Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

kwahiyo unamaanisha wachamungu hawarogwi au kukumbwa na uchawi..ila mkuu ww una majibu mepesi yasiyokidhi haja katika maswali serious ni kama vile hutaki ww umekariri jibu moja tu kwa kila anayeleta shida yake serious wala hujali utajibu "fanya ibada sali sana acha maasi" ukiwa unajibu shida ya mtu mmoja basi jua wapo wengine wengi shida zao zinafanana huoni kama utasaidia wengi.!
Hilo nimemueleza. Ana majibu mepesi kweli
 
Mimi interest yangu zaidi ni kuhusu majini tu na si kingine kama hao washenzi wachawi.Huwa napenda kupata ilm ya hawa viumbe direct kutoka kwa mtu mwenye experience nao hususani kufanya nayo kazi,story za kwenye Qur'an zinazosemaga sijui majini waliumbwa kwa moto,sijui wanakaa sijui kwenye magofu na sehemu chafu naonaga tu kama ni hadithi tu za kutungwa.Sasa nikirudi kwenye swali langu la msingi, iwapo majini ni viumbe wa asili,je inawezekanaje mtu anamtengeneza jini,maana kuna mabwana kama wawili niliwasikia wakilizungumzia hili linalohusiana na majini ya kuyatengeneza na kuyatega sehemu.Na je majini yote yanayotegwa ni ya kutengenezwa au hata majini ya asili yanaweza kutegwa kwa ajili ya kuleta maangamizi
 
Bwana simba nna swali hivi Arsis anasemaje Au ana maaarifa Gani juu ya binadamu Watu Wenye Viganja Vyenye Herufi M.
 
kwahiyo unamaanisha wachamungu hawarogwi au kukumbwa na uchawi..ila mkuu ww una majibu mepesi yasiyokidhi haja katika maswali serious ni kama vile hutaki ww umekariri jibu moja tu kwa kila anayeleta shida yake serious wala hujali utajibu "fanya ibada sali sana acha maasi" ukiwa unajibu shida ya mtu mmoja basi jua wapo wengine wengi shida zao zinafanana huoni kama utasaidia wengi.!
Mbona hii anayotoa ndio solution ya kila kitu ndugu....🤔
Narudia tena hii ndio solution ya kila kitu🤝🤝
Naweza nikakuthibitishia hilo kwa vitendo!!!
Sema sijui namna ya kuweka sawa hii kitu, ila ningetoa somo lisilo rasmi kuhusu namna ya kuwa connected na Mungu direct!!!
Ila naogopa sabb elim yangu ndogo sana (maana mm ntaongea kutokana na experience wala sitotumia vitabu na uthibitisho wa hadithi sana.... Mm ntaongea kinachonitokea, Sasa mwisho ntajitukanisha hapa maana ntashindwa kutoa ushahidi🤝🤝

Na Kama ujuavyo humu wenye elim ni wengi 🚶🚶

(Ila ukiishi kama watu wa zamani ni rahisi Sana kumpata Mungu na kuuona ukubwa wake, hii nimeijaribu kwa baadh ya vitu ni really kabisaaaa
 
kaingia kwenye ukumbi mose ana mada nzito na uhakika atakua na majibu mazito.

Tustahamiliane tu.
Simba
Ndiyo kuna mambo 'yanasubiri'...

Hakuna namna,

Wanajamii inabidi wafanye bidii kutafuta kujua ilivyobora--hakuna 'njia ya mkato' kwa 'maarifa'.

Maarifa yana 'Mbegu ya U-JUA-JI' -- hili linataka nidhamu ya aina yake na siyo mambo ya 'Tumbuizo Asilia' kwa stori stori za maisha...

Na ndiyo, In Shaa Allah, uwezekano wa kufika kwenye 'Shams al Maarif' kwenye huu uzi upo...

Ngoja wadau wakidhi uwezo wa kukomaa na mambo ya kiufundi wa kawaida kwanza...

Hmmm
 
Bwana simba nna swali hivi Arsis anasemaje Au ana maaarifa Gani juu ya binadamu Watu Wenye Viganja Vyenye Herufi M.
Kwa ufupi hatufahamu.

Kama umekiona kitu katika huu uzi, hatuna utabiri wa aina yoyote, isipokua kuna kisa siku za usoni huko cha time travel na kwa kiwango kikubwa kitakua kwa siku za nyuma. Tunaweza kuelezea vilivotokea tu isipokua vichache sana ambavyo havijatokea., tunavisoma kwenye vitabu, si vyetu.
Simba.
 
Mbona hii anayotoa ndio solution ya kila kitu ndugu....🤔
Narudia tena hii ndio solution ya kila kitu🤝🤝
Naweza nikakuthibitishia hilo kwa vitendo!!!
Sema sijui namna ya kuweka sawa hii kitu, ila ningetoa somo lisilo rasmi kuhusu namna ya kuwa connected na Mungu direct!!!
Ila naogopa sabb elim yangu ndogo sana (maana mm ntaongea kutokana na experience wala sitotumia vitabu na uthibitisho wa hadithi sana.... Mm ntaongea kinachonitokea, Sasa mwisho ntajitukanisha hapa maana ntashindwa kutoa ushahidi🤝🤝

Na Kama ujuavyo humu wenye elim ni wengi 🚶🚶

(Ila ukiishi kama watu wa zamani ni rahisi Sana kumpata Mungu na kuuona ukubwa wake, hii nimeijaribu kwa baadh ya vitu ni really kabisaaaa
Mwaga elimu.
Simba.
 
Kwa ufupi hatufahamu.

Kama umekiona kitu katika huu uzi, hatuna utabiri wa aina yoyote, isipokua kuna kisa siku za usoni huko cha time travel na kwa kiwango kikubwa kitakua kwa siku za nyuma. Tunaweza kuelezea vilivotokea tu isipokua vichache sana ambavyo havijatokea., tunavisoma kwenye vitabu, si vyetu.
Simba.
Muelekeo:
Kusafiri kiwakati ni jambo la kuwezekana, ni jambo ambalo katika ulimwengu wetu limekuwepo kwa miaka mabilioni na mabilioni...

'Viumbe watu' wasio na asili ya hapa duniani wamekuwa wakitumia huo uwezo kusafiri na kutukiza sehemu mbalimbali za ulimwengu, hapa duniani viumbe watu hawa wamekuwa wakija na kuondoka na wakati wote... Viumbe watu wengine wenye huo uwezo pia wamekuwepo duniani kwa miaka mamilioni, wanaishi chini ardhini--hata chini ya bahari... Wengine ni wa namna ya 'watu mijusi' na wengine ni watu karibia kama sisi binadamu tulivyo... Vipo visa na sababu inakuwaje wapo hapa lakini sisi hatujui... Lakini si kweli kuwa watu hawajui--sehemu ya hata visa ambavyo nimepata kuvifuatilia hapa nyumbani vina kila dalili baadhi ya watu wamekutana na hawa viumbe watu wakasimulia kama 'majini', 'vibwengo' n.k... Watu wa Tibet, India, Afrika ya Kusini, Zimbabwe na kungine kwengi wanajua kuhusiana na 'Mashetani' hawa -- kama ambavyo baadhi ya makabila hapa Tanzania husimulia watu wake kwa sanaa na visa -- na kama hayati Mzee Credo Mutwa alivyopata kusimulia kwa kirefu sana, ukweli kuhusu hawa ni sehemu ya 'mizungu' ya Kiafrika... Losang Rampa, katika visa vyake vinavyokwenda na usemi "Ni Bora Kuwasha Kamshumaa Kuliko Kukilaani Kiza", anafununua mengi na hata anafundisha mambo -- jinsi wao Watibeti, wamekuwa wakijua habari za watu wanaoishi chini ardhini, wageni ambao wamekuwa wakija na kuondoka duniani, ufundi wao wa 'kusafiri kiwakati' kwenda mbele ya wakati nyuma ama mbele ya wakati, kusafiri hadi sayari za mbali n.k. Kadri tutavyobarikwa nafasi, tutafasiriana habari zake na labda tutajenga msingi kufundishana kufanya hayo yote...
 
== Kumbukumbu la Torati: Miongozo kwa ‘Miundo Hai’==

Miongozo ni msingi wa dira/maono, dhima na basi ‘matendo’ ya wanajamii—mambo yenye kuyakinisha muktadha akilifu wa ‘kujichagulia’; mapana ya ujamii na mambo yake.

Kwa Nchi-Dola na jamii ya ‘Watanzania’, kwa mfano, msingi ya Dira, Maono na Matendo—katika kipindi cha Uasisi wa sura ya Nchi na Tawala ni Maendeleo na Kujichagulia katika misingi ya Demokrasi na Ujamaa: Ujamaa na Kujitegemea; Haya basi kuwepo kwa misingi ya Kikatiba na Utashi wa ‘Wananchi’ kupitia ‘Wawakilishi wa Wananchi’ katika kuitaasisisha ‘Katiba ya Ujamhuri’. Ndivyo basi, nchi-dola kiufundi ni ‘kiumbe cha Kufikirika’--chenye kusadifu matamanio ya UTU-MAISHA-UISHO wa wanajamii wenyewe wenyekuhusikana na ‘Kiumbe cha Kufikirika’.

‘Kiumbe cha Kufikirika’ ni chombo cha kimafikara kwa ajili ya misingi ya kujichagulia na tena chenye ushiriki wa ‘Hisia’ na ‘Kujisikia’ katika akili na utambuzi wa Mwanajamii: Utambuzi kumbaizi katika Jamii/Wanajamii—mambo ya ‘Uzalendo’ na ‘Kujitoa/Kuipenda Nchi’ – nchi ya mtu na watu wake. Kiufundi, hili ndilo asili khasa ya zingatio la maombi katika ‘Hali ya Neema’--Wakati wa kuimba wimbo wa Taifa, kuwa na adabu, nidhamu na Msimamo thabiti; wenye kuakisi kusudi la ‘Dua’, ‘Neema’ na ‘Uwepo’ wa kile kilicho khasa ni ‘asili ya Uzima/Kujaza Pumzi ya Uzima katika Miili ya Uweza’ na ‘Kheri ya vyote’—vyenye kuonekana na visivyoonekana; ‘MUNGU’.

UTU-MAISHA-UISHO, kiuono na ufikirifu mifumo ni jambo mtambuka kwa viumbe vyote vyenye nasibu ya Usentienti, Konsayansi na Ufahamu; kwa mintarafu ya hili, Ubinadamu ni namna moja ya usura-kiumbe wenye Usentienti, Konsayansi na Ufahamu. Utu unawezekana kwa viumbe vyenye usura-kiumbe asio wa kibinadamu pia; kwa hivyo ni ‘Ushamba’ kudhani dhana ya kile kilicho ni khasa asili ya Uzima/Kujaza Pumzi ya Uzima katika Miili ya Uweza’ na ‘Kheri ya Vyote’ kina ‘mapendeleo’ na ‘Utu’ wa kibinadamu.

Viumbe vyote venye usentienti, konsayansi na ufahamu, kiuono na ufikirifu mifumo, vina nasibu ya ‘Ontolojia ya Taasisi’, ‘Uono/Kujiwazia UTU’ na ‘Sura na Mienendo ya Utamaduni wake’. Kwa hivyo ni ‘Ushamba’ kama si kasumba kudhania ‘MUNGU’ ni ‘CHANZO CHA UZIMA/UJUMLA WA MAWEZEKANO YA MAMBO YOTE/ULEZI’ ambacho, katika hicho, kiumbe fulani ni Bora kuliko kingine… Ama kudhani, kimoja kinatangulia kingine kwa Ubora eti kwa kuwa Ulimwengu wa Madhahiri huwa na kana ‘wakati wa hiki kuwepo’ na tena vivyo hivyo ‘wakati wa kile kuwepo’…

‘MUNGU’ kuwa ni ‘CHANZO CHA UZIMA/UJUMLA WA MAWEZEKANO YA MAMBO YOTE/ULEZI’ , kiuono na ufikirifu mifumo, ni ishara ya ‘Jua la Maarifa na Maarifu’ katika akili na utashi, tena kadiri ya ‘Roho ya Utambuzi’ kuhuisha mazingira ya miili ya uweza na utendaji wake kama kiumbe—kiumbe chochote kile chenye ‘sura dhahiri’ ama ‘sura iliyositirika’ mbele ya kimojawapo chenye upeo wa namna yake kiufahamu na utambuzi. Kwa mintarafu ya hivi, ‘Sonafi’ ni mbegu ya ‘UTU-Kiumbe’ yenye kuhaisha na kuhuisha ‘miili na uweza wa kibinadamu’ kwa kadiri ya (1) Hisia na Kujisikia--’Usentienti’, (2) Akili ya Udhamirifu wa Mambo--’Konsayansi’, na (3) Mwanga wa Nuru ya Utambuzi/Kujitambua--’Nuru ya Ufahamu’. Basi ndiyo yawa, ‘upandaji mbegu’ ni muktadha akilifu wa nafsi ya duniani, nafsi-roho na Roho ya Uzima wote. Tena basi, sonafi ndiyo nguzo ya pumzi na uzima kwa utu—ufunguo kwa mambo ya fizikia na metafizia ya ‘kujiwazia UTU’ kupitia ‘miili ya uweza’.

Sonafi liwe ni neno rasmi katika lugha ya Kiswahili kumaanisha ufafanuzi wa ile ‘asili ya ndani’, asili iliyositirika, ya utu wa kiumbe chochote; asili inayohuisha miili ya uweza ili utendaji wa ‘kiumbe hai’ katika mazingira yake uwe na nafasi ya kujikadirishia mapana ya ustawi wake—mambo ya ‘Uzima wa Miili—Utwaaji Mwili, Mauti, Ufufuko’. Kwenye lugha ya Kiingereza, Sonafi ni kile kile kinachotajwa kana ‘Soul’ ama pia ‘Divine Spark’--Cheche ya ‘Nuru Manani ya Ufahamu’… Kuwa kwamba etimolojia ya neno ‘Soul/Sonafi’ ni asili ya yote mawili: (1) Jua (Sol) na (2) Nafsi (Kiswahili/Kiarabu kwa neno ‘Self’) — Ku-Jua na Kujitambua kiutu. Basi ndiyo yawa, kwa Rizayati ya Elimu 3.0, Sonafi ndicho kiini mujarabu cha ILIMU—Jua la Maarifa na Maarifu ya ‘Uungu’; ambavyo pia ‘Elimu ni Bahari na tena metafizikia yake ni ILIMU’.

Elimu na metafizikia ya Elimu ni mambo ya maingiliano ya dhahiri—dhahiri macho na dhahiri kiini macho; mambo ya vinavyoonekana na visivyoonekana. Kwa mintarafu ya hivi, kile ambacho injili hueleza la Yesu fundisha jinsi ya kuyajua ya ‘Waja Wema’ kwa ishara ama/na matendo, ni ukweli wa muktadha akilifu wa kuyabaini yaliyodhahiri na yale yaliyositirika. Kwa mintarafu ya haya, sonafi ni ‘kitovu cha uweza wa kawaida na tena uweza mwingine wenye kupitiliza kawaida. Kwenye Injili, mambo ya uwezekano wa kupitiliza kawaida ya uweza, matendo na dhahiri husemwa ni ‘Matunda ya Imani’; kwamba (1) Udhamirifu, (2) Dhumuni, na (3) ‘Nia Uweza’ vinaweza hata ‘kuhamisha Milima’; mambo ya kusafiri/kusafirisha/kujisafirisha tokeo upahala hapa hata pengine—Telepotia ama pia Kupeperuka.

Uweza wa kawaida wa kimiili ni muktadha akilifu wa mapana yote ya kudra na uweza vyenye kuleta silika na matendo ya kiumbe katika mazingira yake ya asili; mambo kama vile utu wa kibinadamu kumudu mwili wenye miguu, mikono, kiwiliwili na kichwa ambavyo kiwiliwili na kichwa hufanya uenyeji wa ‘moyo’ na ‘akili’ kwa ajili ya ‘Hisia, Mafikara na Ufahamu’ kupitia mishipa ya fahamu(fuvu, uti wa mgongo na Ubongo), pumzi (Mapafu) na riziki za kimiili(Moyo, Matumbo na ‘Mifumo yote ya Nyama na Uzima wake’). Kwa mintarafu ya haya, sonafi ni chachu wa ‘uzima wa miili’ inayohusikana na pumzi, fahamu na mashikizano ya yaliyodhahiri na yasiyodhahiri.
Kama unadhan unakijua kiswahili basi soma hizi post za huyu mwamba,dah hatar sana
 
Ndiyo kuna mambo 'yanasubiri'...

Hakuna namna,

Wanajamii inabidi wafanye bidii kutafuta kujua ilivyobora--hakuna 'njia ya mkato' kwa 'maarifa'.

Maarifa yana 'Mbegu ya U-JUA-JI' -- hili linataka nidhamu ya aina yake na siyo mambo ya 'Tumbuizo Asilia' kwa stori stori za maisha...

Na ndiyo, In Shaa Allah, uwezekano wa kufika kwenye 'Shams al Maarif' kwenye huu uzi upo...

Ngoja wadau wakidhi uwezo wa kukomaa na mambo ya kiufundi wa kawaida kwanza...

Hmmm
Ungeweka link tukufate jwenye uzi wako badala ya kuharibu uzi kwa copy and paste.
 
Mleta mada kaeleza mambo mengi makubwa ila juu juu (siwezi sema kakosea maana target yake ni kufikisha ujumbe kuhusu alichokiona baada ya kufunguka macho, na alhamdulillah ujumbe umefika,,,, japo utata umebaki mwingi kwenye vichwa vya watu)

Ngoja nisawazishe eneo dogo hapa kwajinsi ninavyoelewa!!
Mada kubwa mezani ni SPIRITUAL AWAKENING

Viumbe wa kiroho... Ni viumbe wote ambao hawaonekani kwa macho ya kawaida (malaika, majin n.k kila mtu anawafaham kwa mujibu wa imani yake) viumbe Hawa huwa na connection kwa watu maalum pekee

Watu maalum ni hawa 👉 Manabii na mitume, wachamungu sana, waganga wa kichawi na watu waliopendelewa

Ili uwe kwenye special group lazima uwe connected na source of power yoyote kati ya hizi
A. Mungu
B. Ibiris

Sasa viumbe wa kiroho wao pia wapo makundi mawili tu.... Kutokana na uanachama wao kweny hizo source of power (hapo either awe upande wa Mungu au Shetani🤝

Sasa hao special group pia wananamna yao ya kuwasiliana na hao viumbe.....
Baadhi ni hisia, ndoto, telepathy na kuona

(Hii njia ya kuona ndio njia ya juu zaidi tuseme ndio maqam ya mwisho.... Sasa huwa unaanza kwa kupanda daraja
Utaanza njia ya hisia, ndoto, telepathy mwisho utaona🤝

Mleta mada yupo kwenye special group upande wa watu waliopendelewa... Maana hajafata process wala hajaandaliwa ila karushwa daraja moja kwa moja

(Kwa imani ya kiislam huwa Kuna watu wanazaliwa wakiwa n mawalii wa Mwenyezi Mungu,,,,, kitu ambacho n nadra sana mtu kukipata

Au mfano mtu ufanye ibada mpk uwe nabii😁😁😁🏃
Ngum sana, nabii huzaliwa akiwa tayar ni nabii


(Dah mambo ya kiroho huwa yanamaelezo mengi sana...... Ila ukiweza kuwasiliana na viumbe wa kiroho hii Dunia umeiweza🤝
Njaa kwako sahau, kuonewa kwako sahau, kukataliwa kwako sahau,,, hii ni Siri ambayo wazungu wanaitumia sana

Ushuhuda:
Baba yangu alikuwa na uwezo wa kwenda kwenye mlima wowote au mto mkubwa, akifika anawaita watawala wa huo mto au mlima wanakuja live anawaeleza anataka nn kutoka kweny himaya yao halafu wakielewana kazi kwisha
(Anaenda kweny kaburi la mtu aliyekufa anamuamsha anaongea nae akimaliza anarudi kulala..... (Najua hapa ntaonekana muongo)
Anazama kweny maji anatoka mkavu bila kuloana
Anaweza kuchukua ile sarafu ya zaman inayotafutwa kila kona
SIMBA MBILI au Rupia (akafanya yake akamtoa yule Simba na king George wakakaa na kuanza mazungumzo

Alikuwa na uwezo wa ajabu sana.....

Note: source yake ya Power haikuwa GOD
(Kwenye hii Dunia ukitaka kuwa mtu hatari we chagua njia moja upite hiyo kikamilifu utaona balaa lake.... Kama n Mungu swali sana acha dhambi kwa ukamilifu wake utaona utavyokuwa hatari

Kama n upande wa shetwani... Roga sana, usisite kutoa mtu kafara Yani kuwa nyambisi haswaa utaona ibiris atavyokupenda😂

Fanya juu chini upate mapenzi either ya Mungu au Ibiris.... Usikubali kukaa katikati maana utakuwa mtumwa
Usikubali kukaa katikati maana utakuwa mtumwa... Hakika mwanga na ukuongoze
 
== KUTOKA ilivyo ni kujichagulia Njia iliyo Sahihi na Kheri kwa ‘Uzima wa Mwili’ ==

Miundo, Mifumo na Matendo yote, kwenye fremukazi ya uono na ufikirifu mifumo, ndiyo hasa mambo yajayo na ualama wa (1) Mraba (Dhamma ijayo na Sovereini Jumuifu), (2) Pembe Tatu ‘ya Mbingu’ na ‘ya Nchi’ kutenganishwa na ukatikati wa Ulali wa mapana ya Dhamma, na (3) Torati (Miongozo kwa ajili ya NISHANI ya UTU BORA).

‘Kuumba mtu kwa Mfano wetu’ , ni nasibu ya ‘matendo katika metafanusi’. Kwa mintarafu ya hivi, kile kiumbe-mtu kwa sura-umbo na unasibu wake ni matokeo ya ‘Mbegu-Utu’ kwa ajili ya Dhamma, Kudra, Silika, Rehema na Fadhili ya UTU-MAISHA-UISHO. Basi ndiyo yawa, Hisia na Kujisikia hufafanua na kuyakinisha muktadha wa akilifu wa ‘Maisha na Kujichagulia’ kulingana na ‘Miundo ya Utendaji wa Kijamii’ na ‘Ushawishi’ wa Kitaasisi ndani ya Wanajamii wenyewe.

Kudra na Silika ndiyo yale kwenye wale wazungumzao lugha ya Kiingereza wangeliyataja kama ‘Virtue’ na ‘Character’; Basi ndiyo yawa ‘Dhamma’ ni muktadha akilifu wa yale yote yajayo na mafundisho ya Buddha kuhusu ‘Gorudumu la Dhamma’ na ‘Njia ya Wongofu’. Tena basi, yawa kwamba matendo yote hubayanisha ‘mifumo’ ambayo Udhamirifu ama/na Matendo vinaasili ya pembetatu—muktadha akilifu wa ‘Trishikisha’.

‘Kuumba mtu kwa Mfano wetu’ , ni nasibu ya ‘matendo katika metafanusi’ ambavyo ‘Kujiwazia Utu’ hukopa maudhui kutoka kwenye Uzabibu 13—Ufahamu Kristu. Kwa mintarafu ya hili, mifumo hai yote kupata mbegu za kudra na silika kutoka kwa ‘Kristu’. Basi ndiyo yawa, Kristu ni ‘Metafanusi’ ya ‘Miili yote ya Uzima na Uweza’. Kuwa kwamba, Kristulojia ndiyo ile habari ya ‘Hapo Mwanzo Kulikuwa na NENO, Naye Neno alikuwa ‘Nuru’...; Tena basi, Habari za Yesu kupata kusema alikuwepo Kabla ya yote—Kabla ya hata kuumbwa kwa Ulimwengu Dhahiri ni dhihiri la ‘Ufahamu Kristu’-- Ufahamu Kristu ni Usentieti, Konsayansi na ‘Roho ya Utambuzi’ katika muktadha akilifu wa NENO LA UZIMA.

‘Kuumba mtu kwa Mfano wetu’ , ni nasibu ya ‘matendo katika metafanusi’ ambavyo vile vilivyodhahirika huwa na lugha ya kimaelekezo ya utendaji na kumbukumbu za kimpangilio, programu, kwa ajili kukua na kuongezeka. Kwa mintarafu ya haya, muktadha akilifu uliyo ni programu kwa ajili ya (i) kujiunda, (ii) kujisuka kiwakati na (iii)kujidumisha vizazi vyake; ndiyo ‘sehemu’ ya ‘Neno la Uzima’. Basi ndiyo yawa, mambo ya ‘programu mahsusi’ ya kiumbe hai chenye usentienti, konsayansi na ufahamu ni ‘Habari Njema’ iliyositirika katika ‘Sonafi’ ya Kiumbe Hai chenyewe ili kumuwezesha na kumnasibisha na (1) mambo dhahiri , na (2) mambo yaliyositirika; kupitia matendo yaki- ‘Bayo-fizikia ya Kikwantumu’.

‘Kuumba mtu kwa Mfano wetu’, ni nasibu ya ‘matendo katika metafanusi’ ambavyo vile vilivyodhahirika huwa ‘Uzao wa Matunda Uliowaziwa kwa Kutangulia’. Kwa mintarafu ya hili, Matunda ni muktadha akilifu wa ‘Mti wa Uzima’; Kiufundi ‘Mti wa Uzima’ ni ujumla wa nasibu ya Ustawi na Utamaduni wa ujumuiko wa jamii kwa uzazi (kujamiana) na ‘Udhamirifu wa Furaha’ kupitia ‘kazi/utendaji’ ama/na ‘Kuunganika/Kukomunika’ na ‘Roho ya Uzima Wote’. Basi ndiyo yawa, kutokeo kwenye mapokeo ya ‘Injili’ na ‘Matendo ya Mitume’ huzungumzwa kana ‘Kristu’ ni ‘Tumaini la Vizazi Vyote’. Tena basi, hiyo ni kwa kuwa Kristu ni ‘Fanusi ya Mti wa Uzima’ na mambo yake…

Miundo, Mifumo na Matendo ndiyo ile asili khasa ya ‘Mafumbo yote ya Imani’. Kiuono na Ufikirifu Mifumo, Ustawi na Utamaduni ni ‘Utukufu’ wa ‘Metafanusi’ iliyositirika na huku kumbe ndiyo ile asili khasa ya Dhamma, Kudra, Silika, Rehema na Fadhili kwa UTU-MAISHA-UISHO. Kwa mintarafu ya hivi, Dhamma ni MRABA wenye asili ya (1) MOTO, (2) UPEPO, (3) MAJI, na (4) ARDHI/NCHI. Basi ndiyo yawa, MRABA mwingine wa MISINGI wa MTU KUJICHAGULIA KIWAKATI ndiyo huruzuku nasibu ya ‘Unyoofu’ na ‘Mapenzi Mema’ ya Mja; ambavyo ada ya Mja Mwema ni ‘Muda kuja Kunena’ – Muda kuja kunena ile fahari ya Utu – Utu wa yule mwenye Kutenda kwa ‘Maungwana’ ama ‘Kiburi’; Hauwezi kupanda Pilipili ukaja kuvuna Parachichi...

Mfano mahsusi ya ‘Udhamirifu wa Furaha’ na ‘Ujumuiko wa Kizazi/Vizazi’, ni shauri la UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI. Kiuono na Ufikirifu mifumo, manne haya ni kwa ajili ya ruzuku ya Rehema na Fadhili ya UTU-MAISHA-UISHO. Kwa mintarafu ya hivi, Dhamma ya Utaifa la Tanzania ni kusudi kwa matamanio ya kheri kwa ajili ya ‘UTUKUFU wa KIJAMII’ wenye miongezeo/Torati ya mapana ya LIBERTI-UuMOJA-UJAZI-UTANGAMANO. Basi ndiyo yawa, ‘Unyoofu’ na ‘Mapenzi Mema’ hukadirisha ‘Mstari’ na ‘Uduara’; vifanyavyo pande nne za MRABA wa DHAMMA.

Mfano mahsusi ya ‘Udhamirifu wa Furaha’ na ‘Ujumuiko wa Kizazi/Vizazi’, ni shauri la UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI. Kiuono na Ufikirifu mifumo, manne haya ni kwa ajili ya ruzuku ya Rehema na Fadhili ya UTU-MAISHA-UISHO. Kwa mintarafu ya hivi, Muktadha akilifu wa Utendaji – Utendaji (1) Kiroho, (2) Maadili na (3) Miiko una zindiko ambalo ndiyo msingi wa kulijenga, kulidumisha na kulilinda Taifa la Watanzania. Basi ndiyo yawa, hakika ya UTU-MAISHA-UISHO wa Watanzania ni fanusi ya ‘Uhuru na Umoja’ kwa matamanio ya Ujamaa wa Kweli; Ambavyo Rehema na Fadhili hukadirika kwa Imani ya Watanzania Wenyewe katika Udhamirifu wa kuwa ‘Waja Wema’; Uja wema katika ‘Maugwana’ na si ‘Kiburi’…

Mfano mahsusi ya ‘Udhamirifu wa Furaha’ na ‘Ujumuiko wa Kizazi/Vizazi’, ni shauri la UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI. Kiuono na Ufikirifu mifumo, manne haya ni kwa ajili ya ruzuku ya Rehema na Fadhili ya UTU-MAISHA-UISHO. Kwa mintarafu ya hivi, ‘Wakati ni Ukuta’ kwa kuwa Riziki ya Mtu/Mwanajamii huja kwa nasibu ya mawili (1) Kazi, na (2) Neema. Basi ndiyo yawa, UTU-MAISHA-UISHO ni fanusi ya ‘Kazi na Sala’; Uugwana ni Kujiamini na Unyenyekevu katika njia za kile kilicho ni Khasa asili ya Uzima wetu wa Miili—Miili-Akili-Roho. Kiburi si Maungwana, kwa kuwa ni ‘kutangatanga mbali’ na ‘Karamu ya BWANA’-- Karamu ilivyo Daima kuandaliwa kwa wale wenye ‘Mioyo Safi’…

Mioyo safi, Kiuono na Ufikirifu Mifumo ndiyo asili khasa ya Utu wa Dhahabu kwa Nchi ya Tanzania, ambavyo ‘moto’ ni alama ya ‘kusafisha/kutakasa utu’. Kwa mintarafu ya hili, Upendo ni ufunguo kwa ajili ya utu wema; huu haukai katika moyo mtu mpaka yeye aifanye nafasi katika moyo wake ili matamanio na uhitaji wake visukumwe na makusudi yenye kheri kwake na jamii yote. Basi ndiyo yawa, moyo safi ndiyo udhamirifu ‘kumpenda jirani kama unavyojipenda mwenyewe’ ama pia ‘Kutomtendea mwingine vile usivyopenda wewe kutendewa’. Tena basi ndivyo, Rangi ya Utu Wema ni ‘Njano ya Dhahabu’—Njano ya Dhahabu ijayo Mwenge unaowaka Juu ya Mlima Kilimanjaro; kuwa huo ndiyo alama ya uwepo wa tumaini, upendo dhidi ya chuki na heshima badala ya madharau...

Ujamaa wa Kweli, Kiuono na ufikirifu mifumo ndiyo muktadha akilifu wa ‘Sovereini Jumuifu’. Kwa mintarafu ya hili, Ujamaa ni Imani na tena udhamirifu wa UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI miongoni mwa wanajamii. Basi ndiyo yawa, Demokrasia ni Masikilizano, Uhuru wa Kujidhihiri Utu na pia Uhuru wa Kujichagulia yale yajayo na kudra, siha njema na UTU BORA. Tena basi, Utu bora ni nidhamu, matendo na Hekima kwa ajili usivilai na utamaduni wenye kheri ya pamoja na tena wakati wote. Kwa nchi ya Watanzania, usivilai na utamaduni huu ndiyo dhana ya Uzalendo wenye ‘Utu wa Dhahabu’ kutokea ‘MASHARIKI’…

Rangi za Ujamaa, jamii moja yenye UTU Bora ndiyo ni ‘Zambarau’ ya mchanganyiko wa UBLUU wa Anga na NYEKUNDU ya NCHI/ARDHI; na tena, ‘Njano ya Dhahabu’ kwa chochote chenye kuwakilisha UTU na KUJICHAGULIA: Gurudumu la Dhamma kwa ‘kusudio Dhamma’…

Chief hakika andiko lako au maandiko yana maarifa mengi tatizo lugha kiswahili unayotumia ndio shida,yaan ni kiswahili lkn kigumu sana

Mimi huwa ni mbishi wa kutaka kuelewa lkn huwa inaniwia ugumu kuelewa ujumbe wako

Ebu naomba uandike kwa lugha nyepesi,kwasababu inafika kipindi mtu unapoteza hamu ya kusoma kwa lugha iliyotumika
 
Mimi interest yangu zaidi ni kuhusu majini tu na si kingine kama hao washenzi wachawi.Huwa napenda kupata ilm ya hawa viumbe direct kutoka kwa mtu mwenye experience nao hususani kufanya nayo kazi,story za kwenye Qur'an zinazosemaga sijui majini waliumbwa kwa moto,sijui wanakaa sijui kwenye magofu na sehemu chafu naonaga tu kama ni hadithi tu za kutungwa.Sasa nikirudi kwenye swali langu la msingi, iwapo majini ni viumbe wa asili,je inawezekanaje mtu anamtengeneza jini,maana kuna mabwana kama wawili niliwasikia wakilizungumzia hili linalohusiana na majini ya kuyatengeneza na kuyatega sehemu.Na je majini yote yanayotegwa ni ya kutengenezwa au hata majini ya asili yanaweza kutegwa kwa ajili ya kuleta maangamizi
Kama ushasema "sijui" si uulize uelimishwe?

UnKataa wachawi wakati mwenyewe unajiita roho ya kishetani?
 
Mbona hii anayotoa ndio solution ya kila kitu ndugu....🤔
Narudia tena hii ndio solution ya kila kitu🤝🤝
Naweza nikakuthibitishia hilo kwa vitendo!!!
Sema sijui namna ya kuweka sawa hii kitu, ila ningetoa somo lisilo rasmi kuhusu namna ya kuwa connected na Mungu direct!!!
Ila naogopa sabb elim yangu ndogo sana (maana mm ntaongea kutokana na experience wala sitotumia vitabu na uthibitisho wa hadithi sana.... Mm ntaongea kinachonitokea, Sasa mwisho ntajitukanisha hapa maana ntashindwa kutoa ushahidi🤝🤝

Na Kama ujuavyo humu wenye elim ni wengi 🚶🚶

(Ila ukiishi kama watu wa zamani ni rahisi Sana kumpata Mungu na kuuona ukubwa wake, hii nimeijaribu kwa baadh ya vitu ni really kabisaaaa
Nadhan tuko kujifunza elimu kwa mapana yake,wewe eleza uzoefu wako kuna kitu tutajifunza

Mwenye uzi mwenyewe kuna mambo huwa anaandika lkn tunasoma tu ingawa hayaafikiani na uelewa au kwa jinsi tunavyofahamu,kwahiyo mwaga elimu
 
Nadhan tuko kujifunza elimu kwa mapana yake,wewe eleza uzoefu wako kuna kitu tutajifunza

Mwenye uzi mwenyewe kuna mambo huwa anaandika lkn tunasoma tu ingawa hayaafikiani na uelewa au kwa jinsi tunavyofahamu,kwahiyo mwaga elimu
Kama lipi hilo?

Usifikiri unachoelewa wewe ndio kila kitu. Mimi kuna vingi wewe unavyo sivielewi na kama ninavielewa umevikosea nitakueleza wazi hivo sivo, ni hivi...

Binadam tuna kasoro ya kudhani tunachofahamu sisi na mwenzetu anakifahamu au fikra zatu sawa na za mwengine.

Uelewa na ufahamu wako ni tofauti na wangu na mimi halikadhalika, kama utafanana ni kwa uchache wake tu, sio kwa wingi wake.

Ndio maana Mwenyezi Mungu katupa mwongozo, ili hata tutapohitilafiana tusipotee njia. Turudi kwenye njia iliyonyooka kwa kujikumbusha kutwa mara tano kwa uchache.
Simba.
 
Arsis nimeguswa na swala au changamoto ya madam Farijala wa Farijala kuhusu mumewe,hakika huyo mwanaume mwenzetu anaumia sana lkn na dada yetu anaumia pia,kwasababu si nature ya mwanamke kulea familia,yaan analea lkn ni mzigo mzito kwake sana
Sasa kuna ushauri ulimpa wa ibada na kuacha maasi kitu ambacho ni sahihi kabisa,lkn inajulikana Mwenyezi Mungu ndio suluhisho la kila kitu sisi wengine ni sababu tu,kwahiyo kama kuna sababu ya kumpa kama ni dawa au namna nyingine yoyote basi msaidie ila mponyaji ni Allah

Kwangu mimi nashauri huyo mumeo wakati wa kuoga aweke chumvi ya mawe katika maji yake na iwe sehemu ya zoezi lake la kila siku,hiyo ni dawa ya asili ya kuondoa uchafu mwilini ya kichawi na kishirikina

Ila asiweke imani juu ya hiyo chumvi kwamba itamsaidia ila anapoweka chumvi katika maji anuie mfano wa hivi EWE MWENYEZI MUNGU HAKIKA WEWE NDIO ULIYO UMBA HII CHUMVI NA KUIPA NGUVU YA KUONDOA UCHAFU NA.MIKOSI NA MABALAA,NAOMBA KUPITIA HII CHUMVI IWE NI SABABU KUNITAKASA NA MABALAA YOTE YA KICHAWI,NUKSI NA UBAYA WOWOTE ULIO KATIKA MWILI WANGU

Kwa nia hii utakuwa umemtegemea Mwenyezi Mungu na si chumvi kama chumvi

Nakumbuka kipindi fulani pamoja na kufanya ibada nilitumia chumvi kuogea mara kadhaa,kuna matokeo yalionekana ikiwemo kuota usiku kitu kama majini yametoka nyuma ya mgongo wangu na.kusema huku yanapaa kutoka ndani kwenda nje ya nyumba "wewe si unajifanya mjanja sawa " baada ya kuamka niliwaza sana juu ya ile ndoto

Kwa kifupi habar za chumvi kuwa sehemu moja wapo ya tiba ya asili inakubalika sana na si uchawi,ila nasisitiza usiegemeze kuwa chumvi ndio suluhisho la shida zako ila Mungu kwanza na chumvi ni kama sababu tu

Kama vile tunavyokunywa dawa za hospitalini,anayetuponya ni Allah na dawa ni sababu tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom