Dhana yako si sahihi. Ingekuwa hivyo, watu wote waliowahi kuwa marais au viongozi wa nchi duniani wangekuwa ni matajiri sana kama yeye. Lakini ukweli siyo hivyo ila kwa wale wachache waliowahi kupata tuzo kama za Noble prizes. Huyu Mkapa hakupata tuzo zozote za kimataifa kama zile alizopata Nyerere lakini yeye ni tajiri mkubwa kuliko Nyerere liocvha ya kuwa Nyerere alikuwa ni mwalimu wake na ndiye aliyempa kazi ya Urais, kama siyo matokeo ya wizi kutumia nafasi yake ya urais. Sasa hivi anatafuta nafasi ya kuhalaliasha wizi wake kwa kutumia mlangoi wa nyuma. Tunamsubiri Sumaye naye arudi atufungulie benki kubwa au kampuni kubwa ili kuhalalisha pesa alizovuna kinyume cha sheria wakati wa utawala wake.