yellow java
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 1,283
- 2,332
Mkuu samahani...Inatokea post namba 2179.
Vionjo vya Arsis 4 Kumwokoa Msukule Unguja 6.
Kwa mara ya kwanza nikawepo kwenye kesi ya Majini na Watu.
Akaanza kuongea Kamanda wa kijini, aksema:
Sisi kwa heshima na taadhima kiubwa tunamwachia Simba aendeshe hii mhakama kwa sabau oinahusisha majini na wanadamu na kwa utukufu wa cheo yeye ana cheo kuliko sisi wote hapa. Na ushahidi wa hili ni pete alioivaa. Tunaomba nyoosha mkono juu uuoneshe ushadi wa nilichokisema.
Sauti ya rsis; Nyoosha juu mkono wa pete simba usiogope, tupo salama.
Nikamwabia kwa kichwani, poa, nikanyoosha mkono juu kwa kuelekeza jiwe linapoonekana kwa kuelekea kwao. Ukatoka mwangaza kwenue ile pete kama imepigwa na miale ya jua, ikamulika rangi nyekundu kwa sekunde kadhaa.
Kijan: inatisha simba, shusha tu kono anzisha kikao, mimi siwezi kukuingilia kwa hadhi ulionayo hapa.
Kushusha mkono nikaona majini wote kama wameinamisha vichwa wansikiliz nitasema nini;
Mimi: sikilizeni nawaambia. Makosa yaliotendeka ni makubwa kwa kiwango chpochote kile, namwachia Kija hapa aendeshe hiki kikao kwa niaba yangu, mimi nitakuepo hapa kuhakikisha hadhulumiwi haki yake mtu wala jini.
Nikawa najishangaa nilivyochomoa zigo kubwa lile, kabla sijawaza kitachoendele, Kamanda akaanza...
Kamanda; Kama aliyoamrisha mkuu tunakuomba Kijana usimamie hii kadhia kwa niaba ya Simba.
Kijana; Kadhia imenza! Nimekubali kuendesha hii kashia na nitamuomba mkuu hapa aridhie tuendeshe hii kadhia mimi na Kamanda, kwani kuna binadam namajini wameshirikiana kufanya maovu. Naomba Mkuu Simba uridhie ombi langu.
Mimi: Nimerishia. Kamanda mtaendesha kushirikiana na kijana hapa.
Kamanda Nimerishia mkuu.
Kijana; Kamanda anza wewe kadhjia upade wa majini.
Kamanda: Hii kadhia ni nzito na hukumu yake ni kifo. Haya wale majini wote wasiohusika na hii kesi waondoke. Naomba iwe hivyo kwa binadam vile vile. Kasoro wanaoendesha kikao tu.
Kuna kundi la majini likachomoka pamoja na Jini 2. wakaondoka wakapotea kichakani huko, poakabaki majini wachavhe tu wale wa kichawi na binadam ni wale wachawi tu.
Kamanda: Kosa lenu mnalielwa enyi majini wote miopo hapa? Asielielewa aseme hataraka.
Wakajibu tunaloielewa.
Kamanda: Mnaelewa makosa yenu hukumu yake ni nini? Wakiajibu kw apamoja kifo au atakvyoamua mkuu wa kuendesha kashia hii.
Kamanda; Kwa kua wote mmekiri kposa na wote mnaielewa hukumu. Mimi naamuru kuwaua mara mja itakua hamjalipa adhabu ya kutosha itakua ni kama msamha kwenu hapa duniani. Naamuru mkafungwe na hapo kifungoini kila kosa moja mtafungwa miaka 10 ya kibinadamu na kila anaemaliza kifungo chake atauliwa au itakavyoamuliqa baadae na wafalme. haya wanajeshi mnajuwa cha kufanya njooni muwachukue hawa wakaanzekutumikia adhabu zalo kiuanzia dkika hii.
Mimi nikajionea ajabu, hakuna kuchelewa hakunakuramba remba. Tiuukabaki binadam na wachawi na kamanda tu.
Kamanda, : sasa zamu ya watu kuhukumiwa, haya Kijana, nakuachowa wewe, upande mmpoja tumemaliza.
Kijana; Hili kosa kibinadam vile vile hukumu yake ni kifo. Wale wanaoolewa kosa lao waseme, wote kimya. Nitauliza mara ya pili wale wasioelewa kosa lao waseme. Kuna yule mwanamke alikua kimbele mbele, kujle wakati tunamfungua yule binti, aksema mimi sifahamu kosa langu.
Kijana akasema huyu mchukueni anataka kuichelewesha kshia, akafungwe na majini na aadhibiwe mpaka akiri kosa lake.
Majini ya kijeshi yakaja kama binadam, yakambeba yakaondokja nae.
Kijana; Nyinyi mliokaa kimya nawualiza mara ya mwisho kama hjaajibu tunapitisha asdhabu.
Dereva; Mimi siijui hii kadhia kwanini nimeletwa hapa?.
Kijana; Mchukueni huyu kama yule mwanamke.
Kijana haya; Mliobaki nyinyi wachawi wakubwa hamtaki kiusema?
Wote kimya kabisa.
Kijana; Na hawa wachukueni iwe kama wale wale wa mwanzo.
Wakachukuliwa wachawi wote, hakuna aliesema lolote wala kuguna. Nadhani wote wameelewa kuja mwisho wao wa kua duniani umefika.
Kijan: haya tumemaliza kashia.
Kamanda; Tufanyie dua mkuu, kazi imefanikiwa, sisi turuhusu tuondoke turudi makwetu.
Kijana: Mimi niruhusu pia niondoke lakini naahidi tutawasiliana. Isipokua mimi nitaondoka na nyinyi mpaka alipowachwa binti, kunamaagizo nataka niwape pale nihakaikishe usalama upo lakini nikimaliza nasafiri.
Mimi: Sawa, kadhia imefungwa tuondoke.
Tukaagana na kamanda, akaondoka na majeshi yale yote akjaingia kichakani akapotea. Tukaondoka na gari ile ile iliyotuleta akaendesha yule kijana. Njiani akasema:
Kijana; Hii gari hatuoni mtu, hii gari ya kijini, wewe Mkuu haujaistukia?
Simba: Niliona kitu nikataka kuuliza, lakini n9asikia Arsis ananambia usiulize kitu. Nikaacha kuulizanione mwisho wake.
Kijana; Uliona nini?
Pale juu bububu kuna kile kizuizi cha polisi hatukusimama kabisa na hakuna polisoi alietusimamisha wala kutuuliza na gari ya mbele yetu sijui yuliipita vipi maana sikuona kuikwepa wala kuipita na yenyewe ilikua imesimama. Tumeipita kama haipo.
Kijana; Ulikua mbali na mawazo, toka tulipotoka ndio ilikua hivyo hivyo
Itaendelea
Simba.
Simulizi imekuwa fupi na kidogo sana kuliko mabishano ya Adam kitu ambacho sio lengo la Uzi huu.
Mafunzo ,simulizi pamoja na vipande vidogo vidogo vya elimu tupewe kuliko kubishana kitu kile kile sijui Adam na Hawa na vitu visivyo na faida.