Mkuu Candid Scope,
Tatizo siyo lugha, tatizo ni chama kukosa hoja za maana ambazo zitaweza kukirejeshea chama haiba ambayo imepotea mbele ya wananchi/wapiga kura.
Nape Nnauye alianza kwa kishindo sana. Wiki mbili za mwanzo tangu alipoteuliwa kuwa Katibu wa Uenezi na Itikadi, alionekana kuanza kurejesha imani kwa wananchi.
Baada ya kufungwa mdomo amekosa cha kuongea na hivyo imebidi tu aanze kuleta vioja na lugha za kejeri. Hizo lugha za kejeri ndizo zinazidi kuongeza matope na haiba ya CCM inazidi kupotea. Hata wale waliokuwa na imani japo kidogo, ndiyo watazidi kuipoteza kabisaaa.
Kwa sasa Nape Nnauye amejiweka kwenye kona mbaya kwa sababu ya mambo yafuatayo:
1. Aliahidi kwamba mafisadi wataondoka na kuwaachia CCM iliyo safi (hapa aliwalenga Lowassa, Chenge na Rostam). Hoja hiyo imeenda na maji na sasa hivi haiongelewi tena maana amegundua kwamba hilo haliwezekani.
2. Alitamba kwamba mafisadi wataandikiwa barua, na alisema baada ya Pasaka barua wangepelekewa. Mpaka leo hakuna fisadi hata mmoja aliyepewa barua.
3. Nape Nnauye alisema mafisadi wamepewa siku 90 za kujitazama then wajiondoe na wasipoondoka watafukuzwa. Katibu Mkuu (boss wa Nape) akasema hakuna cha siku tisini na wala hilo halimo kwenye majumuisho ya makubaliano ya kikao cha NEC.
Hoja ambayo ilikuwa inampa nguvu Nape ilikuwa imejengwa kwenye msingi wa hoja ya ufisadi, lakini hoja hiyo imepoteza mwelekeo kutokana na hayo matatu juu. Nape amejikuta mahali ambapo kila anachokisema kinaonekana kupingana na maboss wake (Msekwa na Mukama). Swala la barua, Msekwa alisema wao hawafanyi kazi kwa kupitia vyombo vya habari (limeisha kimya kimya). Swala la siku 90, Mukama akasema halimo kwenye tamko la NEC. Swala la mafisadi watatu ambao walikuwa wakilengwa na Nape, Mukama alisema CCM haina list ya mafisadi. But Nape alisema anawajua na kwamba wameambiwa wazi na walitajwa majina kwenye vikao, sasa kwanini Msekwa na Mukama wanaingia mitini?
Nape yuko njia panda na si ajabu anajuta kwanini alitamka hayo maneno wakati wa ile mikutano ya mwanzo ya Operation Vua Magamba. Maneno aliyoyatamka amekuta hayatekelezeki au walio na uwezo wa kuyatekeleza, hawataki au wanaogopa. Sasa inabidi aje na vijembe, vioja na lugha za kejeri, typical Mzee Makamba na Tambwe Hizza.