Inatokea post namba 81.
Nikabeba bakora yangu nikaelekea kwenye uwanja, nikaukuta uwanja mweupe kama umesafishwa, kutazama saa ya simu yangu ilikua saa 9 kasoro dakika 1, nikaona nimefika kwa muda muafaka, nikasimama natazama huku na kule nashangaa shangaa, uwanjani, kwa mbali, mwisho wa kiwanja kile kutupu, kuna kama miti miwili mitatu na yenyewe sio mikubwa sana, nikaona kama kuna mtu kavaa baibui kwa mbali, nikatoa salaam kwa sauti hajaitika, nikaanza kusoma dua, ile nasoma dua, yule mtu akapotea mbele ya macho yangu, ingawa ilikua kama mita 30 kutoke kwangu lakini kulikua ni mchana kweupe, kupotea kwake ikawa kama kayeyuka kwa kwenda chini ya ardhi na kwa mbali nikaona kama lile baibui limebaki pale nikawa nalisogelea kulitazama huku nasoma dua ndogo ndogo, kufika kama hatua kumi na pale, nikaona ardhi ni nyeupe, hakuna baibui hakuna mtu. Nikacheka, nikawa narudi pale kati ya uwanja, ile nafika kati ya uwanja nikajiuliza kwa sauti, yuko wapi aliyenitaka nije, itakua ndoto tu ile, nikawa naondoka, ile naanza kuondoka, nikasikia sauti ikiniita Bwana Mkubwa, nikageuka kutazama pande zote sikuona kitu sauti ikaendelea kunambia, huwezi kuniona, tafuta kitu ukae chini hapo nikajibu, wewe nani, mimi staki kukaa, ile kusema sitaki kukaa, kama nguvu fulani ikanivuta chini, nikajikuta nimekaa chini, nikitaka kunyanyuka nashindwa, nikapata kama hofu fulani, Ile sauti kwa upole wa kawaida, ikanambia usiwe na wasi wasi kaa chini, huwezi kunyanyuka hapo, ni mimi nimekuita, mimi naitwa Arsis. Akaendelea kunituliza kwa sauti ya kawaida, nisiwe na wasiwasi. Nikamwambia ramsis? Huyo si firauni, akanijibu akasema, kweli Ramses ni katika mafirauni, mimi sio Ramses, ni Arsis. Nilikuwepo pia wakati wa Ramses, namfahamu.
Ikawa wakati tunaongea kama mwili umejiachia na naweza kusimama, nikasimama sauti ikanambia tena, kaa chini tulizana. Uliza chochote unachotaka, naona una maswali mengi sana unajiuliza. We niulize tu, mimi nipo hapa kwa ajili yako. Nikawa nasita kumsemesha. Akanambia nisikilize kwa makini. Mimi nipo hapa kwa ajili yako, babu yako anajua habari zangu, hajwahi kuniona mimi hata siku moja, ni kama hivi ninavyoongea na wewe tu.
Hiyo pete ulioivaa ni yangu na mimi nimekuzawadia, hio pete ni ya zamani sana na inawindwa na kila mtu na majinni wajinga wajinga wanaitaka sana hiyo. Nikamuuliza, wanaitakia nini? Akasema ukiwa na hiyo pete ndio unakua u karibu na mimi na ukiivaa hio mimi nakua nipo chini yako, hio pete yangu lakini mimi siruhusiwi kuivaa toka nilipooneshwa, mimi kazi yangu kuilinda na anapokufa anaeivaa mwenye pete hio naichukua namtafuta mwenye vigezo vya kuivaa. Kwa sasa nimekaa nayo miaka zaidi ya 925 bila kupata mtu wa kumpa hio pete aivae, nimeacha salamu nyingi sana, mpaka mwaka juzi, nikatumiwa salamu nije kukuona kama una vigezo, nikawa nakufatilia sana, nikaona vigezo unavyo na vingine utajifunza kadiri siku zinavoenda.
Kwa ufupi, hio pete, unaweza kuivaa kidole chochote, mkono wowote, na kila utapoivaa utaiona ipo sawa, haikeri mkononi. Unaweza pia kuivua wakati wowote, lakini kumbuka, ukiivua lazima uiweke kwenye kijaruba chake. Haitakiwi ikae bila ulinzi wangu hata nusu dakika, kukupotea hiyo ikiwa umaivaa ni kitu hakiwezekani, wala haiwezi kuvuka kwa bahati mbaya. Ikikaa kwenye kijaruba chake hakunaambae haimuhusu hio pete akaweza kukinyanyua. Wewe si umekiona kawaida unakibeba inakifungua unakitazama, lakini jaribu kwa wengine uone kama watawea kukibeba. Nikamwabia, nakuamini, sina sababu hya kujaribu. Akaendelea kusema, ukinihitaji wakati ewowote wewe niute gtu. leo namalizia kwa hayo tu, usiku saa tatu uje hapa uniite, tutaongea zaidi na tayarisha maswali yakuniuliza. Uliza chochote utakacho kukijua, nipo hapa kwa kukupa elimu ambayo watu wengi sana hawana. Babu yako amenisikia tu habari zangu kwa mwenye hio bakora, lakini hajawahi kuongea na mimi isipokua huwa kuna vitu tunamuotesha ndani ya hii miaka mitatu, toka nilipokuona wewe. Mwenye hio bakora ni rafiki yangu wa miaka mingfi sana. Hio bakora nayo sio ya mchezo mchezo, lakini yeye mwenyewe atakufahamisha. Nikamwabia nifahamishe tu, kwani kuna ubaya? Akanambia, hakuna ubaya lakini mwenye ndio atakufahamisha vizuri zaidi. Unakumbuka ulivyolala leo mchana uliiweka wapi? Nikamwabia pembeni yangu, akanambia unakumbuka ulivyoamka uliikuta wapi? Nikamwabi nimeikuta imesimama kwenye ukuta wa pango. Ile sauri ikacheka, ikanambia haya kwa heri tutaonaana saa tatu usiku. Uje peke yako, ukija mwengine yeyote hatutoweza kuwasiliana, hautakiwi uje na mtu ukija kuniona. Kwaheri, akaniaga na mimi niawa natabasamu narudi pangoni.
Kufika pangoni nikaingia kwa ndani ya pango, nikaiweka fimbo pale chini kwa kulaza chini. Kuiweka tu, ikaanza kunyayuka yenyewe ikasimama ikasogea pembeni ukutani ikajiweka pale. Nikacheka kimoyomoypo. Huku najisema makubwa haya. Mara nikasikia hodi nje.
Kutoka nje ya pango, nikawakuta vijana wa babu wamekaa, wakanambia ulikua wapi Bana mkubwa, tumekuja muda hatujakukuta, tumekutafuta kote hatujakuona, kumbe upo hapa ndani mapangoni? Kabla sijawajibu, waksema leta pilau lile tuli[pige, bibi huko kasema tuje kula na wewe usile peke yako. Nikatoka na lile kapu la chakula wakaandaa pale tukakaa tukapiga pilau, ilikua pilau ya nguvu kweli, pilau ya kamba.
Mooja wa wale vijana akasema hao kamba bwana wanaitwa taiga, hao ndio kamaba ghali kabisa wakati wa msimu, hao ni lazima msimu ukianza ni lazima apelekewa babu na bibi pale nyumbani, hao wa pilau hiyo ni fresha wa alfajiri hao, hawajaguza friji hao. Hao ni wakubwa kasi sio wa kawaida wana nyama kweli. Tena usiku tutakula hao hao wa kuchoma, baadae tukawavune bwawani kwao. Wapo leo, wengi hawapajui pale.
Tukala pilau tukamaliza, kulikua n chiupa ina juisi ya machungwa, tukaipiga pale. Nikawaambia leo hatuna haja ya kula tena. Wakacheka yule nnae kaa nae pangni akasema usiku baridi huku, bibi kasema tukawavune tuwatengeneze wa kuchoma, yeye atakuletea rojo lake la kulia hawa, atakuja nalo babu usiku. Nikawaa mpbia poa, kweli usiku kuna kibaridi huku.
Tkakaaa kaa wananip story za kamba na namna wanavyotengeneza pesa msimu wa kamba. Wakasema kuanzia miezi miwili mitatu ijayti tutakua hatungji msimu, babu alimleta mtaalam wa ufugaji kama tumeshaanza kuchinga njia ya maji na bwawa upande ule, wakanionesha kwa kidole. Babu kafanya jambo la maana sana, lakini yuke mtaalam akasema huku pa asili tusipaguse kabisatupaache hivi hivi, hawa kamba wa asili huku ni bota mara mia kuliko wale trutakaowafuga, ingawa mbegu tutato hapa hapa, watakua tofauti kasema. Nikawaambia naona itakua kama kuku wa kienyeji na broila, wakacheka, wakasema hata mtaalamu kasem hivyo kwa sababu wale wa kufuga kuna vyakula vya atatufundisha kuvitengezeza ili wawe wanakua haraka. Tutaona jamani, itakuaje.
Itaendelea.