Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Leo hapa kutakucha!
Ndiyo, japo nina serious reservations kuhusu Mkapa, lakini naungana na BongoTz kuwa Mkapa, ni mtu safi ukiliganisha na hao wengine. Mkapa anabebeshwa mzingo mzito hapa. Mtu mmoja hawezi akabadili uozo wa taifa zima kwa kipindi kifupi cha miaka kumi tu. Hata Marekani yenyewe bado inaendelea kukubwa na kadhia za mabillioni ya dola ingawa wawo wamekuwa huru kwa miaka 232. Unakumba Enron na mengineyo...!?
 
You know I posted this thread to test and see how smart or foolish Tanzanians really are, and most of you (indeed) have proved to be the latter.

Foolish people.

Acheni kukaririshwa mambo na inner circle wa Kikwete hapa!

Be smart people.

1. Specific – We are very specific to condemn the actions of GRAND CORRUPT Mkapa

2. Measurable – The Damages he has done is Measurable it worth $500,000,000, which could be invested in our own modern Mining companies with Tanzania government could have 100% ownership

3. Achievable – We have achieved to Know what he thought we will never Know

4. Realistic – For you to know we real you will see how he is going to Jail soon

5. Time – This is the time we can’t take it and anymore and therefore he has to be Example, instead of being a former president he will be a precedence
So the question is who is SMART between you and us
 
BongoTz,

Mkuu nitakupa mtililiko mdogo sana ambao unafahamika kwa wananchi na nakuomba unipe jibu kutoka rohoni mwako kwa kusoma na kuelewa nilichoandika kwani naelewa wazi unafahamu kwa kirefu zaidi ya haya nitakayo andika...

Ni hivi:-
1. Nyerere alipochukua nchi alikuta hakuna kitu (Mtaji) akakopa fedha na kujenga miundombinu, viwanda na kadhalika hadi fedha zikamwishia, hakuacha kitu benki zaidi ya madeni...lakini vitu zimesimama ila wananchi hawakupata kufaidi uwekeshaji huo.

2. Kaingia Mwinyi akaona kuwa vile Viwanda havina faida kwa wanawe (Watanzania) akaamua kuviuza na fedha akalipa madeni aliyoyaacha Nyerere, hakuweza kujenga miundombinu isipokuwa kuacha uwanja wazi kwa wananchi kuingia ktk Utandawazi na soko huria ktk kuboresha uchumi wa nchi..Naye Benki hakuacha kitu zaidi ya madeni mapya.

3. Kaingia Mkapa akaona hali ngumu akakopa fedha na pia kudai wale wote walikuwa wakidaiwa na serikali toka serikali ya mwalimu..Akazidisha kodi zote zinazohusiana na uagizaji wa mali nje bila kuboresha uzalishaji ndani - Akauza mashirika yote ya Umma na kujaza fedha benki..
Lakini kabla hajaondoka akapiga panga nusu, akauza mashirika yote kwa bei ya njugu kujinufaisha yeye na marafiki wake, akachukua hata nyumba za wananchi kuwagawia rafiki zake (Mugabe style)...Mwisho wa yote akatuachia madeni pia..

Nani mbora kati ya hawa..na kwa nini?
 
You know I posted this thread to test and see how smart or foolish Tanzanians really are, and most of you (indeed) have proved to be the latter.

Foolish people.

Acheni kukaririshwa mambo na inner circle wa Kikwete hapa!

Be smart people.

Kama unaona kwamba watu wote hapa JF ni foolish isipokuwa wewe basi ingekuwa vyema usingeleta topic yako kujadiliwa na ma-foolish.

Lakini mimi sintaona haya kukuonea haya kukuambia wazi kwamba wewe ndiyo foolish mkubwa.
 
Kuna mengi yamesemwa/andikwa kuhusu Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mh. Benjamin William Mkapa: "Oh, mkapa ni fisadi," "Mkapa alitumia madaraka ya Urais vibaya," "Mkapa ajitete mbele ya umma," "Blah... blah... blah..."

Lakini ukweli ni kwamba: ni Mzee Ben, na sio Mzee ruksa, wala this Kikwete guy, ambaye ameifanyia nchi hii mema na mazuri. Ikumbukwe kuwa baada ya uchaguzi mkuu wa 1995, Mkapa alipokea nchi iliyokuwa katika hali mbaya kupindukia.

Rushwa ilikuwa imekithiri. Pato la taifa lilikuwa chini. Ukwepaji kodi ulikuwa katika kiwango cha kuogofya. Na miundo mbinu ilikuwa imechoka kupindukia.

Ni chini ya utawala wa mzee Ben ndipo watanzania kwa mara ya kwanza tulipoanza kuona sera ya taifa kuhusu uchumi ikipewa kipaumbele. Miundo mbinu ikiboreshwa. Pato la taifa likikua. Na kamba dhidi ya vita ya rushwa ikikazwa.

Lakini pia katika viongozi tuliowahi kuwapata, ukimuacha Mwalimu, ni Mkapa peke yake aliyekuwa na ubavu wa kupinga kuendeshwa na nchi za Magharibi. Mwinyi alikuwa anajikojolea wahisani wakikohoa, Kikwete (sote tumeshuhudia) anacheza samba kila mara nchi za magharibi zikimuamuru afanye hivyo.

Yes, kuna mabaya amabayo Mkapa ameyafanya ktk kipindi cha miaka 10 akiwa ikulu: (1) mikataba mibaya hususani madini (ambayo hata hivyo ni mwanasheria mkuu ndiye anapaswa kulaumiwa);(2) kumuachia mke wake a—dictate badhi ya shughuli za kiserikali ( one of his weakness). (3) kujihusisha na bishara akiwa ikulu (which is a minor thing)...

Cha msingi hapa ni kujua kuwa Mkapa sio Malaika bali mwandamu. na kama mwadamu, naye pia anahadawa na tamaa ya kuwa na maisha yaliyotulia. You know, financial security and all those things, kwa ki-inglish.

Hitimisho: Hapa suala ni kwamba, Kikwete and his inner circle wameshaona kuwa wamechemsha big time, hivyo wanachokifanya ni kumchafulia mzee Ben jina ili watu wasipate fursa ya ku-compare utawala wake (mtalii Kikwete) na ule wa mzee Ben (mtu safi).

Tunafahamu kuwa Mkapa ni ndugu yako wa Damu, Lakini hatuko personal hapa, Tunajariku kuelewesha kuwa Mabaya alaiyoyafanya Mzee wako.

Pili usipokiri sasa utapata shida katika maisha yako ya kisiasa mbeleni.

Wewe Nicolus Baba mkwe wako ndiye attorney wa serikali kule kiwira sio, Mzee Mbuna hayo yote tunajua, Ila we are giving you more Time Kutubu kabra hujaanza kulaaiwa na watanzania wanaolala njaa.
 
You know I posted this thread to test and see how smart or foolish Tanzanians really are, and most of you (indeed) have proved to be the latter.

Foolish people. Acheni kukaririshwa mambo na inner circle wa Kikwete hapa!
Be smart people.

Yaaani inner circle wa Kikwete ndio walionunua Kiwira kwa bei poa tena bila kulipa hata senti moja?

Hao inner circle wa Kikwete ni nani hasa wakati sasa hivi tunajua kuwa Lowassa na Mkapa ni kundi moja!
 
Mkandara, at least wewe una-think big kidogo. Analysis yako ina make sense kiasi. Ila kumbuka kuwa mashiraka hayo unayodai kuwa Mkapa aliya-uza kwa bei ya njugu kujinufaisa, yalikuwa yanatia serikali hasara (huu sio ujamaa mkuu). So, ni bora kuyauza kwa bei nafuu kwa makaburu (watu wapate ajira, kodi ikusanywe) kuliko kuyaacha yakiwa jumba la maonyesho.

Plus, bear in mind that in today's global economy you can't just be a protectionist. You will suffocate your economy. It's all about economic interconnnections with the rest of the word. It's globalization.

Globalization is here to stay whether we like it or not, people.

I have to concede, though, kwamba we jumped to this globalization thing so unprepared (naamnisha utawala wa Mkapa), ila tusimshikie bango Mzee Ben kupita kiasi wananchi. let's learn from our mistakes, and move on.
 
Babu, Mkapa ni dugu yako nini? Mbona unamtetea kwa nguvu zote. Kulikoni? Ama umekuachia 10% ?

Sidhani kama ni ndugu yake wala nini, ila hajui kitu anachokisema.

Katoa idea dopey haina mfano, kwamba wanaomchafua Mkapa ni inner circle wa Kikwete!
 
Mkandara, at least wewe una-think big kidogo. Analysis yako ina make sense kiasi. Ila kumbuka kuwa mashiraka hayo unayodai kuwa Mkapa aliya-uza kwa bei ya njugu kujinufaisa, yalikuwa yanatia serikali hasara (huu sio ujamaa mkuu). So, ni bora kuyauza kwa bei nafuu kwa makaburu (watu wapate ajira, kodi ikusanywe) kuliko kuyaacha yakiwa jumba la maonyesho.

Plus, bear in mind that in today's global economy you can't just be a protectionist. You will suffocate your economy. It's all about economic interconnnections with the rest of the word. It's globalization.

Globalization is here to stay whether we like it or not, people.

I have to concede, though, kwamba we jumped to this globalization thing so unprepared (naamnisha utawala wa Mkapa), ila tusimshikie bango Mzee Ben kupita kiasi wananchi. let's learn from our mistakes, and move on.

Waulize Wamarekani globalization inavyowafanya vibaya hata kununua chupi made in USA imekuwa shida na hawa ndiyo Taifa kubwa na sasa wanalia na kusaga meno sembuse sisi Tanzania!!
 
BongoTZ you may have alot of talent but not bongo. The best nickname should be FisadiTZ!.

Mauzo ya Radar-Mkapa
Wizi wa Bank Kuu-Mkapa
Ununuzi wa ndege kwa bei ya juu-Mkapa
Mikataba mibaya ya madini-Mkapa
Tatazo la Umeme na Mikataba-Mkapa
Kampuni ya makaa ya mawe kuuzwa bila kunadi bei-Mkapa

Tanzania tumepata nini kwenye mikataba ya madini?? Wanakijiji wa hizo sehemu wamepata nini?. Uchumi wa Africa si Tanzania tu unakuwa kila mahali na sababu ya Tanzania kukua kwa sasa ni kwasababu tuna resources nyingi na India na China zinakuwa Kiuchumi.Usimsingizie Kikwete anamatatizo yake lakini ufisadi mkubwa nchini kwetu umefanywa na Mkapa na anastahili kufungwa au hata kupigwa risasi kwa aibu aliyoiletea nchi yetu. kikwete ameruhusu vyombo vya habari kuwa huru hata kama vikimsema vibaya na anahitaji pongezi kwa hilo. Mwinyi alikuwa bora kuliko Mkapa na ukiwauliza Watanzania wachague raisi kwa mapenzi na maendeleo Mkapa atashika mkia. Hivyo ndugu FisadiTZ amka usingizini na tunashukuru mungu huyu jamaa kwa afya yake mungu atamchukua tu mapema atoe aibu kwa nchi.
 
FisadiTZ said "wewe una-think big kidogo" kama vile watu wote hapa ni wajinga!. Watu wengi hapa ni wasomi na kusema hivyo inaleta fikra kwa watu kwamba wewe ndiyo unajua yupi ana think big!!. Webmaster hii topic haina misingi ni propaganda tu.
 
I suppose baadhi yenu (Mwanakijii especially) mmekasirishwa sana kwa mimi kutumia neno 'foolish." You don't have to. "Foolish person" kwa definition yangu ni " someone who is easily tricked". Nasema "easily ticked," coz Kikwete's inner circle wame-manufacture nyingi ya hizi kashfa kuhusu mzee Ben, kisha wakazi-leak kwenye press, bloggers nao wakazidakia, huo moto hauzimiki. The daunting quesion is: kwanini watu hawataki ku-pose na kujiuliza, "wait a minute, kwanini Kikwete anaacha hizi kashfa ziende unaswered kama Mkapa ni fisadi kweli?"

Well, kama hujui, lallow me to educate you: Kikwete anajua kuwa ameshachemsha kuhusu suala zima la kuiongoza nchi. Anajua fika kuwa muda wake ukiisha, historia itamhukumu vikali kuhusu utendaji wake na ule wa Mkapa. Therefore, ili kuwapumbaza watanzania wameamua kumchafuria Mkapa jina kwa nyingi ya hizi false scandals.

On the record: Mkapa sio ndugu yangu. Mimi najaribu tu kuwa objective hapa, ok. Ndio maana kama umesoma thread yote "Mkapa ni mtu safi. Period." Nimeelezea pia mabaya ambayo Mkapa ameyafanya. And yes, kuna makosa mengi ameyafanya, nakubariana na nyie. Ila kwa jinsi ambayo amekuwa trashed/disrespected (recently), inaonyesha kuwa kuna juhudi za makusudi ku- tarnish legacy yake. Na people behind campaign is no one but Kikwete's inner circle.
 
I read BongoTZ post, couldnt believe what I was seeing, took some aspirin and went to sleep hoping that when I wake up it would all just be a dream. I have woken up and sadly it is true - some one has confirmed what I always feared, my beloved country has gone to the dogs. I would have said more except that in my rush to deal with BongTZ, I came across two statements that go thus;

1.You know I posted this thread to test and see how smart or foolish Tanzanians really are, and most of you (indeed) have proved to be the latter. Foolish people.

2. Acheni kukaririshwa mambo na inner circle wa Kikwete hapa!

These two statements summarize it all - we are dealing with a delinquent. It wont be worth giving him the honour of intellectual discussion. He does not deserve it. I rest my case.
 
Warioba; Tusiruhusu Kashfa zitugawe

Na Yahya Charahani

WAZIRI Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba ameonya dhidi ya utamaduni wa kuchafuliana majina ulioibuka miongoni mwa jamii kwa kuwa utakapokomaa utasababisha wananchi kusahau mambo ya msingi na kusababisha vurugu.

Akizungumza jana ofisini kwake Oysterbay, Dar es Salaam Jaji Warioba alisema, amestushwa na utamaduni huo ambao unaonekana kukomaa kiasi cha kumgusa mtu muhimu kama rais.

"Nimeulizwa maswali mengi baada ya kutoka 'orodha ya mafisadi', nimeipata, lakini ninachoweza kusema hakuna jipya katika orodha ile, zaidi ya kupakana matope, kwani orodha ile inafanana kabisa kimtiririko tuhuma zake na orodha mbili zilizopita,"alisema.

Alisema ameona yaliyoandikwa katika ile orodha inayoitwa 'list of shame' mengine yamemstua sana, nchi ikifikia kumtaja rais ni fisadi imefika mbali, na kwamba mtu hawezi kutoa tuhuma kama hizo mpaka awe na ushahidi mzito usioacha shaka.

Alisema rais ni alama ya taifa na kwa maana hiyo mtu anapomtaja rais kuwa fisadi na kisha akaendelea kujigamba kuzungumzia juu ya hilo hatimaye ina maana hakutakuwa na uongozi wa taifa, itakuwa ni hatari.

Alitoa mfano kama tuhuma za namna hiyo zinaendelea ina maana kuwa wananchi wanaweza kukosa imani na serikali yao suala ambalo ni hatari na halitakiwi kufumbiwa macho.

"Unapomtaja rais kama fisadi unakuwa na unataka kufanya wananchi wakose imani na serikali yao suala ambalo ni hatari, wananchi watakimbilia wapi kama wanayetaka kumkimbilia naye anachafuliwa," alisema.

Hivi karibuni Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk Willibrod Slaa, aliwataja vigogo 11 wengi wao wakiwa katika Baraza la Mawaziri la Serikali ya Awamu ya Nne kwamba ni mafisadi waliohusika na ubadhirifu wa mabilioni ya fedha za umma.

Miongoni mwa waliotajwa na Dk Slaa akishirikiana na Mwanasheria wa chama hicho, Tundu Lissu, ni makatibu wakuu wawili, mwanasheria pamoja na viongozi wengine waliokuwa katika serikali ya awamu ya tatu.

Dk Slaa aliwataja vigogo hao wiki iliyopita katika Viwanja vya Mwembeyanga, Temeke wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa vyama vya upinzani katika mikoa 11 ya Tanzania, ikiwa ni kutimiza ahadi yake aliyoitoa mwezi uliopita katika Viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia tuhuma, Jaji Warioba alishangazwa hata Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kutajwa katika baadhi ya ripoti wakati rekodi yake inaonyesha kuwa kafanya mengi mazuri, lakini taarifa zinazotolewa zimelenga tu kumchafua.

Kwa muelekeo ulivyo sasa alisema, inaonekana kwamba kuna njama na jitihada za makusudi za kuchafua majina na kisha kusumbua utawala uliopo kukimbizana na hoja za ufisadi wakati mambo ya msingi yakiachwa bila kutekelezwa.

Alishangaa kwamba kila kukicha viongozi wanatishia kwenda mahakamani suala ambalo linaonyesha kuwa viongozi wanatumia muda huu kujibu tuhuma badala ya kushughulikia masuala ya maendeleo ya taifa.

"Sikatai Mkapa ni binadamu anaweza kuwa na mambo yake, lakini siyo kiasi cha kufuta rekodi yake. Hivi kweli mtu unaweza kweli kufuta rekodi ya Mkapa kwa utendaji wake uliowezesha kushusha inflation ya asilimia 30 alipoingia madarakani hadi tano wakati anaondoka, kisha ukatoa tuhuma za jumla jumla tu, hivi nadhani si sawa," alisema.

Aliorodhesha miongoni mwa mambo yaliyofanywa na Rais Mkapa ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za afya, elimu, uchumi miundombinu na vitu vingine.

Kwa mtazamo wake alisema kuwa, baada ya uchaguzi mambo ya msingi ambayo sasa yangekuwa yakishughulikiwa ni pamoja na uboreshaji wa kilimo, kukabiliana na tatizo la bei za umeme kuwa juu, mfumuko wa bei na vinginevyo, lakini badala ya kushughulika na hayo, suala lililowekwa mbele ni kuchunguza dosari za viongozi.

Hata hivyo aliitaka jamii kutoacha kupambana na viongozi wala rushwa iwapo kunakuwapo ushahidi wa msingi na uthibitisho usioacha shaka, lakini jamii hiyo hiyo isitumie mwanya huo kujineemesha kisiasa.

"Sisemi kwamba viongozi wala rushwa wasiandamwe la hasha, waandameni iwapo mna ushahidi wa kutosha na msiishie kuwataja tu songeni mbele zaidi kuhakikisha haki inatendeka," alisema.

Pia alisema ni muhimu vyombo vya habari na jamii vikasisitiza katika kuwapo utawala bora, lakini si kwa kiwango cha kusahau vipaumbele vingine katika jamii.

Alisema inavyoonekana kama kuna jitihada za makusudi za kuchengesha mambo ya msingi kwa jamii yasishughulikiwe, ili suala liwe ni moja tu kukimbizana na tuhuma ambazo zinatolewa na kisha kutofuatiliwa.

Hali hii anasema Warioba kuwa huenda ikasababisha muda si mrefu masuala yaliyolisumbua taifa kipindi kilichopita yakarudia tena kusumbua, sababu mwelekeo unaonekana ni kukimbizana na kujibu tuhuma.

"Wiki chache zilizopita nilikuwa Mara kwa shughuli za uchaguzi, nikasikia kwenye vyombo vya habari Mungai analalamika watu wanampaka matope eti mara wanamwita si raia, inashangaza sana, hivi kweli mtu kama Mungai anaweza kuhojiwa vitu vya ajabu kama hivi, tunakokwenda siko," alisema.

Aliwachekesha waandishi wa habari pale alipojibu swali aliloulizwa na mmoja wa waandishi wa habari aliyetaka kujua kama alitumwa kutoa taarifa hiyo akajibu : "Sikutumwa na mtu, simo katika siasa, wala serikali mimi ni mtu huru hakuna mtu aliyenituma, nasema ninachokiamini."

Source: Mwananchi

Tag it:?
 
...we are dealing with a delinquent. It wont be worth giving him the honour of intellectual discussion. He does not deserve it...

Safi sana!

Kuna vitu vingine havistahili kujibiwa.
 
" How many legs does a dog have if you call tail a leg? Four. Calling a tail a leg doesn't make it a leg."~~ Abraham Lincoln

In other words, Mkapa will remain to be "Mr. Clean". Hawezi akawa fisadi kama wengi wanavyo wish hapa.

Kuhani you need to stop whining. Your argument is weak, and it defies logic.

Why all the name-calling, homie?
 
" How many legs does a dog have if you call tail a leg? Four. Calling a tail a leg doesn't make it a leg."~~ Abraham Lincoln

In other words, Mkapa will remain to be "Mr. Clean". Hawezi akawa fisadi kama wengi wanavyo wish hapa.

Kuhani you need to stop whining. Your argument is weak, and it defies logic.

Why all the name-calling, homie?

Fisadi Mkapa will remain 'Mr Clean' to people like you who don't have the ability to use their brain, but to many Tanzanians he will always be a FISADI who did not deserve to be the leader of our beautiful country.
 
Back
Top Bottom