Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Hata kama atapigwa danadana, kitendo cha Serikali na Mahakama kuchelewesha kesi kitatafsiriwa kuwa ni kuhodhi na kuficha uchafu na madhambi ya viongozi. Imani ya watu itapungua.

Kumshtaki Raisi kutawapa wananchi mtazamo mpya kuhusiana na Uraisi kama kazi na Cheo. Kutawapa nguvu kumkataa yule atakayeonekana Mvivu, Mzembe au Fisadi.

Akifungua hii kesi 2009/2010 basi CCM mgombea wao kama ni JK machozi bwelele!
 
Ya Mkapa, Ballali na Jeetu Patel

Januari, 16, 2008
Raia Mwema

"Mr. Clean", Ben Mkapa alikaa Ikulu kama Rais wa Tanzania kwa miaka 10. Katika kipindi hicho 1995 – 2005 Benki Kuu ya Tanzania ilishamiri kwa ufisadi katika kiwango ambacho hakijapata kuonekana katika historia ya nchi.

Zaidi ya Sh. bilioni 133 ziliibwa katika akaunti ya nje ya malipo ya madeni (EPA) peke yake. Mpaka sasa hatujajua kiasi gani kiliibwa kwingineko, lakini kwamba "Mr. Clean" aliamuacha mteule wake, Daudi Ballali kuendelea kuwa Gavana wa benki hiyo kwa miaka takriban minane, ni kitu kinachoibua maswali mengi yanayohitaji majibu.

Je, yawezekana katika kipindi chote hicho "Mr. Clean" alikuwa hajui, au hata kupata fununu, kuhusu ufisadi uliokuwa ukiendeshwa kwa kasi katika benki hiyo?

Na kama alijua au alielezwa, je kiongozi huyo, ambaye "si mvivu wa kufikiri" (kama sisi!), alichukua hatua gani kuhakikisha mabilioni ya pesa za wavuja jasho wa nchi hii hayaendelei kuyeyushwa na mafisadi katika benki hiyo?

Na je, yawezekana kweli ufisadi wa kiwango hicho kikubwa ukaendelea katika BoT bila ya Hazina kufahamu au kupata fununu kwa miaka yote hiyo kumi? Na kama ilifahamu au kupata fununu, ilimtonya "Mr. Clean"? Chama tawala CCM nacho kilikuwa wapi kipindi chote hicho?

Kwa hakika, sakata hili la ufisadi wa BoT ni kama vile mchezo wa kuigiza. Swali moja linachochea kuulizwa swali jingine na jibu moja linaibua swali jingine jipya. Maswali juu ya maswali, majibu juu ya majibu.

Ukweli ni kwamba mtandao wa sakata hili la ufisadi BoT ni mkubwa na unagusa wakubwa, na hivyo kuna shaka kwamba, mwisho wa yote, Watanzania hawatafahamishwa ukweli wote.

Kwa mfano katika ‘igizo' hili, kuna ‘msanii' anayeitwa Jayantkumar Chandubhai Patel (maarufu Jeetu Patel). Huyu, vyombo vya habari vimeripoti kwamba ndiye anayemiliki kampuni sita kati ya 13 zilizotajwa katika taarifa ya ukaguzi kuwa zililipwa Sh. bilioni 90.3 za EPA kwa kutumia nyaraka batili na zilizogushiwa.

Jeetu Patel huyo huyo na washirika wake alianzisha benki inayoitwa Bank M; huku yeye akiwa mmoja wa wanahisa wenye hisa nyingi. Kinachoshangaza zaidi ni kwamba Bank M, ambayo Jeetu Patel ni mmoja wa wanahisa wakubwa, inapangisha katika jengo linalomilikiwa na "Mr. Clean" ambalo zamani lilikuwa ni la umma lakini akalinunua wakati wa kipindi chake cha urais!

Hiyo maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba Jeetu Patel na kampuni zake hizo sita amechota pesa za wavuja jasho katika benki ya umma na kutumia sehemu ya pesa hizo kuanzisha benki binafsi inayopanga katika jengo la Rais mstaafu, "Mr. Clean".

Sasa "Mr. Clean" hatunaye Ikulu. Sasa tuna Rais mpya, Jakaya Mrisho Kikwete. Huyu kauona ufisadi unaotisha wa BoT ambao "Mr Clean" hakuuona kwa miaka 10!

Aliuonaje? Aliuona kwa sababu raia wema waliuanika katika intaneti? Aliuona kwa sababu kina Slaa wa CHADEMA na vyombo vya habari viliuanika hadharani? Vyovyote vile, aliuona na akateua kampuni ya ukaguzi ya kigeni kumfanyia uchunguzi – Ernst & Young.

Kwa nini kampuni ya kigeni? Jibu ni kwamba ni kwa sababu hana imani na kampuni za humu ndani. Na katika hilo huwezi kumlaumu; kwani kwa jinsi mtandao wa ufisadi ulivyo mkubwa, huwezi kuziamini kampuni za humu ndani moja kwa moja.

Sasa Ernest & Young wamemaliza kazi yao na kumkabidhi Rais Kikwete ripoti yake. Rais Kikwete ameisoma. Amekasirika na akaamua kumtimua kazi Gavana Ballali ambaye "Mr. Clean" alimwona ni "msafi mwenzie" kwa miaka minane!

Lakini Rais Kikwete hakuishia hapo. Amewaagiza Mwanasheria Mkuu, IGP na Takukuru, kuchunguza na kuwachukulia hatua za kisheria wezi wote wa pesa za BoT; ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali zao.

Hatua nzuri kabisa. Na bila shaka kura ya maoni ingepigwa leo, Rais Kikwete angepanda chati. Lakini swali la kujiuliza ni hili: Ni kweli kwamba, hatimaye, mafisadi hao watafikishwa mahakamani na mali zao kufilisiwa au hatua hiyo ni ya kupunguza tu shinikizo la kina Slaa, wahisani na vyombo vya habari? Si kweli kwamba Ballali ametolewa tu kafara kupoza mambo?

Na je, asasi hizo ambazo Rais Kikwete anataka zichukue hatua - Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Jeshi la Polisi na Takukuru, zilikuwa wapi miaka kumi hiyo ya kipindi cha "Mr Clean" wakati mamilioni hayo yanatafunwa BoT? Hivi zilikuwa zinasubiri zitumwe kazi na Rais?

Pengine jibu ni kwamba hazikuweza kufanya lolote kwa sababu Rais aliyetangulia ("Mr. Clean") hakuwatuma kazi hiyo! Kwa hiyo kila kitu kinategemea Rais aliye madarakani. Rais asipotutuma kazi, basi, tuendelee kulala tu hata kama tuna taarifa kwamba mabilioni ya pesa za umma yanachotwa kwa kasi na mafisadi!

Ninauliza hivyo maana katika kipindi chote cha miaka kumi cha "Mr Clean", na hata katika miaka miwili ya Rais Kikwete Ikulu, hatukusikia hata mtu mmoja akijiuzulu kazi kwavile mkubwa au wakubwa walimzuia kupambana na ufisadi huo!

Hivyo ndivyo tulivyo. Kama Rais wetu habanwi mbavu na kina Slaa na kina Zitto, kama habanwi mbavu na wahisani na vyombo vya habari, basi, hachukui hatua yo yote hata kama ana taarifa zote za ‘usanii' wa mafisadi unavyotumika kuzikausha pesa za umma Benki Kuu!

Na tusisahau kwamba kina Ballali au Jeetu Patel hawako peke yao katika skandali hiyo ya BoT. Yeye anamiliki kampuni sita tu kati ya 13 zilizochota pesa zile za wakulima na wafanyakazi masikini wa nchi hii na kwenda kujijengea mahekalu Oyster Bay, Masaki na kwingineko wanakoishi mamilionea wa nchi hii masikini.

Ndiyo maana tunasema kwamba, kwa tulichokiona katika skandali hii ya BoT, wanyonge sasa tunahitaji kuwa na Robin Hood wetu wa kweli atakayewakaba koo kina Jeetu Patel na kuturejeshea sisi wanyonge pesa zetu zilizoibwa.






 
Huyu asiyekuwa mvivu wa kufikiri fisadi Mkapa likuwa busy kufikiri jinsi ya kutumia wadhifa wake aliokabidhiwa na Watanzania kujitajirisha yeye pamoja na familia yake. Kukopa mamilioni kwa kumia wadhifa wake akiwa Ikulu, kuwaleta Makaburu wa Net Grou Problems waiue TANESCO na kusha kulipwa mabilioni (lazima alifaidika na hawa makaburu) kuandaa hoja ya kununua rada, ndege ya Rais, magari na helicopter za jeshi ili ajipatie rushwa ya mabilioni, kujipatia Kiwira Coal Mining katika mazingira ya kutatanisha, kuandaa mradi wa kuuza nyumba za serikali kwa bei ya bure kabisa ili ajipatie nyumba alizokuwa anazitaka n.k.. Wakati yeye akiwa busy kujitajirisha wajanja wakagundua bwana mkubwa kabisa yuko busy na mlango uko wazi kabisa hakuna hata anayelinda hazina ya Taifa, basi na wao wakaingia mtamboni ili wajitajirishe. Huyu Mkapa anastahili afilisiwe na afunguliwe mashtaka kwa ufisadi wake
 
Unajua nashangaa mwandishi ana hoji wizi wa BOT . Namuulia BM zile pesa alizo pewa kule Swiss akiwa Davod yapata dolla 10 kwa ajili ya vyandarua na hospitali ikiwemo Temeke alipeleka huko ama aliishia nazo ? Maana kila mwaka nauliza hili sipewi majibu . Kama Sharon Stone alijitoa na akapewa cash na the money has never been accopunted for leo utashangaa ya BOT ?
 
Naleta kwako Mzee B. W. Mkapa;
Najua umestaafu ukinara wa nchi yetu;
Najua pia umestafuu siasa;
Najua hujastaafu kuishi nasi!

Tupo pamoja katika shida na raha;
Tunapokumbwa na matatizo;
Tunapokumbwa na mabalaa;
Tunafarijiana, tunapeana matumaini!

Kuna hili la Benki Kuu;
Kuna kukwapuliwa kwa fedha zetu;
Kukwapuliwa kwa fedha ulizotuambia tuzifungie mikanda;
Kuna watu wametupora mchana!

Hili ni janga kuu;
Hili ni balaa letu sote;
Hima sema neno la matumanini;
Hima laani na onyesha fadhaa zako kwa kuzungukwa!

Tungeokoa vifo vingapi vya wajawazito?
Tungejenga barabara urefu gani?
Tungejenga shule ngapi?
Tungefikisha maji salama kwa Watanznia wangapi?!

Nachukia kuamini kwamba uliyajua haya kabla ya sasa;
Nachukia kuamini kwamba hutatufariji;
Nachukia ukijitenga na janga hili;
Natoa machozi nafsini mwangu!

Mzee ongea;
Mzee onyesha huzuni yako;
Mzee tuambie hatukosea kukuchagua;
Mzee sema kuhusu rada, BOT na mengineyo!

Hizi ni hisia zangu za huzuni;
Hizi ni hisia za Mtanzania mmoja;
Hizi zaweza kuwa hisia za Watanzania wengi;
Hizi zaweza kuwa hisia za kizazi kijacho!

TAFADHALI TUSIKILIZE!
 
Huyu Ndugu BWM hawezi kuongea maana MDOMO WAKE UMEJAA PESA
Pesa mdomoni.jpg
AKIFUNUA TU ZITAMWAGIKA. Hawezi kusikitika pamoja nasi kwani kule KIWIRA COAL MINE kunamshitaki. Tangu lini "muuaji" akasikitikia kwa alilofanya?
 
Huyu Ndugu BWM hawezi kuongea maana MDOMO WAKE UMEJAA PESA akifunua tu zitamwagika. Hawezi kusikitika pamoja nasi kwani kule KIWIRA COAL MINE kunamshitaki. Tangu lini "muuaji" akasikitikia kwa alilofanya?
HAKUNA MBAYA KWA KUWA HAWA JAMAA WAMEWEKEZA HAPAHAPA TANZANIA,INGEKUWA WAMEPELEKA ZOTE NJE KAMA ALIVYOFANYA ABACHA WA NIGERIA INGEKUWA NI MBAYA.HUU NI WIZI ENDELEVU NA UNATUSAIDIA WATANZANIA
 
Hivi BWM atarudi kweli kutoka kwenye usuluhishi Kenya, au ndio safari, maana Balali anakuja na Nondo Zote.
 
HAKUNA MBAYA KWA KUWA HAWA JAMAA WAMEWEKEZA HAPAHAPA TANZANIA,INGEKUWA WAMEPELEKA ZOTE NJE KAMA ALIVYOFANYA ABACHA WA NIGERIA INGEKUWA NI MBAYA.HUU NI WIZI ENDELEVU NA UNATUSAIDIA WATANZANIA

Hakika wewe ni FISADI haswa maana inaonyesha umetumwa hapa JF kutupa uchungu anyway uko huru kusema chochote ili tufaidi huenda tutapata wapi hela zetu zilipo.
 
Naleta kwako Mzee B. W. Mkapa;
Najua umestaafu ukinara wa nchi yetu;
Najua pia umestafuu siasa;
Najua hujastaafu kuishi nasi!

Tupo pamoja katika shida na raha;
Tunapokumbwa na matatizo;
Tunapokumbwa na mabalaa;
Tunafarijiana, tunapeana matumaini!

Kuna hili la Benki Kuu;
Kuna kukwapuliwa kwa fedha zetu;
Kukwapuliwa kwa fedha ulizotuambia tuzifungie mikanda;
Kuna watu wametupora mchana!

Hili ni janga kuu;
Hili ni balaa letu sote;
Hima sema neno la matumanini;
Hima laani na onyesha fadhaa zako kwa kuzungukwa!

Tungeokoa vifo vingapi vya wajawazito?
Tungejenga barabara urefu gani?
Tungejenga shule ngapi?
Tungefikisha maji salama kwa Watanznia wangapi?!

Nachukia kuamini kwamba uliyajua haya kabla ya sasa;
Nachukia kuamini kwamba hutatufariji;
Nachukia ukijitenga na janga hili;
Natoa machozi nafsini mwangu!

Mzee ongea;
Mzee onyesha huzuni yako;
Mzee tuambie hatukosea kukuchagua;
Mzee sema kuhusu rada, BOT na mengineyo!

Hizi ni hisia zangu za huzuni;
Hizi ni hisia za Mtanzania mmoja;
Hizi zaweza kuwa hisia za Watanzania wengi;
Hizi zaweza kuwa hisia za kizazi kijacho!

TAFADHALI TUSIKILIZE!
Roya,pole sana hapa ni sawa ni kumpigia gitaa Mbuzi ukitegemea atakatika. Ah wapi, ataendelea kula majani.
 
Ukimpigia mbuzi gitaa asipocheza, dawa ni kumtandika kwa fimbo ataruka kwa maumivu! Kuna siku Mzee ataongea au atachapwa bakora.
 
Ukimpigia mbuzi gitaa asipocheza, dawa ni kumtandika kwa fimbo ataruka kwa maumivu! Kuna siku Mzee ataongea au atachapwa bakora.
RAIS HAWEZI KUSHTAKIWA KWA MAKOSA ALIOFANYA AKIWA MADARAKANI,LABDA YAWE NI MAKOSA AGAINST HUMANITY
 
Yale majumba kule SA ? Vipi Hotels kule Ushelisheli ? Vipi Mgonja na majumba USA ?

Kumbe hata JK anafanya haya maana anajua hataweza kushitakiwa ? We need Katiba change haraka
 
Si lazima mtu kushtakiwa ndipo asikie uchungu/maumivu. Hata kupoteza 'reputation' yako yaweza kuwa maumivu makubwa.
 
CCM hawana mshipa wa noma wala uchungu .Ukidhania hivyo wanakumaliza wakomalie tu . Leo wanambana Ballali wazi JK anachekelea lakini alibanwa mbavu Karamagi JK akasema viwanja visiwe mahakama yeye mbona wanamkomalia Ballali wana ushahidi upi ?
 
Bubu mfundishe hata kuongea kwa ishara.

Hamjaona ishara bado? Siku hizi kila siku kaiknamisha kichwa chini, anaogopa kuwaangalia Watanzania usoni. Mr. Clean amegeuka kuwa Mr. Hog anayebugia kila kinachokuja mbele yake na kugalagala kwenye matope..

Yamemshinda ya TZ, sasa kahamia Kenya.
 
Mtanzania
Ya kenya hayawawezi maana aliua na kupora ushindi wa CUF sawa na KIbaki so he has nothing to tell Mr.Kibaki yuko matembezini tu . Ya Zanzibar hata leo yanawashinda Kenya wataweza ? Unafiki huu .
 
CCM hawana mshipa wa noma wala uchungu .Ukidhania hivyo wanakumaliza wakomalie tu . Leo wanambana Ballali wazi JK anachekelea lakini alibanwa mbavu Karamagi JK akasema viwanja visiwe mahakama yeye mbona wanamkomalia Ballali wana ushahidi upi ?
Poa.. sio lazima tufanikiwe leo ama kesho. Inawezekana wajukuu zetu wakashinda vita hii tunayoipigania leo. Keep it up.
 
Back
Top Bottom