Thanks a lot FMES. Ni mazuri gani aliyoyafanya Mkapa na kuwanufaisha Watanzania wakati alipokuwa madarakani? Mimi kwa maoni yangu hakuna lolote alilolifanya ambalo lilileta neema yoyote kwa Watanzania walio wengi. Kama lipo liwekwe hapa hadharani ili tulichambue kwa mapana na marefu.
Msilete takwimu za IMF na WB za uchumi wa Tanzania kukua kati ya asilimia 5 mpaka 7 wakati alipokuwa madarakani kwa miaka 10. Maana uchumi ukikua kwa kiwango hicho basi ni rahisi Wananchi wenyewe kutamka kwamba wanaona mabadiliko mazuri katika maisha yao ya kila siku maana ajira huongezeka, mishahara huongezeka na hivyo kuongeza purchasing power ya wananchi wa nchi hiyo. Hili halikutokea katika miaka 10 ya Mkapa kuwa madarakani.
Kuhusu jazba hakuna jazba yoyote hayo yaliyoandikwa na wengi ni ya ukweli kabisa hakuna lolote liliongezewa chumvi na kuyajadili si kuonyesha jazba, bali ndiyo ukweli wa mambo.
Ni vigumu kuyaona mazuri ya Mkapa kama tayari una conclusion
Maisha Bora ni ELIMU bila elimu hakuna kitu ,kama unataka kuona mazuri ya Ben kaulize wafanyakazi wa Serikali kati ya miaka 1990-1996 hasa walimu wa shule za misingi.
Wafanya kazi waliacha kazi nakuamua kuwa wafanya biashara, walikua hawalipwi mishahara hasa walimu ,kupata mshahara napo mpaka achape mguu kwenda wilayani maili zaidi ya 50.
Wanafunzi wa msingi kipindi hiki waliingia asubuhi na kutoka jioni bila masomo hakuna walimu.
kipindi hiki walimu walimaliza chuo bila kuajiliwa mpaka miaka 1998 ndio wamepata ajila.
Kushuka kwa Elimu ya UDSM na elimu kwa ujumla ni consequences zinazotokana na miaka hii 1990-1996.
Kipindi hiki kilikua ni kushinda kwenda sekondari wilaya nzima wanaoenda secondari baadhi ya wilaya walikua hawafiki hata wanafunzi 100.
Serikali ilikosa nidhamu ,serikali ilikosa mwelekeo
Rais wa nchi alikua SHEMEJI yani mtani wa wanafunzi.
Mkapa kashika serikali iliyokua ni VIRTUAL serikali .Mwinyi hakuna alichofanya zaidi ya RUKSA yani bidhaa kutapakaa kutoka nchi za nje.
Najua wengi tunampenda Mwinyi kwa sababu tu ktk kipindi chake ndio tuliona Video na films za akina RAMBO ,VANDAME, LANJITI nk
Kila binadamu ana mabaya yake lakini mazuri aliyofanya ni makubwa zaidi ya kiwira .
Mwinyi aliua makampuni yote na viwanda karibu vyote vya umma
MWAtex,mutex,kagera sugar vyote vilikua ni makazi ya NGUCHIRO na si kwamba kulikua na mashine ndani yani hata machine zilikua zinang'olewa na kuuzwa.
Sasa Mkapa kubinafsisha hayo makapi imekua nogwa?? Kampuni zipi zilikua hai wakati mkapa aniingia madarakani kama sio sigara na bia ?
Kwanza hizo masalia ya viwanda hata angevigawa bure kwa watanzania wachache sana wangevichukua na kuviendeleza zaidi ya AZAM,Mengi na Gachuma.
Kumbe cha kuangalia hapa si bei gani kilizwa bali Serikali inaingiza ,mapato na bado nchi inazalisha bidhaa zake.
Tungeyakumbatia hayo maviwanda kwa kudemand mahela mengi na yakakosa watu wa kuyaendeleza serikali ingelikua wapi? ingetegemea sijui nini??