Mtei amefilisika kimawazo - Zitto

Hii si suala la kulumbana, mtei anamtazamo wake na zitto anamtazamo wake na wanachama wengine wanamtazamo wao na chama kina mtazamo wake kama chama ambayo ni makubaliano ya wengi. Sasa kuna haja gani ya kulumbana matokeo yake ni kudhofisha chama.
 
Sasa mlivyokuwa mnalalamika CCM inawatukana kumbe ni Mwigulu na Lusinde yalikuwa mawazo yao binafsi.
Vitu viwili tofauti, kutukana au kutoa matusi na kutoa mawazo kuhusu jambo fulani
 
Mtei yuko sahihi hata mie niliona vile maana kama wajumbe wote 15 wa Zanzibar ni waisilamu kwanini wajumbe wote 15 wa bara wasiwe wakristo? mheshimiwa Kikwete anataka kusema hakuna wazanzibar wakristo angewaweka kwenye wajumbe 15 wa Zanzibar? na hata kama alikosa basi kwa bara angehakikisha wajumbe wa kikristo kuwa 12 na waisilamu 3 ili atleast kubalance uiano maana tayari Zanzibar wote ni waislamu lakini badala yake kaweka waislamu toka bara 6 na wakristo 9 ukijukmlisha waislamu wanakuwa 21 dhid ya 9 wakristo kitu ambcho sio sahihi maana Tanzania idadi kubwa ni wakristo na sio waisilamu

Pia solution ya pili wajumbe wa Zanzibar sio lazima wawe nusu kwa nusu na bara maana wao wazanzibar sio wengi ile kama wabara wajumbe 10 kutoka Zanzibar wangetosha
 
Mbunge wa Kigoma Kaskazini-CDM amesema Mzee Edwin Mtei amefilisika kimawazo kwa kauli yake kwamba tume ya Katiba ina Waislam wengi kuliko wakristo.

Source:JAMBO LEO.

Lazima ikumbukwe kwamba mtu anapozeeka akili yake hurudi kuwa kama ya mtoto mdogo so mwacheni huyo babu aseme maneno yake ya mwisho. Mbona wapo wazee wengi tu wameshaongea pumba.
 
Mzee Mtei kazeeka vibaya.
Ubongo umechoka ndio maana anaropoka tu
OTIS

Ndio maana kuna kitu kinaitwa kustaafu, ukizeeka sana akili inakuwa mgando, ya mtoto mdogo afadhali- hawa wazee wetu sijui kwa nini hawaelewi hilo na kulikubali!!!
 
Mzee mtei ana hoja ya msingi! kuna issue ya mahakama ya kadhi! na TZ kujiunga na OIC.
Democracy-Majority rule! Minority rights.
 
TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
(Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura 83,Toleo la 2012, Vifungu 5, 6 na 7)
______________________________


UONGOZI WA JUU

1. Mhe. Jaji Joseph Sinde WARIOBA - Mwenyekiti
2. Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino RAMADHANI - Makamu Mwenyekiti

WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - BARA

1. Prof. Mwesiga L. BAREGU

2. Nd. Riziki Shahari MNGWALI

3. Dr. Edmund Adrian Sengodo MVUNGI

4. Nd. Richard Shadrack LYIMO

5. Nd. John J. NKOLO

6. Alhaj Said EL- MAAMRY

7. Nd. Jesca Sydney MKUCHU

8. Prof. Palamagamba J. KABUDI

9. Nd. Humphrey POLEPOLE

10. Nd. Yahya MSULWA

11. Nd. Esther P. MKWIZU

12. Nd. Maria Malingumu KASHONDA

13. Mhe. Al-Shaymaa J. KWEGYIR (Mb)

14. Nd. Mwantumu Jasmine MALALE

15. Nd. Joseph BUTIKU
WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - ZANZIBAR

1. Dkt. Salim Ahmed SALIM

2. Nd. Fatma Said ALI

3. Nd. Omar Sheha MUSSA

4. Mhe. Raya Suleiman HAMAD

5. Nd. Awadh Ali SAID

6. Nd. Ussi Khamis HAJI

7. Nd. Salma MAOULIDI

8. Nd. Nassor Khamis MOHAMMED

9. Nd. Simai Mohamed SAID

10. Nd. Muhammed Yussuf MSHAMBA

11. Nd. Kibibi Mwinyi HASSAN

12. Nd. Suleiman Omar ALI

13. Nd. Salama Kombo AHMED

14. Nd. Abubakar Mohammed ALI

15. Nd. Ally Abdullah Ally SALEH


UONGOZI WA SEKRETARIETI

1. Nd. Assaa Ahmad RASHID - Katibu
2. Nd. Casmir Sumba KYUKI - Naibu Katibu





Source: Majina ya Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya Tanzania - wavuti.com 
 
Hii ishu ya mtei mbna source ni JAMBO LEO peke yake sioni mengine yakiandika.....changanya na zako. Na wameikomalia mno.
 
Mbunge wa Kigoma Kaskazini-CDM amesema Mzee Edwin Mtei amefilisika kimawazo kwa kauli yake kwamba tume ya Katiba ina Waislam wengi kuliko wakristo.

Source:JAMBO LEO.

Nioneshe popote niliponukuliwa kusema unavyosema hapa.

Sijawahi kumjibu Mtei moja kwa moja hata siku moja. Kwenye suala hili msimamo wangu niliuweka wazi hat kabla Mtei Hajasema.
Walioandika wameunganisha tu tweets zangu na kauli ya Mtei ambayo siiungi mkono hata kidogo. Mzee was mistaken.

Tume ya Katiba imeteuliwa kwa mujibu wa sheria. Haina Udini. Ina wajumbe ninaowaheshimu sana. Twende tukatoe maoni. Tuache maneno yasiyo na maana yeyote.
 
Zitto anaivuruga CDM, au chadema inamvuruga zitto?? Zitto anapanbana na maadui zake ndani ya chadema wasiotaka kuona chama kinatoka minoni mwa wenye malengo maalum!! Mtoeni zitto ili chama chenu kife ili tanzania iendelee kuwa na amani
uMETAWAZA MAANA NAONA UMEHARA...
 
Nioneshe popote niliponukuliwa kusema unavyosema hapa.

Sijawahi kumjibu Mtei moja kwa moja hata siku moja. Kwenye suala hili msimamo wangu niliuweka wazi hat kabla Mtei Hajasema.
Walioandika wameunganisha tu tweets zangu na kauli ya Mtei ambayo siiungi mkono hata kidogo. Mzee was mistaken.
Tume ya Katiba imeteuliwa kwa mujibu wa sheria. Haina Udini. Ina wajumbe ninaowaheshimu sana. Twende tukatoe maoni. Tuache maneno yasiyo na maana yeyote.

Haa Zitto bana,

kuuma na kupulizia?
 
Re Dini;
Kuzungumzia dini ni kufirisika kisiasa,mana dini zoote tumeletewa na watawala wetu, ya nini zitugawe?? Hata Zitto naye Kachemsha! tutajua dini za hao watu siku wakiapa na si kwa kuangalia majina! Mfano:? Jaji Ramadhan ni dini gani? Pia kuna wakristo wana mawazo mabovu kuliko waislam, na waislam wana mawazo mazuri kuliko wakristu.

Pia kuna wislam hata msikitini hawaendi.

Re Umri:
Hivi wantanzania sijui hata kama wanajua ni aina gani ya rais wanayemtaka, na kama watu kama kina Zitto wana hizo sifa!! hizi infatuations and complacency za rejareja zimesha tu- cost lakini hatujifunzi!

We mtu hajafanya hata kazi ya profession yake, tukamwona delivery yake,consistecy,etc how is he good at choosing right leaders, etc

Nyerere was young yes! but exceptional, so I doubt we keep on try and error.
Tanzania tunataka mtu ambaye pamoja na sifa zote, pia awe na utumishi ulitukuka - which means atakuwa mzee tuu - igana basi hata mfano wa Akina Netanyahu, Ehud Barak, Rick Santorium, Gordon Brown,Mwl Nyerere, etc ---- the list is endless
 
Mbunge wa Kigoma Kaskazini-CDM amesema Mzee Edwin Mtei amefilisika kimawazo kwa kauli yake kwamba tume ya Katiba ina Waislam wengi kuliko wakristo.

Source:JAMBO LEO.

Jamani, tuwe tunaangalia hata source zenyewe kabla ya kubandika hapa JF. Gazeti la Jambo Leo hata nikipewa bure sipokei, heri kutumia Magazeti ya Shigongo kama source kuliko Jambo Leo.
Jambo Leo is good for nothing!
 
Nioneshe popote niliponukuliwa kusema unavyosema hapa.

Sijawahi kumjibu Mtei moja kwa moja hata siku moja. Kwenye suala hili msimamo wangu niliuweka wazi hat kabla Mtei Hajasema.
Walioandika wameunganisha tu tweets zangu na kauli ya Mtei ambayo siiungi mkono hata kidogo. Mzee was mistaken.
Tume ya Katiba imeteuliwa kwa mujibu wa sheria. Haina Udini. Ina wajumbe ninaowaheshimu sana. Twende tukatoe maoni. Tuache maneno yasiyo na maana yeyote.

.
Mh Zitto Kabwe sisi raia tunajiuliza na hata wewe nadhani unajiuliza ni kwa nini magamba mara zote hukutumia wewe kama fimbo ya kukidhalilisha Chadema? Maana mazuri yako ambayo ni mengi hawayaunganishi na Chama moja kwa moja ila yale yanayokinzana.
.
 
Tuheshimu mawazo ya watu wengine. Hata hivyo tu-discourage mawazo yoyote yenye muelekeo wa kukuza tatizo la udini na ukabila.Tutanguleze competency ya watu katika utendaji. tusipokuwa makini huko tuendako na siasa zetu mikutano ya hadhara itakuwa mikusnayiko ya ibada badala ya itikadi za kisiasa katika sera.Kwa nchi delicate kama Tanzania watawala na wananchi,wanasiasa na viongozi wa dini tujitahidi kuwa makini na matamshi yetu.tuna tatizola matabaka ya kiuchumi,ukosefu wa ajira,vijana kutumika vibaya na wanasiasa.sasa tusiongeze masuala ya udini na ukabila.Ni mjadala hatari na hisia za udini na ukabila ni hatari sana.Ni hatari kuwa na wafuasi wako kisiasa kwa sababu ya udini.Hawa wafuasi ni tatizo ambalo huwezi kuleta utangamano in future kwa urahisi

Most of these supporters are illiterate and see the world through the prism of religious prejudice and violence that is largely directed towards other Tanzanians not of their ethnicity or religion.
 
asee...hii thread kina rejao na ritz,watachangia sana ngoja waamke...wapi FF???ila sina imani na gazeti la Jambo Leo laweza kutumika pia kupindisha alichosema Zitto ili kuleta mifarakano.

Mkuu!!!! Ritz kasha amka anachangia hii thread utafikiri anaomba kura huko Arumeru
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom