Hatuna system nzuri, huwa naona ujinga wakati mwingine kuzungumzia ishu za RAIS MSTAAFU, HUKU RAIS ALIYEKO MADARAKANI HAWEZI KUMFANYA KITU, BAYA ZAIDI MKAPA NDIYO KAMWEKA JK!MUULIZENI JK MLIYEMPA KURA!!
Kuuliza maswali ya kiwira, migodi, ni dalili za jamii isiyoweza kufanya lolote, ni kama mbwa anayebweka, ukitaka kuokota jiwe anakimbia.
Tatizo si Mkapa, tatizo ni sisi wenyewe, tatizo ni system, tatizo hatuna utamaduni unaojulikana, hatuna namna ya kuwaonya viongozi, Tatizo hili ni la ujamaa zaidi(tumerithi-zidumu fikra), we need to know the foundations of our country, ikiwezekana tuweke underpinning.
Kelele za MKAPA KILA SIKU MWAKA WA TANO SASA, sidhani kama zinasaidia, siyo mkapa viongozi wooote, ikiwemo na sisi tukifika pale je kitu gani kinamzuia mtu asiibe.Moral? , kuipenda nchi? ubinadamu?
Condom zipo,binadamu wapo, ukimwi, hupo, hatari ya ukimwi inajulikana, lakini wapi! watu if ingekuwa the only means ya kuondokana na tatizo ni kuruhusu uondolewe hamu??
Kama hatutaweza kumwondolea madaraka makubwa rais, kama hatutamprotect kutoshtakiwa, kama hatutachagua viongozi based on their performance, kama tutarubunika na kuwatandikia mazuria viongozi walafi, kama hatutakuwa na migawanyiko juu ya maslahi ya taifa, kama hatutazuia rushwa toka ngazi ya mesenja, then leo tusingelia hivi
we need to rediscuss the foundation of our country from the days of yore
NYAKATI ZA NYERERE ZIMESHAPITA, NYAKATI ZA RAIS NDIYO KILA KITU, NYAKATI ZA YEYE KUWAHAMISHA MAFISADI TOKA SHIRIKA MOJA KWENDA LINGINE, NYKATI ZA RAIS KUTOSHAURIKA NA KULAMBWA MIGUU!!! NYAKATI ZA KUWATETEMEKEA VIONGOZI WETU, NYAKATI ZA KIONGOZI KUWA MTUMWA NA SIO BOSS, ZILE TABIA TULIZORITHISHWA, TUZIANGALIE TENA. NYAKATI ZA KUPAKA RANGI MATOFALI YA SHULE WAKATI KIONGOZI ANAKUJA, NYAKATI ZA KUTENGENEZA BARABARA UJIO WA RAIS, HIZI ZOOOTE ZINAASHIRIA RAIS NI MUNGU MTU, BILA KUONDOA HILI WINGU, TUNABWEKA SAANA.
JK inajulikana amecheza dirty deals nyingi, yet tukampa urais kwa silimia 80% kesho JK ikajulikana kaiba, tutalalamika kwa nani?
Mkapa ameleta mpasuko wa watu, leo Mkapa anapendwa sana kila kona pamoja na ubaya tunaoujua, ndio kuna watanzania wamezoea kuliwa na kuonewa, kuna wasiojua morals, kuna wenye kuishi kwenye dunia ya afadhali huyu.
Wizi ni wizi hata kama anayekuibia anakupenda sana, hatuna utamaduni wa kuwafanya viongozi wetu waogope kuiba mali ya umma kama binadamu wote walivyo na tabia ya kutowaza kufanya mapenzi na wazazi wao!!! tukifika hapa ndio tunashuhudia nchi za wenzetu ukiwa na tuhuma tu unaachia ngazi, ukibambwa tu na mke wa mtu, huna uongozi, sio mpaka ushauriwe kama Chenge la! wewe mwenyewe unaona umefanya kosa kubwa sana, zile nyakati tukiziondoa, tumepona!
Kama hatuna tabia hii, Mkapa angepata wapi? kama Mkapa asingeiba tungejua lini tuna matatizo haya, kuwa hatuna system nzuri, taifa ndio kwanza linakua, tungalie mbele tuzuie yasitokee tena, ILA IKIWA NI WATU TU WA KULALAMIKA BILA KUFANYA JITIHADA ZA KUZUIA LISITOKEEE TENA, JE CHENGE AU ROSTAM AKIWA RAIS??, HAWA TUNAWAJUA JE TUSIOWAJUA??