Katika kauli zilizonishangaza ni hii ya Mzee Mtei kuhusu dini.
Mzee Mtei ameishi zama za Nyerere na nyakati hizo udini na ukabila ulipigwa vita sana.
Nilitarajia mzee awe daraja kati ya generation ya sasa na ile ya baada ya uhuru.
Kwamba mzee aturithishe thamani za nchi hii kama watu wamoja bila kubaguana.
Nilitaraji mzee angekuwa na mifano mzuri wa Nigeria, Kenya, Rwanda, Yugoslavia, Srilanka, Ireland,Spain n.k
Kitendo cha kutenga Watanzania kwa misingi ya dini ni cha kusikitisha sana.
Mkandara ameorodhesha makundi yasiyowakilishwa katika tume, mimi nauliza zaidi, hivi kama ni Waislam Vs Waristo, je wale wasio na dini au wasioamini au wenye dini zao za asili wamewakilishwa na nani?
Je hawa hawana haki katika nchi hii ila tu makundi aliyoyataja mzee Mtei!
Pili, Mzee mtei atuambie hivi tunaenda kuandika katiba ya nchi au tunakwenda kuandika Biblia na Misahafu.
Endapo kungekuwa na masangoma 4 au 5 wenye wanabusara sana katika mambo ya katiba na ambao tungependa watusadie, je hiyo katiba ingekosa uhalali kwasababu tu Hassan na William wameshirikiana na masangoma!
Mzee Mtei endapo tuna watu wanaoweza kutusaidia kufanya jambo la nchi hii, je tunaangalia uwezo wao au majina yao.
Wewe umekuwa waziri mwandamizi, hivi mzee wetu hukumbuki kuwa Bagamaoyo ni maarufu sana kwa viongozi na vigogo kuliko sisi makapuku! Hizo dini za Uislam na Ukristo wanashiriki vipi kwasababu zote zinakataza ushirikina. Kwani mzee dini ni nini hasa, kwasababu mtazamo wako dini ni majina.
Mzee Mtei hoja ya kuwa na wajumbe sawa kwa uwiano wa milioni moja na milioni 40 inamashiko.
Unaposema Zbar imeongeza idadi ya waislam ni kupotosha umma kwasababu unaelewa wazi kuwa asilimia 98 ya wzbar ni waislam na kwa kutumia hesabu za probability una majibu mazuri sana.
Ningeshangaa sana kama wajumbe wa zbar wangekuwa na idadi kubwa kuliko unayoidhani kidini.
Jambo la hatari zaidi ni pale unapojisahau kuwa wewe ni mtu maarufu na mshauri wa mambo ya kitaifa.
Ni nadra sana watu kuweza kutenganisha wewe na fungamano lako la kisiasa.
Kauli yako inatoa nafasi kwa wafitini, wachochezi kupata cha kusema dhidi ya chama chako.
Ingawa sote na wewe ukiwemo tuna uhuru wa kutoa maoni kama haki yetu ya msingi, kauli zako kama mtu mwenye hadhi,heshima na siri nyingi za taifa hili haziwezi kuchuliwa kwa urahisi tu kama Nguruvi3 msaga lami.
Hivyo kauli yako imeleta usumbufu katika jamii, chama chako na wazee wenzako mliolijenga taifa la umoja kwa pamoja.
Wenzako wanaona kuwa una lako jambo katika kuvunja daraja la kizazi kimoja na kingine, ya kwamba wewe unajua nguzo za daraja zipo wapi na ipi inashikilia daraja. Kwa bahati mbaya umeamua kwa makusudi kuishambulia nguzo hiyo.
Ningeshauri kuwa huenda baadhi yetu hatukukuelewa au tumekuelewa vibaya, basi vema urejee na kutoa ufafanuzi.
La sivyo ni vema basi ukachukua hatua za kuomba radhi ili kizazi hiki kifahamu kuwa busara ni pamoja na kusema Samahani.