Vionjo vya Arsis 4 Kumwokoa Msukule Unguja 7.
Inatokea post namba 2331.
Baada ya kurudi tukakaa nje ya nyumba, mimi Kijana na Bakora
Bakora; Wakati wa kutumbua jipu umefika, lakini kama kawaida hatufanyi sisi. aitwe mama yake hapa, na watu wake wa karibu akiwemo mumewe na wagtu wake wa karibu.Tumalizie kazi. Hapa ndio kwenye mbichi na mbivu.
Mimi ; Twendeni tukawaite.
Kijana: Atkwenda Jini1 kishazoeleka mazikoni na hajulikani kabisa kama ni Jini, sijui ana mbinu zipi, hayo mengine mtaulizana wenyewe kwa muda wenu. Isipokua nagfahamu, wakati sisi tupo bububu kulikua na kikao kikubwa huku na wanawake na mamake sasa anajua kila kitu na amesgamuona binti yake.
Sisi twendeni tukale, Mama yake na wengine tutawakuta hapa pamoja na ndugu wengiune na mwenye hii nyumba, tutakuja na wageni kuyamaliza. Simba utajionea watu wanavyoumbuana leo. Na ni lazima iwe hiyo ili kufunga hii kazi.
Sawa; Twendeni.
Tukaondoka kwa miguu, mimi Bakora na Kijana. tukafika mazikoni, mwenyeji watu akatuona,
Mwenyeji; Mmekuja wakati muafaka chakula ndio kinaletwa, njooni tule, njooni mkae na mimi.
Bakora: Poleni sana na msiba?
Mwenyeji; Ndio njia yetu sote, tusikumbushane, ni majonzi makubwa jamani.
Chalkula kikaletwa tukala pale kumaliza ikaja kahawa wakati tumekaa ytunakunywa kahawa. Akaja mtoto kumuita mwenyeji wetu, akatuomba radhi akaingia ndani. Akakaa kama robo saa. kutoka...
Mwenyeji; mambo ya kina mama, hawajiwezi bila sisi, wameniomba twendeni kule kwa dada yake mke wangu, sio mbali na hapa. Kuna kikao cha kifamilia, wanawake wameshatangulia huko, na kuna masheikh wawili, Sheha wa mtaa na majirani mmoja wao na engine ambao hawapatikani kwenye simu wameenda kuitwa, tuwasubiri kidogo wattakaofika mapema tutaenda nao na nyinyi masheih zangu nimeagizwa twendeni wote tusiwawache pekeenu msibani Huyu bwana, huku anaioneshea mimi, nimeambiwa mamake atakua huko pia, na weewe mgeni wake na sheikh wenu, twendeni na mimi na wengine wakishakamilika. Wanafamilia wengine watakua huko, ndugu, jamaa na marafiki, watakuwpo. Utafikiri kuna kikao cha mirathi huko na alietutoka ni binti mdogo.
Mimi; Nikacheka.
Bakora; Shughuli haina dogo hata uwe ni msiba.
Mwenyeji; Kweli Sheikh, si unaona nyinyi mmetoka bara, tumejuana kwa huu msiba.
Kijana; Labda kuna heri huko?
Mwenyeji: Inshallah hakuna zaidi ya heri, naona Sheha kishafika bado hao majirani wawili, aah, wale anakuja pamoja. Hatuna cha kusubiri wengine watakuja hukohuko sio wageni napo.
Wakafika wote tukaenda gtukakaribushwa kwa vilio tulipofika hakuna asielia. Tukawekwa kwenye ukumbi mkubwa,m wanawake wakarudi ndani, tukaa wote, ni ukumbi mkubwa wa kifahari, ukoo huu unaonesha unajwieza.
Tukaongea ongea.
Sheha; Haya waiteni kinamama tuyamalize nimekuja na makaratasi na kalamu, uzoefu umenikumbusha mambo haya lazima awepo katibu na Mwenyekiti.
Kina mama wakaja, wana familia wazee na vijana, wa familia ya baba na mama wa binti, mara kidogo wakaja wanaume wengine wazee na vijana wakatambulishwa kua ni ndugu wa karibu wa wafiwa. Ikawa tumejaa pale.
Sheha; kuna mwengine tunamsubiri au tuanze? Kina mama sasa mufanye subira ya vilio, na kikao kiende salama. msheikh someni dua tuanze. Ikasomwa dua fupi.Kikao kikaanza.
Sheh;, haya jamani hizi kopi nimeleta, hazina makuu, kila moja ijazwe kwa mkono na kila mmoja aandike jina lake uhusiano na marehemu na asaini, tuzikusanye baada ya hapo tutaanza kikao.
Tulipomaliza kujiandikisha majina, wakateuliwa mwenyekiti ambae ni kaka na baba wa marehemu (mwenyeji wetu) na katibu ni kijana moja anaonesha msomi wa kwenye ukoo upoande wa wanaume na Sheha akasema na kina mama mmoja nae achukue maelezo ya kikao, namuona Bi... ana uzoefu wa ukatibu serikalini tena huyo anaandika kwa shorthand na yeye aandike kivyake.
Mwenyeji: kwani kuna urithi jamani?
Sheha; Subiri mwenyekiti akupe ruhusa ya kuongea ingawa wewe ni mzazi, vikao hivi haviendi hivyo. haya mwenyekiti nzisha kikao.
Mwenyekiti; jamani kwanza tunashukuru kuwepo hapa, kikao kianze, maana hata mimi sujui tuongee nini kwani vikao namna hii mara nyingi hua ni vikao vya kuandika alivyoviacha marehemu ,lakini hapa naoina mareehemu kaacha wadogo zake, mama na baba, ndugu jamaa na marafiki, au alikua na mali zake?
Mwenyeji; Anazo laki ni ni guo na vitu vitu vyake na sisi kwa kua ni wazazi tutaamua zifanywe nini baada ya matanga kuisha, hakuna zaidi, labda viherini na vicheni vyake vya dhahabu ndio vya thamani.
Mwenyekiti: Sheha tupe muongozo.
Sheha; kama alivyosema baba mazazi mimi naona yupo sawa, au wajumbe mnasemaje? Kama kuna mwenye ushauri auseme tuendelee.
Wakatazamana hapo. lkini wote kimya.
Mwenyekiti; naona hakuna, sasa alieitisha kikao atueleze alichotuitia tumalizane.
Katibu; Mimi nimeitisha hiki kikao cha dharura, kwa habari zilizozippata leo afajiri baada ya kusali. Nimehakikisha za kweli na ndio nikaitisha kikao kwa ushauri wa Sheoikh nani hii hapo na Huyu DSheikh mgeni, akamuonesha Bakora na Sheikh mmoja maarufu tu anajulikana Unguja katika tuliokuepo.
Katibu: Mimi naomba wahusika wajielezee wenyewe. Huyu bwana hapa ndio muhusika mkuu wa kikaoo hiki, na anafahamu kwanini tupo hapa ingawa ni jirani tu. Akamyooshea kidole afisa mmoja kanona nona hivi.
Afisa akaanza kutaka kubabaika.
Bakora: Shehe ongea tararatibu na kwa ufasaha, wewe sio mgeni na mimi.
Kwa upande wa wanawake nikaona pale yupo Jini 2 lakini hatishi kabisa, kajitanda kama wanawqke wengine tu, kawaida.
Afisa: Jamani yaliotokea yametokea, mimi naanza kwa kuomba msamaha.
Mwenyekiti; Mbona sielewi mnachokiongea, ni mimi tu sielewi au?
Katibu: Huyo md*anajifanya haelewi, afisa nakusihi usitupotezee muda, umesshatupoteea muda wa kutosha, tuna mambo yetu ya kufanya. Anza kuelezea kama ulivyotueleza baada ya alfajiri.
Nikaona Bakora kama kabadilika hivi;
Afisa: jmani binti anaesemekana marehemu, yu mzima hajafa ni mambo ya kichawi tu.
Nikaona watu wengine ganzi, kina mama wakaanza kulizana pale. Tukawapa kama dakaika moja.
Mwenyekiti; makubwa haya.
Sheha; Endelea, na kina mama nyamazeni tuna kazi nyingine za kufanya.
Mwenyekiti kua na kauli.
Sheikkh wa Unguja; Jamani naomba kuongea kidogo. Mimi binafsi nilisitika sana leo baada ya kusali alfajiri nilopitwa kushirikishwa haya mambo. Sikua na taha hata kidogo na nataka kuyaona yanafikia mwisho, maisha yaendelee. baada ya alfajiri tumekuja tukashuhudia binti yu hai, mzima wa afya, na mamake anafahamu na mwenye nyumba hii anafahamu na ndugu wengine waliopo hapa wanafahamu, kasoro baba mzazi tu. kwa hio Afisa haya tunayaweka wazi tu ili maisha yaendelee, huna la kuficha afisa au mwengine yeyote, tuongee kiuwazi na ukweli umeshadhihiri. Au mnasemaje jamani?
Watu wakasema. kweli.
Sheha; labda mimi nimuongoze kwa maswali na atoe majibu, tusipoteze muda.
Mwenyekiti; Sawa, anza Sheha.
Sheha: Jieleze unaitwa nani na unafanya nini, tusipoteze muda.
Afisa; Mimi naitwa... nafanya kazi wizara... ni mkurugenzi mkuu pale wizarani.
Sheha; Nini kinaendelea?
Afisa; Hiki kikao nimeitwa hapa ili yatoke kinywani mwangu.
Sheha; Sema haraka hiki sio kikao cha siasa.
Afisa; Mimi ndie nilipanga kumtorosha binti kwa sababu za kishirikina na tamaa na mvuto wa kishirikina. Binti hatukumuua lakini ndio asingeonekana tena naisha. Ningekua mimi nje ya mji kwa mambo ya kishirikina, kama mke wangu.
Sheha endelea; Tumefanya mazingaombwe kishirikina na wachawi wa chama chetu cha wachawi na wanga. Tuliozika jana ni mgoimba tu, binti yupo na nyote kwa sasa mnaujua ukweli na yuko wapi.
Mwenyeji; Mimi ni mzazi wake na sijui mnachokiongea.
Afisa: Haina haja ya kuficha au kusema uongo, tumeshaumbuka, unayajua yote.
Watu wote tukawa kama tumepigwa ganzi, tukabaki kimyaaa, ytunasikiliza.
Mwenyeji; Wewe eleza yanayokuhusu, ya wengine achana nayo.
Afis; Huyu bwana na mimi tupo chama kimoja lakini huyu binti yake ilikua anajua kua hauliwi ndio akakubali kutupa ushirikiano kwa malipo makubwa tu, ilikua tumpe millioni 100 kidogo kidogo. Asingeweza kukataa kwa sababu alikua anahitaji pesa kwa ajili hya madeni ya nyama na damu za watu anaypodaiwa kwenye chama.
Chama chetu kuna ada ya kila mwanachama, nayo sio pesa wala mali, ni nyama na damu za watu. Huyu anadaiwa, imebidi apate pesa watumwe watu walete damu na nyama alipedeni lake lifutike. Akakubali, tukashirikiana, ameshalipwa millioni hamsini na ameshapeleka kulipa nusu ya deni ndio hii kazi ya binyti ikafanyika, bado hajalipwa nusu, ilikua mimi nimkamilishie ndio na yeye akamilishe, lakini ndio yametokea yaliotokea. Natumai nimejieleza vizuri.
Katibu: bado, sema mngemfanyia nini huyo binti?
Afisa: Huyo binti ilikua tunamuwahi hedhi yake ya kwanza, napewa mimi inachanganywa na kote, na mambo yetu mengine. Inakua nakunywa na kukogea mpaka hedhi ikate, Baada ya hapo mimi nambikiri, damu ya bikira nayo inachanganywa na dawa na shahawa zangu nakunwa na kujipaka mwilini ili kuleta nguvu na mg'aro na kujilindia hadhi yangu na kua na kauli kazini.
Sheha: Tulizana kwana unatutia kinyaa. Haya eleza wewe baba mtu.
Baba; Mimi jamani kama alivyoeleza, naona hapa hakuna pakuchomokea, kweli mimi ni mshirikina lakini sijafikia kwenye uchawi, siujui, mimi naufanya tu ushirikina kwa kuwatumia waganga na wachawi, niliingia hicho chama chao miaka mingi tu katika kujitafutia mali. Ilipofikia ndio kama alivyosema Afisa.
Mwenyekiti akanyanyuka akamzaba kofi kubwa mdogo wake.
Mwenyekiti; Kumbe ni mnyama wewe tunaishi na mnyama kwenye ukoo, wewe ni zaidi ya nyoka..
Sheha; Subiri kaka.
Mwenyekiti; Haya na ue-meaza-anzaje, nani kakakuingiza kwenye ushirikina?
Mwenyeji; Mimi nilienda kmwenye kwa mganga kusafisha nyota, tukaanza masharti madogo madogo, kila miaka inavyokwenda ananambia ukileta damu adimu ndio mambo yako yanazidi kunyooka na nyota inazidi kusafishika. Nilianza na jogoo, nikaja mbizi, nikaja kondoo, nikaja ng'ombe, nikaja ngmia, nikaja mpaka binadam wa kununua, sasa imefikia siwezi kulipa zaidi ya damu ya binadamu na nyama za watu, ikabidi niuze kilicho changu, ilipotokea fursa ndio nikaongea na huyu bwana, mengine yaliofata mnayaelewa.
Mwenyekiti; Sio mkeo alokuingiza kwenye ushirikina?
Mke; Koma kama ulivyolikoma ziwa lala mamako, wachawi wakubwa nyinyi, mie ningekuwemo si ndio ningetajwa kwanza. Mimi nilimkanya siku nyingi mambo yake ya waganga huyo mshenzi, lakini sikujua kafikia kwenye uchawi, nilikua najua ya mbuzi na kondoo. Wewe usijifanya huna habari, mpaka mkeo anayajua nimeshamwambia akueleze nyingi ili umkanye mdogo wako, lakini ulikua unapuuza kwa visenti wanavyokupa. Mmelikoroga sasa mlinywe.
Bakora; Samahani, mimi ni mgeni, yule mama hahusiki na chochote ni mcha Mngu sana, ucha Mungu wake ndio uliopelekea hata huyu binti hakudhurika. Tuendelee na kikao.
Itaendelea
Simba.