Mkuu jmushi, FMES alikuwa anajulikana hapa JF kama mzee wa dataz, jamaa alikuwa na access ya information nyingi sana hasa kutoka ndani ya CCM kabla ya mwanzo mwa mwaka 2010, tatizo ni kuwa alikuwa na nia ya kugombea na kuamua kujianika na watu waka-connect dots kama ilivyofanyika kwa tarishi wa OBL na mwisho wa siku wakagundua kuwa yupo Abbottabad. Tokea hapo amekuwa hana kitu cha maana tena zaidi ya kutetea watu wake wa karibu wanapokuwa attacked. Kwa kuanzisha thread kama hii ni wazi kuwa he's nothing kwa upande wa dataz za" wazee wa sauti za umeme" na usitarajie kitu chochote chenye maana kwa upande wa dataz ni Blah blah blah. Sikuwahi kuwaza kuwaza hata siku moja kuwa FMES anaweza anzisha thread iliyo hewani na ya ki-malaria sugu namna hii.
Nafikiri tunahitaji kuongelea mambo yenye manufaa kwa Taifa badala ya hizi blah blah blah za Ki-Tambwe Hiza. Kawaida unatuhumu mtu, anakupatia facts then unaangalia kama ni za kweli unakubaliana nazo kama hukubaliani nazo peleka mahakamani. Wahasibu kuna kitu wanaita support document kama hizi zipo, basi tungelee hali ngumu ya maisha, uchumi mmbovu, wizi wa mali za umma unaofanywa na waliokabidhiwa kuzitunza, CCM (waliomadarakani).