Mokiwa: Hatutaongozwa na wanyoa vipara

Mokiwa: Hatutaongozwa na wanyoa vipara

Mkuu ni kuwa tumejua kwa kuchelewa kidogo ila kwa sasa wakae vizuri, heshima watapata kwa matendo yao sio "kiongozi wa dini" basi ndio iwe kama neno la Mungu!!!!

Wapo baadhi wa hovyo tu miongoni mwao!!!!

Uongozi bora hauna uhusiano wa kuwa na nywele au kuwa kipara!! Inasikitisha UKIONA WATU TUNAOWATEGEMEA KUWA VIONGOZI WA KONDOO WA MUNGU WANAGEUKA KUWA CHUI na kweli kwa wakati tulionao heshima yao watapata kwa matendo yao na wala si kwa majoho wanayovaa!!
 
na kazi ya kichwa siyo kufuga nywele. ila wazembe wasidhani hapa namtetea January makamba lah hasha ni heri nikawe mkimbizi kuliko kutawaliwa na wahuni kama hawa kina makamba.

jeshi letu wakubwa jeshi wameridhika basi kila mtu anadhani anaweza kuwa command inchief, hii nchi ilipaswa kuwa chini ya jeshi kwa angalau miaka mitano ijayo ili tutengeneze katiba ya wananchi kwanza.


Kamanda Matola, hapo kwenye nyekundu naona umechukia munkali umekupanda mpaka povu limekutoka!! Naunga mkono hoja yako!
 
January-Makamba.jpg


Niliwahi kusikia mahali huyu mhuni alikwiba mtihani wa kidato cha sita.

Swalama sheikh Ngongo. Pole na muendelezo wa milipuko ya mabomu hapo chini ya mlima meru.

Huyu January Makamba alifutiwa matokeo ya kidato cha nne Galanos Secondary School Tanga baada ya kuthibitika kukwiba mitihani, na sio ya kidato cha sita.
 
Last edited by a moderator:
Askofu kasema wanyoa ''unga'' maarufu kama vipara, sio wenye vipara. Kunatofauti kati ya wanyoa 'unga' na wenye vipara

Pia kasema nchi hii ni changa inahitaji damu iliyokomaa kutuongoza,

Hata hivyo, ni dhahiri askofu ametumia fasihi ktk kuwasilisha ujumbe ambao yeye anaona unafaa. Sina tatizo anaposema nchi inahitaji damu iliyokomaa kutuongoza. Tunahitaji akili iliyokomaa, mawazo yaliyokomaa kukabili changamoto tulizonazo. Hatuhitaji, utotoutoto, utoziutozi na tabia zinazofanana na hizo
 
hivi wewe una credibility gani hapa jf ya kumuita mdau nguli intellectual olesaidam kwamba ni mburula?

basi wewe ndio rais wa mambulula.

U-intellectual wake ndio unampa kibali kutetea ujinga? Kwani hapa JF kuna malaika wasiotakiwa kuguswa hata kama wakisema ujinga? Jitambue ndugu yangu.
 
Swalama sheikh Ngongo. Pole na muendelezo wa milipuko ya mabomu hapo chini ya mlima meru.

Huyu January Makamba alifutiwa matokeo ya kidato cha nne Galanos Secondary School Tanga baada ya kuthibitika kukwiba mitihani, na sio ya kidato cha sita.

Aliiba mtihani wa form IV au sio? Kama mtihani wa form IV tu unamshinda nchi ndio ataweza kuiongoza? Akagombee urais wa kuongoza familia yake......
 
Last edited by a moderator:
Uongozi bora hauna uhusiano wa kuwa na nywele au kuwa kipara!! Inasikitisha UKIONA WATU TUNAOWATEGEMEA KUWA VIONGOZI WA KONDOO WA MUNGU WANAGEUKA KUWA CHUI na kweli kwa wakati tulionao heshima yao watapata kwa matendo yao na wala si kwa majoho wanayovaa!!

Jaribu kumeuelewa askofu kwanza kabla ya kutokwa povu....Askofu ametumia lugha ya picha kufikisha ujumbe wake kwa hadhira iliyokusudiwa. Kama huelewi jambo ni bora ukauliza kabla ya kuchangia kwa mhemuko wa chuki ya kidini!!!!!
 
juzi tulikuwa harambee kuchangia ununuzi wa gari ya paroko, niliwaeleza wazi natoa pesa yangu lakini gari ni lazima ubavuni iandikwe kwa maandishi makubwa kwamba gari hii ni ya parokia gani ili itambulike, mwenye magendo yake akodi tax ndio aende night club na guest house.

mokiwa hana akili na ndio maana waanglicana wamempiga chini uaskofu mkuu, jacob zuma ananyowa kipara na wasouth wamemwamini, hivi kama msomi wa level ya phd kama mokiwa anakuja na reasoning za kitoto namna hii bora mwanangu nimpeleke veta tu akapate ujuzi. tuna ombwe la wasomi wasioelimika Tanzania.

Mokiwa yuko sahihi---ametumia lugha ya picha kufikisha ujumbe wake. Unadhani kwamba January Makamba ana ubavu wa kuongoza nchi hii iliyojaa mafisadi ndani ya chama chake? Chaguo la watanzania mwaka 2015 ni Dr Slaa.
 
Aliiba mtihani wa form IV au sio? Kama mtihani wa form IV tu unamshinda nchi ndio ataweza kuiongoza? Akagombee urais wa kuongoza familia yake......

Hawa viongozi vijana wa ccm majanga, wote sifa za wiziwizi tuuuuu.kuna mwingine tena naibu waziri aliiiba kura huko shinyanga, naye kalewa kwelikweli madaraka hadi kudiriki kumtukana balozi wa uingereza. We trust mnyika a young teenager of the century, soo cool and born a leader.mNYIKA ANATANGAZWA NA WATU HAJITANGAZI KAMA HAYA MAJIZI YA MITIHANI NA KURA
 
Mkuu Matola,

Kama issue ni Mokiwa kumung'unya maneno,you are right.
Sasa tukija kwenye point ya Msingi.
Huyu mhuni hafai kuwa hata Balozi wa nyumba kumi.
Amshukuru sana JK kwa majina ya miungu wake wote kwa kumbeba mpaka alipofikia,hana sifa yoyotee ya kuwa alipo zaid ya kubebwa na System.
Nadiriki kusema huyu ni mtu wa hovyo na kilaza kupata kutokea kwenye Cabinet ya tokea Nyerere mpaka JK.
Naungana na wewe,no bora nikawe mkimbizi Somalia kuliko kuwa Chini ya Rais kama huyu kilaza mwivi wa mtihani wa kidato cha sita.

Exactly! You nailed it comrade...take five!
 
Mheshimiwa Mwita Maranya wazima sana siku nyingi sijakusikia nikadhani labda umekimbilia kubeba mabox ughaibuni.Mkuu wangu mabomu Arusha ni muendelezo wa siasa mbovu za watawala wetu ni bahati mbaya hawana mkakati wa kuondokana na kadhia hii labda lingemlipua mkuu wa mkoa kazi ingefanyika.Unajua wananchi wengi wa Arusha wana amini Kenya inahusika sana kwakuwa kwao hakukaliki wameamua kutufanyizia ubaya Tanzania.

Nikirejea kwa huyu kijana aliyebebwa na Baba yake kipindi kile akiwa katibu mkuu wa CCM eti naye anautaka uRais kweli Kikwete kaushusha sana uRais kaufanya mrahisi hadi wajinga wajinga kama huyu Makamba anadhani kuhudhuria mikutano na uzururaji wa Kikwete ndio sifa kuu ya wadhifa huo Mwenyezi Mungu utupitilishie mbali na hili janga la wahuni wasiokuwa na haya wala aibu.

Swalama sheikh Ngongo. Pole na muendelezo wa milipuko ya mabomu hapo chini ya mlima meru.

Huyu January Makamba alifutiwa matokeo ya kidato cha nne Galanos Secondary School Tanga baada ya kuthibitika kukwiba mitihani, na sio ya kidato cha sita.
 
Last edited by a moderator:
sawa mkuu nimekuelewa wewe una akili nyingi, je unaweza kutueleza JK Nyerere alikabidhiwa nchi hii ikiwa changa wakati ana umri gani?

Nyerere wakati anaingia ikulu alikuwa msomi wa Masters ya Edinburgh na alishaonyesha kwa vitendo kwamba ana uwezo wa kuongoza nchi baada ya kumng'oa mkoloni. Makamba is below 30 na hana sifa yoyote ya kuongoza nchi hii iliyojaa mafisadi wazoefu kutoka chama chake cha CCM! Chaguo la watanzania mwaka 2015 ni Hon Dr Slaa.
 
Kichwa cha Mokiwa ni sawa na Kitalu cha kukuzia/kuoteshea Nywele hakina jukumu lingine lolote, kama PHD Holder anataka tuchague Rais kwa Wingi wa Nywele zake basi Taifa limefikia Point of No Return.

Lugha za kwenye biblia hizo, kama huna maono hutakaa ukaelewa, utaishia kuikosoa biblia kila siku na ushetani wako!
 
Huyu askofu anatumia nn kufikiri. Aibu zake kuwa na kauli kama hiyo. :angry::angry:
 
Lugha za kwenye biblia hizo, kama huna maono hutakaa ukaelewa, utaishia kuikosoa biblia kila siku na ushetani wako!
Kwenda zako, kitabu gani hicho. Kawadanganye wadogo zako. Weka hichi kitabu cha biblia kinachosema hivyo, tumbafu
 
Askofu alikuwa na maana ya mbali zaidi ya hii, ametumia "Wanyoa Unga" kama kiwakilishi tu katika fasihi.

Wewe umemwelewe. Kwani Mwl Nyerere aliposema JK bado kijana mwaka 2005 hakujua kuwa JK alikuwa na Umri mkubwa kuliko umri wa Mwl Nyerere wakati anaingia ikulu mwaka 1961? Nyerere alitumia umri kidiplomasia tu. Alikuwa na maana kuwa JK hafai kuwa Rais. Na sasa tumevuna tulichopanda.
 
Back
Top Bottom