Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,048
Intelejensia ya Dunia katika karne ya 21 imebadilika sana! Nchi nyingi duniani sasa zinafanya kazi kutengeneza nguvu na ushawishi kwenye uchumi!
Kupata nguvu na ushawishi kwenye Uchumi kunahusisha kutengeneza matajiri wakubwa wenye pesa wanaoweza kuwekeza, kushawishi uwekezaji, kuongeza ajira na mapato ya nchi kupitia ushawishi kwenye uwekezaji
Ukienda Misri kuna Nasser Sawaris anaemiliki viwanda vingi vya cement na shareholder wa kampuni kubwa zaidi ya vifaa vya michezo ulaya Adidas
Ukienda Afrika kusini Kuna Patrice Motsepe
anaemiliki shares nyingi kwenye makampuni mbalimbali ya madini
Ukienda Nigeria kuna Aliko Dangote mwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa cement , Sukari na mafuta na sasa anatengeneza refinery ya kwanza ya mafuta katika Bara la Africa
Tanzania tunae Rostam Aziz mmiliki wa kampuni ya Caspian, Taifa Gas, Tigo na Zantel! Huyu kuaminika kwake kunafanya kuwa mtu ambae Tanzania tunamtegemea sana kwenye kishawishi uwekezaji mkubwa unaotengeneza fursa za ajira na kukuza mapato na Uchumi wa nchi yetu
Urusi wanao wengi akiwemo Roman Abramovich aliyekuwa mmiliki wa club ya Chelsea
Marekani ndo usiseme wanao wengi na wanazidi kuzalisha wengi kila siku kama Jeff bezoz, Bill Gates, Warren Buffet, Elon Musk na wengineo wengi
Mfano wa kazi nzuri za Rostam Aziz kwa Tanzania ni huu! Katika ziara aliyoambatana na Rais Samia Marekani, ameweza kushawishi uwekezaji mkubwa katika kilimo hapa Tanzania kupitia Benki ya maendeleo Afrika.
Hongera Rais Samia, naiona akili kubwa sana kwako inayoenda kuibadili haraka sana Tanzania kiuchumi
Kupata nguvu na ushawishi kwenye Uchumi kunahusisha kutengeneza matajiri wakubwa wenye pesa wanaoweza kuwekeza, kushawishi uwekezaji, kuongeza ajira na mapato ya nchi kupitia ushawishi kwenye uwekezaji
Ukienda Misri kuna Nasser Sawaris anaemiliki viwanda vingi vya cement na shareholder wa kampuni kubwa zaidi ya vifaa vya michezo ulaya Adidas
Ukienda Afrika kusini Kuna Patrice Motsepe
anaemiliki shares nyingi kwenye makampuni mbalimbali ya madini
Ukienda Nigeria kuna Aliko Dangote mwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa cement , Sukari na mafuta na sasa anatengeneza refinery ya kwanza ya mafuta katika Bara la Africa
Tanzania tunae Rostam Aziz mmiliki wa kampuni ya Caspian, Taifa Gas, Tigo na Zantel! Huyu kuaminika kwake kunafanya kuwa mtu ambae Tanzania tunamtegemea sana kwenye kishawishi uwekezaji mkubwa unaotengeneza fursa za ajira na kukuza mapato na Uchumi wa nchi yetu
Urusi wanao wengi akiwemo Roman Abramovich aliyekuwa mmiliki wa club ya Chelsea
Marekani ndo usiseme wanao wengi na wanazidi kuzalisha wengi kila siku kama Jeff bezoz, Bill Gates, Warren Buffet, Elon Musk na wengineo wengi
Mfano wa kazi nzuri za Rostam Aziz kwa Tanzania ni huu! Katika ziara aliyoambatana na Rais Samia Marekani, ameweza kushawishi uwekezaji mkubwa katika kilimo hapa Tanzania kupitia Benki ya maendeleo Afrika.
Hongera Rais Samia, naiona akili kubwa sana kwako inayoenda kuibadili haraka sana Tanzania kiuchumi