Mzee Butiku: Watanzania hawajaridhika na uwekezaji wa bandari, serikali isione aibu kuachana nao

Sexless

JF-Expert Member
Mar 11, 2017
21,563
50,415

Mzee Butiku anasema kwa namna kelele zilivyo nyingi kuhusu suala la bandari serikali Ina namna mbili tu..
1. Kiheshimu hofu na maoni ya wananchi kwamba hawajaridhika na suala hili, au
2. Kuwapuuza wananchi na kuendeleza na suala hili.

Lakini wapime madhara ya kila uamuzi watakaoifanya.

Alipoulizwa kuhusu ushirikishwaji wa wananchi kama haukuwa wa kutosha. Mzee Butiku amesema hadhani kama ushirikishwaji ulikuwepo, na kama uliikuwepo basi ulifanywa ktk namna ambayo haikuwa bora, kwani hata yye ni mwananchi lkn hajauona huo ushirikishwaji.

Ameulizwa endapo hoja za serikali kutetea suala la DP je, zinajibu hoja za wananchi? Mzee Butiku amejibu kuwa hazijubu ndiyo maana mjadala haukomi.

Ameonya wale wanaowatisha wanaotoa maoni kinzani na kusema tabia hii inajenga hofu na kujenga taifa la woga.

Anaongeza kwa kusema kuendelea na suala hili ni kuhatarisha umoja na muungano wetu.
---

Mzee Butiku: Rais ameruhusu tuzungumze, Watanzania bado waoga
"Nianze kwa kutoa shukrani kumshukuru na kumpongeza Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa mabo mawili kwanza kuruhusu Watanzania kuzungumza...tulikuwa na woga...lakini tangua Rais aingie ametuambia tuzungumze, waziwazi...ukweli

"Kwa maoni yangu Watanzania bado wanao uwoga...wana wasiwasi...hawana hakika kama maamuzi haya yaliyofanywa na serikali ni kwa faida ya nchi yao, hiyo sauti unaisikia wakati wote kwa ngazi zote"

Source: ITV Kipindi cha dk 45.
 
Amesema watanzania wasichokozwe kwenye mali zao wasikilizwe na wasibezwe mambo wanayoyahoji kabla jua halijazama


Usiku mwema wakuu naona swala la Dp world likileta anguko kubwa kwa serikali ! maana ccm imeona wao ndio wenye akili kuliko wananchi wenyewe wanaoshauri mkataba wa bandari urekebishwe, wengi wamejiuliza ni elimu gani wananchi wanatakiwa kuipata kuhusu mkataba huo?
 
Alipoulizwa kuhusu ushirikishwaji wa wananchi kama haukuwa wa kutosha. Mzee Butiku amesema hadhani kama ushirikishwaji ulikuwepo, na kama uliikuwepo basi ulifanywa ktk namna ambayo haikuwa bora, kwani hata yye ni mwananchi lkn hajauona huo ushirikishwaji.

Wazee ni hazina
 
Amesema watanzania wasichokozwe kwenye mali zao wasikilizwe na wasibezwe mambo wanayoyahoji kabla jua halijazama


Usiku mwema wakuu naona swala la Dp world likileta anguko kubwa kwa serikali ! maana ccm imeona wao ndio wenye akili kuliko wananchi wenyewe wanaoshauri mkataba wa bandari urekebishwe, wengi wamejiuliza ni elimu gani wananchi wanatakiwa kuipata kuhusu mkataba huo?
Ameuma na kupuliza

USSR

Sent from my TECNO B1c using JamiiForums mobile app
 
Mida hii-ya shauri hili la Bandari yetu salama-CCM hatutizamani usoni, manake hujui nani yupo wapi....

Mzee wetu Butiku, tuachie busara zako, wenye kusikia wasikie au kama wanavyotupasha...wakimeza wakitema ni shauri yao'

Mpaka kieleweke
No to DPW No to Neo-Colonialism.

Chagua kwa Umakini 2025
 
Tungeweka nguvu nyingi kwenye katiba ingekuwa jambo zuri zaidi
 
Kuiondoa Serikali ya CCM ni ngumu
Haina ugumu wowote ule. Then Kanali Kikwete aliweza ndani humo humo....
hata kama kukiwa na katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, maana wanashikilia majeshi.
Ondoa hofu ndugu yangu....CCM kwishney!
Njia pekee ni coup d'etat itakayofanywa na wanajeshi wenyewe.
Wananchi ndio wenye Nchi....Ndio unasikia Jeshi la Wananchi. Serikali ya Wananchi, Bunge la Wananchi...Uamuzi wetu tu

Jeshi, Bunge, Tume ya Uchaguzi, Katiba vyote hivi vipo mikononi mwa Wananchi...ni Uamuzi wetu wenyewe kama tunataka kuongozwa kwa fasheni hii au Lah. Ni uamuzi wetu.
 
Back
Top Bottom