JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umeelezewa kusikitishwa na matukio ya kukamatwa kwa watetezi wa haki za binadamu, jana Machi 23, 2022 Wilayani Ngorongoro.
-----------------------------------------------------------------------------------------
NGORONGORO: TAMKO BAADA YA DIWANI KUSHIKILIWA NA VYOMBO VYA USALAMA
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umetoa tamko la kusikitishwa na matukio yanayoendelea Wilayani Ngorongoro yanayohusisha kukamatwa kwa Watetezi wa Haki za Binadamu na wengine wakidaiwa kusakwa na Jeshi la Polisi.
Kaimu Mratibu wa THRDC, Leopold Mosha amesema Machi 23, 2022, madiwani wa Malambo na Arash walishikiliwa kwa muda kuhojiwa na Jeshi la Polisi ikidaiwa ni kuhusu mgogoro wa wakazi wa Wilaya ya Ngorongoro wanaotakiwa kuhamishwa.
Mosha anasema: “Jana (Machi 23) madiwani hao walishikiliwa kwa muda, wakahojiwa baadaye kuachiwa, upande wa Diwani wa Kata ya Arash, Mathew Siloma alichukuliwa na Polisi, hadi muda huu (Machi 24) mawakili wetu hawajaonana naye.
"Mawakili walipofika Kitu cha Kati Arusha wamefanikiwa kuonana na RCO ambaye amesema Siloma yuko katika vyombo vingine vya usalama, hayupo kwao, lakini ameahidi watakapomrejesha hapo kituoni watapata nafasi ya kuonana naye na kuzungumza naye, hivyo mawakili wetu wanaendelea kusubiri."
-----------------------------------------------------------------------------------------
NGORONGORO: TAMKO BAADA YA DIWANI KUSHIKILIWA NA VYOMBO VYA USALAMA
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umetoa tamko la kusikitishwa na matukio yanayoendelea Wilayani Ngorongoro yanayohusisha kukamatwa kwa Watetezi wa Haki za Binadamu na wengine wakidaiwa kusakwa na Jeshi la Polisi.
Kaimu Mratibu wa THRDC, Leopold Mosha amesema Machi 23, 2022, madiwani wa Malambo na Arash walishikiliwa kwa muda kuhojiwa na Jeshi la Polisi ikidaiwa ni kuhusu mgogoro wa wakazi wa Wilaya ya Ngorongoro wanaotakiwa kuhamishwa.
Mosha anasema: “Jana (Machi 23) madiwani hao walishikiliwa kwa muda, wakahojiwa baadaye kuachiwa, upande wa Diwani wa Kata ya Arash, Mathew Siloma alichukuliwa na Polisi, hadi muda huu (Machi 24) mawakili wetu hawajaonana naye.
"Mawakili walipofika Kitu cha Kati Arusha wamefanikiwa kuonana na RCO ambaye amesema Siloma yuko katika vyombo vingine vya usalama, hayupo kwao, lakini ameahidi watakapomrejesha hapo kituoni watapata nafasi ya kuonana naye na kuzungumza naye, hivyo mawakili wetu wanaendelea kusubiri."