jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,375
- 25,453
Hivi ni kwanini viongozi wetu watuone watanzania hamnazo kiasi hiki? Hapa hawajui kuwa wananchi na rais si personal issues,ni mkataba wa kisheria kuwa tukikuchagua unafanya haya na haya kwa mujibu wa katiba ya jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,na kama kuna sheria zilizovunjwa basi haki inatendeka na si kurudisha issue muhimu za Taifa letu kwenye siasa na kutufanya wote wajinga.NDOTO za baadhi ya Watanzania za kutaka Bunge la Jamhuri ya Muungano limuondolee kinga Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, ili aweze kushtakiwa kwa tuhuma za kutumia vibaya madaraka yake na kujihusisha na biashara akiwa Ikulu inazidi kuingia wingu zito baada ya baadhi ya wanasiasa kuweka bayana kuwa jukumu hilo ni la wananchi.
Hapa sheria ichukue mkondo wake kama Rais mstaafu alizivunja na mwananchi wala hana haja ya kuulizwa hilo,hatuwezi kusem eti wananchi waamue,wananchi walishaamua na yeye akafanya tofauti,sidhani kama wananchi wangemchagua kama wangejua kuwa atafanya hayo madudu aliyoyafanya,na kwasababu wananchi walimwamini na kumchagua na kuwekeana naye mkataba chini ya kiapo kwa kutumia katiba ya nchi na mojawapo ya vitabu vitakatifu,na kwamba ulinzi wa mali za Taifa ikiwa ni mojawapo ya majukumu hayo yaliyopo chini ya mkataba,huwezi kudai eti wananchi ndiyo wenye maamuzi tena,hapa ni sheria na haki needs to take place.
Superman,inaelekea huna huruma na wananchi kabisa,matabaka ni shida kubwa sana tuliyonayo bongo na inayokomaa kwa kasi na pia empathy wengi wetu hatuna,na hata kama tunayo,basi ni based on hayo matabaka,shangaa unamwonea huruma Mkapa na mimi nawaonea huruma watanzania masikini. Tunaposema "Kupumzika" kabla hatujarosolve issues na concerns za wananchi kuhusiana na wizi wa mali zao chini ya mikataba ya ulinzi na uendelezaji wake kwa manufaa ya wote,tutakuwa tumewakosea haki na ni sawa na kudumaza demokrasia,mendeleo na uwezo wa kufikiri wa wananchi walio wengi wenye mahitaji muhimu ambayo ni haki yao lakini yamegeuzwa kama mitaji ya kuwapora haki zao za kimsingi na hivyo kubakia kama watumwa....Inasikitisha saaana!
Na wanachofanya wanasiasa hao ni kuendelea kuzitumia fedha walizoiba kuwalaghai wananchi kwa kuwatumia viongozi wengine waliochaguliwa na wananchi hao,tatizo ni kwamba wanapalilia Tanzania ambayo inaweza kukosa amani.
Nawaeleza kabisa viongozi hao kuwa dunia imebadilika na wasidhani watafunika kombe tu,it won't work like that,mambo yatakuja kubadilika siku moja na watu watajitolea kupigania uhuru upya,je wanataka hilo?
ccm ilijipatia umaarufu kwasababu ya harakati za uhuru,hilo litapita,ndio historia hiyo tunatakiwa tujifunze ili Taifa lisipitie huko,only if its neccessary....Mataifa makubwa tu kama USA walipigania Uhuru na baadaye wakaanza kuzichapa wao kwa wao,na migogoro kedekede,sisi tuna historia yetu na si lazima tupitie kama yao,lakini ukweli ni kwamba you can not full all the people all the time even if its true that you can fool some of them sometimes...
Kuna watanzania ambao hawatakubali kuona wanao na wajukuu zao wakiwa na potential ya kuwa watumwa ama masikini wa kutupwa kwenye Taifa lao, kama mnafahamu hilo ndugu viongozi,basi ni budi muwe makini.