Hapo kumshitaki rais mstaafu atapigwa danadana hadi achoke mwenyewe. Kesi ya kwanza itabidi aombe mahakama imfutie "immunity" ya kutoshitakiwa, na hii itasikilizwa kwa miaka 5, halafu watatoa uamuzi kwamba hawezi kufutiwa. Atakata rufaa kwa miaka mingine 5. Halafu ndipo ije kesi ya msingi. Unadhani hadi hapo bado watakuwa na nguvu za kuendelea na kesi hiyo? Wote mwenye kushtaki na mshtakiwa watakuwa weshajichokea kwa uzee! Ndipo upande wa utetezi utakapokuja na hoja za kudai mteja wao ni mzee sana au ni mgonjwa, hawezi kuhimili mashtaka. Hiyo itaendelea kusikilizwa tartiiiibu hadi mzee wa watu atakaporejea kwa Mola wake peacefully!
Kwa kujikumbusha tu, jaribuni kutafuta habari ya kesi ya Gen Augusto Pinochet wa Chile, ambaye hadi anafariki akiwa na miaka 87, bado kesi yake ilikuwa katika "danadana", walianza kudai kikatiba hawezi kushtakiwa, ana "immunity", ikachukua miaka mingi tu kusikiliza hiyo kesi ya immunity na hatimaye kutamka ana kesi ya kujibu. Kisha mawakili wake wakaja na madai ya "senility and ill health", kwamba mzee Pinochet is "too ill to stand trial", nayo ikawa na lots of legal wrangle. Hadi anafariki at 87, kesi ya msingi ilikuwa haijasikilizwa.
Ushauri kwa nd Makani na wenzie wenye mawazo hayo ni kwamba badala ya kupoteza muda kupambana na mtu mmoja (ambaye dalili zinaonesha wazi kuwa kwa mfumo uliopo haiwezekani kumshinda), ni bora kuelekeza nguvu katika kuubadilisha mfumo huo ili huko mbeleni watu wasiwe na nafasi ya kufanza hayo madudu wanayomtuhumu nayo Mkapa, na pia kuwezesha hatua rekebishi kuchukuliwa dhidi ya watakaokiuka.