Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Nyerere, alimjua Mkapa kwa sababu alijua kuwa Mkapa ameshagombea mara karibu kumi uongozi wa ndani ya CCM na kunyimwa, na kila alipouliza why? Aliambiwa sababu, lakini kwa vile alikuwa mwanafunzi wake Pugu, akaamua kutojali na kumpa urais anyways,

Sasa Nyerere, hakuwa fisadi no way, lakini aliwajua mafisadi na wengine kina Kahama, Bomani, Kimario, Msuya,aliwakumbatia sana, hata kabla hajafa Nyerere alijua kuwa Mkapa na wenziwe wameiba NBC kwa kuiuza bei poa, yaani Idd Simba, Sumaye, na Kigoda, wakishirikiana na Mpungwe, na Kazaura,

Wazee msituchokoze uchungu, tumeliwa inatosha, mwacheni mzee wa watu Nyerere alale salama peponi, ingawa tutalipia for the rest of our life ujinga wetu wa kumuamini kuwa yeye tu ndiye aliyekuwa na akili, sasa tukubali tu yaishe, maana tuliyataka wenyewe na bado tunaendelea kuyataka kwa kuwachagua anyways, maana ni Mkapa huyo mhuyo aliyetulazimisha kumchagua Muungwana, meaning kuwa bado hatujaamuka!
 
naona hapa Es umeguswa pabaya . Ila nimekubali jambo zuri ambalo umelisema kwamba Mzee aliwajua mafisadi lakini akawakumbatia ila yeye hakuwa FISADI.
 
Hapana, nadhani Nyerere ndiye alikuwa mkuu wa mafisadi hawa. Itakuwaje akaweka msimamo wake bayana, tena wenye ukali na kimaandishi juu ya baadhi ya viongozi wanyenyekevu kama hawa hapa (JF ilishaweka orodha hiyo mara nyingi humu); na kumbe anawatetea mafiadi ambao alikuwa anajua maovu mengi yawahusuyo kama akina Mkapa?

Itabidi sasa tukubali kwamba Nyerere hakuwa na nia nzuri na waTanzania.
 
"Hakuna mtu anayemjua mtu. Mtu hujijua mwenyewe" (N.Ngabu Original quote)
 
Nyerere na Mkapa:

Nyerere hakuwa fisadi; na ni kweli hakumjua Mkapa kwa vile Mkapa alikuwa mnafiki sana. Wakati Mkapa anawekwa madarakani na Nyerere, hakuwa na utajiri wowote; ndiyo maana hakusita kutaja mali zake zikiwamo nyumba moja ya kawaida huko Masasi, nyumba nyingine ya kawaida aliyokuwa amejenga nadhani Kiluvya, n'gombe wachache wa kufuga, pamoja magari mawili: moja likiwa lile la ubunge pamoja, na pesa zisizozidi milioni tano kwenye account ya NBC, na dola za kimarekani zapata elfu moja hivi katika account ya kigeni kwenye mojawapo ya benki za hapo nchini.

Mkapa aliendelea kuwa mwadilifu kinafsi wakati wote wa uhai wa Nyerere hadi pale Nyerere alipokufa. Kuanzia mwaka 1999 ndipo Mkapa akaanza kuonmyesha rangi yake ambayo hakuwa amemwonyesha Nyerere.

Makosa ya Nyerere:

Nyerere alikuwa na tatizo kubwa sana la kujiamini kupita kiasi. Hata lile jaribio la ujamaa, hakutaka kuwasikiliza akina kambona. Alijiamini sana, na mwihsoni akashindwa.

Alipokuwa akiambiwa kuwa Mkapa ni mnafiki, yeye hakutaka kata kata kumwangalia Mkapa kutokea pembe nyingine. Marehemu Balozi Mwakasyafuka alitoa tahadhari kuwa alikuwa anajua undani wa Mkapa na kusema ukweli kuwa Tanzania tunakalia kaa la moto kwa kumchagua Mkapa kutuongoza, lakini ndiyo hivyo. Nyerere akawa haambiliki; alimwamini Mkapa kupita kiasi.

Ukweli ni kuwa kama Nyerere angemjua Mkapa sawasawa, no way angetumia nguvu zake zile kumpigia debe mwaka 1995, hadi kusema kuwa asingeweza kulala usingizi Butiama kama nchi ingechukuliwa na watu wasio na mwelekeo kama wapinzani (eti Mrema na Marando) wakati huo.
 
Nyerere, alimjua Mkapa tena nje ndani, tena kwa karibu sana,

kwa sababu alikuwa akimjua Lowassa kwa karibu sana, ingawa hakuwa mtoto wake wala ndugu yake, wala kiongozi aliyefanya naye kazi kwa karibu, mpaka akamkatalia urais, sasa iweje kuwa hakumjua Mkapa aliyekuwa waziri wake wa nje?

Watanzania inabidi tukubali ukweli, kwamba tumekuwa wajinga for too long, ndio maana tunakazania kuitangaza JF kwa nguvu zote tulizonazo, ni kwa sababu tunajaribu kuamshana kutoka kwenye usingizi mzito sana tulionao, Mkapa alikuwa Elimu na Sayansi, nani aliyekuwa hajui kilichokuwa kikiendelea huko betweeen Mkapa na Mahalu? Eti mnasema Mwalimu, alikuwa hamjui Mkapa? Wakuu tunaambiwa kuwa kipindi cha Mwinyi, hata Usalama walikuwa wamechoka na kuamua kumpa Mwalimu, info zote za serikali na ndio maana wakampa hata za Lowassa, na za Ikulu kuwa pango la kufanyia biashara haramu, sasa mnataka kutuambia kuwa kwenye hizo info hazikuwepo za Mkapa?

Mwalimu, alimpigia makelele Mwinyi, kuwa ni mwizi, lakini hakutuomba msamaha wananchi kwa kutuchagulia kiongozi mbovu, the next thing akarudia tena mchezo wake na kutuchagulia Mkapa again mambo yakawa yale yale, lakini akanyamaza kimyaa, sasa leo maa-pologists mnasema hakumjua Mkapa? Eti Mwalimu hakujua kuwa CCM ilishindwa kwenye uchaguzi wa mwaka 1995 kule visiwani?, sasa kama alijua hilo how could you put past him kuwa hakumjua Mkapa? Mbona hakusema kitu kwenye ishu ya Zanzibar kama kweli alikuwa ni malaika kama wengi hapa mnavyotaka tuamini? hivi wakuu kweli tunaelewa maana ya siasa na mwanasiasa au tunabahatisha tu?

Wewe kweli ni rais wa nchi, watoto wako wote wanasoma bongo, waziri wako wa nje watoto wake wanasoma US toka wakiwa watoto wadogo, tena in the middle ya siasa ya ujamaa, wakati wananchi wanakula njano na foleni ya kipande cha sabuni mbuni, halafu unasema kuwa humjui waziri wako wa nje? Vijana hebu muache haya masiala, wewe kweli unaamini kuwa Mkapa aliandika mali zake zote? wananchi wa bongo tulikuwa tumelala sana usingizi, matokeo yake tukaruhusu aliyeamka Mwalimu na alioamka nao kina Mkapa, kutuchezea na bado tunaendelea kuchezewa, ndio kwanza tunajaribu kuamka, lakini bado kazi ni nzito saana ya kuamshana, ndio maana ni lazima tuitangaze JF kwa nguvu zote, maana huwezi ingia hapa ukaendelea kulala!

Mwalimu, alale pema peponi, lakini alikuwa akimjua tena vizuri sana Mkapa, kuliko hata sisi wananchi, lakini tunasahau kuwa Mwalimu, alikuwa ni mwanasiasa, alikuwa pia akiangalia legacy yake ambayo ilishamiri sana under Mkapa, Nyerere Foundation imewika under urais wa Mkapa, na sio Mwinyi, hebu nyie Nyerere apologists tuambieni zile shillingi millioni 300 ambazo Mkapa alikuwwa akitoa kwa hiyo foundation alikuwa akizitoa wapi? au under what budget? Mwinyi, na kundi lake walikataa kata kata kumpa Mwalimu hizo hela, na kuna wakati Mwalimu, alikuwa bado ana demand kusafiri kwenye ndege ya rais na Mwinyi alikuwa akikataa, lakini yote haya aliyafanya under Mkapa, kwa hiyo si kweli kabisaa kuwa kwa kumchagua Mkapa, Mwalimu alikuwa hajui anachofanya no way wakuu!

Tunasema kuwa Mwalimu, hakuwa mfisadi, lakini hakuwa na tatizo na mafisadi waliokuwa wakimsujudia, Mkapa included, kusema Mwalimu, hakumjua Mkapa ni very naive thinking kama sio kujua what makes siasa na wanasiasa, to be politicians, siasa sio dini wakuu au charity, siasa ni utawala na power ndani yake, na pia tukumbuke kuwa power siku zote huwa ina-corrupt hata wachungaji kina Mtikila!
 
Marshal

Unajua mojawapo ya weakness za Nyerere katika kupima uadilifu wa mtu ilikuwa ni jinsi mtu anavyojilimbikizia mali. Sasa kwa vile wakati huo Mkapa hakuwa na mali, ndiyo maana alidhani kuwa ni mwadilifu. Nyerere alimshitukia Lowassa siyo kwa sababu nyingine yoyote bali tu kwa vile alimwonaamejipatia mali nyingi kwa muda mfupi. Kiutendaji, ni wazi kuwa Lowassa alikuwa anonekana kukubaliwa na wanachi wengi sana wakati huo.
 
Yeah....kama kweli Mwalimu alikuwa mtu wa haki na usawa kwa nini hakukemea dhuluma waliyomfanyia Hamad mwaka '95. Yaliyotokea Kenya hivi juzi si ndio yale yale yaliyotokea Zenj mwaka huo...
 
A man is as honest as his options.

Kuna tabia katika CCM inayoonekana kuwa ndiyo mtindo.Kiongozi huwa anakuwa na nidhamu ya woga au mnyenyekevu wa kimbinu, almuradi hajafika ofisi kuu anayoitaka.Watu watamuangalia na kusema Bwana Safi (Mkapa) au kijana mnyenyekevu (Kikwete).Akipata kufika Ikulu husahau hayo yote kwa kuwa yeye ndiye anakuwa mkuu wa wote na hakuna wa kumbabaisha, hususan kwa sababu hata huyo mzee kifimbo mwenyewe aliyekuwa na bashasha la ushawishi keshajiondokea kitambo.

Sasa kusema kweli kwa mtindo huu kumjua mtu ni vigumu, kama ilivyosemwa mwanzo, ukimuangalia Mkapa wa 95 (Mr. Clean) na Mkapa wa 2008 (Mr. Kiwira) unaona watu tofauti, Kikwete ndiyo kabisa hata hakusubiri muhula wa kwanza uishe.

Lakini mimi nilimkataa Mkapa na Kikwete.Hata mwanawe mwenyewe alisema "Watanzania mmekwisha" Mkapa alipochaguliwa urais, unategemea nini?
 
Hapana, nadhani Nyerere ndiye alikuwa mkuu wa mafisadi hawa. Itakuwaje akaweka msimamo wake bayana, tena wenye ukali na kimaandishi juu ya baadhi ya viongozi wanyenyekevu kama hawa hapa (JF ilishaweka orodha hiyo mara nyingi humu); na kumbe anawatetea mafiadi ambao alikuwa anajua maovu mengi yawahusuyo kama akina Mkapa?

Itabidi sasa tukubali kwamba Nyerere hakuwa na nia nzuri na waTanzania.
Zomba anasema kila siku humu kwenye JF kuwa nyerere ndiye fissadi wa kwanza wa Tanzania, ahsante kwa kulitambuwa hilo.
 
Nyani Ngabu,

"Hakuna mtu anayemjua mtu. Mtu hujijua mwenyewe" (N.Ngabu Original quote).....
Mhhhhhh! hili somo jipya kabisaaa inabidi tuifanyie uchunguzi wa kisayansi...

Unajua Njabu, kuna hii sayansi nyingine ya kuwa hakuna mtu anayejisikia sauti yake mwenyewe akiongea ila mtu hufahamu kile alichosema!...na kufikiria kuwa amesikia.. Uhakika wa sayansi hii ni kwamba hakuna mtu anayejua sauti yake mwenyewe kwa hiyo kama watu wanasikia sauti zao wakiongea ni lazima wawe wanazifahamu sauti zao kwani huongea kila siku... Ukitaka kuhakikisha sayansi hii rekodi sauti yako mwenyewe ukiongelea jambo fulani...hakika utashangaa kusikia sauti hiyo na kama umeshtukizwa utakataa kuwa ni sauti yako unless kama utakumbuka kuwa ni wewe uliye yasema hayo...
Binafsi nimejaribu mtihani huu na hakika nilifikiria sauti hiyo ilikuwa ya mtu mwingine kabisa!!!
Hivyo basi Nyerere alimjua Mkapa vizuri isipokuwa hakutaka kuamini na Mkapa yawezekana mwenyewe hakujijua kabisa kuwa ni Fisadi hadi pale alipokuwa ktk mtihani... ndio maana viongozi huchaguliwa na watu sio mapendekezo ya mtu mmoja ama mgombea mwenyewe. Leo hii ukimuuliza hata Lowassa, Mramba, Sumaye na hata Jeetu Patel kuwa wao hawafai kuwa viongozi watakuona wewe ndiye mwendawazimu!...Kumbuka hata Firaun na Hitler alijiona wao kuwa viongozi bora kuliko wote duniani.
 
Marshal

Unajua mojawapo ya weakness za Nyerere katika kupima uadilifu wa mtu ilikuwa ni jinsi mtu anavyojilimbikizia mali. Sasa kwa vile wakati huo Mkapa hakuwa na mali, ndiyo maana alidhani kuwa ni mwadilifu. Nyerere alimshitukia Lowassa siyo kwa sababu nyingine yoyote bali tu kwa vile alimwonaamejipatia mali nyingi kwa muda mfupi. Kiutendaji, ni wazi kuwa Lowassa alikuwa anonekana kukubaliwa na wanachi wengi sana wakati huo.

Kichuguu:

Ngoja tuweke katika lugha ya siasa. Tuviite hivyo vipimo vya uadilifu ni Litmus Test. Litmus test alizotumia Nyerere zilikuwa mbovu sana. Mtu aliyekuwa balozi wa Tanzania katika umoja wa mataifa na kulipwa kwa US dollar awe na account ya kigeni yenye dollar 1000 huo ni uzembe.
 
Sasa kwa vile wakati huo Mkapa hakuwa na mali, ndiyo maana alidhani kuwa ni mwadilifu.


Watoto wa Mwalimu wanasoma bongo maisha yao yote, wa Mkapa wanasoma nje, lakini Mwalimu alidhani Mkapa hana hela kabisa wala mali?
 
Nyani Ngabu,


Mhhhhhh! hili somo jipya kabisaaa inabidi tuifanyie uchunguzi wa kisayansi...

Unajua Njabu, kuna hii sayansi nyingine ya kuwa hakuna mtu anayejisikia sauti yake mwenyewe akiongea ila mtu hufahamu kile alichosema!...na kufikiria kuwa amesikia.. Uhakika wa sayansi hii ni kwamba hakuna mtu anayejua sauti yake mwenyewe kwa hiyo kama watu wanasikia sauti zao wakiongea ni lazima wawe wanazifahamu sauti zao kwani huongea kila siku... Ukitaka kuhakikisha sayansi hii rekodi sauti yako mwenyewe ukiongelea jambo fulani...hakika utashangaa kusikia sauti hiyo na kama umeshtukizwa utakataa kuwa ni sauti yako unless kama utakumbuka kuwa ni wewe uliye yasema hayo...
Binafsi nimejaribu mtihani huu na hakika nilifikiria sauti hiyo ilikuwa ya mtu mwingine kabisa!!!
Hivyo basi Nyerere alimjua Mkapa vizuri isipokuwa hakutaka kuamini na Mkapa yawezekana mwenyewe hakujijua kabisa kuwa ni Fisadi hadi pale alipokuwa ktk mtihani... ndio maana viongozi huchaguliwa na watu sio mapendekezo ya mtu mmoja ama mgombea mwenyewe. Leo hii ukimuuliza hata Lowassa, Mramba, Sumaye na hata Jeetu Patel kuwa wao hawafai kuwa viongozi watakuona wewe ndiye mwendawazimu!...Kumbuka hata Firaun na Hitler alijiona wao kuwa viongozi bora kuliko wote duniani.


Mkandara:

Unalalamika nini kaka? Mkapa katuachia uwanja wa mpira wa kisasa na JK kaleta kocha kutoka Brazil.
 
Jamani eeh...sasa tuache kumlaumu Nyerere kwa kila kitu. Hata kama Nyerere alimu-endorse na kumpigia debe Mkapa ni sisi wananchi ndio tuliomchagua. Nyerere hakutushikia bunduku kichwani na kutulazimisha kumchagua Mkapa. Tulikuwa na haki sawa ya kuwachagua wengine waliogombea uraisi mwaka huo.

Tutaacha lini kumlaumu huyu mzee wa watu jamani? Sio haki kabisa kumrushia lawama mtu ambaye hayuko hai kujitetea mwenyewe. Mzee wa watu aliaga dunia mwaka 99. Mwaka uliofuata tukamchagua tena Mkapa. Najua kuna mtakaosema alianza ufisadi katika muhula wake wa pili. Sawa, hiyo labda ni kweli. Sasa kama tunajua hivyo ndivyo ilivyokuwa na kama inavyosemwa ushahidi wa ufisadi wake upo tena mwingi tu, ni nini sasa kinachotuzuia kumchukulia hatua za kisheria au hatua zingine zozote zile zinazofaa? Au tunamsubiri Nyerere afufuke ndio aje amchukulie hatua yeye?

Watanzania kweli bado hatujajua jinsi kuwajibika kwa matendo yetu. Tunapenda sana kutumia njia rahisi na za mkato na kulaumu wengine...ooh wakoloni hivi...wakoloni vile..Nyerere hivi...Nyerere vile...CCM hivi...CCM...vile...wapinzani hivi...wapinzani vile....viongozi wetu hivi...viongozi wetu vile...lakini hata siku moja husikii sisi wananchi tukiwajibika kwa makosa yetu. Mkapa bado tunaye...sasa kinachotuzuia sasa hivi ni nini? Halafu nikisema Miafrika Ndivyo Tulivyo mijitu inanibishia...saa ingine nataka sana niseme shauri yenu..au shauri letu..
 
Kichuguu:

Ngoja tuweke katika lugha ya siasa. Tuviite hivyo vipimo vya uadilifu ni Litmus Test. Litmus test alizotumia Nyerere zilikuwa mbovu sana. Mtu aliyekuwa balozi wa Tanzania katika umoja wa mataifa na kulipwa kwa US dollar awe na account ya kigeni yenye dollar 1000 huo ni uzembe.


Correct!! Hivyo ndivyo ilivyo; vipimo vya uadilifu vya Nyerere vilikuwa shallow sana. Kwa hiyo ilikuwa ni rahisi sana kwake kuwa spoofed na wanafiki kama Mkapa na mawaziri wengi aliofanya nao kazi!

Lakini, siyo kweli kuwa alimweka Mkapa pale akifahamu kuwa atafanya madudu haya aliyofanya; hakujua kuwa Mkapa atafanya vile.
 
MZEE F ES
Umesema yote, naamini kuwa wewe unaijuia nchi yako vizuri. Mimi ukweli naouona kabisa, labda naweza hata kukubali kuwa Nyerere aliwakumbatia kina Msuya na petty mafisadi wengine, tena ni vizuri members wametaja majina yao, wote tinaona ni baba zetu na kaka zetu.
Lakini how do you see the whole thing kumtajirisha mhindi na M-iran. Why would someone let them use them to steal from us. Inasikitisha sana, wazee wetu na sisi wenyewe wadogo zao na watoto wao, wote tunafanywa wapumbavu na kina Patel na kina Aziz, can you just imagine.
Kibaya zaidi hao jama wanatamba kabisa kuwa, tumewaweka mfukoni. Na wahindi huku maeneo ya Posta na upanga wanatamba kama nini, wanapiga, kutukana watanzania, na ujinga mwingine wote bila, wakijua kuwa sheria ziko chini yao.
Sina hakika kuna wahidi wangapi magerezani, lakini nina hakika kuna wengi tu wamevunja sheria na wanapeta tu! And we call ourselves free men and women!
Kama alivyosema Nyerere ni bora turudi kwenye ukoloni, kama sisi tumeshindwa kujiongoza! Inasikitisha sana kweli!
 
Correct!! Hivyo ndivyo ilivyo; vipimo vya uadilifu vya Nyerere vilikuwa shallow sana. Kwa hiyo ilikuwa ni rahisi sana kwake kuwa spoofed na wanafiki kama Mkapa na mawaziri wengi aliofanya nao kazi!

Lakini, siyo kweli kuwa alimweka Mkapa pale akifahamu kuwa atafanya madudu haya aliyofanya; hakujua kuwa Mkapa atafanya vile.

Lakini matatizo mengi ya viongozi weusi wa mwanzo ni kuongoza nchi au jumuia kwa mtindo wa Parokia kwa kuwafanya watu waamini kile wanachosema.

Leo nimesoma Wall Street Journnal kuhusu uchaguzi South Carolina na wanawema kwa desturi huko kusini mwa Marekani kampeni anapiga Pasta wa kanisa au Mkongwe wa siasa. Pasta akishasema mpeni kura mtu fulani basi imetoka hiyo.

Wanasema kuwa wazee huko South Carolina walikuwa hawajuhi kuwa Barack Obama ni mtu mweusi na hao ndio wapigaji kura. Imebidi wapiga debe wa Barack Obama kutumia DVD na posta za mkewe kuonyesha kweli Obama yupo karibu nao.

Na kuna kijana aliyekuwa anampigia debe Obama alivutwa pembeni na Mkongwe wa siasa na kuambiwa African Americans' immediate needs are more important than making history electing black president.

Nadhani Nyerere naye ali-fall katika mtego huu wa kuamini kuwa watanzania walitaka kufanya history mwaka 1995 lakini history ilikuwa kwake sio important zaidi ya legacy ya siasa zake. Ben alichaguliwa kuendeleza legacy za Ujamaa lakini kwa bahati mbaya kawa YUDA msaliti.
 
MZEE F ES
Umesema yote, naamini kuwa wewe unaijuia nchi yako vizuri. Mimi ukweli naouona kabisa, labda naweza hata kukubali kuwa Nyerere aliwakumbatia kina Msuya na petty mafisadi wengine, tena ni vizuri members wametaja majina yao, wote tinaona ni baba zetu na kaka zetu.
Lakini how do you see the whole thing kumtajirisha mhindi na M-iran. Why would someone let them use them to steal from us. Inasikitisha sana, wazee wetu na sisi wenyewe wadogo zao na watoto wao, wote tunafanywa wapumbavu na kina Patel na kina Aziz, can you just imagine.
Kibaya zaidi hao jama wanatamba kabisa kuwa, tumewaweka mfukoni. Na wahindi huku maeneo ya Posta na upanga wanatamba kama nini, wanapiga, kutukana watanzania, na ujinga mwingine wote bila, wakijua kuwa sheria ziko chini yao.
Sina hakika kuna wahidi wangapi magerezani, lakini nina hakika kuna wengi tu wamevunja sheria na wanapeta tu! And we call ourselves free men and women!
Kama alivyosema Nyerere ni bora turudi kwenye ukoloni, kama sisi tumeshindwa kujiongoza! Inasikitisha sana kweli!

Bongo:

Nasikia kilio chako lakini mwizi ni mwizi. Ukiangalia matangazo ya kuomba misaada yanayotolewa na NGOs kama World Vision yanasikitisha. Watoto wa kiafrika wamenyanyapaa kwa njaa, magonjwa na uchafu, wakati huo huo waziri kiongozi mzalendo anaiba pesa na kuziweka kwenye mabenki Uswizi.

Kwa Tanzania tusiangalie utoto wa nyumbani, dini au mzawa. Mwizi ni mwizi tu.
 
Back
Top Bottom