Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

anazuga tu,hana lolote. kama mwendaji hasa habwatuki angelishaenda zamani. si wamtizame mtikila kuhusu kesi ya kadhi,nnampinga lkn akisema hutenda.

hawa wengine wasaniii tu
 
"...apelekwe mahakamani akashitakiwe, na kama hawana wa kumshitaki, mimi najitolea nitakwenda kumshitaki," alieleza Bw. Makani.

Kulingana na kauli hiyo hapo juu ambayo inaonekana ndiyo nukuu ya maneno yake mtagundua kwamba huyu Mzee in effect amesema hivi:

1. Katiba inaruhusu(kulingana na tafsiri ya Chadema) aliyewahi kuwa Rais kushitakiwa akishatoka madarakani.

2. Kama hawana(sijui akina nani hapa, wananchi? Upinzani? au wote) hawana mtu(wakili pengine) wa kutekeleza hilo yeye anajitolea.

3. Hivyo basi hakuahidi kwenda kumshitaki Mkapa ila tu ametangaza kutoa offer hiyo ikiwa watakosa mtu(wakili) wa kufanya hivyo(si ajabu akadai uthibitisho kuwa kweli wamekosa wakili kabla ya yeye kuamua kujitosa!).

4. Mengine anayodaiwa kusema naona ni Siasa za majukwaani kwa kwenda mbele...
 
Kila mtu naona anadandia hii meli, lakini, on a more serious note, kama angeahidi kwenda au angeyasema hayo mahakamani pale kisutu akiwa ameshafungua kesi, nk apo ningejua kuwa yuko serious zaidi..
 
Keil
JF Senior Expert Member

Makani apania kumburuta Mkapa kortini
-----------------------------------------------------------------

Makani apania kumburuta Mkapa kortini

*Adai Rais huyo mstaafu amekosa kinga
*Asema kifungu cha Katiba kinapotoshwa

Na Suleiman Abeid, Shinyanga

SAKATA la tuhuma za ufisadi wa baadhi ya viongozi nchini limechukua sura mpya baada ya mmoja wa wanachama wakongwe wa CHADEMA, Bw. Bob Makani, kutangaza kusudio lake la kumfikisha mahakamani Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa.

1. .. alitangaza kusudio hilo juzi alipokuwa akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Shinyanga katika viwanja vya shule ya msingi Jomu...

2. ... na kusema kuwa kifungu hicho hakitoi kinga kwa makosa binafsi, yaliyotendwa na Rais mstaafu.

3... kuna mambo aliyoyatenda ambayo hayaruhusiwi kufanywa na Rais akiwa Ikulu.

4... Alisema ibara ya 46 ya Katiba ya nchi inasema Rais hawezi kushitakiwa kwa makosa aliyoyafanya akiwa Rais, “CHADEMA inasema, tafsiri yetu ni kwamba ibara hiyo inamlinda tu Rais kwa mambo aliyoyafanya akiwa Rais...



In the political short term, Bob Makani, ambaye professionally, ni mwanasheria anaweza kuonekana kuwa ni opportunist, lakini kwa maoni yangu ni kwamba in the long term political au legal strategies, Makani anajenga a very strong legal argument, against no tonly Mkapa, bali hata regime itakayokuwa in power,

Maana ukiisoma kwa makini hoja ya Makani, ni clear kuwa kinacho-miss kwenye hii ishu sasa hivi ni political will tu, na sio kwamba kweli sheria inamlinda Mkapa, in full kama rais mstaafu kwa sababu alipokuwa akisaini mikataba ya serikali alikuwa anafanya hivyo kama rais, lakini alipokuwa akianzisha biashara na waziri wake Yona, alikuwa ni kama raia kwa sababu sidhani kama kwenye contracts za kufungua biashara hizo kuna any mention ya kuwa mimi Mkapa rais wa Tanzania, ninameamua kushirikiana na waziri wangu wa fedha Yona kufungua kampuni binafsi ya biashara,

Labda, a bigger question inapaswa kuwa ni wakati gani a sitting president wetu anapokuwa kwenye term yake ya miaka mitano, anakuwa sio rais, na legally lazima kufanyike challenges mahakamani on hii ishu,

I do not know personal za Makani na hiii ishu, lakini ninamuheshimu mwanasiasa yoyote Tanzania, leo anayejaribu kuuendeleza huu mjadala kwenye public, kwa sababu ndio the best thing you can do for now, na baadaye kuufanya part of the agenda ya debate za uchaguzi bongo, kwenye hili ninaaamini wiht all my heart and soul kuwa Mkapa, is ni a big trouble in the future,

Temporary, Yes, hes is fine, mimi ningekuwa yeye ningeaanza sasa ktafuta njia za kujisafisha legally, ila ninamuhakikishia kuwa one of this days hizo mali zake kama kuna any ambayo sio ya hallai itarudi tu mikononi mwa wananchi!

Respect kwa Bob Makani, for keeping the debate a live, that is all we can do for now, kumkosesha usingizi maana believe me kila inaposemwa mkuu huongeza pombe kali tu, na mkuu mwingine Luwassa, naye siku hizi amjiunga huo unywaji wa kifo, kulikoni?
 
FMES,

Tatizo hapo ni je kweli Makani anataka kufanya hivyo? Mimi naona
na yeye anatikisa kiberiti tu kama akina Nkono.

Kama anataka kumpeleka mahakamani si afanye sasa? Anasubiri nini?
 
Mkuu Mtanzania,

Heshima mbele mkuu, kwenye hii ishu kuna political na legal side, kwa hiyo ni nafasi nzuri kwa mwanasiasa yoyote nchini sasa hivi kujaribu kutafuta umaarufu wa temporary, mimi ninachoheshimu na ni the best political strategy kwa upinzani, ni kuendelea ku keep this thing a live kama wanavyofanya sasa hivi, ili hatimaye ije iingie kwenye national political debate, wakati wa uchaguzi,

believe me kuna siku tutamchagua rais atakayetuahidi kuwa akiingia in the office, atawa-prosecute marais wa zamani kama wana makosa kisheria walipokuwa madarakani, na hiyo hope itafanikiwa iwapo tu hiii debate iatendelea sasa kwenye public,

That is my take on it.
 
Kama anataka kumpeleka mahakamani si afanye sasa? Anasubiri nini?

Mimi ninachoona Makani amejenga hoja anatest kama kweli inafanya kazi kabla hajakurupuka kwenda makamani.

Unajua hata waliotuhumiwa kuwa ni FISADI walijenga hoja, baada ya kutest wakaona kuna failure ndani yake. Wakanyamaza kimya, mpaka washikwe mashati.

Mbinu hiyo naona anaitumia makani kuangalia hoja yake kama inakubalika kabla hajahamua kingine.

Ukiangalia kwa undani ana hoja inayotaka majibu labda tu mimi ningemshauri afungashe makablasha yake aende mahakamani hili tupate tafsiri ya kisheria.
 
akp2bmnkby2.jpg



Tunakusubiri tuu bado una miaka kadhaa ya kuendelea kula pension ya WTZ.

Credit: Mjengwa blog
 
Tulimsahau Mkapa, huyu jamaa kamchafua sana.... Kwa kweli ametumka maneno makali sana, japo naona anastahili kwani ukimya wake na ukimya wa viongozi wetu unatisha na kuashiria KILA JAMBO RUKSA ALIMRADI UWE KARIBU NA MFALME

Mkapa anapochuuzwa na kina Hiza

Nkuzi Kwanzi



KWA aliyesoma utumbo wa mtu anayetapatapa kwa kujifanya msemaji wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, aitwaye Tambwe Hiza, atakuwa amesikitika na kuwashangaa Mkapa na Hiza.

Licha ya utetezi wake kuwa mfu na usio na mashiko, ni tahadhari kwa Mkapa kuwa kama hatakuwa makini, waganga njaa watamtumia wakijionyesha wanampenda, kumtetea na kumjali ilhali ukweli ni kwamba wanapaza sauti ili awasikie na awatupie makombo.

Hakuna mtu aliyetapatapa kipindi hiki kama Hiza. Alianza na kuvizushia vyama vya upinzani huku akijirejesha kundini alikokuwa kwa kulamba matapishi yake.

Hakujua kuwa CCM waliishaistukia janja uchwara ya wachumia matumbo na matapeli wanaohama hama vyama kukidhi njaa zao.

Kutokana na usuhuba na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, Hiza na makapi wengine walifinyangiwa ofisi na idara ya uani ya propaganda!

Jaribio la kuuza machukizo ya kundi hili wakati wa kutapatapa kutetea bajeti mikoani, waliishia kuzomewa.

Hiza hakuchoka kuusaka mkate na kuridhisha wasitiri wake. Aligombea ujumbe wa NEC na kubwagwa kama taka. Ameona hii janja ya nyani kutofanikiwa, amedandia utetezi mfu wa Mkapa.

Kwa mtu mwenye akili timamu na hekima na anayemjua Mkapa vizuri na zigo la madhambi yake, hawezi kupoteza muda wake kutaka kufanya muujiza wa kumsafisha.

Hiza ni nani akilinganishwa na vigogo kama Daudi Mwakawago, Jaji Mark Bomani, Joseph Butiku na watu wengine wenye majina na waliomuonya Mkapa kuwa anachojaribu kufanya ni kujichimbia kaburi na hakistahili kufanywa na mtu wa nafasi yake?

Watetezi wa Mkapa wanamdhalilisha sawa na wapambe wa utawala wa sasa wanavyousukumizia motoni. Hakuna kitu kibaya kama kumdanganya mtu. Maana ni kumfanya ********.

Kibaya zaidi ni kudanganya nawe ukajidanganya. Adui yako kweli muombee njaa. Hiza anajifanya kama Mtanzania aliyekuwa ughaibuni wakati ukweli kuhusu Mkapa ukiwekwa njia panda ili kila mpita njia ajionee na kuhukumu.

Hiza ataleta jipya gani iwapo akina Kingunge, Makamba, Mwanri, Warioba wamechemsha? Hiza anajua nini zaidi ya kuendeshwa na mkuno wa njaa tumboni?

Bahati mbaya CCM nayo imekula hasara. Maana kama kuna fasheni inayotumika kuiibia na kuitapeli si nyingine ni watu kuhama vyama au taaluma zao tayari kupewa kazi ya kuzoa uchafu wake wasiuweze. Dawa ya yote haya ni kusafisha nyumba yako na kuwa msafi.

Hiza asiyejua hata kujenga hoja zaidi ya kulalamika na kusifia, ana msaada gani kwa Mkapa iwapo ameshindwa kujisaidia mwenyewe kiasi cha kusaidiwa kwa njia ya kudhalilishwa? We Hiza we, tafuta njia ya uhakika ya kuishi na siyo salata na urongo.

Hata bata bingwa wa kuchokoa taka huwa halali chooni wala kujisifia matendo yake. Yeye kama hayawani hana jinsi. Hayo ni majaliwa yake. Nepi siku zote ni nguo ya aibu si vizuri kujisifia unepi wala fisi mpenda mizoga hajisifii ufisi wake. Hiza ni mahuluku wa ajabu anayeonekana kuendeshwa na njaa kiasi cha kuvuka mipaka!

Na hili inabidi liwe somo kwa watawala wasio waadilifu. Ufisadi unamtoa mtu utu na heshima kiasi cha kutetewa na majambazi wa kisiasa. Tangu lini kuku akamtetea mwewe hata ahaidiwe kutoliwa vifaranga vyake? Visipoliwa vyake vya wenzake vitaliwa. Je, kuna usaliti mchafu kama huu?

Mkapa kwa kutetewa na vyangu wa kisiasa, anazidi kumomonyoka na kuonekana mhalifu japo hataki aeleweke hivyo. Hakanushi wala hata kuwakemea kimya kimya huko wanakokutana kama wanakutana.

Je, Mkapa anawatuma akina Hiza kufanya kazi chafu kwa ajili yake au wanajikomba na kujipendekeza ili lau waambue makombo? Kama ni mkakati, basi umeshindwa hata kabla ya kufanyiwa kazi.

Hivi nani anadhani Watanzania ni majuha na wendawizimu kumsikiliza au kumwamini kiumbe asiyejiamini wala kuamini anachosema? Nani mpuuzi amuamini mkaanga sumu na majungu.

Hiza anadhani kuwa alipokuwa Mbeya hivi karibuni alijivua nguo hadharani kwa kukiri kuwa alikuwa mpika majungu mkuu alipokuwa CUF? Je, ameokoka lini kuacha kilema hiki cha akili hadi tumwamini?

Mkapa, kwa viwango vyovyote ni msomi, hata kama elimu yake aliitumia vibaya. Tangu lini msomi akatetewa na mbumbumbu mzungu wa reli? Ni ajabu kipofu kumtetea mwenye macho au shehe kutetewa na mlevi! Hii inazidi kumfanya Mkapa aonekane si Mr Clean kama tulivyoaminishwa.

Wazungu husema ‘show me your friends I will tell you who you are’. Na Mkapa japo amekataa kujitetea, bado hajahukumiwa kiasi cha kutetewa na vibaka na wasaka mkate. Ni aibu na hatari kwake.

Watu wenye majina yao, japo walipotea njia kama akina Jaji Joseph Warioba walijaribu wakazomewa na kusutwa, sasa wamenywea itakuwa Hiza!

Aliponiacha hoi Hiza ni pale alipowasingizia marehemu. Anadai Oscar Kambona alikuwa mwanazuoni! Pia anadai alipomtuhumu mwalimu JK Nyerere eti Mwalimu alinyamaza! Uongo, tena unaonuka.

Kama Hiza kaishiwa hoja afunge mdomo. Kwani Nyerere alieleza bayana kuwa hana tatizo na madai ya Kambona bali anachoomba auleze umma na vyombo vyake zilipo na zikiwapo basi wazichukue.

iza anachokifanya ni kujenga mazingira mazuri ya kuweza kujuana na Mkapa (kama atakuwa naye ameishiwa kiasi hicho) kwa kujifanya ni mtetezi wake. Tumewaona wengi hata waliofanya utapeli kwa kusingizia walitekwa na CCM kumbe ilikuwa ni kuwachuuza wenzao.

Ila tunakokwenda mchezo huu ni hatari. Maana ni usaliti. Wanachofanya ni kujipaka mafuta halafu wanakwenda kupita kati kati ya moto.

Kwa mtu anayeunga mkono mambo ya Mkapa na biashara zake za Ikulu iwe ni kwa njaa zake au upenzi wake au kwa vile alinufaika chini ya utawala wake, ni adui wa umma.

Nafasi haitoshi. La muhimu ni wananchi kuanza kuongeza idadi ya maadui wao kama umma ambapo hili genge jipya linalotumiwa au kujipandikiza kutetea uoza na kuhujumu harakati zao inabidi liangaliwe kwa jicho baya.

nkwazigatasha@yahoo.com
www.mpayukaji.blogspot.com

http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/11/21/makala1.php
 
eeh bwana wee, kama Hiza ni binadamu wa kawaida mwenye akili za kawaida, nahisi huu utakuwa ndiyo mwisho wake wa kuandika utumbo! Yaani, sasa hii ni balaa, jamaa kamuanika uchi wa nyama. Ingekuwa mtu mwingine, hata kupita mitaani mtu utaogopa maana utafikiri kila mtu ana hii article anasoma. Pole Hiza wee, kuna njia nyingi za kuishi ndugu yangu, CCM wataendelea kukudhalisha hadi lini?
 
Masatu kama source Tanzania Daima what's a problem...?Ofcourse Uhuru,Mzalendo hawawezi kuandika haya...
 
Tatizo siyo source, Je ujumbe ni wa kweli? au mwandishi kamsingizia Hiza? kama Hiza alifanya utetezi kwa Mkapa basi ujumbe umefika bila kujali source.
 
Tulimsahau Mkapa, huyu jamaa kamchafua sana.... Kwa kweli ametumka maneno makali sana, japo naona anastahili kwani ukimya wake na ukimya wa viongozi wetu unatisha na kuashiria KILA JAMBO RUKSA ALIMRADI UWE KARIBU NA MFALME



http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/11/21/makala1.php

HATUMSEMEI MWALIMU KTK TUHUMA ZA OSCA KAMBONA BALI TUNAREJEA TUKIO ZIMA LA MWALIMU,KAWAWA NA JAMAL KUTUHUMIWA KUWA WANA UTAJIRI MKUBWA NDANI NA NJE YA NCHI; NI KWELI OSCAR ALIMTUHUMU YEYE PAMOJA NA KAWAWA NA JAMAL PALE JANGWANI AND I THINK IT WAS 1992 NA NATHUBUTU KUKIRI KUMUONA KAMBONA AKIWA NA MZEE MICHAEL KAMALIZA KWA MARA YA KWANZA TANGU KUZALIWA KWANGU,AKIWA MWENYE SIHA NJEMA NA MVUTO NIKAMSIKIA AKIKIRI KUWA ALIAMBIWA WATU WA DSM MASIKU HIZI HAWAOGOPI MAGARI BALI MVUA LAKINI AMEFADHAISHWA NA UMMA WA DAR ES SALAAM ULIOKUJA KUMLAKI WAKATI KUNA MVUA KUBWA,NI MVUA ILIKUWA KUBWA NA NI SIKU HIYO LILE JUKWAA LA PAPA JOHN PAUL II PALE JANGWANI LILIPOVUNJIKA NAMI NIKIWA MIONGONI MWA WATU TULIONUSURIKA,KAMBONA ALISEMA " MWALIMU SI MASIKINI KAMA MNAVYOAMINI,ANAO UTAJIRI MKUBWA SANA HUKO USWISI ,KAWAWA NA JAMALI HAWA NAO NI MATAJIRI WAKUBWA SANA,NINA USHAHIDI DHIDI YAO KWA AKUNTI NA MAJINA,ATAKAYEPINGA AENDE KTK SHERIA NA YEYE ATATOA USHAHIDI WAKE HUKO.

THE VERY NEXT DAY TUKAAMBIWA NA MAGAZETI YETU ZAMA HIZO KUWA MWALIMU AMEMTAKA BWANA KAMBONA ATHIBITISHIE UMMA JUU TUHUMA HIZO JUU YAKE KTK KIPINDI KISICHOZIDI SIKU SABA (kiraracha style) AU LA ATAMSHUGHULIKIA KISHERIA.

HAKUNA ALIYETHIBITISHA WALA KWENDA MAHAKAMANI MPAKA WOTE LEO NI MAREHEMU; LAKINI KUNA MTU MMOJA AITWAYE KASISI MTIKILA YEYE ALIKUJA NA MPYA ALIPOMTUHUMU MWALIMU KWA KUMWITA MWIZI ETI KWA SABABU YEYE KTK UHAI WAKE HAKUWAHI KUMUONA MWALIMU AKIMLILIA MTU ANAPOFARIKI IWEJE AMLILIE JAMAL!!!!

AKASEMA HUYU NI RIGHT HAND WAKE SASA AMEKUFA NA KUONDOKA NA KILA KITU NA NDIO MAANA ANALIA SANA MWALIMU!!!! HAKUISHIA HAPO AKASEMA KWA KUHOJI IWEJE NYERERE ASHINDWE KUMLILIA SOKOINE NA AMLILIE MUHINDI(GABACHORI) JAMALI, KUNA GAZETI LILITOA PICHA YA MWAL.AKIPANGUSA MACHOZI WAKATI ANATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA KUSAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA AMIR JAMAL.[/B

]Nimeitoa hii ili jamii ndani ya Jambo forums isipoteze kumbukumbu vizuri juu ya kutuhumiana na hatimaye kila mtu kumpuuza mwenziwe na maisha yakasonga mbele. Ahsante sana
 
Mining sector under the microscope: Kiwira coal deal also up for review

-As Bomani committee seeks to make full use of terms of reference

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

THERE are strong indications that the latest government mining sector review committee will also probe the controversial privatisation of the previously state-owned Kiwira coal mine, whose majority shares are now owned by a private company set up by former president Benjamin Mkapa and senior minister Daniel Yona while both were still in public office.

The committee’s chairman, Judge Mark Bomani, made it clear in Dar es Salaam yesterday that the team may look into the Kiwira coal mine issue after concluding its ongoing review of major gold mining contracts in the country.

Responding to a direct query by THISDAY if the committee intended to review the Kiwira coal mine privatisation contract, Bomani said: ’’Right now, we are mainly focused on gold mines. After we conclude this process, our terms of reference give us the liberty to review any other mining contract.’’

He added: ’’We will reach that stage later. And when we do reach that stage, we may summon anyone relevant to our work.’’

The committee’s terms of reference include to review mining contracts and other key documents related to the sector; to evaluate the mining taxation system; and to review the government’s present regulatory system on mining.

The committee will also look into the rights and duties of the government and private investors respectively in mining sector issues; hold talks with the Chamber of Mines and other stakeholders; and make relevant recommendations to the government.

President Jakaya Kikwete has given the Bomani committee three months to conclude its work and submit its much-anticipated report and recommendations for action.

Well-placed sources in government say the committee may expand the scope of its probe by reviewing other contracts pertaining to the mining sector as a whole, apart from the existing Mineral Development Agreements (MDAs) between the state and foreign-owned gold mining companies operating in the country.

Located in Mbeya Region, Kiwira is the country’s only bona fide coal mine, with an average annual output in excess of 35,000 tonnes of the key mineral - most of which is consumed locally for power generation.

Investigations by THISDAY have established that in December 2004, Mkapa and Yona � while still serving as president and minister for energy and minerals, respectively - jointly registered a private company called Tanpower Resources Company Limited, with various close relatives including wives, children and in-laws in tandem.

At the time of its registration, the first listed directors of Tanpower Resources were the then first lady Mrs Anna Mkapa; Yona himself; Nicholas Mkapa (the then president and first lady’s son); Joseph Mbuna (Nicholas Mkapa’s father-in-law); and one Evans Mapundi.

Among other things, the company was licensed to ’’deal with coal mining in order to generate electricity for consumption and sale; to generate power generators, transmitters and general distributors; and to provide power and general projects management, project appraisers and consultants.’’

It has further been established that Mkapa and Yona - through their positions in government - were also directly involved in the privatisation of the then state-owned Kiwira coal mine. And in mid-2005 - just a few months after its incorporation - Tanpower Resources entered into a joint venture with the government to acquire 70 per cent of the Kiwira coal mine shares. The private company later increased its shareholding in the coal mine to 85 per cent, leaving the government with just 15 per cent.

Nicholas Mkapa - the president’s son - was then appointed to the board of directors of the renamed Kiwira Coal and Power Limited Company, while his father-in-law (Mbuna) became board chairman.

It has also been verified that the privatised Kiwira Coal and Power Ltd was also given control of the Kabulo coal prospect, a nearby but separate area formerly owned by the government, with proven reserves of up to 14 million tonnes of coal. The Kabulo coal deposits were previously under control of the State Mining Corporation (STAMICO), a government-owned agency.

When tabling his ministry’s 2006/07 budget estimates mid-last year, the then Minister for Energy and Minerals, Dr Ibrahim Msabaha, told parliament that the government had concluded negotiations with owners of the Kiwira Coal and Power Ltd company to expand power generation capacity to 200 megawatts by ’’using coal reserves at Kiwira and Kabulo.’’

Dr Msabaha, who has since been moved to the East African Community ministerial portfolio, disclosed in the House that the government, Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) and Kiwira Coal and Power Ltd had in March 2006 signed an agreement of intent for development of the $271.8m (approx. 326bn/-) Kiwira coal-fired power project.
 
Sakata la Mkapa Wapinzani wampinga Kikwete

sogeza Habari Zinazoshabihiana
• Rada yawakalia kooni Kikwete, Mkapa 24.02.2007 [Soma]
• Mkapa: Nchi ni changa kuhimili 28.10.2005 [Soma]
• Mkapa: Sina nongwa na Serikali ya Rais Kikwete 08.05.2006 [Soma]

Sakata la Mkapa
Wapinzani wampinga Kikwete

*Wadai mkopo wake uliwaweka Watanzania rehani
*Wasema alikiuka Sheria ya Maadili ya mwaka 1985

Na Reuben Kagarukki

VYAMA vya upinzani vimemtaka Rais Jakaya Kikwete, asimkingie kifua Rais mstaafu, Bw. Benjamin Mkapa, kuhusiana na madai kuwa alifanya biashara wakati akiwa Ikulu vinginevyo atalipeleka Taifa pabaya na kusababisha tuhuma nyingi kuibuliwa dhidi yake.

Kauli hiyo ilitolewa na viongozi wa vyama vya siasa Dar es Salaam jana walipozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti kuhusu msimamo wa Rais Kikwete alioutoa jana kwenye hotuba yake kwa Taifa kupitia kwa wahariri na wakuu wa vyombo vya habari kuwa Serikali yake haina mpango kumchunguza Rais msataafu Mkapa kutokana namadai hayo.

"Tuhuma hizi ni nzito kwa rais aliyeondoka Ikulu juzi, kutozifanyia kazi ni jambo la hatari kwa sababu mambo mengi yatazidi kuibuka," alisema Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw. James Mbatia.

Alisema ingawa sheria haimkataza Rais kufanya biashara akiwa Ikulu, lakini kitendo cha Rais Mkapa kukopa benki bila dhamana ni kinyume na Sheria ya maadili ya viongozi ya mwaka 1985.

"Hapa kuna mgongano wa kimaslahi, Rais akiwa Ikulu hawezi kubinafsisha urais wake kwa ajili ya maslahi yake binafsi, lakini kitendo cha kuchukua mkopo bila dhamana ni sawa na kubinafsisha urais kwa maslahi yake," alisema Bw. Mbatia.

Alisema, Bw. Mkapa alipoingia madarakani alitangaza kuwa yeye ni mtu wa uwazi na ukweli na kuweka wazi mali zake, lakini leo hii inashangaza anaondoka madarakani bila kutangaza mali alizonazo.

Bw. Mbatia alisema kama Bw. Mkapa hatatangaza mali zake kama ilivyo sasa, tuhuma nyingi zitazidi kumkabili jambo ambalo si zuri kwa mustakabali wa Taifa.. "Uwazi na ukweli wake ungesaidia kumuondolea tuhuma zinazotolewa...lakini bila kufanya hivyo yanaweza kutokea kama yaliyotokea kwa marais wa Zambia na Malawi baada ya kumaliza muda wao," alisema.

Alisema Rais Kikwete hapaswi kuzipuuza tuhuma zinazotolewa dhidi ya Bw. Mkapa. "Anasema hawezi kufanyia kazi taarifa za kwenye vyombo vya habari, mbona Mrema (Augustino) aliposema Mkapa amehongwa sh. milioni 900 iliundwa tume ya kuchunguza tuhuma hizo?"alihoji Bw. Mbatia.

Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Bw. Augustino Mrema, alisema kitendo cha Rais Mkapa kukopa kwenye benki bila dhamana ilikuwa ni sawa na kuwaweka rehani Watanzania.

Alisema kibaya zaidi benki hiyo ilipigiwa kelele sana wakati wa ubinafsishaji,lakini ilikingiwa kifua na Serikali yake. "Rais Kikwete anasema hana ushahidi, ni ushahidi gani anataka?"Alihoji Bw. Mrema na kumtaka aunde tume itakayowashirikisha wapinzani.

Bw. Mrema alisema alianza kumtuhumu Rais Mkapa kabla hajaondoka madarakani na kukumbushia madai yake kuwa alipewa kipande cha dhahabu na tuhuma za kesi ya sh. milioni 900 ambayo alishinda.

Alisema yeye anachotaka ni kuundwa kwa tume itakayojumuisha wapinzani ili kumchungumza Rais Mkapa.
 
Makani apania kumburuta Mkapa kortini

sogeza Habari Zinazoshabihiana
• CHADEMA yakosoa sh. bilioni 1 za CCM 29.08.2006 [Soma]
• 'Katiba irekebishwe' 30.11.2006 [Soma]
• Sakata la Mkapa Wapinzani wampinga Kikwete 08.06.2007 [Soma]

*Adai Rais huyo mstaafu amekosa kinga
*Asema kifungu cha Katiba kinapotoshwa

Na Suleiman Abeid, Shinyanga

SAKATA la tuhuma za ufisadi wa baadhi ya viongozi nchini limechukua sura mpya baada ya mmoja wa wanachama wakongwe wa CHADEMA, Bw. Bob Makani, kutangaza kusudio lake la kumfikisha mahakamani Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa.

Mwana CHADEMA huyo ambaye ni mjumbe wa kudumu katika kamati ya utendaji ya Taifa ya chama hicho, alitangaza kusudio hilo juzi alipokuwa akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Shinyanga katika viwanja vya shule ya msingi Jomu.

Bw. Makani alisema baadhi ya watu wamekuwa wakikitafsiri vibaya kifungu cha Katiba ya nchi kinachozungumzia kinga ya kushitakiwa kwa Rais mstaafu na kusema kuwa kifungu hicho hakitoi kinga kwa makosa binafsi, yaliyotendwa na Rais mstaafu.

Alisema hali hiyo ndiyo imesababisha Rais aliye madarakani hivi sasa aogope kumshughulikia Bw. Mkapa, kwa madai kuwa anafahamu wazi kuwa kuna mambo aliyoyatenda ambayo hayaruhusiwi kufanywa na Rais akiwa Ikulu.

Alisema ibara ya 46 ya Katiba ya nchi inasema Rais hawezi kushitakiwa kwa makosa aliyoyafanya akiwa Rais, ambapo Rais Jakaya Kikwete anatumia mwanya huo wa kutomshitaki Bw. Mkapa kwa vile alikuwa Rais.

“CHADEMA inasema, tafsiri yetu ni kwamba ibara hiyo inamlinda tu Rais kwa mambo aliyoyafanya akiwa Rais...apelekwe mahakamani akashitakiwe, na kama hawana wa kumshitaki, mimi najitolea nitakwenda kumshitaki,” alieleza Bw. Makani.

Aidha Bw. Makani alimwomba Rais Kikwete avunje Baraza la Mawaziri na kuliunda upya akiwaacha wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Alisema hali ya vitendo vya ufisadi na rushwa nchini imesababisha wananchi kuwa na hali ngumu kimaisha ambapo tofauti ya mapato kati ya maskini na tajiri imekuwa kubwa zaidi.

Alisema wakati kundi kubwa la wananchi wenye kipato cha chini wanapata matatizo ya maisha, wapo watu wanakula chakula kwa mrija na kwamba nchi hivi sasa inaelekea pabaya.

Kwa upande mwingine, Bw. Makani alisema hali ya mambo ndani ya CCM hivi sasa si nzuri na kwamba chama hicho kinaelekea kusambaratika.

Aliwataka wana CCM ambao wanaona mbali kuanza kujitoa ndani ya chama hicho kabla hakijasambaratika na kutoa mfano wa Dola ya Warumi, ambayo ilisifika kwa ukali, lakini ilifikia sehemu ikasambaratika.

“CCM inasambaratika, kama kuna mtu wa CCM hapa namwomba ahame kabla haijasambaratika, Dola ya Warumi ilikuwa kali lakini ilisambaratika, itakuwa CCM? Sasa hivi imegawanyika na imebinafisishwa," alisema Bw. Makani.

"Sasa hivi ukitaka kuwa kiongozi ndani ya CCM lazima uwe tajiri, nafasi zinapatikana kwa zabuni, kama unazo fedha utashinda na kama huna kwa heri,” alieleza Bw. Makani.

Alisema hata muasisi wa CCM marehemu Mwalimu Nyerere akifufuka leo, hawezi akajiunga na chama hicho tena na kwamba anaamini atajiunga na CHADEMA.
 
Babu, fanya kweli kama anavyofanya mtikila,

Hizi za bla bla za kutishiana kufunguliana kesi mahakamani tumeshazichoka.

Kama umeamua na sheria zinaruhusu wewe fanya kweli, tuko nyuma yako.
 
Back
Top Bottom