Hii taarifa kama niya kweli, it attracts more curiosity than answers to any queries watu wameuliza in the past...Ngoja nijaribu kuwa na positive spin... lakini kazi ipo.... Kwanii.. hawa akina Mzindakaya wako wangapi Tanzania?? Watolewe list basi alafu media ifanye kazi - mimi ntalingoja hilo!
...
Hivi, ndio tuseme yeye mwenye Rais Msataafu hana mfano wake yeye binafsi anaoweza kuutumia? Yaani yeye kununua hizo mali zilizokuwa zinauzwa? Kwani process iliotumika akpata Mzindakaya anaweza share na public how it all worked?
...
Taasisi.
Hawa wakina Mzindakaya wako weeengi...inategemea aina ya 'ubinafsishaji' walioufanya ndani ya awamu ya Mkapa-
Kwa mfano:
-IGP anapokuwa na mazahanati, mashamba, mimagari etc hata anafikia kuwa mwanasiasa kwa kugawa misaada kwenye 'jimbo' lake..huu nao ni ubinafsishaji au?
-PM anapokuwa na shamba+mifugo mpaka mingine majuzi ime-raba hadi vyombo vya dola vikaingilia, huo nao ni ubinafsishaji au?
-Idd Simba anapohodhi miradi kibao nayo ni ubinafsishaji au?
-Waziri EL(as he then was) anapohodhi kakijiji ka nyumba huko Ars nao ni ubinafsishaji au?
-Magufuli anapojiuzia kakisiwa kalikokuwa ngome ya wajerumani kwa kisingizio cha kununua nyumba ya serikali(..in this I stand to be corrected..) huo nao ni uwekezaji wa wazawa au?
-Yote tisa- kumi ni pale Mkapa anapogeuza Lushoto kuwa kituo cha kitalii kwa hoteli yake ya kitalii na jumba lake la kifalme huko kwenye iliyokuwa ikulu ya wajerumani- yeye naye alibinafsisha au? kama ndio mbona hazungumzii hilo?
Na kwa taarifa za kuaminika mara baada ya kufungua hoteli hiyo alipeleka fliers kwa wenye makampuni ya utalii ili wampelekee wageni- huo tuuite uwekezaji wa wazawa au?
..bila ku-mention nyumba alizonunua mama Mkapa maeneo mbalimbali hapa nchini katika sera ya kuuza nyumba za serikali...
There is a long list of this..but the issue is..kweli Mkapa ameona hilo la Mzindakaya na ng'ombe wake 3000 ndo national issue?
Huu ni upuuzi!