako hilo gumu sana, hua silipendi. Kwa sabau kwanza Mwarabu anataka awe anaongea Kiswahili vizuri, anakipenda sana Kiaarabu, halafu alimuhurumia sana yule binti kwenye ile kazi, akawa kila siku anataka kujua anaendeleaje, Arsis akamshauri afanye nao urafiki. Ndio hivo gtu. Mwenyewe mkikutana mtauliza zaidi.
Mimi; Kwa hio Pemba sina kazi yoyote> Na Dokta nani kamwambia aje kwangu, na kwanini?
Jini 1; Babi yako kamwambia Sheikh amwambie aje kwako ili na wewe uende Kojani ukapaone. babu yako anakupenda sana.
Mimi: babu anaamua bila kunishauri.
Jini 1; Kama hutaki kwenda pia hakijaharibika kitu, mwambie tu babu yako hauendi, sas hivi ujue unaenda kwa ajili yake tu, sio kua kuna kazi yoyote ya kufanyika, kazi zilizopo ni Kamanda na Majini wakubwa wa kwa Kina Mzee Ali, hata yule anaekuja kwa Mzee Ali mkubwa yule, lakini hao anaoongea nao kamanda wakubwa zake. Mzee Ali mwenyewe kashangaa, kawaida yule haji kabisa mpaka Mzee Ali awe na kazi ngumu, lakinimhofu aliokua nayo yule jini mpaka Mzee Aliu kaihisi.
Mimi; Kwa hio miminiende tu Pemba?
Jini 1; Hilo siqwezi kukujibu kabisa, hilo ni lako, babu yako na Dokta na Sheikh wa Unguja. Mimi simo wala mama wala Arsis. SisiArsis katushauri twende sherehe za Kojani na majini wa Kipemba, walipo dunia nzima watahudhuria siku hio, wakituona na wewe huko kwa sherehe za Kojani wtajuheshimu na kukuogopa kila watapokuona. Wrewe na Dokta mtapata hesgima kubwa sana. Mie nakwenda Simba, hakuna jingine.
Mimi; Haya kwaheri
Nikatoka uani nikakuta hakuna mtu, Mama na wife wapo jikoni, nikaenda jikoni moja kwa moja.
Mimi; Habari za hapa wapishi mahiri?
mama; Tumeabiwa mgeni anaekuja ni Dokta, mkeo anamtayarishia vilosoloso, mimi nimelazimishwa tu nirudie kupika kuku wa jana, ili mkeo ajifunze.
Wife; Mzee hawa wangu atawapenda zaidi, nimeweka secret ingrdients zangu, watakua watamu hao, mpaka wewe mama ukiwala utauliza.
Mama; Mavitu yenu mpaka mtazame kwenye internet, mi i siyawezi, wacha nikakoge. kazi kwako bibie.
Wife; Hata mimi tayari nakwenda kukoga, akatoka huyo, twenda Simba.
Tukaondoka na mke wangu tukaenda chumbani kwetu, kuingia tu akaingia bafu akaniita, njoo huku. Nikajua njaa zke hizo, maana huyu njaa zake zinakuja timing ambazo hakuna binadam anategemea. SAlivoniita tu, akanitia njee ya ghafla na mimi. Kuingia akanambia funga hil lango kwa ndani, huyo bibie hua anaingia tu humu, kama hana akili vizuri.
Mimi; Si mjukuu wa Simba, mtoto wa Simba?
Woife; Sitaki kabisa kumuhusisha na mambo ya Kisimba, abaki kua simba kwa jadi tu sio kwa mila na desturi zao, mume wangi sisi si tumeachana nazo, kwanini watoto zetu wazifate?
Mimi; Naona na mama na mzee wanaheshimu hilo.
Wife; kabisa tena.
Muda wa kusali ulipofika Mzee akatoka kwake, nikamsikia ananiita, kawaid ayake anaita mara moja tu, Simba, time. kamaliza. nikajitoharisha nikatoka nkamkuta uani tukafatana masjid.
baada ya sala kulikua kidogo kidogo Imam anantangaza darsa jipya litaloanza Jumamosi mpaka Jumatano kila siku, darsa la ni ni Rizki. Hili somo nikahudhuria, likua zuri sana, kila siku ikawa linaanza baada ya kusali magharibi mpaka Isha, nikawa nikimaliza darsa, usiku nafata regference zote tulizopewa. Ustadh aliekua anatoa hilo darsa alikua msomi wa Chuo kikuu cha Azhar na reference zake nyingi zilikua za Masheikh wa Azhar.
Tukarudi na na mzee baada ya hoituba za Imam na maelekezo elekezo ya mamboi ya Masjid.
Kuingia nyumbani nikamkuta mshikaji yupo nje.
Mshikaji; Vipi mwanangu Imam kasemaje leo huko mbona mmechelewa au kawapiga sura ndefu ndefu?
Mimi; hata, alikua anatangaza darsa la nini rizki linaanza Jumamosi.
Mshikaji; Hayo ndio mambo, hilo sikosi hilo, watu tunataka tujue mambo ya riziki.
Mimi; Mbona upo nje?
Mshikaji; Si unajua mambo ya wanawake, alipofika tu mgeni wamechukuana ndani huko, si unajua hao lazima wakaoneshane mapambo ya nyumba ndani huko. Nikasepa, nigande uani peke yangu kama jini?
Nikascheka tu, thinkinga ya mshikaji wangu ni tofauti na watu wote.
Mimi; Kumbe, hua wanaoneshana mapambo ya nyumba?
Mshikaji; Sasa wanawake si ndio wanapamba nyumba? Unafikiri kwa ajili yenu ya mnaokaa ndani? Hakuna hio, hayo mapambo kwa ajili kutambia wanawake wenzao, hii nimenunua Dubai, hii niletewa kuto China. ndio hivyo tu...
Mwanangu, ingia kaamshe amshe basi tule tusepe, unajua woife to be kesho kazi; lazima apumzike mapema.
Mimi; kwani sisi hatwendi kazini?
Mshikaji; Sisi si tupo nyumbani, huyo si mwanamke unajua kutembeza gari peke yake usiku, noma.
Mimi; Si wwewe utampeleka?
Mshikaji; Mie hakuna noma, anytime nampeleka, lakini namuonea huruma yeye.
Mimi; haya wacha niwahi kuamsha amsha, hata mimi nataka kupumzika mapema leo.
Mshikaji: Si umeona mwanangu? maana leo kulikua kuna zigzaga gereji huko sio ya kawaida. Mi bosi bosi yote ile inataka migaro yao ifanyiwe service ipate kwenda kula bata week endi. Duniani kote magari tanafanyiwa service weekendi ili yakianza kazi wiki znima hakunanoma. Bingi tu mwanangu ndio utaona migari ya serice ya serikali ndio inajaa Jumatano na Alhamisi.
Mimi; Nilikiua sijaliona hilo.
Mshokaji; mwanangu kwanza madereva wanafosi wapate hela za wikiendi.
Mimi' Kivipi?
Mshikaji; Wale si laima gari ikitpoka gereji itiwe ijawe tena full tanki, sasa mifuta yote iliokuwapo kabla wanvyonza wanauza, mipesa kibasa wanafyonza, na wakitiliwa mapya, nusu tanki zao, mibongo mijizi mwanangu usisikie.
Mimi; Sikulifikiria kabisa hilo, nilifikiri labda wana mgao wao kwa Mzee?
Mshikaji' Wewe kumbe Dingi humjui, Dingi hachukui kazi ya kumpa mtu hela kabisa, anasema kazi yake ni hela kwanini atie rushwa? Dah Dingi noma mwanangu, akikusikia hata unaongelea hilo anakua mbogo hapo hapo. Mjaribu uone. Dili zake za kishua Dingi. Sa mtaalamu kama yule mipesa ya haramu ya nini?
Mimi; Kweli lakini, kazi zilizopo za watu binafsi hatutoshi pale.
Mshikaji; kwani hao madrereva wa binfasi si ndio maana wakijua gari service, hawaleti kwetu mpaka niende mimi na wengine kutaleta? wanajua kwa dingi hakuna longo longo la katafuyte spea wala kanunue hiki wala kile, wao wakileta gari, wakiisubi wanapigwa msosi wa bure kwa mamalishe, wale tani yao. Hapo ndio nampendea Dingi, kwa misosi tu, madereva wote wa binafsi wa serikali wanasifu hilo kwa mzee. Mnyoinge mnyongeni haki yuake mpeni, yanakula kwa uroho wao mpaka ynakitazama chakula, yakishavimbiwa utayakuta kule gereji mwisho, yanalala chini ya mkungu. Ngoja kuna siku tawanyuyia upupu ndio wataacha mchezo huo.
Mimi; Sasa kwanini ufanye hivyo mshikaji wangu, vibaya.
Mshikaji; Mwanangu unajua usingizi na uvivu unaambukiza, sasa sisi tunachakarika wao wanalala kule, washashiba wanajamba jamba hovyo kuchafua mazingira tu.
Nikamwacha anaongea nikaingia ndani.
....
Naomba wazoefu wa JF wakusaidie namna ya kuzipata, kuna njia nyepesi ya kufata ID yangu ukafika kwenye nyuzi zangu zote.Hizo nyuzi Zipo Wapi Simba la masimba!!
Niliyoyasomawenye hizo nyuzi zake zingine, ni kama upo coco beach unauliza baharini wapi.
Mie nakushauri huna hata sababu ya kuzisoma, ni ushetani uliopindukia.