Mokiwa: Hatutaongozwa na wanyoa vipara

Mokiwa: Hatutaongozwa na wanyoa vipara

Mokiwa yupo sahihi, sema utata unakuja kwamba yeye ni mfuasi na mpiga kampeni wa Lowasa, isije kuwa kauli hiyo haitokani na maono mema isipokuwa anamsemea White Hair...
 
askofu wako ndio amekurupa shika adabu yako, mokiwa ni muhuni tu sawa na wahuni wengine ndio maana kanisa la Anglican wamemuweka pembeni si askofu mkuu tena.
Wataalam wa kiswahili jitokezeni mtusaidie akina Matola watatutoa roho! Je, katika tungo hiyo askofu alimaanisha hivyo anavotuhumiwa?

Tukipeni nafasi kiswahili wakuu, tusikurupuke kumtukana askofu kumbe alimaanisha zaidi ya mnyoo!!
 
Wataalam wa kiswahili jitokezeni mtusaidie akina Matola watatutoa roho! Je, katika tungo hiyo askofu alimaanisha hivyo anavotuhumiwa?

Tukipeni nafasi kiswahili wakuu, tusikurupuke kumtukana askofu kumbe alimaanisha zaidi ya mnyoo!!

mbona umewekewa hata picha halisi mkuu ?
 
Huwezi kutenganisha MOKIWA na Dhehebu la ANGLIKANA na huwezi kutenganisha Anglikana na USHOGA, Masharti ya CHADEMA kupewa misaada ni sera ya USHOGA, kuna nini nyuma ya pazia kufuatia kauli ya MOKIWA?

kwani hiyo 40% budget support serikali ya ccm mnapewa kutoka mataifa ya magharibi huwa mnawekewa sharti la kutowabugudhi mashoga?nakumbuka kikwete alipoulizwa kuhusu msimamo wa serikali yake dhidi ya mashoga alishindwa kuweka msimamo km aliouweka Museven. mbona hii nchi inaendeshwa kwa kodi za mashoga? ulikuwa hujui?
 
huyu askofu alituaminisha kuwa jk ni chaguo la mungu , aombe kwanza radhi ndio asikilizwe ....
aliyesema jk ni chaguo la mungu ni askofu kilain na si mokiwa na ni chanzo cha kuhamishiwa bukoba toka makao makuu dar na pengo
 
Akizungumzia sakata la kuibuka kwa watu wanaojitangaza kuwania urais, Askofu mstaafu ndugu Valentine Mokiwa amesema kuwa nchi ya Tanzania bado ni changa sana hivyo haipaswi kuongozwa na wanyoa 'unga' maarufu kama 'vipara'.

"Nchi yetu bado ni changa sana hivyo sii busara kuongozwa na wanyoa 'unga'.Tunahitaji damu iliyokomaa kutuongoza". Alisema Mokiwa huku akionekana dhahiri kumlenga mmoja wa watu ambaye ametangaza nia ya kuwania urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania hivi karibuni kupitia kituo kimoja maarufu duniani cha runinga ya idhaa ya Kiswahili.

Labda nimepitwa na wakati: kunyoa unga ndiyo kunyoa upara? Mokiwa anaweza kuifahamu hiyo lugha ya mitaani kuliko sisi wa mitaani? I doubt kama askofu Mokiwa katamka hiyo kwani hamna ushahidi wowote. Pia hakuna mchangiaji hata mmoja aliyesema kamsikia Mokiwa akiongea hayo maneno ya ajabu. Naamini mleta mada katunga tu haya maneno nasi tunachangia bila kujua.
 
na kazi ya kichwa siyo kufuga nywele. ila wazembe wasidhani hapa namtetea January makamba lah hasha ni heri nikawe mkimbizi kuliko kutawaliwa na wahuni kama hawa kina makamba.

jeshi letu wakubwa jeshi wameridhika basi kila mtu anadhani anaweza kuwa command inchief, hii nchi ilipaswa kuwa chini ya jeshi kwa angalau miaka mitano ijayo ili tutengeneze katiba ya wananchi kwanza.

Mkuu mbona unajistukia? Ukishikilia usiachie, wacha kuwa kama SIGARA KALI.
 
Kama askofu jukumu lake ni kuwaelekeza waumini wake sifa za mtu anayefaa kuchaguliwa kuwa raisi na kuwachagulia nani anafaa au nani hafai!!
 
Labda nimepitwa na wakati: kunyoa unga ndiyo kunyoa upara? Mokiwa anaweza kuifahamu hiyo lugha ya mitaani kuliko sisi wa mitaani? I doubt kama askofu Mokiwa katamka hiyo kwani hamna ushahidi wowote. Pia hakuna mchangiaji hata mmoja aliyesema kamsikia Mokiwa akiongea hayo maneno ya ajabu. Naamini mleta mada katunga tu haya maneno nasi tunachangia bila kujua.
Kasema hivyo Mokiwa...!!
 
unaongea nini wewe mburula, ina maana wanyoa vipara na viduku walipoifikisha nchi hii? acha kuropoka bure, kama hujui jambo ni bora ukakaa kimya kuliko kutetea ujinga!

hivi wewe una credibility gani hapa jf ya kumuita mdau nguli intellectual olesaidam kwamba ni mburula?

basi wewe ndio rais wa mambulula.
 
Ukisoma gazeti la Mtanzania la leo ukalinganisha na kile alichokiandika afisa habari wa waziri mkuu, Bonny Makene jana usiku kwenye ukurasa wake wa Facebook, utaona kuwa habari ya leo iliandikiwa baa au watu wote wanaomshabikia Lowassa walipewa habari hiyo waisome kabla haijatoka kwenye gazeti jambo ambalo ni kinyume na miiko ya kazi za jamaa hawa.
Lakini pia siasa za kutumia vyombo vya habari kuchafuana zimepitwa na wakati; watanzania wanachotaka ni kiongozi anayeweza kusaidia kujenga taifa letu.
Sisi watanzania tunatakiwa kujadili aina wa kiongozi tunayemtaka kuongoza nchi yetu.
Mtanzania wanarudia kosa walilolifanya mwaka 2005 walipotumika na rais Kikwete na Lowassa, wakafikiri watanzania ni wajinga na gazeti likaporomoka mara baada ya uchaguzi. Kila mtu alikuwa na imani kuwa kuwaleta wahariri wazuri kungeweza kusaidia kujenga heshima ya gazeti hili.
Lakini pia, ni wazi viongozi wa dini kama askofu Mokiwa wanatumika na wanasiasa kufanikisha malengo ya kisiasa.
Askofu Mokiwa ni mmojawapo ya watu waliosaidia kuwapatanisha Lowassa na Mengi eti kusaidia “dhehebu lao kutoa rais hajaye”.
Hata kama wanataka mtu wao awe rais lakini si busara kutumia nafasi zao kusema mtu hawezi kuwa rais kutokana na kunyoa “unga”.
Tena kiongozi wa dini anatumia lugha za mtaani na gazeti linaloongozwa na wahiriri wanatumia maneno hayohayo.
Hao wahariri wajiulize wataenda wapi baada ya uchaguzi wa 2015? Kilichompata Jenerali na Salva ni funzo tosha kwa watu hawa.

 
juzi tulikuwa harambee kuchangia ununuzi wa gari ya paroko, niliwaeleza wazi natoa pesa yangu lakini gari ni lazima ubavuni iandikwe kwa maandishi makubwa kwamba gari hii ni ya parokia gani ili itambulike, mwenye magendo yake akodi tax ndio aende night club na guest house.

mokiwa hana akili na ndio maana waanglicana wamempiga chini uaskofu mkuu, jacob zuma ananyowa kipara na wasouth wamemwamini, hivi kama msomi wa level ya phd kama mokiwa anakuja na reasoning za kitoto namna hii bora mwanangu nimpeleke veta tu akapate ujuzi. tuna ombwe la wasomi wasioelimika Tanzania.

Wala hakuwa na maana hiyo. Alikosa ujasiri wa kumtaja mtu anayedhania hana sifa za kugombea u Rais. Njia nzuri ya kumwengua mtu ni kuanisha vigezo vinavyotakiwa.
 
hahaahahahah jamani hizi muda mwwingine ni tafsida tu. Mfano badala ya kumwita mtu huyu ni "MUUZA GONGO" unaweza ukasema huyu ni "MFAMASIA MZAWA"
 
Khaa!!! Poor analysis. Hivi Askofu ni jina lake au ni cheo chake?? Tusije tukajichanganya maana kuna kina jenerali ulimwengu, Nahodha vuai nk
 
Huwezi kutenganisha MOKIWA na Dhehebu la ANGLIKANA na huwezi kutenganisha Anglikana na USHOGA, Masharti ya CHADEMA kupewa misaada ni sera ya USHOGA, kuna nini nyuma ya pazia kufuatia kauli ya MOKIWA?

Leo sikua na mpango wakuchangia chochote humu jamvini, nilioona unatoa comment ya aina moja mara mbili umenilazimisha kufanya hivyo:-
  1. Askofu mstaafu Mokiwa hakuchaguliwa mara ya pili, hivi kama kanisa hili linafuata mambo ya ushoga na huyu bwn hakuchaguliwa maana yake ni nini kama sio yeye sio shabiki wa mambo hayo so maaskofu wenzie wakampiga chini kwenye uchaguzi!!!? Think it and come back!!!!
  2. Iliwahi kuelezwa humu ndani kua CDM wanapewa misaada na kile chama cha Christian Union cha Ujerumani, ninavyo fahamu makao makuu ya Anglican, hilo kanisa linalo daiwa kutetea ushoga ni Uingereza, hicho chama cha Ujerumani ni Lutheran (makanisa haya 2 hayana uhusiano sana), sasa hoja yako hapo iko wapi!? And remember Lutheran makao yao makuu yako huko huko Ujeruman. Uhusiano wa ushoga wa CDM hapo mbona siuoni?
  3. Uganda wamekataa hayo mambo ya ushoga kwa vitendo, IMF, World Bank pamoja na nchi nyingi za magharibi wameisha zuia misaada kwao, hapa kwetu bado misaada inaendelea, hivi huoni kama ccm na ushoga vina connection!? THINK again brother
 
juzi tulikuwa harambee kuchangia ununuzi wa gari ya paroko, niliwaeleza wazi natoa pesa yangu lakini gari ni lazima ubavuni iandikwe kwa maandishi makubwa kwamba gari hii ni ya parokia gani ili itambulike, mwenye magendo yake akodi tax ndio aende night club na guest house.

mokiwa hana akili na ndio maana waanglicana wamempiga chini uaskofu mkuu, jacob zuma ananyowa kipara na wasouth wamemwamini, hivi kama msomi wa level ya phd kama mokiwa anakuja na reasoning za kitoto namna hii bora mwanangu nimpeleke veta tu akapate ujuzi. tuna ombwe la wasomi wasioelimika Tanzania.

pamoja ni askofu ana kawaida ya kwenda maeneo hayo?
 
Back
Top Bottom