Nilitaka kumuoa binti wa Dini tofauti na yangu vita kubwa ikaibuka. Kuna kitu gani kati ya hizi dini mbili?

Wanajificha chini ya mwavuli wa "Mungu ni mmoja", na kwamba dini yao ni ya amani wakati kila siku wanamwaga damu za watu wasio na hatia kwa jina la huyo Mungu wao.

Ni kweli wanabuabudu mungu mmoja ambaye ni Allah. Na Wakristo wanamuabudu Mungu mmoja ambaye ni Yehova. Hatujawahi kushirikiana kumuabudu Mungu mmoja, iwe Allah au Yehova
Mkuu hizi dini zote zimemwaga damu za watu wasotajika idadi, ni vile hatuelezwi yaliyokuwa yakitokea hapo zamani tu.

Na sasa Uislamu sababu ni contemporary basi unapata attention yote ila kuna mishenzi iliua watu kifala ikatumia Ukristo manina zao kama ilivyo mishenzi ya sasa inayotumia Uislamu.
 
wewe unaamini MUNGU mmoja
kama unaamini MUNGU mmoja
basi ALLAH na YEHOVA ni huyo huyo
kama unaamini MUNGU wa IBRAHIM(ABRAHAM)
Basi na WAISLAM tunamuamini MUNGU huyo huyo
kama ibrahimu aliamini MUNGU mmoja na WAKRSTO wanamfuata IBRAHIM
na WAISLAM tunamfata IBRAHIM tunaamini MUNGU mmoja
Sisi waislam tunapingana na wanaoabudu masanamu wanaoabudu Viumbe wanaoabudu mizimu na wanaobudu MIUNGU

FALSAFA ya UISLAM ni KUAMINI MUNGU MMOJA na KUAMINI MITUME YAKE na KUAMINI MUHAMMAD ni MTUME WAKE

na hiyo pia NDIYO ilikuwa FALSAFA ya YESU wakati wote akihubiri INJIRI
YESU alihubiri MUNGU MMOJA na akafundisha neno kwa kuwaambia yeye ni MTUME WA MUNGU amekuja kuitangaza INJIRI ya MUNGU
Hapana, hauko sahihi kabisa.
Falsafa ya imani ya kiislamu ni tofauti kabisa na falsafa ya imani ya kikristo. Nitafafanua hapa kwa kifupi.

Waislamu na wakristo kusema wanaamini Mungu mmoja haina maana kuwa wanaamini katika Mungu yule yule. Mimi ninaweza kuwa ninaamini mungu mmoja ambaye ni mbuzi, na wewe unaamini mungu mmoja ambaye ni ng'ombe, je tunaamini mungu yule yule?

Kuhusu Ibrahimu, wakristo wanaamini katika Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo, Mungu huyo ambaye alimtoa Yesu afe msalabani kwa ajili ya dhambi za ulimwengu na kisha kumfufua siku ya tatu na kisha kupaa mbinguni. Habari za Mungu huyo wanazisoma kupitia Biblia. Wakati waislamu wanaamini katika Mungu wa Ibrahim na Ishimaili, ambaye alimpa utume Mohammad ili watu wamfuate, na habari za Mungu huyo wanazisoma kupitia Quran na hadithi za mtume.

MY TAKE
1. Mungu anayeaminiwa na wakristo ni tofauti na Mungu anayeaminiwa na waislamu.

2. Ibrahimu anayeaminiwa na wakristo habari zake ziko kwenye Biblia, na Ibrahimu anayeaminiwa na waislamu habari zake ziko kwenye Quran na hadithi za mtume, ni watu wawili tofauti ukiwasoma kiundani.

3. Misingi ya dini ya Kikristo (inayosimamia katika Yesu) ni tofauti kabisa na misingi ya kiislamu (inayosimama katika Mohammed). Yesu na Mohammad hawafanani na wala hawaelewani, mmoja anabeba sifa za uungu (Yesu) na mwingine anabeba sifa za utume (Muhammad) kwa mujibu wa imani husika.
 
wewe unaamini MUNGU mmoja
kama unaamini MUNGU mmoja
basi ALLAH na YEHOVA ni huyo huyo
kama unaamini MUNGU wa IBRAHIM(ABRAHAM)
Basi na WAISLAM tunamuamini MUNGU huyo huyo
kama ibrahimu aliamini MUNGU mmoja na WAKRSTO wanamfuata IBRAHIM
na WAISLAM tunamfata IBRAHIM tunaamini MUNGU mmoja
Sisi waislam tunapingana na wanaoabudu masanamu wanaoabudu Viumbe wanaoabudu mizimu na wanaobudu MIUNGU

FALSAFA ya UISLAM ni KUAMINI MUNGU MMOJA na KUAMINI MITUME YAKE na KUAMINI MUHAMMAD ni MTUME WAKE

na hiyo pia NDIYO ilikuwa FALSAFA ya YESU wakati wote akihubiri INJIRI
YESU alihubiri MUNGU MMOJA na akafundisha neno kwa kuwaambia yeye ni MTUME WA MUNGU amekuja kuitangaza INJIRI ya MUNGU
Wacha ubishi, Allah na Yehova ni Miungu tofauti. Allah alihubiriwa na Mudi wakati Yehova alihubiriwa na Abra na Yesu. Kuna miungu mingi sana sheikh wangu wakiwemo Miungu ya wabudha na wahindu, Wewe baki na Mungu wako kama anakusaidia ila usilazimishe Alla wako ni sawa Budha au Yehova wa watu wengine, Sisi wabantu Mungu wetu anaishi kwenye milima, makaburini, mapangoni au kwenye miti mikubwa, tuache kama tulivyo,
 
yeye akiwa ni Muislam na mie Mkristo;

Alikua pisi haswa, mtoto mkaree kila angle na anayajua mapenzi haswa, nikasema tabu za nini hasa ukizingatia bint mwenyewe ananitii kila nnalomwambia, sikua na upinzani wowote kwake, najipigia mwenyewe tu ki uhakika.

Sasa nilivyotangaza tu kumuoa na kuwaambia ndugu na jamaa kwamba kuna sehemu nimenasa na sasa nabeba jiko jumla hapo sasa ndio vita vikazuka, mwanzo nikaona ni mambo ya kawaida "jamaa wanaingilia maisha ya watu tena, hawa hawanijui hawa?" Lakin nikashangaa wazazi wote pande mbili wanapinga, wajomba wameshika mabango kwamba watu wa dini ile nyingine hakuna kabisa hawafai, nikasema eeh maji mazito kuliko damu ya mtume?

Binti alikua so so down, hana mzuka kabisa, mie na fosi bibie tulia wala usiwe na hofu dini tumeletewa na mabeberu tu, lakin ikamshinda nguvu maskini binti wa watu analia, maza ake nae kaja juu anasema kijana mkristow hakanyagi hapa kwangu, huba likakosa connection kabisa kimzaa mzaa tu, tukawa tunakulana tu na binti akawa anasema haoni future sa itakuaje? Nikamwambia basi tuzae tu wataelewa, akasisitiza mtume alishapinga kuzaa nje ya ndoa, basi ikaishia ivyo tu na sasa binti yupo na shekhe wake msoma visomo.

Hivi hua kuna bifu la chini chini kati ya hizi dini mbili? na raia hua hawasemi au ni nini? why wakule ni wakule na wa huku ni wa huku hakuna kuingiliana?
kumbe ni wewe hadi huku upo. ww ulitaka umuoe au umchezee mdogo wangu
 
Hayo ni maneno yakujifariji tu niwaambieni kitu ukweli siku zote haukimbiwi suala la mahaba na utiifu kwa mwanaume mmezidiwa Sana na wanawake wakislamu nyinyi mchowazidi uchakarikaji na usomi kwenye sifa zao lazima muwape na nyie kwenye sifa Zenu tutawapa bahati mbaya kwenu wamewazidi kwenye sehemu ambayo ndio Wanaume akili zetu zipo hapo yaani tunaiita sensitive area.Kwasababu ya wengi wenu kukosa sifa hizo kuu za wanawake wakislamu ndio maana mnatufanya tuwakimbilie lakini mngekuwa na hizi sifa wala tusiangaika na wanawake wakislamu kabisa
Wewe Sema unapenda vishungi usiwasingizie wanaume wenzio.
 
Upendo, utii, nidhamu na uchaji Mungu
Haya mambo hakuna asiye yajua.

Kibaya ni vile mnayahubiri lakini ninyi we nyewe hamyaishi.

Kwenye ndoa zenu ni vurugu kila siku. Usaliti, dharau, kiburi,

Maisha ya kawaida mmejaa unafiki, uchawi, rushwa..hamana hata chembe ya upendo.. ila mnajificha kwenye kivuli cha dini.

Nakataa mwafrika na dini ni unafiki tu. .. Acheni watoto waoane kama wamependana .

...
 
Wewe Sema unapenda vishungi usiwasingizie wanaume wenzio.
Hapana siwasingizii ebu fungua uzi wa namba hii uone kura zitaenda wapi utaona kabisa wanawake wakislamu watapata kura nyingi na ukizingatia hizo kura utakuta zinatoka kwa Wanaume wakikristo hata tukiwa kwenye vikao vyetu vya Wanaume unakuta hili halikwepeki kwenye mjadala na unaona Watu waliopitia kwenye hiyo situation wanatoa ushuhuda wao
 
Tukio kama hili lilishamtokea Kaka yangu. Yeye alipendana sana na Binti ambaye ni Muislam, tena Baba yake ni Shehe kabisa. Bro aivyoenda kujitambulisha aliambiwa labda abadili Dini ndio itawezekana. Vinginevyo hawezi kupata mke pale.

Kwa kuwa walikuwa wanapendana basi Binti akashika ujauzito wa Bro. Wazazi wa Binti walivyogundua tu, walimfukuza kwao na wakawa wamempiga marufuku asirudi tena kwao na hata ndugu zake wengi nao ni kama vile nao walimtenga.

Bro aliamua kuishi tu na yule Mke wake bila kupata baraka za wazazi wa Binti. Walikuwa wakiishi vizuri tu na walibahatika kupata watoto wawili hadi mwaka jana Mke wa Bro alipopata ajali ya Gali kisha kufariki.

Wazazi wa Binti bado waligoma kuupokea mwili wa Binti yao hata alipofariki hata kwenye mazishi hawakuja. Bint alizikwa Kiislam kwa msaada wa majirani na waislam wenzake na sisi ndugu wa mwanaume.

(Rest In Peace Shem wangu, ulikuwa na upendo wa kweli, mcheshi na uliwahi kunijuza kuwa hukupenda kuwa kwenye ndoa za wake wengi kama ilivyokuwa kwa Baba yako, kuna vitu uliviona na ukavichukia).

Tukio hili la Bro lilinifanya nijifunze kitu, kila ninapopata Dem wa dini Tofauti na yangu najikuta nalikumbuka hili tukio.
 
Hapana siwasingizii ebu fungua uzi wa namba hii uone kura zitaenda wapi utaona kabisa wanawake wakislamu watapata kura nyingi na ukizingatia hizo kura utakuta zinatoka kwa Wanaume wakikristo hata tukiwa kwenye vikao vyetu vya Wanaume unakuta hili halikwepeki kwenye mjadala na unaona Watu waliopitia kwenye hiyo situation wanatoa ushuhuda wao
Ingekuwa hivyo walioa waislamu ndoa zisingevunjika
 
Dah umenikumbusha kaka yangu alipomfata ex wangu eti niachane nae kisa ni dini tofauti tena alimfata na panga hiki kisa natamani niazishie uzi yale mahusiano nilipigwa mikanda sana home😬
Hebu leta kisa hicho huweza kikawa na mafundisho fulani
 
Tukio kama hili lilishamtokea Kaka yangu. Yeye alipendana sana na Binti ambaye ni Muislam, tena Baba yake ni Shehe kabisa. Bro aivyoenda kujitambulisha aliambiwa labda abadili Dini ndio itawezekana. Vinginevyo hawezi kupata mke pale.

Kwa kuwa walikuwa wanapendana basi Binti akashika ujauzito wa Bro. Wazazi wa Binti walivyogundua tu, walimfukuza kwao na wakawa wamempiga marufuku asirudi tena kwao na hata ndugu zake wengi nao ni kama vile nao walimtenga.

Bro aliamua kuishi tu na yule Mke wake bila kupata baraka za wazazi wa Binti. Walikuwa wakiishi vizuri tu na walibahatika kupata watoto wawili hadi mwaka jana Mke wa Bro alipopata ajali ya Gali kisha kufariki.

Wazazi wa Binti bado waligoma kuupokea mwili wa Binti yao hata alipofariki hata kwenye mazishi hawakuja. Bint alizikwa Kiislam kwa msaada wa majirani na waislam wenzake na sisi ndugu wa mwanaume.

Tukio hili la Bro lilinifanya nijifunze kitu.
Mambo ya Imani magumu sana mkuuu...!! Unaweza kuishi maisha ya mawazo na utumwa hata ukipuuzia vipi bado kuna kitu kitakuwa hakipo sawaa
 
Unavyo kuwa mjinga, mimi najua mpaka babu yake babu yangu mimi alikuwa Muislamu. Kama nyinyi kwenu hamna elimu za nasabab zeni ni nyinyi, sisi tuko tofauti na nyiny
Mbona unapanic..
Hiyo siyo dini ya babu yako wala mama yako wala mjomba wako.
Dini yenyewe umeletewa mkuu no matter babu wa kizazi cha pili au vipi.

Binadamu anazaliwa hana dini na sio kila imani inafaa kwa watu wote.
 
Tukio kama hili lilishamtokea Kaka yangu. Yeye alipendana sana na Binti ambaye ni Muislam, tena Baba yake ni Shehe kabisa. Bro aivyoenda kujitambulisha aliambiwa labda abadili Dini ndio itawezekana. Vinginevyo hawezi kupata mke pale.

Kwa kuwa walikuwa wanapendana basi Binti akashika ujauzito wa Bro. Wazazi wa Binti walivyogundua tu, walimfukuza kwao na wakawa wamempiga marufuku asirudi tena kwao na hata ndugu zake wengi nao ni kama vile nao walimtenga.

Bro aliamua kuishi tu na yule Mke wake bila kupata baraka za wazazi wa Binti. Walikuwa wakiishi vizuri tu na walibahatika kupata watoto wawili hadi mwaka jana Mke wa Bro alipopata ajali ya Gali kisha kufariki.

Wazazi wa Binti bado waligoma kuupokea mwili wa Binti yao hata alipofariki hata kwenye mazishi hawakuja. Bint alizikwa Kiislam kwa msaada wa majirani na waislam wenzake na sisi ndugu wa mwanaume.

(Rest In Peace Shem wangu, ulikuwa na upendo wa kweli, mcheshi na uliwahi kunijuza kuwa hukupenda kuwa kwenye ndoa za wake wengi kama Baba yako).

Tukio hili la Bro lilinifanya nijifunze kitu, kila ninapopata Dem wa dini Tofauti na yangu najikuta nalikumbuka hili tukio.
Nimewaza mengi mkuu..daah hizi dini hizi..
 
Back
Top Bottom